Mhe. Rais usikubali eneo la Jangwani kutumika kama uchochoro wa kula pesa, limegeuka mradi wa kifisadi

Mhe. Rais usikubali eneo la Jangwani kutumika kama uchochoro wa kula pesa, limegeuka mradi wa kifisadi

Leak

JF-Expert Member
Joined
Feb 22, 2012
Posts
52,916
Reaction score
43,505
Wasalaam wana jamvi.

Bila shaka kila Mtanzania aliyepata wasaha wa kupita jangwani atakubaliana nami na Watanzania wengine kuwa Jangwani kunahitaji suluhu nyingine na si kila leo kutoa mchanga na kuchimba mitaro kwa sababu hivyo vyote havijawahi kuwa suluhu kabisa pale Jangwani kwani kila leo kero la eneo lile imekuwa ikiongezeka na kila mvua inaponyesha na ni sehemu ambayo imekuwa ikizua maswali mengi kuhusu weledi wa watendaji wa serikali na mamlaka husika hasa TANROADS, NEMC NA JIJI LA DAR-SALAAM.

Mhe. Rais, Unajua fika kabisa eneo hilo linahitaji suluhu kubwa tena ile ambayo imekuwa ikisemwa kila leo na kila kiongozi wa serikali na wa jiji la Dare-salaam kuhusu kujengwa barabara ya juu au daraja ili kuondoa kero ya kila leo mvua zinapoanza.

Mhe. Rais, Eneo la Jangwani sasa limegeuka mradi wa watu kujipatia pesa ndio maana kila leo watendaji na mamlaka zinafanya yale yale kila leo na kupeleka fedha pale kila leo kufanya yale yale ambayo yamekuwa hayaleti suluhusho miaka yote.

Mhe. Rais, Jangwani ni aibu tena sana kama utaruhusu tena Serikali iendelee kupeleka pesa pale eneo la Jangwani tena mabilioni kila mwaka kwa kisingizio cha kutengeneza mitaro na kutoa michango halafu na bado mvua zikinyesha hakuna ambalo linakuwa limefanyika ni kama hela inatupwa pale na kuliwa.

Mhe. Rais, TANROADS na wenzao wanakwenda kutupa pale tena bilioni 4 kwaajili ya kutoa mchanga na kuchimba mitaro jambo ambalo wamekuwa wakilifanya ni miaka kumi sasa na wamekuwa wakipeleka hela zaidi ya hizo pale pale.

Mhe. Rais tunaomba usikubali tena matumizi mabaya ya hela pale ....pamegeuzwa chanzo cha pesa wakati yanayofanyika hayatatui kero lengwa.......eneo lile limegeuzwa uchochoro wa kula hela.

Mhe. Rais usikubali pesa kuendelea kuliwa pale jangwani.
 
Una mshauri aliesababisha tatizo(cause)? ,Hayo wayafanyayo wengine ni effects tu (causality principle)
 
Lijengwe daraja usawa wa kuanzia pale taa za bondeni hotel hadi usalama
 
Nilitegemea umuulize kwanini akiwa waziri alizamisha Hela yetu kwa kujenga Kituo cha mwendokasi badala ya unalalamikia matokeo.
 
Una mshauri kwa kuwa wewe unapajua Jangwani kuliko yeye? Wewe una taarifa za pale kuliko analizonazo?
 
Hivi nchi yetu imelogwa na nani?yaani huyu mtoa hoja bila shaka ni middle class citizen ambaye ana elimu above O Level na ufikiri wake ndio kama huu,je sisi tulioko huku Lingusenguse ambao toka uhuru hakuna jipya ufikiri wetu utakuaje?kabla ya kupigania nchi iwe na taasisi imara na zenye kujitegemea mtoa hoja anakimbilia kwa mpangaji mkuu wa pale Magogoni!na kwa taarifa yako tungekuwa tunajielewa mtoa hoja ungeweza kufungua mashitaka mahakamani dhidi ya idara zinazohusika na barabara ile na sio kumpigia magoti no 1.amka mkuu
 
Back
Top Bottom