Mh. Edward N. Lowassa anapata wapi nguvu ya pesa?

Mh. Edward N. Lowassa anapata wapi nguvu ya pesa?

Wana JF, kwa nini watu hawatilii mashaka utajilli wa BAKHRESA, DEWJI, na kila kukicha wanazungumzia wa Lowassa? hao wengine, hata kama waliongeza utajili kwa njia nyingine, basi chanzo chao kinaeleweka. Hivi Baba yake Lowasaa alikuwa mfanya biashara wa nini vile? Naomba mnikumbushe.

Hivi mnakumbuka nani vile aliagiza zile LAND CRUISERS (za mara ya kwanza, (yaliyokuwa yanaitwa mashangingi ya wabunge) kwa wabunge wote)???? Kumbukeni kwamba wakati ule serikali iliknunua magari na kwuakopesha wabunge, kabla ya hapo walikopeshwa LAND ROVER 110.
Ni kiongozi gari alisimamia hili deal? Ile 10% ilikwenda wapi? Imagine 10% of all the Land cruisers???

Wakati ule Lowasa alikuwa ana madaraka gani kule kwenye ofisi waziri Mkuu?

Hiii inaweza kusadia kuelezea, kwa kiasi fulani, utajili wa ajabu kwa mtu ambaye almost maisha yake yote amekuwa mfanyakazi wa serikali.

Mkuu, sisi wa zamani tunaikumbuka hiyo. Hicho ndo kilifanya Mwalimu amkatae EL.
 
Tuzidi kumwomba Mungu amjaalie EL afya njema up to 2015.
 
Pasco,

Nimepita tu ... ninaogopa kuuliza maswali maana huwa unayakwepa.
Keil, umefanya busara kupita tuu bila kuuliza maswali pia ni kweli kuna maswali mengi juu ya Lowassa mimi nayakwepa kwa sababu kwanza mimi sio CCM, pili mimi sio kibaraka wa Lowassa, sio mpambe wake na wala sio msemaji wake, sijatumwa wala silipwi bali nayafanya haya kwa mapenzi mema ya taifa letu!.

Maswali mengine nayakwepa just to save the best for the last maana ngoma ikipigwa sana mwishowe hupasuka!. Hii ngoma ya mkesha, saa hizi ni katikati ya usiku, hivyo sitaki kuipiga sana hii ngoma isije tupasukia kabla hakujechwa!.
 
El akiingia madarakani nchi hii itakua na maendeleo, at the minimum mwelekeo mzuri kama Rwanda ya Kagame ilivyo.
Jamaa siyo muoga, mfuatiliaji na mtekekezaji. Kuna vitu vingine vya kiijinga tu vinafanywa na JK haviingii akilini, Mwakyembe kwa mfano alikua analalamika Bungeni eti Rais alidanganywa na NMB kwamba imechangia hela ya miradi ya maendeleo Kyela na kumkabidhisha Rais hundi FEKI awape wananchi wa Kyela!!!! Huyu ni Rais wa nchi anafanyiwa hivyo na yeye yupo kimya tu.
El hana sifa za kijinga hivyo, alienda Kigoma kwa DC Mongela alikataa kusomewa taarifa ya maendeleo, alikua anataka aone hayo maendeleo, siyo kusomewa taarifa na kuimbiwa kwaya na kuangalia ngoma na kupanda ndege na kurudi zake.
Watu wengi wanaompinga Lowassa wanapenda status quo na wakati huohuo wanalalamika maendeleo hakuna.
Ni taahira peke yake anayefanya kitu hichohicho kila siku na kutegemea matokeo tofauti.
Kwame Nkrumah, asante kwa hili, kama jf ni reflection ya cross section ya jamii yetu Watanzania, basi safari ya ukombozi wa kweli bado ikingali mbali!.

Kusema ukweli sijawahi kuwazia kuingia kwenye siasa, ila issue ya ignorance ya watu wetu inataka kunilazimisha kufika huko, kusema kweli kuna baadhi ya mijitu Mitanzania ni mijinga ajabu mpaka natamani nishike nyundo ni komelee misumari ya sense kwenye mibichwa yao!.
 
aisee, nimekumbuka sredi moja ya MS ulipokiri kuwa weye u-mutu ya bahasha bin mishiko!!! teh teh.................... aisee, kweli hapa mujini, kila mutu itie akili yake kumukichwa!!!!....................... but, jamani, mbona 2015 bado mbali???....................... tutafika kweli???.........................
Akili Kichwani, kama ulidhani mimi ni mtakatifu you must be wrong!, vile vi little brown envelopes vya media nimeshavikunja sana tuu mpaka sasa mimi ndio navigawa!.

Kama unaishi kwa ujanja ujanja kuvitegemea hivyo vibahasha, ili uweze kuvivuta vingi, lazima urefushe muda wa kazi kwa kuanza mapema!, hivyo this is the right time kuanza kuvuta, tena kwa kuzingatia nilianzia kausafiri ka boda boda, sasa niko kwenye bajaj, mpaka kufika 2015, Vogue itakuwa barabarani!.
 
Najiuliza na kukosa majibu Mh.Lowasa si mfanyabiashara,zaidi ya kuwa mbunge,nimejionea siku za hivi karibuni katika vyombo vya habari akichangia mambo mengi hasa katika miradi ya maendeleo  nakatika taasisi binafsi na zamakanisa.Huyu mweshimiwa pesa anazitoa wapi?je alikwisha tangaza mali zake hadharani?na kipato chake kiko vipi?Alipokuwa waziri katika awamu ya tatu kwa nini akufanya hivyo?na alipokuwa waziri mkuu kwa nini alishidwa kufanya hivyo?Na kwa nini safari zake na hotuba zake zinapewa umuhimu mkubwa katika vyombo vyetu vya habari?

Anayejua pesa anatoa wapi ni yeye mwenyewe na mkewe, kuhusu habari zake kupewa kipaumbele na vyombo vya habari labda anafanya mambo yanayoigusa jamii.
 
Kwame Nkrumah, asante kwa hili, kama jf ni reflection ya cross section ya jamii yetu Watanzania, basi safari ya ukombozi wa kweli bado ikingali mbali!.

Kusema ukweli sijawahi kuwazia kuingia kwenye siasa, ila issue ya ignorance ya watu wetu inataka kunilazimisha kufika huko, kusema kweli kuna baadhi ya mijitu Mitanzania ni mijinga ajabu mpaka natamani nishike nyundo ni komelee misumari ya sense kwenye mibichwa yao!.

Ngoja twende nao taratibu wataelewa tu ikifika 2015.
 
Acha tu, kuna watu nimeamini sasa si tu wanaweza kuuza huo utu, wanajiuza miili na akili zao, kwa ajili ya viji pesa.... ni hatari sana kwa watoto waliuo na wazazi wa aina hii.....

Wanaojiuza ni waliongia mikataba ya kinyonyaji ya Bulyanhulu, Kahama, ATC, TRL na mingine mingi. Lowassa aliweza kuvunja mikataba isiyo na ufanisi kama hii. mfano ni CITYWATER na mkataba wa kuuza eneo lote la Mnazi Mmoja. NI nani unamjua amewahi kufanya hivyo kama si Nyerere, Sokoine na Lowassa?
 
Most of the Tanzanians can not wait to see this happen.
By the way, why EL Ikulu? Kwani hakuna watu wengine? kwani asipopata huo urais itakuwaje?
Kama ni mtu safi hakuna haja ya kumsafisha, hana haja ya kutafuta symphy ya makanisa. Akae Kimya then CCM will pick him.
Kama ni mtu safi kama unavyosema, kwa nini hakuwa na guts za kumjibu Nyerere?
Mind you, EL alirudi kwenye cabinet badala ya kumpeka JKM kwenye safari yake ya Mwisho kule Butiama.
Okada, ndani ya CCM hakuna zaidi ya Lowassa!. Dr Salim ni "spent force", Sitta ni too ambicious ana pupa na papara ( "mwenye pupa hadiriki kula tamu"). Magufuli ni dictator tena huyu anaweza kuamuru utekelezaji wa ile adhabu ya kunyongwa itekelezwe instantlyhalafu rufaa ifuatie baadae, tofauti yake Mrema, Magufuli ni genius upstairs!. Dr. Shein is too good kwa uchafu uliopo CCM, who else?. Mwandosya/Mwakiembe ndio hivyo tena (I Wish then get well soon). Nani kwenye CCM ana guts za kulinusuru taifa hili hapa lilipofikia hoi bin taaban!. Kitu kinachaweza kuifanya CCM isimteu Lowassa ni uoga wao maana nakuhakikishia Lowassa akiingia, hadi JK atasimamishwa kizimbani kwa kosa la ....(naomba nisilitaje tusije itwa wachochezi)!.

Kwenye hili la usafi wa Lowassa nimeisha lizungumza sana!. CCM are devils!, but betwen the two devils, choose the lesser!. Kati ya Mashetani CCM, Lowassa ndiye mwenye afadhali!. Anaiba na kuketa maendeleo, hii mijizi mingine mbona nayo inakwiba, inafanya nini?.

Guts za kumjibu Nyerere?!. Hii ndio ameonyesha ukomavu na heshima ya kiafrika kwa wazee wetu!. Ulitaka ajibizane na Mwalimu?. Wewe ukimkosea Baba yako ukigombezwa utajinyamazia au utajibishana nae?. Alichofanya Lowassa was very right, ukikosa unakaa kimya na kama ni kitu cha kutia hasira usithubutu hata kuuleta uso wako mbele zake!.

Hii la heshima na ushujaa, Lowassa ni mpaka amepitiliza!, just imagine zigo la Richmond alilotwisha!. Zigo hili linamwelemea lakini yupo tuu, amejinyamazia!. Niambie nani mwingine ndani ya CCM ana kiwango cha ustahimilivu na uvumilivu hata wa nusu tuu ya Lowassa?. Hakuna!.
 
Kama Lowassa ni msafi

1.Kwa nini alifukuzwa ukurugenzi wa AICC kwa kujilimbikizia mali ?,alifukuzwa na Juliasi Nyerere.

2.Kwa nini alijiuzulu kwa sakata la Richmond ambalo nyie mnadai hakuhusika,na kwa nini ameendelea kuficha ukweli hadi sasa kama ni mtu anayetakia mema taifa hili? mbaya zaidi kwa unafiki wake alidai anajiuzulu kwa sababu watu wanautaka uwaziri mkuu wake.

3.Atakuwaje mkombozi wa pili na wakati amekuwapo kwenye serikali kwa miaka mingi sana na hatujaona "something so special" from him?.Afadhali hata magufuli tunaona impact kila sehemu anayoenda.

4.Ni maamuzi magumu gani ambayo mnasema Lowassa ameyafanya? Usitaje kujiuzulu kwa sababu hayo pia ni maamuzi magumu kama ya jambazi anayeenda kuvunja nyumba ya mtu.Amejiuzulu ili kuendelea kulindana na aidha wezi wenzake au wazembe wenzake

Until unijibu maswali haya kiufasaha,ntahamia rasmi kwenye kambi ya Lowassa.
Gracious, natumaini mengi ya majibu ya maswali yako umeshayapata kupitia michango mbalimbali na sikukujibu wewe specifically ili kuondoa dhana ya tunamsafisha kutafuta uubgwaji mkono na watu!. No, tunamshafisha ili kuwafungua macho Watanzania waone jinsi CCM ilivyo chafu imeoza kwa rushwa na ufisadi toka juu mpaka chini kiasi kwamba huyo Lowassa ambaye wamemtoa kafara kuonyesha CCM ni safi na yeye ndie mchafu, its quite the opposite Lowassa sasa ndiye msafi na ndiye pekee ataweza kuipatia nchi hii ukombozi wa kweli!.
 
Pasco huu uswahiba wa kubebeana zigo lote lile, kweli?
Binafsi kama kweli alimbebea swahiba wake zigo la dhambi basi hatufai...
Ndio maana kuna concept za reward and punisment; huwezi kuwa rewarded kwa kukosea au kuwa punished kwa kufanya kwa usahihi! Ningemuona wa maana kama tu angemwacha anayestahili adha u ajibebee adhabu yake, angekuwa katusaidia saaana watanzania...
Kama upendo wake kwa swahiba wake na nchi yake limekuwa kosa, then tumhukumu kwa hilo!. Ila kwa sisi tulio na imani ya Kikristo, Lowassa ana upendo wa Agape kwa chama chake!. Kwa maana jinsi Mungu alivyoupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanawe mpendwa wake, aje kuukomboa ulimwengu, ambapo alizibeba dhambi zetu na kwa kuteswa kwake, sisi tuliponywa!.

Vivyo hivyo kwa jinsi Lowassa alivyoipenda chama chake cha Mapinduzi, akajitoa nafsi yake, akaubeba msalaba wa Richmond, na kwa kuteswa kwake, CCM ikaponywa!.

Kuna mahali tumeelekezwa tuchukuliane mizigo kwa upendo!. Ule msemo wa kila mtu atauchukua mzigo wake mwenyewe, unaapply kwa ile siku ya mwisho tuu, ile siku ya hukumu!.

Mimi sio mwana CCM na sina chama, hivyo nyinyi wana CCM wenye mapenzi ya dhati kwa chama chenu, just imagine ingekuwaje kama Lowassa asingebeba hilo zigo la Richmond?!. Mngekuwa wageni wa nani saa hizi?. Hao mnaowasifia kwa kuwaimbia nyimbo za shangwe na mapambio si wangeshaozea Keko kitambo!. Badala ya kumshukuru Lowassa kwa kukinusuru chama chenu ndio kwanza mnampigia vuvuzela la kujivua gamba?. CCM isipomsimamisha Lowassa, itapata laana ya ukosefu wa shukrani na itaadhibiwa milele!.
 
bado nawe una mawazo mgando kuwa n2 akishateuliwa kugombea urais kwa tiketi ya ccm bac ataingia ikulu??? watu walikua wanamhofia magufuli tu pale ccm ndo angalau angekua na ubavu wa kucmama na Dr wa ukweli 2015... naye ndo hivyo tena kishaanza kuboronga kwa kauli zake za kupiga mbizi. Endelea kumsafisha Lowasa at the end of the day u'll find that ur efforts=zero
Ndugu yangu Malunkwi, kumbe wewe bado hujajua kuwa CCM ndicho chama chenye hati miliki ya kutawala nchi hii milele?. Amini nakuambia CCM hata ikisimamisha jiwe, linachaguliwa sembuse Mtakatifu Lowassa!.
 
Pasco,

EL ni mwizi wa mali za umma, na hiyo ndo source ya mtaji wa utajiri anaokuza kila siku ya iendayo kwa Mungu. Nina mashaka na ulipaji wake kodi huko TRA, kwani pale kwenye makampuni yake ya hapa Dar wakaguzi wa TRA wanagwaya kuyakagua.

EL hawezi kuonyesha chanzo halali alikopata mtaji wa biashara zake, ila atatumia njia ya ku influence watakao hoji jambo hili kwa kuwahonga kidogo. Ndo maana hata katika ripoti ya Mwakyembe kwenda kwa IGP kuhusu njama za kutaka kuuliwa yeye, Mengi na Dr. Slaa alitajwa mtoto wa Lowasa alivyokuwa anawapelekea nyama na chakula ma hit - men. Mwakyembe na Dr. Slaa wamemlipua mara nyingi EL kwamba ni fisadi, anajua wana evidence ya hili ndo maana anataka waondoke duniani.
Kwa kujua udhaifu wa law enforcers, EL anawa control kwa remote, ile report IGP hakuishughulikia zaidi ya kumshauri EL aachane na mpango anaotaka kufanya.
Narudia tena: neno rahisi la kufafanua utajiri wa EL ni kwamba ni kutokana na wizi wa mali za umma.
Ndugu yangu Wambandwa, Tangu baada ya Baba wa Taifa, waliifuatia wote ndio hivyo tena, mmoja alitoa ruksa za kila kitu hivyo kujenga matabaka ya wenye nacho na wasio kuwa nacho. Aluyefuata alifanya biashara mahala patakatifu, sasa hivi pale ni pango la wahalifu, hivyo kumpitisha Lowassa makes no difference.

Nakubaliana na wewe CCM wote wezi, ila kwenye wezi hawa, kuna wenye afadhali, na Lowassa ndio miongoni mwao!.
 
mkuu huwa nakuheshimu sana lakini linapokuja swala la EL upeo wako huwa unapotea kabisa na kuongea vitu vya ajabu kabisa ambavyo havifanani na ww

Naomba kujua bei yako namimi nizisakae pesa ili unitungie mapambio ya kunisifu na kunipa sifa za kijinga ambazo sistahili.
Knowless, kwanza asante kunigeshimu, heshima ya kweli inajegwa, haiji tuu hivi hivi, sasa kama nilijijengea heshima huko nyuma lakini kwenye issue hii ya Lowassa ninajivunjia heshima yote niliyojijengea!, then nakubali heshima hiyo na ipotee.

Mimi siogopi kugombana na rafiki/ndugu na jamaa zangu katika jambo ambalo tutakuja kupatana!. Kuhusu Lowassa bora tugombane tuu na heshima ishuke, mbele ya safari tutapatana tuu na nitaijenga tena!.

Nikimalizia la bei yangu, amini usiamini mimi sina bei, ni bure kabisa!. Kama una issue yoyote kwa maslahi ya taifa, nitasimama na wewe kama ninavyosimama na El ateuliwe kuwa mgombea wa CCM!.
 
Pasco

Wewe usitudanganya hapa,Kwa namna yoyote ile huwezi kumtenganisha Lowassa na Richmond hasa kwa nafasi aliyokuwa nayo ya mtendaji mkuu wa serikali.Mtapiga tick tack zote lakini ana case ya kujibu katika richmond.Kama halimhusu kwa nini awajibike kwa kitu kisichomhusu,basi kama aliwajibika kwa kisichomhusu hilo nalo ni kosa ambalo linamwondolea credit pia.

Pasco,huwezi kusema ati tujitenge kuongelea Richmond tunapomwongelea Lowasa,Coz Lowassa ni Richmond na Richmond ni Lowassa,we dont care men behind the scenes.
Gracious, hili la kumtenganisha Lowassa na Richmond, tusiandikie mate, wino upo and its only a matter of time!.
 
El akiingia madarakani nchi hii itakua na maendeleo, at the minimum mwelekeo mzuri kama Rwanda ya Kagame ilivyo.
Jamaa siyo muoga, mfuatiliaji na mtekekezaji. Kuna vitu vingine vya kiijinga tu vinafanywa na JK haviingii akilini, Mwakyembe kwa mfano alikua analalamika Bungeni eti Rais alidanganywa na NMB kwamba imechangia hela ya miradi ya maendeleo Kyela na kumkabidhisha Rais hundi FEKI awape wananchi wa Kyela!!!! Huyu ni Rais wa nchi anafanyiwa hivyo na yeye yupo kimya tu.
El hana sifa za kijinga hivyo, alienda Kigoma kwa DC Mongela alikataa kusomewa taarifa ya maendeleo, alikua anataka aone hayo maendeleo, siyo kusomewa taarifa na kuimbiwa kwaya na kuangalia ngoma na kupanda ndege na kurudi zake.
Watu wengi wanaompinga Lowassa wanapenda status quo na wakati huohuo wanalalamika maendeleo hakuna.
Ni taahira peke yake anayefanya kitu hichohicho kila siku na kutegemea matokeo tofauti.

Hebu jikumbushe ubabe wake ulivyogonga mwamba kwa DC wa Shinyanga mjini.
 
Pasco,

Nimepita tu ... ninaogopa kuuliza maswali maana huwa unayakwepa.

Ni kwlei kabisa, kwa maana hadi sasa hakuna aliyweza kujibu utajili wake umetokana na nini. waakti watetezi wake walipigania rekodi yake ya utendaji (ambayo inafutwa kabisa na ufisadi wake), wana JF wanauliza utajili wake umetoka wapi? This is the dilema, ndio maana huu mjadala hauishi
 
Nina maswali matatu tu kwa pro EL;
1. Kwani ndani ya CCM hakuna mtu mwingine zaidi ya EL?
2. Kwa nini EL anautaka SANA urais?
3. Kama anataka kuwasidia wa TZ, hawezi kusaidia kwenye capacity nyingine?

Nitafurahi nikijibiwa ili niweze pima kina cha maji!

Usitegemee majibu ya maana kwa maswali haya. hawa watu wanaroho ngumu kama paka, (kama ya EL) yaani wanang'ang'ania mada ilkiyokufa, haina nguvu za hoja, lakini wapo tu!
 
Back
Top Bottom