Mhandisi: Uwanja wa ndege Mwanza umekosewa, vigezo havikuzingatiwa

Mhandisi: Uwanja wa ndege Mwanza umekosewa, vigezo havikuzingatiwa

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869

MHANDISI - UWANJA WA NDEGE MWANZA UMEKOSEWA, VIGEZO HAVIKUZINGATIWA UWE WA KIMATAIFA




Hayo yameelezwa na mhandisi wakati mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. Amos Makala alipofika kuangalia ujenzi unaoendelea.

Mhandisi huyo anafafanua kuwa maelekezo ya mwanzo waliyopewa wakati wa uanzishwaji wa mradi yamebainika kuwa yana mapungufu mengi kimataifa .


Mwanzoni ujenzi ulikuwa wa kuweza kupokea abiria 150 lakini ili uwanja utambulike ni wa kimataifa unatakiwa uwe na vigezo vya kupokea abiria 300 na kuendelea kwa wakati mmoja.
1685884774121.png

Majengo yaliyopo ndege ikishusha abiria wengi wengine watabaki nje wakipigwa na jua au mvua kwa kuwa hakuna nafasi ya kutosha na hilo ni pungufu mojawapo la vigezo uwanja wa kimataifa

Mkuu wa mkoa, CPA Amos Makala ahoji hata kama ilikuwa maelekezo ya wakati huo kwanini utekelezaji wa mradi haukuzingatia vigezo vya kimataifa huku kuna wataalamu pia kwanini mkoa haukushirikisha wadau kama TAA, ICAO, mashirika ya ndege, wahudumu wa abiria n.k

Bilioni 16 za ziada inatakiwa ili kubadilisha mradi jengo la abiria toka bajeti ya awali ya bilioni 13 hivyo jumla kubwa kuwa bilioni 29 kutokana na makosa yaliyofanyika awali.

Mkuu wa mkoa, CPA Amos Makala aagiza sasa mamlaka ya viwanja vya ndege na wadau wengi muhimu kitaifa na kimataifa wahusishwe na kazi hiyo iondolewe toka manispaa Halmashauri ya Ilemela Mwanza ambayo haina ujuzi na kuwa mikononi mwa taasisi na mamlaka zitakazowezesha mradi huo ukamilike kwa viwango vya kimataifa .


HISTORIA TOKA MAKTABA :

20 September 2019


Mradi wa uwanja ulianza 2019
AHADI YA RAIS MAGUFULI UJENZI WA JENGO LA ABIRIA UWANJA WA NDEGE MWANZA SASA RASMI YAANZA KUFANYIWA




Utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyotoa mnamo tarehe 15 ya Mwezi July 2019, kuiagiza Halmashauri ya Jiji la Mwanza kutoa Sh 2.2 bilioni na Manispaa ya Ilemela itoe Sh 1.8 bilioni na kufanya jumla Sh4 bilioni kutoka mapato ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa jengo la abiria katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza.

Hatimaye agizo hilo limeanza kutekelezwa, kwani maandalizi ya awali kuelekea ujenzi wa jengo hilo umeanza mapema hii leo.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella ametembelea eneo lililotengwa kwaajili ya ujenzi wa jengo hilo la abiria kujiridhisha kwamba kazi imeanza au laa.
 
Walipata maelekezo ya wanasiasa 2019, pia tatizo la kutoshirikisha watakaokuwa customers, wadau wataalamu wa mahitaji ya usafiri wa anga na wazoefu katika miradi mikubwa ya kimkakati.
Miradi mingi sana Tanzania haijafuata uhalisia wa maeneo
Mf kuna stendi imejengwa Kijichi watu hawapo na hawaendi kabisa, sasa wanatafuta eneo wajenge tena Mbagala
 
Miradi mingi sana Tanzania haijafuata uhalisia wa maeneo
Mf kuna stendi imejengwa Kijichi watu hawapo na hawaendi kabisa,sasa wanatafuta eneo wajenge tena Mbagara

Ni kweli miradi mikubwa haiangalii mbele wala kuzingatia mambo mengi ya msingi bali miradi inaburuzwa na kuchagizwa na matamko ya viongozi wanasiasa.

Mradi wa SGR Reli mpya unasababisha mafuriko wakati wa mvua sababu ni kuwa kuna masuala ya msingi hayakufuatwa wakati wakijenga tuta kubwa la reli, je reli na treni hii ya umeme wataweka senyenge kilometa zaidi ya 2,000 pande zone jumla kilometa 4,000 katika mtandao mzima wa reli n.k n.k

Maswali ni mengi na inabidi miradi ihakikiwe huku ujenzi ukiendelea ama sivyo nchi itajaa majanga endelevu
 
Ni Uwanja wa Ndege au Jengo la Abiria? Mbona habari na muktadha haviendani?
Ndio kusema kukurupuka au kutojua matumizi sahihi ya lugha,?

TOKA MAKTABA​

Rais Magufuli apeleka bilioni 9 Mwanza​


MONDAY , 30TH OCT , 2017
NA GERALD KITALIMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kuamuagiza Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano profesa Makame Mbarawa kupeleka bilioni 9 Mwanza katika ujenzi wa Uwanja wa ndege.



Magufuli%20na%20pesa%20.jpg

Rais Magufuli ameagiza hilo leo Oktoba 30, 2017 akiwa jijini Mwanza wilayani Ilemela katika uzinduzi wa daraja la waenda kwa miguu la Furahisha ambapo ametaka fedha zaidi ya bilioni 9 zipelekwe Mwanza katika upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza ili uwe uwanja wa kimataifa.

"Nimesikia kuwa mkandarasi anadai zaidi ya bilioni tisa, sasa Waziri naagiza mwambie huyo mkandarasi kuwa wiki hii atapata hizo fedha zote bilioni tisa kwa ajili ya upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza, nataka uwanja huu uwe uwanja wa kimataifa akamilishe uwanja huu kabla sijamaliza muda wangu, kwani asipokamilisha ndani ya muda huo hapo atalala lele, nataka wafanyabishara wa samaki wasiende nchi zingine kwa ajili ya kusafarisha samaki zao' alisisitiza Rais Magufuli.

Mbali na hilo Rais Magufuli amesema serikali yake imekusudia kujenga meli kubwa itakayobeba watu 1200, na tani za kutosha na magari katika ziwa Victoria.
Rais Magufuli yupo jijini Mwanza katika ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo ziara hiyo imelenga kuzindua daraja la Furahisha ambalo tayari limeshazinduliwa na baadaye atazindua kiwanda
 
AMOS MAKALA - NIMEKUWA MKUU WA MKOA DAR ES SALAAM NA MKOA WA MBEYA HAKUNA HALMASHAURI INASIMAMIA VIWANJA VYA NDEGE



UJENZI WA JENGO JIPYA UWANJA WA NDEGE MWANZA WAKWAMA, MAKALA ATOA MAELEKEZO


30 May 2023
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Amos Makalla ameagiza mchakato wa makabidhiano ya Jengo jipya la Abiria la Uwanja wa Ndege kutoka kwa Mkuu wa Mkoa kwenda kwa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) ufanyike kwa haraka ili ujenzi uendelee baada ya kusimama kwa muda mrefu.

Akizungumza baada ya kufanya ukaguzi katika jengo jipya la abiria linalojengwa kwa Fedha kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza na Ilemela pamoja na Serikali kuu CPA.Amos Makalla amesema kuwa hakuna sababu yoyote ya Mradi huo kuendelea kusimama licha ya kosoro zilizopo za kiufundi.

Ujenzi wa Jengo jipya la Abiria katika Uwanja wa Ndege Mkoa wa Mwanza ulianza tangu Mwaka 2019 kwa maagizo ya Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa awamu ya Tano kwa gharama ya zaidi ya Shilingi Bilioni 13 lakini hadi sasa zimetumika zaidi ya Shilingi Bilioni 9 huku Halmashauri ya jiji la Mwanza wakichangia zaidi ya Shilingi Bilioni 1.45 ,Ilemela zaidi ya Shilingi Bilioni 1.42 huku Serikali kuu ikiwa imechangia zaidi ya Shilingi Bilioni 9.

Source : Gazeti la DAILY NEWS
 

MHANDISI - UWANJA WA NDEGE MWANZA UMEKOSEWA, VIGEZO HAVIKUZINGATIWA UWE WA KIMATAIFA




Hayo yameelezwa na mhandisi wakati mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. Amos Makala alipofika kuangalia ujenzi unaoendelea.

Mhandisi huyo anafafanua kuwa maelekezo ya mwanzo waliyopewa wakati wa uanzishwaji wa mradi yamebainika kuwa yana mapungufu mengi kimataifa .


Mwanzoni ujenzi ulikuwa wa kuweza kupokea abiria 150 lakini ili uwanja utambulike ni wa kimataifa unatakiwa uwe na vigezo vya kupokea abiria 300 na kuendelea kwa wakati mmoja.
View attachment 2646002
Majengo yaliyopo ndege ikishusha abiria wengi wengine watabaki nje wakipigwa na jua au mvua kwa kuwa hakuna nafasi ya kutosha na hilo ni pungufu mojawapo la vigezo uwanja wa kimataifa

Mkuu wa mkoa, CPA Amos Makala ahoji hata kama ilikuwa maelekezo ya wakati huo kwanini utekelezaji wa mradi haukuzingatia vigezo vya kimataifa huku kuna wataalamu pia kwanini mkoa haukushirikisha wadau kama TAA, ICAO, mashirika ya ndege, wahudumu wa abiria n.k

Bilioni 16 za ziada inatakiwa ili kubadilisha mradi jengo la abiria toka bajeti ya awali ya bilioni 13 hivyo jumla kubwa kuwa bilioni 29 kutokana na makosa yaliyofanyika awali.

Mkuu wa mkoa, CPA Amos Makala aagiza sasa mamlaka ya viwanja vya ndege na wadau wengi muhimu kitaifa na kimataifa wahusishwe na kazi hiyo iondolewe toka manispaa Halmashauri ya Ilemela Mwanza ambayo haina ujuzi na kuwa mikononi mwa taasisi na mamlaka zitakazowezesha mradi huo ukamilike kwa viwango vya kimataifa .


HISTORIA TOKA MAKTABA :

20 September 2019


Mradi wa uwanja ulianza 2019
AHADI YA RAIS MAGUFULI UJENZI WA JENGO LA ABIRIA UWANJA WA NDEGE MWANZA SASA RASMI YAANZA KUFANYIWA




Utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyotoa mnamo tarehe 15 ya Mwezi July 2019, kuiagiza Halmashauri ya Jiji la Mwanza kutoa Sh 2.2 bilioni na Manispaa ya Ilemela itoe Sh 1.8 bilioni na kufanya jumla Sh4 bilioni kutoka mapato ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa jengo la abiria katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza.

Hatimaye agizo hilo limeanza kutekelezwa, kwani maandalizi ya awali kuelekea ujenzi wa jengo hilo umeanza mapema hii leo.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella ametembelea eneo lililotengwa kwaajili ya ujenzi wa jengo hilo la abiria kujiridhisha kwamba kazi imeanza au laa.

Mtanikumbuka
 

TOKA MAKTABA​

Rais Magufuli apeleka bilioni 9 Mwanza​


MONDAY , 30TH OCT , 2017
NA GERALD KITALIMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kuamuagiza Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano profesa Makame Mbarawa kupeleka bilioni 9 Mwanza katika ujenzi wa Uwanja wa ndege.



Magufuli%20na%20pesa%20.jpg

Rais Magufuli ameagiza hilo leo Oktoba 30, 2017 akiwa jijini Mwanza wilayani Ilemela katika uzinduzi wa daraja la waenda kwa miguu la Furahisha ambapo ametaka fedha zaidi ya bilioni 9 zipelekwe Mwanza katika upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza ili uwe uwanja wa kimataifa.

"Nimesikia kuwa mkandarasi anadai zaidi ya bilioni tisa, sasa Waziri naagiza mwambie huyo mkandarasi kuwa wiki hii atapata hizo fedha zote bilioni tisa kwa ajili ya upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza, nataka uwanja huu uwe uwanja wa kimataifa akamilishe uwanja huu kabla sijamaliza muda wangu, kwani asipokamilisha ndani ya muda huo hapo atalala lele, nataka wafanyabishara wa samaki wasiende nchi zingine kwa ajili ya kusafarisha samaki zao' alisisitiza Rais Magufuli.

Mbali na hilo Rais Magufuli amesema serikali yake imekusudia kujenga meli kubwa itakayobeba watu 1200, na tani za kutosha na magari katika ziwa Victoria.
Rais Magufuli yupo jijini Mwanza katika ziara ya kikazi ya siku mbili ambapo ziara hiyo imelenga kuzindua daraja la Furahisha ambalo tayari limeshazinduliwa na baadaye atazindua kiwanda
 

Attachments

  • 97454149-7AA9-40B3-8D7E-2212450B5192.jpeg
    97454149-7AA9-40B3-8D7E-2212450B5192.jpeg
    23 KB · Views: 10
11 Feb2023
Mwanza, Tanzania

🔴NEWS: UFAFANUZI UJENZI JENGO LA ABIRIA UWANJA WA NDEGE MWANZA ULIPOFIKIA



Adam Malima afafanua changamoto za mchoro mradi wa uendelezaji wa uwanja wa ndege wa kimataifa Mwanza.

Adam Malima tunataka kushindana na Entebbe na ukanda huu mzima wa maziwa makuu wa Afrika ya Mashariki na Kati

Watalii toka Ulaya, China, Marekani n.k kwenda Serengeti, Burugi-Chato, Masai-Mara Kenya n.k watatumia uwanja wa Mwanza pale utapokamilika na kuingiza mapato kwa Halmashauri za Ilemela na Nyamagana za jiji la Mwanza kutokana na uwekezaji walioweka halmashauri hizo.

Jiji la Mwanza hata hivyo halina hoteli za hadhi ya kutosha dege la abiria 200 likishuka na abiria kutoka Ulaya na China hivyo mkuu wa mkoa Adam Malima asema wadau wa mahoteli nao wajipange kwenda na fursa hiyo ili mradi wa uendelezaji wa airport utapoisha kuwe na vitanda ktk hoteli za hadhi na restaurant kuwapatia huduma wageni .

Maono ya Adam Malima airport ya kimataifa ya Mwanza na maeneo yanayokabiliana na uwanja huo waMwanza :

 
Yawezekana bajeri ilitosha kipindi cha Magu lakini kwa kubana myanya ya upigaji. Sasa tufikirie pia uwezekano wa kuongeza sifuri kama ilivyofanyika kwenye manunuzi ya ndege.
 
Back
Top Bottom