Mh. Vicky Kamata CV ...[ Mungu tuokoe]

Status
Not open for further replies.
mkuuu kwa hizi fani za kisanii inawezekana tu!
mtu mwenye advanced Dip ya Acc/Finance etc anaweza kufanya master!
mashaka ni hiyo miezi 9 kamili! ikumbukwe kuna vile vijilikizo
ambavyo lazima vifidiwe! labda amefaanya kwenye centre ya mitihani..teeeeeeeeeh!

masters bila 1st degree inawezekanaje???
 
Kwani hiyo Public relation ya ESAMI sio degree??
 
Kuna nini mbona iko poa tuu

Ni kweli, kwa mtazamo na uelewa wako mkuu.
Lakini kwa wanaoelewa MSc. ni nini, haiwezekani ukatoka certificate level hadi MSc. level na kupata cheti chs MSc. kwa mwaka mmoja tu!!! Kwa mfumo uwao wote na pahala popote duniani naamini hakuna kitu kama hicho.
 
CV ya mtu sio issue. Ila anaweza ku-deliver? Kwani Thomas Edison aliyevumbua bulb baada ya kufanya experiment mara elfu kumi( 10,000 x) alikuwa na masters ya nini? Bill Gates ambaye ni owner wa Microsoft(unatumia Windows PC?) ana degree? Tatizo la watu walio wengi Tanzania wanaangalia CV za watu kana kwamba CV ndio zinazoleta maendeleo ya nchi yetu. CV zenye PhD,masters lukuki zimejaa maofisi ya serikali lakini zainabakia kucheza karata tu,ufanisi hamna.

Tukokane na huu upuuzi wa kufikiri kuwa CV za watu ndio kielelezo sahihi cha kumthamini mtu na thamani ya kile ambacho mtu anaweza kufanya. CV ina umuhimu wake lakini muhimu zaidi ni "deliverables"
 
Kazaliwa September 1978 akaanza primary mwaka 1983. Mnaojua mahesabu atakuwa kaanza la kwanza na miaka mingapi? Tena enzi za mwalimu za kushika sikio la kushoto kwa mkono wa kulia kupitia juu ya kichwa?

miaka 5 baba
 


Naona kuna vitu havijakaa sawa. Hizo publications ziko wapi maana online hakuna kitu! Au nivi-home work vya kawaida yeye anaita publication? Pia ukiangalia kwenye elimu mwaka 2005 hakuonekana kama anasoma popote, lakini ukija kwenye publication ametoa case study hii: V. Kamata: The Impact of Microfinance Scheme in Boasting Women Income - A Case Study of Pride Tanzania, SAUT, Mwanza. Au alikuwa anafanya private research?

Pia nilitegema kama amefanya MSc iwe 2008/2009 maana sidhani kama hicho chuo kinaanza January. Ifanct hakuna Southampton solet - kinaitwa Southmpton Solent. Pengine ni typing error ya office ya bunge.
 

Unstoppable, kuna makosa makubwa kwenye hiyo cv kiasi cha kutilia mashaka. UK kuna Southampton Solent University tu, lakini hii cv inaoensha Solet! Hata hivyo kama ni Southampton Solent there is no way under the sun watampokea mtu straight toka certificate ya PR/Customer care aingie kwenye MSc. Hata MA haiwezekani. Na ukisoma vizuri hana working experience ambayo pengine ingeweza kutumika ku-wave baadhi ya masharti ya kujiunga na course. Hapa kuna mashaka. Na ni MSc ya nini?
 
Hata hizo publications ni za kimagumashi,yeye kazi yake ni investigation na impact tu? Kama kafanya hizo publications why she is not technical in her publications? Uroda ndo ulomfikisha pale alipo,utashangaa m2 kama huyu muda si mrefu atakuwa docta.Hii ndo bongo bana.Hata ulaya magumashi tupu,watamkubaliaje m2 mwenye cert kusoma master degre? Halafu ni mwongo kwa umri,itawezekanaje mtoto mwenye umri wa miaka 4 na miezi 3 Aanze kusoma shule ya msingi enzi hzo! Chekechea alisoma lini?
 

I agree. Lakini nafikiri wengi tunacho- question sio hasa level ya elimu; bali ukweli wa kilichoandikwa hapa kwenye CV. It is possible aliyeiandika hiyo CV hakuwa makini na anachokifanya hivyo kusababisha "credibility" ya Vicky kuwa questionable. Kumbuka hata kama unaweza ku-deliver kiasi gani lazima uwe credible ili upate hiyo opportunity ya-kudeliver. Hii sio tuu kwenye siasa bali popote pale kama kweli your serious on what you do.
 
hahhahah tatizo tuliofoji vyeti tuko kibao,mie am sure hapa uk alidanganya ana first degree huwa hawachunguzi sana sema hapo bongo ameshindwa kudanganya public sababu watu wanamjua......
 
Tukokane na huu upuuzi wa kufikiri kuwa CV za watu ndio kielelezo sahihi cha kumthamini mtu na thamani ya kile ambacho mtu anaweza kufanya. CV ina umuhimu wake lakini muhimu zaidi ni "deliverables"
hatujadili CV tunajadili ni jinsi gani watunga sheria wetu wasivyo jiamini na kutojiamini kwao kunapelekea kuwa wadanganyifu na watumwa wa elimu vyeti,wewe unadhani ukiletwa mswaada wa kuwabana wachakachua elimu mtu kama huyo unategemea mchango wake utakuwa nini?...Fikiri,chukua hatua,Watunga sheria wetu wengi ni makarume kenge na hawana msaada katika jamii ya Watanzania.
 
Km CV ndo zingekuwa zinatuletea maendeleo au zinafanya kazi ingekuwa kaz kweli kweli. Kuna watu wana CV nzuri sana tena genuine zisizo na magumashi kama hii, lakini ndo wezi wakubwa, mafisadi na watafuna nchi hii.

Mwacheni ale maisha yake Honorable lol
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…