Mh. Rais unahujumiwa na Ummy Mwalimu kupitia TAMISEMI. Sio mtenda haki

Mh. Rais unahujumiwa na Ummy Mwalimu kupitia TAMISEMI. Sio mtenda haki

Afrikasana

JF-Expert Member
Joined
Oct 27, 2021
Posts
320
Reaction score
288
Kupitia ukurasa wa ofisi ya Rais TAMISEMI,imeripotiwa kwamba waziri wa TAMISEMI amatoa maelekezo kwa katibu tawala mkoa wa Tabora kumshusha cheo mwalimu mkuu wa shule ya Makazi iliyopo wilaya ya Uyui mkoani Tabora. Ummy amedai kwamba mwalimu huyo ana hana maadili na sio muadilifu. Ninaviarifu vyombo vinavyotenda haki kwamba Tanga jiji ambapo ni jimboni kwa Ummy pameoza.

Mosi; Yupo mkuu wa shule ambaye alikua anaishi kinyumba na mke wa mwalimu mwenzake. Mkuu huyo wa shule ambaye aliteuliwa na kuwa mkurugenzi alisababisha ndoa ya mwalimu mwenzake kufa. Mwanamke huyo aliyesaliti ndoa yake na mkuu huyo wa shule nae ni mwalimu na alikua akifanya kazi shule moja na mgoni wake.

Suala hilo lilikua wazi hata wanafunzi wanajua maana mkuu huyo wa shule ambaye kwasasa ni mkurugenzi alimhamishia mke wa mtumishi mwenzie shuleni hapo. Jambo hili lipo wazi Afisa Elimu Sekondari analijua, katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC)Tanga analijua,aliyekua mkurugenzi analijua lakini hawakumchukulia hatua kwakua wote ni walewale. Je Ummy hili halijui? Kwanini huyo mtumishi mmetoa mapendekezo akapanda cheo tena bila aibu unashusha watu vyeo wakati kwako kumeoza.

Pili;Yupo Afisa Elimu Taaluma amenyanyaswa na Afisa Elimu sekondari mpaka akaamua mwenyewe kuacha kazi na ameikimbia ofisi. Ummy anajua wazi namna mama wa watu alivyonyanyasika akaikimbia ofisi. Mkurugenzi aliyeondolewa ofisini pamoja na Afisa Elimu Sekondari mbona hujawashuhulikia. Wewe husikii harufu ya ngono na malalamiko kwenye halmashauri ya Tanga?

Hujasikia malalamiko ya rushwa ya ngono? Hujui watu waliopewa nafasi kwasababu zinazoendana na rushwa? Kipi hukielewi wewe Ummy kuhusu dhuluma wanayofanyiwa watumishi jijini Tanga? Kwanini ukapigiie kelele mbali wakati kwako kumeoza pananuka? Ummy kama umemmudu kumdanganya na kumhadaa Mh. Rais sawa ila Mungu yeye yupo na hadhihakiwi. Acha kuumiza watu wanaofanya mambo madogo wakiwa mbali wakati upo ndani mwako na wahalifu unakula na kunywa nao

Tatu; Wapo makatibu wa TSC wa Tanga na Mkinga. TSC makao makuu walituma watu wao kufanya ufuatiliaji wa ubadhirifu walioufanya makatibu hao. Walikua wanasainiana na kula hela za serikali wenyewe wawili bila kushirikisha watumishi wengine kwenye ofisi zao. Hakuna hatua zilizochukuliwa aidha na wewe Ummy au katibu wa TSC Dodoma.

Je, kama hawakutaka kuchukua hatua kwanini waliingiza serikali gharama za kutuma watu kufanya ufuatiliaji? Ummy hili nalo hulijui? Au halipo TAMISEMI? Unapiga sana kelele kwenye halmashauri za wenzako ila wenzako Tanga unawachekea ili uonekane mtu poa usiena tabu. Tenda haki au tulia kama mtangulizi wako kwenye wizara hiyo, acha mbwembwe. Usipochukua hatua juu ya hayo machache huna sifa ya kutembea halmashauri nyingine kusimamisha watumishi kazi na kuwashusha vyeo wengine.

Kwaleo ninamuachia Ummy kazi ya watu wachache, nitampandia tena jukwaani akifanya uonevu.

Mh. Rais tambua kwamba Ummy anafanya maigizo na ukandamizaji hivyo anaonekana kama anakuhujumu wewe pale ambapo hatendi haki tena kwa makusudi
 

🥺 utawasikia wananchi tuwe wazalendo huku wakiongeza tinted katika magari yao na posho kibwena.Hakuna haki duniani isipokuwa akhera
Ummy amezungukwa na wabadhirifu, wasokua na maadili jimboni kwake ndio makada wenzake. Hawezi kutenda haki
 
Ummy amepewa hicho cheo sio kwa weledi bali kwa urafiki hivyo wananchi wanahujumiwa!! Huyu angefaa kama ni lazima kuongoza Wizara ya wanawake ,watoto na wazee; huko angefaa. It is time now Samia reshuffled her cabinet and made these necessary adjustments.
 
Peleka Twitter Kannada tutoke draw mabadiliko yajayo jumuishi ya wizara ya jinsia
 
Ummy amepewa hicho cheo sio kwa weledi bali kwa urafiki hivyo wananchi wanahujumiwa!! Huyu angefaa kama ni lazima kuongoza Wizara ya wanawake ,watoto na wazee; huko angefaa. It is time now Samia reshuffled her cabinet and made these necessary adjustments.
Ummy aliwasimamisha wakurugenzi akina Mwakabibi nk wakati yeye mkurugenzi wake aliyemuweka madarakani amefukuza watumishi kazi na akachukua wake zao kirahisi. Yule bwana ujue akimpenda mke wa mtumishi halafu mwanaume akawa mkali nyumbani ujue huyo atatafutiwatu kosa afukuzwe kazi

Ummy anafanya maigizo lakini watanzania wanamuangaliatu na wanalia na Mungu
 
Too trivial issue to be dealt directly with the minister.

Hebu Wasilisha kero hii kwa RAS
Ofisi ya RAS Tanga wanajua upuuzi unaoendelea lakini wanalindana.

Watumishi ambao wamefanya kazi na mahawara wa aliyekua mkurugenzi wa Tanga jiji waliishi maisha ya tabu sana wengine wamefukuzwa kazi na wengine kuhamishwa vituo vya kazi bila utaratibu ili kufanya mahawara hao waonekane washindi.

Ummy anajua na kesi zipo TAKUKURU hazifanyiwi kazi.

TAKUKURU nao wameoza. Tanga isukwe upya mifumo yake imekufa
 
Ummy aliwasimamisha wakurugenzi akina Mwakabibi nk wakati yeye mkurugenzi wake aliyemuweka madarakani amefukuza watumishi kazi na akachukua wake zao kirahisi. Yule bwana ujue akimpenda mke wa mtumishi halafu mwanaume akawa mkali nyumbani ujue huyo atatafutiwatu kosa afukuzwe kazi
Ummy anafanya maigizo lakini watanzania wanamuangaliatu na wanalia na Mungu
Huyo mkurugenzi hajakutana na watoto wa mjini kama mimi, yaani umchukue mke wangu na bado na ajira yangu ninyang'anywe....jela au kifo ndio itakuwa haki yangu, huyo mkurugenzi uchwara.
 
Tunaomba wahusika wafuatilie jambo hilo pmj na mengine.
Labda iundwe Tume huru. Watu walifukuzwa kazi na mkurugenzi aliyeondoka akishirikiana na maafisa utumishi.
Kesi za kubambikwa zipo tele Tanga na rushwa zinatembezwa waziwazi kwa anayetumwa kuhoji.
Yule mkurugenzi aliyemaliza muda wake nikinara wa rushwa mpaka TAKUKURU aliwanunua na anawapa maelekezo na wanatekeleza
Polisi walinunuliwa hawakua nalakusema
Wakaguzi wa nje wakija walinunuliwa kwa bei ya jumla
Tanga rushwa na ngono maofisini ni fasheni. Halmashauri imeoza. Ummy anaelewa
 
Kabla hqujashushwa cheo ulikuwa kimyaaa hausemi lolote kuhusu hayo maonevu na mauozo ya wenzako.

Sasa umeguswa mfupa, yowe hadi majirani wanakosa usingizi
 
Back
Top Bottom