Mgongano: Serikali Vs. Mwanahalisi - Mipaka ya Maoni?

Mgongano: Serikali Vs. Mwanahalisi - Mipaka ya Maoni?

Mkuu wangu Ushi Wa Rombo,

Heshima mbele sana, msimpe nafasi huyu jamaa akaharibu flaw ya hii habari maana bado, tunaendelea kuzi-monitor hizi habri muhimu sana maana some how somewhere ninaamini kwamba jupi linataka kupasuka huko ndani ya CCM.

Sasa msimpe nafasi huyu jamaa kuubadili huu mjadala kuwa yeye kama anavyotaka sasa badala ya taifa letu, mind you huyu jamaa wala sio raia wa Tanzania kama mimi na wewe, ndio maana hulilia sana dual-citizen ipitishwe, lakini tulishawafahamisha wabunge wengi kwua wakipitisha hiyo basi Tanzania tutegemee watu wengi kama huyu bwana kuja kutuchafulia amani ya taifa letu.

Pole sana kwa kazi hii mkuu FMES.
Tuko pamoja kuwakoma hawa mafisadi
Nimekuwa msomaji mzuri sana wa Mwanahalisi, sijasikia Kikwete akikanusha ama kukaripia habari zinazoandikwa Mwanahalisi. Ninachokumbuka ni kwamba, wakati Kubenea alipomwagiwa tindikali, JK alienda hospitali ' in person' kwenda kumjulia hali na kumwambia kwamba asikatishwe tamaa na watu (isomeke M.A.F.I.S.A.D.I) wasiomtakia mema yeye na taifa kwa ujumla.
Kwa sababu hiyo basi naamini kabisa kwamba JK anajua kabisa kinachoendelea katika sakata zima hili, ndio sababu kaamua kukaa kimya.
Tuendelee kulumbana!
 
Pole sana kwa kazi hii mkuu FMES.
Tuko pamoja kuwakoma hawa mafisadi
Nimekuwa msomaji mzuri sana wa Mwanahalisi, sijasikia Kikwete akikanusha ama kukaripia habari zinazoandikwa Mwanahalisi. Ninachokumbuka ni kwamba, wakati Kubenea alipomwagiwa tindikali, JK alienda hospitali ' in person' kwenda kumjulia hali na kumwambia kwamba asikatishwe tamaa na watu (isomeke M.A.F.I.S.A.D.I) wasiomtakia mema yeye na taifa kwa ujumla.
Kwa sababu hiyo basi naamini kabisa kwamba JK anajua kabisa kinachoendelea katika sakata zima hili, ndio sababu kaamua kukaa kimya.
Tuendelee kulumbana!

Jk kwenda kumuona Kubenea hospitali haina maana kama serikali haikufanya lolote kuwakamata waliofanya tendo hilo.
 
Naona sinema sasa inakaribia kuisha, maana adui amekabwa na kuumizwa vibaya sana muda wowote anaweza kufa na kumpa ushindi starling na picha iishe.

pig up Saed Kubenea, watanzania wanakutegemea na wapo nyuma yako
 
Jk kwenda kumuona Kubenea hospitali haina maana kama serikali haikufanya lolote kuwakamata waliofanya tendo hilo.

Huu ni muono wako wewe mtu mmoja sio lazima uwe standard ya kila mwananchi, na sio alzima wa kwako tu nido uwe sawa! Kwenye siasa kuna mitizamo mingi sana katika kila ishu na it is okay kuwa nayo!

Mkuu IDIMI,

Shukrani kwa maneno yako mazito sana, tunaendelea kupambana na mafisadi mkuu, sasa ni tunajiweka sawa kuweka utetezi kwa Kubenea iwapo hii ishu itaenda kwenye sheria, kazi ni nzito lakini uzuri ni kwamba tupo wananchi wengi sana behind Kubenea, maana yeye anasimamia taifa letu.
 
Naona sinema sasa inakaribia kuisha, maana adui amekabwa na kuumizwa vibaya sana muda wowote anaweza kufa na kumpa ushindi starling na picha iishe.

pig up Saed Kubenea, watanzania wanakutegemea na wapo nyuma yako

Saafi sana, ndio tunachohitaji yaani kumpa Kubenea, kila support maana it comes times mambo ya kuzungukana yanachosha, kila siku wa-Tanzania wanasema sema maneno mengi lakini hakuna anayegusa panapotakiwa, Kubenea went straight to the point, let the chips fall where they may!
 
Huu ni muono wako wewe mtu mmoja sio lazima uwe standard ya kila mwananchi, na sio alzima wa kwako tu nido uwe sawa! Kwenye siasa kuna mitizamo mingi sana katika kila ishu na it is okay kuwa nayo!

Mkuu IDIMI,

Shukrani kwa maneno yako mazito sana, tunaendelea kupambana na mafisadi mkuu, sasa ni tunajiweka sawa kuweka utetezi kwa Kubenea iwapo hii ishu itaenda kwenye sheria, kazi ni nzito lakini uzuri ni kwamba tupo wananchi wengi sana behind Kubenea, maana yeye anasimamia taifa letu.

Agreeing to disagree nafikiri tuko page moja!
 
1.
Hivi huyu mtu anayetiwa Nchimbi ni nani na alianzia wapi na ni kwanini nasikia ana nguvu sana?

Kwa kifupi Nchimbi, ni mtu wa kusini kama Mkapa, alipoamua kuingia kwenye siasa aliwatumia wa kusini wenziwe kuanzia na Kingunge, mpaka akamfikia Mkapa, akiwa rais, akaweza kujijenga kisiasa mpaka kufikia ksuimama mwenyewe kwa kuwa karibu sana na Lowassa, ambaye ndiye siku zote amekua aki-run UV-CCM,

Sasa nguvu yake inawategemea sana Lowassa na Rostam.

2.
Pili hivi huyu Ridhiwan anajua kweli kuwa anatumiwa na mafisadi kumuangusha babaye? analijua kweli hili huyu kijana au anabebwa tuuu?

Naomba dataz mkuu

Kwenye hili anatumiwa bila kujua, lakini baba yake alishahituka siku nyingi sana, kuwa anatumiwa ndio maana akamuondoa.
 
Jk kwenda kumuona Kubenea hospitali haina maana kama serikali haikufanya lolote kuwakamata waliofanya tendo hilo.

Mkuu GM,
Naona hujanilelewa nilichokuwa namaanisha.
Kama ulifuatilia tukio lile, utakumbuka kwamba JK aliahidi kwmba serikali itahakikisha inachukua hatua kali kwa wahusika wote wa tukio lile, na matokeo tumeyaona.
 
Saafi sana, ndio tunachohitaji yaani kumpa Kubenea, kila support maana it comes times mambo ya kuzungukana yanachosha, kila siku wa-Tanzania wanasema sema maneno mengi lakini hakuna anayegusa panapotakiwa, Kubenea went straight to the point, let the chips fall where they may!

Mkuu FM,

Hapa ni kuwa amelitoboa jipu ambalo hata huko ndani wao kwa wao wanaongea ila hakuna mtu wa kuyatoa nje. Kubenea anaonyesha courage aliyonayo ya kusimamia what he believes no matter what the cost!
 
Yes, Mungu ni mwema. Hutoa nafasi hata pale ambapo matumaini hakuna tena. Tungeyajua je haya, kama sio utaifa? tungejuaje bila wanahabari, tungejua je bila vyombo hivi bora vya mawasiliano, tungejua je bila kuwa wana wa nchi wenye kuipenda nchi yao!

Bravo Jamii forums, bravo Kubenea. Vita bado ni nene ila Hakika tutashinda na hatimaye kufaidi matunda ya nchi yetu. Nadhani pia kuna sababu ya kujenga mazingira ya kuwezeshana ili kuweza kupigana vita hii vyema. Tuwekeni taratibu za kufaa katika hili!
 
Mh ninachojua kuwa Ridhiwan na Beno ni marafiki wa siku nyingi sana na hata Muungwana anajua urafiki wao na Beno alikuwa kama mmoja wa familia ya Muungwana na sidhani kama Beno anaweza akawa mpuuzi wa fikra akafikia stage ya kununuliwa na akina Lowassa na RA, na Ridhiwani aendelee kumpigia debe rafiki yake mh sidhani kwa kweli... N'way ngoja tuone labda kuna ukweli

Maneno yako ni kweli na ni mazito, lakini muungwana hakua na sababu ya kumuondoa Ridhiwani, kama anaamini kuwa haya unayoyasema yanaweza kumsaidia kisiasa.
 
Mkuu GM,
Naona hujanilelewa nilichokuwa namaanisha.
Kama ulifuatilia tukio lile, utakumbuka kwamba JK aliahidi kwmba serikali itahakikisha inachukua hatua kali kwa wahusika wote wa tukio lile, na matokeo tumeyaona.

Mkuu FM,

Naona basi tulikuwa hatujaelewana, kwa kukusumbua kidogo, naona kama vile nilipitwa hapo, sikuwa na taarifa serikali ilichukua hatua gani na matokeo yake ni yapi, I feel bad kukurudisha nyuma na kukukwaza ila kuuliza sio ujinga ni kutaka kufahamu tu Mkuu.
 
Naona basi tulikuwa hatujaelewana, kwa kukusumbua kidogo, naona kama vile nilipitwa hapo, sikuwa na taarifa serikali ilichukua hatua gani na matokeo yake ni yapi, I feel bad kukurudisha nyuma na kukukwaza ila kuuliza sio ujinga ni kutaka kufahamu tu Mkuu.

Mkuu niweke sawa hapa ni nini hasa kinachosemwa, maana kama ni ishu ya Kubenea toka amewajibu saa tisa mchana serikali haijajibu bado, nafikiri ni lazima wakam-consult Muungwana kwanza,

Je ndio swali lenyewe au?
 
Yaani huyu Rostam hana aibu kwenda kumuhonga Kubenea?!!!! naombeni ruks nimtukane kidogo....... Msinifungie jamani hasira zimenipanda.

FMES; Kwa nini Saed hakumpeleka kwa Hosea hata kama ni chama moja!!! je, anaushahidi na hili au nimerukia tu kwa kuwa ndo kawaida yake ya kutuona c watanzania ni wadanganyika? mwambie akuja sisi. akae chonjo.

Hizi mtikila mchungaji wa shetani wakati anasema chadema walimuuwa Chacha huu haukuwa uchochezi?

Maskini nyiee....
 
muungwana anewasili hapa mbeya saa 12 jioni, wanachi walikuwa wanamsubiri airport tangu saa tisa, huenda amechelewa akiwa anaandaa majibu ya kubenea, toka airport alikuwa kwenye gari mpyaa kabisa vx 8, alikuwa na tabasamu kama kawaida
 


My Take:

Hapa the sagga inaelekea kuzuri, according to the dataz ni kwamba Ridhiwani amekua akimnadi kwa nguvu sana huko behind the scene, mgombea wa Lowassa na Rostam, anayeitwa Beno hili halijawahi kwua siri na limesemwa sana na magazeti, sasa kama Ridhiwani anamanadi mgombea wa Lowassa si ndio maana yenyewe ya kutumwia nao, au?

According to more dataz ni kwamba Muungwana alishashituka na hili la kutumiwa kwa mtoto wake, kwa hiyo last two weeks amemhamishia huyu mtoto wake kwenye nchi moja huko majuu kwa excuse ya kwenda kusoma ingawa the goal ni kumficha kabsia to the public,a.

Kaka mengine sema lakini hili ni uongo na uzandiki wa hali ya juu. Si kila kinachosemwa kwenye magazeti ni kweli na haswa kinachosemwa na "anayejiita" SAID KUBENEA. Tunathamini mchango wake na ni muhimu kuulinda lakini ukweli wa kazi yake unajulikana.

BENO MALISA sio chaguo la MAFISADI maarufu lakini hilo jungu la kumhusisha nao limepikwa muda mrefu sana. Kama angekuwa mtu wao si angechukua mamilioni waliyotaka kumpa wakati wa uchaguzi wa halmashauri kuu kama walivyofanya wenzake wengi vijana kwa wazee waliokubali kujidhalilisha kupanga foleni kwa yule nyang'au wa LOWASA. Ni Beno ndiye niliyekutana naye katika mabasi akisafiri mikoani kutafuta kura wakati wenziwe walikuwa wakipishana na mashangingi. Hivi sasa inabidi ategemee gari la baba yake kujiandaa na uchaguzi lakini mafisadi wamezusha kuwa wamempa gari ilo kama walivyowapa wengine ambao tunawafahamu.

Kaka semeni mengine lakini hili la uswahiba BENO na ROSTAM LOWASSA and Company si la kweli. Labda nipate habari zingine tofauti na nilizonazo.

Kuhusu RIDHWAN kusafiri ni uzandiki mwengine. Fuatilia ujue kama amefichwa kama usemavyo wewe ama ameenda masomoni. Sasa kaka kama utaona kwenda masomoni ni kumficha mtoto na ndio ushahidi wa kuwa Kikwete ameshtukia mwanaye anatumiwa then hapo kuna tatizo kaka...

Tafuteni mengine lakini sio hili kaka....

Tanzanianjema
 
Kwa nini Saed hakumpeleka kwa Hosea hata kama ni chama moja!!! je, anaushahidi na hili au nimerukia tu kwa kuwa ndo kawaida yake ya kutuona c watanzania ni wadanganyika? mwambie akuja sisi. akae chonjo.

Hivi kweli mkuu unaweza kupeleka kesi ya Rostam kwa Hosea?

Mkuu naomba kusema hivi kinachoendelea sasa hivi ni vita kali sana kati yetu wananchi na mafisadi, sasa huu ni wakati wa wananchi kuwa waangalifu na kuamua ni upande gani wanataka kujiunga nao, lakini sisi wengine tulishaamua siku nyingi sana kuwa tuko upande wa Kubenea, na tuko radhi for anything katika kumlinda na kupambana na mafisadi, kwa sababu taifa ni letu sio lao!

Risk anayoichukua Kubenea sio ndogo wka wale tunaojua vizuri kinachoendelea na tunamuombea kwa Mungu asimame hivyo hivyo mpaka mwisho, ni rahisi sana kukaa nyuma ya PC na ksuema anything lakini usiombe kufanya ya Kubenea kwenye ground zero, inahitaji moyo sana!

Na tuko wengi sana nyuma ya Kubenea.
 
Back
Top Bottom