Mh. Rais Inawezekana Kabisa Unahujumiwa bila kujijua

Mh. Rais Inawezekana Kabisa Unahujumiwa bila kujijua

Shark

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2010
Posts
29,775
Reaction score
29,746
Habari Mheshimiwa Rais,

Nikiri wazi Mimi sikua mshabiki wako, sababu pia sikua mshabiki wala mfuasi wa Chama ulichopo. Na hata ulipoanza kua Rais sikua na matumaini yoyote kwako, sababu kubwa hasa ni kua wewe ulikuwepo kwenye madaraka enzi zile za jamaa yule. Hivyo nilijua uongozi wako hautokua tofauti na wa bwana yule.

Lakini soon ulipoanza rasmi Urais nilianza kupata imani na wewe. Yapo mengi uliyoyabadilisha ambayo yalianza kuleta matumaini kwetu. Maneno ya "UNAUPIGA MWINGI" yaliibuka kila sehemu, kutokea kwa wafuasi wako mpaka sie tusio wafuasi wako.

Mama yangu Inawezekana kabisa hili la wewe kusifiwa limewatisha hata wafuasi wa Jamaa yule, shujaa wetu. Inawezekana hawafurahii kabisa uyafanyayo na sifa uzipatazo hivyo wanataka wakuharibie.

Mimi nakuomba usiingie kwenye mitego yao. Hii michezo mbona hawakuifanya kipindi hicho? Mbona waziri wako MWIGULU hakutoa wazo la miamala wala kuongeza bei za mafuta enzi za shujaa? Huku ni kukugombanisha na sisi ili tukuchukie na zile sifa za UNAUPIGA MWINGI zifutike, maana zilikua kwa namna moja ama zingine sifa hizi zinamshusha Shujaa.

Pili inaweza kua ni mipango ya 2025 Mama yangu. Watu walijipanga kuingia 2025 baada ya shujaa kumaliza kipindi chake, ila sababu umeingilia kati na kuanza upya hivyo watatakiwa kusubiri mpaka 2030. Sasa ili usifike huko ndio kukuchomokea mambo kama haya. Wanaona 2030 mbali kwao kusubiri.

Nakuomba tena Mama yangu ufikirie tena hivi vimeo unavyochomekewa, na uwe makini navyo. Mafuta ndio "trigger" ya mfumuko wa bei wa bidhaa mbalimbali za muhimu. Na kwenye miamala ya tigopesa/mpesa ndio wengi wa kipato cha kati na chini hufanya miamala yetu, sababu hatuna hela za kuweza kukaa benki.

Yangu ni hayo tu Mama yangu,
 
Yanayofanyika yana baraka zake! Anahujumiwa kivipi! Maamuzi si yanafanyika kwenye baraza huko!.Na yeye ni mtoa maamuzi wa mwisho!.wengine chawa tu!

Msitake kumkwepesha lawama ! Lazima alibebe hili!. Mbona Jpm kutwa kucha mlikua mnaporomosha nyuzi humu?! Tulieni!.
 
Yote yana baraka zake,lao moja japo msingida kaamua kumuhujumu kwa wananchi achukue msingida mbio zake za kuutaka uraisi bado zipo
 
Alitaadharishwa aziondoe zile sumu zote asuke engine upya watamuangusha.Mbona Mkapa alipiga chini wizara nzima akaweka safu yake na yakaenda mambo
 
Mnayahitaji maendeleo makubwa ,je yatoke mbinguni?

Hivi kufunga mikanda ili AJIRA ZIENDELEE KUTENGENEZA ni kosa?

Hivi kufunga mikanda ili kuwalipa posho kabla ya PAYROLL kuingia kwa wale vijana 8000 walioajiriwa TAMISEMI na WIZARA YA AFYA ni kosa?

Hivi kufunga mikanda ili kuimaliza project ya SGR na BWAWA LA MWALIMU NYERERE ni kosa?

Tunahitaji mikanda ifungwe na wazungu na wakenya ili tupige hatua za maendeleo?!!!

#KaziIendelee
#MwiguluYukoSahihi
 
Sijui ni Kwa namna gani serikali itazima taarifa zinazozunguka mitaani kuwa inataka watu warejee kutumia huduma za kibenki Kwa lazima,

Ila habari ndio hiyo.
 
Watanzania tunayataka maendeleo ila hatuhitaji kupita njia ngumu za kuyafikia.

Hayati JPM alitupitisha njia ngumu kuyafikia hayo.

Kodi zilikusanywa kwa NGUVU na wako walioumia....AJIRA ZIKAPUNGUA BAADA YA WAO KUUMIZWA.

Leo ajira zinafufuliwa na tunagawana maumivu ,bado wachache wetu wanaleta "pang'ang'a".

#KaziIendelee
 
Yanayofanyika yana baraka zake! Anahujumiwa kivipi! Maamuzi si yanafanyika kwenye baraza huko!.Na yeye ni mtoa maamuzi wa mwisho!.wengine chawa tu! ..Msitake kumkwepesha lawama ! Lazima alibebe hili!. Mbona Jpm kutwa kucha mlikua mnaporomosha nyuzi humu?! Tulieni!.
Ahaaa kumbe wewe team legacy?
 
Back
Top Bottom