Mtoto,
Pengine mimi ndio sikuelewa kifungu cha sheria ulichoweka lakini inaposema hivi:- Rais hatakuwa na uwezo wa kulivunja Bunge wakati wowote, isipokuwa tu- blaaa blaa blaaa!
Nimeelewa kwamba kama moja ya kifungu hicho ipo basi rais anaweza fanya hivyo WAKATI WOWOTE. Hili neno wakati wowote linabeba uzito mkubwa zaidi kuonyesha kwamba hakuna sababu wala kusubiri maamuzi ya mahakama. Sijaona kifungu kinachomtaka raios apeleke mashtaka au malalamiko yake kwanza mahakamani inapotokea au anapoona ulazima wa kuvunja bunge kutokana na vifungu hivyo.
Ndivyo nilivyoelewa mimi, na pengine ndivyo marais wengi huvunja bunge pasipo kusubiri mahakama..Ikiwa nimeelewa vibaya naomba somo mkuu wangu.