Mgomo wa wafanya biashara ni wa kipuuzi kuwahi kutokea! Wao inawahusu nini mlaji akipandishiwa bei bidhaa? Wao ni wapeleka kodi tu anayelipa ni mlaji

Si kweli ungea kikodi zaidi.mlaji wa mwisho ndio anayebeba mzigo wa kodi na mfanyabiashara ni wakala tu wa hizo kodi sasa inakuwaje kwamba inapunguza uwezo wa mfanyabiashara kununua?hiyo ni principle gani ya kodi?
Mfanyabiashara akienda kununua bidhaa zake duka la jumla au kiwandani anapewa Bure hailipi kodi ya VAT?

Akitoa mizigo Bandarini ya biashara aliyoagiza nje hailipi kodi ya VAT?
 
Unafirw*
 
Mauzo yakishuka maana yake kuna mtu hataweza kula, kuvaa, kujenga na kushindwa kabisa kujikimu kimaisha, na hapo ndipo kutakapotokea hasira za wananchi kudai haki zao

Wao wafanyabishara inawahusu nini maumivu ya walaji?
Mfanyabiashara anapokuwa katika biashara yake.
Upande mwingine pia ni Mlaji.
Pia huyo upande mwingine ndo Mwananch.
Kwa hiyo yupo sahihi.
 
Huna akili! Kwenye nchi ambayo aina mifumo ya kuaminika ya kiutawala wafanyabiashara wasipochukua hatua unafilisika asubuhi tu!

Wewe unaleta mzigo kwa kufata taratibu zote! Mwenzako yeye anatumia ubovu wa mifumo anaingiza mizigo sokoni kimagendo anauza bidhaa kwa bei ya chini! Unafikili kinachofata kwa wazalendo wanaopitisha mizigo ki halali ni nini?! Kipindi cha JK wafanyabiashara kama gsm walikuwa wanapitisha mizigo kimagumashi na wanauza bei ya chini utashindana nao sokoni?!

Kuna watu wawekezaji wanapewa tax holiday ya miaka 5! Harafu hao hao wanaingiza bidhaa sokoni kwa soko la reja reja hutashindana nao?!

Mimi nalipa pango na kodi halafu mtu mwingine anaweka biashara kibarazani kwangu ana bidhaa kama yangu yeye halipi pango wala kodi zozote! Utashindana nae sokoni?! Tatizo hujawahi kufanya biashara ila unatoa maoni kuhusu biashara! Maoni yako yangekuwa na maana kwenye nchi zilizo serious sio uku kuliko jaa rushwa na ufisadi na mifumo iliyo palalalaizi.
 
wewe sio mfanyabiashara wala sio mteja wao.
 
Hoja
 
Sasa kàma nyie walaji mmelala kwanini msisaidiwe?? Nyambafu
 
Bei ikipanda wahitaji lazima wawe wachache hali inayofanya Mauzo yashuke lakini pia una habari watu sasa hivi wanaogopa kwenda hospital wakihofia gharama.
 
Hao wafanyabiashara ni wajinga na mimi nashangaa kwa nini serikali inaangalia nao.ningekuwa mimi raisi ningeenda kupiga makofi ya serikali ili waende wakafanye biashara Burundi.
Kwa akili za aina hii kama Taifa, hakika tuna safari ndefu kweli kweli.
 
Uko sahihi sana ndugu Nsanzagee, kwamba walichopaswa kufanya wafanyabiashara ni kuongeza tu bei ya bidhaa na huduma zao Ili mlaji wa mwisho (mwananchi) ndiye aumie kisawasawa ili kama akitambua kuwa anaumia ndiyo sasa achukue hatua dhidi ya watunga sera na serikali yao kwa kuansamana na kugoma kama wanavyofanya Kenya sasa.

Lakini Mimi nadhani hawa wafanyabiashara wana kitu kingine zaidi ya hiki unachofikiri wewe (kuwa ni wajinga tu). Hapana si wajinga. Wako sahihi na wanajua wakifanyacho.

Aidha, ukumbuke kuwa nao ni wananchi.

Ukiachilia mbali kazi yao ya biashara, lakini pia wanahitaji huduma zingine muhimu kama elimu, barabara, huduma bora na nafuu za afya, usafiri na usafirishaji, mawasiliano, maji safi na salama, mazingira bora na salama ya kuishi, amani na usalama nk

Kugoma kwao si tu kwamba kunahusu biashara zao. Kunatuhusu hata sisi wateja wao, walaji wa mwisho wa huduma zao wanazotupa

Wewe unafikiri wafanyabiashara wanajisikiaje iwapo wanalipa kodi, ushuru na tozo nyingi ambazo wanaona kabisa kuwa zinaenda kwenye mifuko ya viongozi wa umma wachache na kutajirika pasipo kutoa jasho na wakati huo huo huduma za kijamii kama nilivyozitaja hapo zikiwa duni na za hovyo?

Unadhani hao wafanyabiashara hawahitaji maji? Umeme wa uhakika? Elimu bora kwa ajili ya watoto wao? Barabara bora kwa ajili kupita na magari yao?

Wewe unadhani wanajisikiaje kuwaona watu tuliowaamini kama viongozi waadilifu kugeuka kuwa wezi na mafisadi waliokubuhu kwa fedha za umma zinazolipwa kama kodi, tozo na ushuru mbalimbali Ili kutoa huduma bora kwa watu wote?

Mfano ni hili skendo la ufisadi wa sukari ambalo viongozi wetu wachache wakiongizwa na waziri wa sekta ya Kilimo (Hussein Mohamed Bashe), yule wa fedha (Mwigulu Lameck Nchemba) na Bodi ya Sukari Tanzania kushirikiana na baadhi ya kampuni za wafanyabiashara wachache mafisadi na wezi kuiba au kuihujumu mapato ya nchi zaidi ya TZS 700bn huku wabunge (wawakilishi wa wananchi) nao wakihongwa Ili kufunika wizi na ufisadi huo.

Wewe unafikiri wanajisikiaje hawa wafanyabiashara? Yaani wao wabanwe kulipa Kodi kubwakubwa huku wenzao wachache wajanja wajanja wakipewa misamaha kinyume kabisa cha sheria na utaratibu?

Kwa hiyo: HAPANA wala sio wajinga na wala sio wapumbavu kwa kuchukua maamuzi ya kugoma. Wameanza wao na sisi wananchi tunatakiwa kuwaunga mkono badala ya kuwatukana na kuwataja wapandishe bei ya bidhaa na huduma zao.

Shida iko kwako wewe Nsanzagee na wananchi wenzako!!
 
Huyo mlaji ana uwezo wa kulipa hiyo kodi? Serikali si. Ilishindwa kukusanya hizo kodi za kichwa ambazo sasa zimerudi kama Vat?
Mlaji hana uwezo wa kulipa hiyo kodi ndo maana mkusanyaji (mfanyabiashara) analalamika,
 
Huu uzi umeandika kwa makusudi ili tukujibu kwa lugha mbovu tupigwe ban?
 
Waliogoma haswa ni importers yaani wale ma tycoon, kuna wachuuzi na ma tycoon, kuna waliofungua jana na leo lakini wakienda kuchukua mizigo wahusika wamegoma,Huna jinsi hapo itabidi ufunge,
 
Kama umesoma basi ujue unawadharirisha waliosoma waonekane wapuuzi.

Ukutaka kujifinza kwa vitendo kajaribu kufungua biashara kariakoo hata kuuza chupi za mtumba tu,.
 
Wewe ndio mpuuzi,mshenzi na takataka kama Ndomu ambayo CCM wakishaipigia bao wanaitupa chooni. Kama hujawahi kufanya biashara shut up you stinking and wrotten mouth💩💩
 
Kenya wanachofanya unawaunga mkono jinsi wanavyopora maduka ya watu na Hadi vyakula vya mama nitilie
Biashara zimefungwa na Bado wanavunja milango ya maduka na kupora
 
Waliogoma haswa ni importers yaani wale ma tycoon, kuna wachuuzi na ma tycoon, kuna waliofungua jana na leo lakini wakienda kuchukua mizigo wahusika wamegoma,Huna jinsi hapo itabidi ufunge,
Wakiendelea utasikia Kuna siku serikali Haina pesa za kulipa mishahara ya wanajeshi Sababu ya Kodi kupungua
 
Huyu ni kula kulala au anaishi kwa shemeji hajui kitu
Mkuu OKW BOBAN SUNZU kutoa maoni haijawahi kuwa ni kosa la jinai

Nadhani pia, bado hukuelewa mtazamo wangu umewahi kutoa wazo lako la mwisho kwa kuwa tu umeshachoshwa sana na sera za maccm

Mimi nataka sera hizo ziendelee kwa kasi ili wananchi wengi watakapochoka ndio tuone faida ya migomo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…