Mheshimiwa Rais sidhani kama kupenda Kwako kila mara ' Kumtajataja ' hadharani TISS DG Dkt. Kipilimba ni sawa Kiuweledi

Mheshimiwa Rais sidhani kama kupenda Kwako kila mara ' Kumtajataja ' hadharani TISS DG Dkt. Kipilimba ni sawa Kiuweledi

Noted na Wewe siyo wa Kwanza Kunikongole / Kunisifia hivi kwa uwezo wangu ( hapa Jamvini na hata katika Jamii niliyopo ) ila labda nikuambie tu kuwa hata Mimi napenda na nahitaji sana niwe ambavyo Wewe na wengineo humu / hapa Jamvini mnataka niwe ila kumbukeni tu ya kwamba hata katika ' Saikolojia ' imethibitika kuwa Watu wenye ' Uwerevu / Ujiniazi ' huwa pia wana ' Kasoro ' fulani ambazo hata ufanyeje haziwezi Kurekebishika labda mpaka dunia ikigeuka.

Ninachokuomba tu Mkuu Wewe chukua tu yale mema yangu hapa ila yale yangu ya ' Kipopoma ' nakuomba nianchie mwenyewe kwani sidhani kama nitakuja kubadilika. Wapitie Watu wengine ambao unawajua wako vizuri Kichwani / Kiakili / Kifikra kisha utagundua ya kwamba pamoja na kupewa ' Zawadi ' hiyo na Maulana / Mola ila wana ' Mapungufu ' fulani fulani pia ya hapa na pale.

Kikubwa tuvumiliane tu Mkuu au vipi?
Umenena vyema mkuu.
 
hata mimi sijawahi kuona hata kufika kwenye ufunguzi ikiwa kuna mwakilishi sehemu husika
labda ndio utaratibu mpya
 
Kwani nimetaka ' ufafanuzi ' wa Kimantiki au ' mabishano ' nawe? Hopeless!
Wewe ndio hopeless...unataka watu wakujibu kupinganq na unavyowaza wewe!!

Unataka watu wakuunge mkono tu wakati umetaka watu waje wajadili, sasa unamwonaje mwenzio hopeless.

Shida sana aisee!!!!
 
GENTAMYCINE ni popoma tu unajidai mjuaji kila kitu. Mbona kila Mara tumesikia na kuona madirector was usalama Marekani na kwingineko wakitajwa?
 
Mwacheni Magufuli afanye kazi, kila siku yeye tu.
Hivi huwa hamna kazi ninyi, ndiyo maana tumechelewa kimaendeleo kama taifa.
Na wewe mwenye kazi unatafuta nini huku? Au na wewe huna kazi? au kazi yako ni kukusanya habari za mitandaoni?😀😀
 
Sasa mbona kipindi anateuliwa kuwa DG media zote za ndani na nje zilichapisha habari na kubandika picha zake sasa hao maadui unaowasema wanashindwa kwenda google na kupata picha ya huyo Kipilimba na pia siku anaapishwa tukio si ilichukukuwa live na video zipo youtube.

Kiongozi mkuu wa idara nyeti asiweze kujulikana hio kitu hakipo popote pale duniani.Mkuu wa intelijensia wa Rwanda bwana Emmanuel Karenza ,chief wa kenya bwana kameru ukitaka picha zao ,information google utazikuta kibao.

Binafsi sijaona mantiki ya hoja hii.
Bila shaka ni hoja ya kipopoma,you're right.
 
Anateuliwa na kutangazwa hadharani, anaapishwa kweupe ikulu mbele ya paparazi, kafanyakazi sehemu mbalimbali n.k. huko kote ni kutajwatajwa hadharani.

Wewe hapa tayari umetaja kuwa mko wengi humujF. Kjazuia maamuma wa mambo ya intelegensia wasichangie. Wakati mambo kwa maana ya kuyafamu ya itelegensia yako kibao mitandaoni na shule yake iko ukitaka ni kuita na kuisoma. Kisicho fahamika ni opetesheniz zao wanazofanya maana ni siri kama hazijavuja/ kuvuishwa. Watu wa Tiss mliomo humu jf endeleeni kuchangia kama mwenzenu alivyo waomba. Hii haina tofauti na ile unajua mimi nani!!! Kumbe ndio hulka imeshaota mizizi hivi.?

Labda tiss ianzishe utaratibu wa black DG ambaye ndiye atakaye kuwa akimtuma huyu hadharani DG.
 
Huwa napenda na nafurahi sana kukutana na ' Majiniazi ' wachache wa mfano wako hapa Jamvini JamiiForums. Nimekukubali mno.
Ndiyo maana uteuzi wa CDF Ulileta kwaro kwa cheo chake hakutakiwa kuwa CDF wakati mbele yake kulikuwa na Ma Lieutenant General zilikiukwa taratibu.
 
Sidhani anamaanisha hivyo mbona wengine anatambua uwepo wao. Je ingeeleweka vipi anamtambua uwepo mkuu wa polisi asitambue uwepo wake? Hiyo ni itifaki tu
Kwa nini kila kwenye mikutano yake awatambue uwepo wake, kwani hizo hafla zinakuwa zinahusu mambo ya ulinzi?
 
Sasa mbona kipindi anateuliwa kuwa DG media zote za ndani na nje zilichapisha habari na kubandika picha zake sasa hao maadui unaowasema wanashindwa kwenda google na kupata picha ya huyo Kipilimba na pia siku anaapishwa tukio si ilichukukuwa live na video zipo youtube.

Kiongozi mkuu wa idara nyeti asiweze kujulikana hio kitu hakipo popote pale duniani.Mkuu wa intelijensia wa Rwanda bwana Emmanuel Karenza ,chief wa kenya bwana kameru ukitaka picha zao ,information google utazikuta kibao.

Binafsi sijaona mantiki ya hoja hii.
Embu tuwekee picha yake maana hatumjui sie wengine
 
Ndiyo maana uteuzi wa CDF Ulileta kwaro kwa cheo chake hakutakiwa kuwa CDF wakati mbele yake kulikuwa na Ma Lieutenant General zilikiukwa taratibu.

Tunamzungumzia Rais Dkt. Magufuli na Mkurugenzi wa Idara / Taasisi ya Usalama wa Taifa na sijui hilo la Mkuu wa Majeshi Tanzania ( CDF ) hapa limekuwa ' logically connected ' vipi Mkuu.
 
Na kweli wewe popoma, kama Rais mwenyewe anajulikana, sembuse dg tiss?! Nadhani ukikua utaelewa mambo ya aina hii, ma-dg wote wa tiss tangu enzi za mwalimu watu wanawajua mpaka wanakolala!! hebu kula erythromycine kidogo utulize kipindupindu.
 
Ni punguani tu anaweza tetea mambo ya siri siri, dunia ya leo kuna siri??? kwanza hii kasumba ya TISS kuoperate kisi siri wakati wanatumia pesa za walipa kodi ilipaswa ibadilishwe, bajeti yao ni siri, kazi zao ni siri, taratibu za uajiri ni siri..ndio maana mambo mengi sana nchi imefeli..leo tuna mgogoro na ACACIA wakati mambo hayo ya mchanga kusafirishwa na wao walikuwepo, kwa sababu ya usiri siri huo wengi wa wanaoajiriwa ni aidha ndugu wa waliomo TISS au wanafahamiana vyovyote vile..sasa na huyu analeta kukosoa mtu kutambulishwa tu..sasa km yeye hapendi kutambulishwa nini kinamfanya akae high table????
 
FB_IMG_1543424176142.jpg
 
ANGALIZO

Naomba kama unajijua kabisa kuwa uwezo wako wa kuona vitu vya umbali / unyeti / umuhimu wake basi katika huu ' Uzi ' kaa nao mbali kabisa na waachie wenye ' akili ' zao na ' Wachambuzi ' wa masuala haya ya Kijasusi ambao wapo ( tunao ) wengi humu na Sisi Mangumbaru na Mapopoma wengine tuwe watazamaji tu kuliko Kuchangia halafu ukajikuta umevapa / umekosea.

HOJA KUU

Nashukuru sana Mwenyezi Mungu kwamba karibia awamu zote za nchi hii nilikuwepo japo ya Hayati Baba wa Taifa ilinikutia nikiwa bado katika Ndoo ya Kuogea na nalilia Uji wa Buruga ( namaanisha nikiwa bado Kichanga kabisa ) ila kwa awamu ya Mzee Mwinyi niliishuhudia bila kusahau ya Mzee Mkapa na ya Mzee Kikwete na sasa nipo hii ya Mheshimiwa Dkt. Magufuli natiririka na naserereka nayo.

Katika Awamu zote hizo sikuwahi hata Siku moja kuwasikia hao Watangulizi wake Rais Dkt. Magufuli wakiwa na tabia ya kupenda ' Kumtajataja ' au hata kupenda kuonyesha kwamba Mkurugenzi Mkuu wa Idara Nyeti nchini ya Usalama wa Taifa ( TISS ) yupo eneo ambalo Wao wapo ila ilikuwa ni mpaka tu labda Mtu akutonye / akuambie.

Nimejuiuliza maswali mengi sana kwani Marais wote Wastaafu walikuwa hawapendi kuwatajataja Wakuregenzi wao Usalama wa Taifa ( TISS DG ) lakini kwa Awamu hii ya Gwala / Tano Rais Dkt. Magufuli anapenda mno ' Kumtaja ' na hata kupenda ' Kumuinua ' Kitini Mkurugenzi wa sasa Dkt. Modestus Kipilimba na bado sijapata jawabu / jibu ila najua kupitia ' Majiniasi ' waliotukuka wa Jamvi hili la JamiiForums leo nitayapata.

Sikuishia tu hapo kama kawaida yangu huwa napenda kwenda ' deep ' zaidi kufanya ' references ' na Mataifa mengine mbalimbali kuanzia na haya Jirani ( tunaofanana kwa Vingi ) kisha hupenda pia kuangalia na yale Mataifa makubwa ambayo yana uwezo mkubwa wa Kuanzia Uchumi, Kijeshi na Kiusalama kuliko Tanzania yetu hii na sijaona mahala ambapo Marais wao huwa wanawataja hovyo tena hadharani Wakurugenzi Wakuu wa Idara zao ' Nyeti ' za Usalama wa Taifa ila kwa Tanzania naona hii tabia inaanza Kuzoeleka.

Kwa maoni au mtazamo wangu mdogo tu ( mnaojua zaidi mtanisaidia ) kwa asili ya hizi nchi zetu tena ambazo zina ' Majaribu ' na ' Matatizo ' mengi ya Kimsingi huku kukiwa na ' Maadui ' wengi wa ndani na nje sidhani na siafiki kabisa tena kwa 100% kwa Wakurugenzi wetu hawa wa hii Idara / Taasisi muhimu kama si nyeti ya Usalama wa Taifa ( TISS ) kutajwatajwa hovyo kwa Watu na hata kujulikana kwakuwa Tanzania ya sasa imejaa Watu wa ajabu ajabu wenye ' maslahi ' yao ' hasi ' na nchi hii hivyo kuna uwezekano na Wao wakaanza Kumjua na Kumzoea kisha hali ikaja kuwa mbaya zaidi huko mbeleni.

Na sidhani pia kama hata ' Kiuweledi ' hivi anavyofanya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano Dkt. Magufuli la kupenda ' Kumtajataja ' Mkurugenzi Mkuu wa Idara / Taasisi ya Usalama wa Taifa ( TISS DG ) Dkt. Kipilimba ni sahihi na kama itapendeza nadhani Watu wa ' Itifaki ' ambao nina uhakika kuwa wengi wenu tunatiririka na kuserereka pamoja 24/7 hapa JamiiForums hili mtaliangalia kwa hayo mapana yake ili utaratibu ule ule uliozoeleka wa zamani wa hawa Wakurugenzi kutojulikana sana au kutajwatajwa hovyo uendelee kwani Kwangu Mimi kwa ' Mazingira ' ya nchi yetu ulikuwa ni utaratibu murua / mujarab / sahihi kabisa kuliko huu wa sasa aliouanzisha Amiri Jeshi Mkuu na Rais Dkt. Magufuli.

Huu ulikuwa ni mtizamo wangu Mimi kama GENTAMYCINE ila nitashukuru na Watu wengine nao wakija hapa wakichangia huku wale ambao ' watanikosoa ' basi wanikosoe ha ' Hoja ' nzito nzito kwani hata Mimi nataka Kujifunza jambo hapa kutokana na kwamba yawezekana huu utaratibu wa sasa ukawa ndiyo sahihi kuliko ule ambalo nimeukariri / nimeuzoea. Nia na madhamuni tupate afya ya Kimjadala na ya Kimantiki juu ya hili ' Suala ' kusudi mwisho wa Siku wote tupate ' maarifa ' na ' ufahamu ' zaidi.

Karibuni!

Nawasilisha.
Binafsi sioni shida wala kosa, kosa liko kuwataja maafisa [Watumishi] waliochini ambao ndio wahusika wa majukumu ya kazi. Tena tulipofika tumechelewa sana huyu DG wao, manake inapaswa kuwa Taasisi na si Idara. Ili awe na maamuzi rasmi akilipoti kwa Rais na kuwa na wajibu wa kisheria kutenda mamboi kwa maslahi ya Taifa. Mataifa makubwa Mabosi wa Taasisi hizo ufahamika na wala haina shida. Tatizo ni pale mtu atakapotaja watendaji wa chini ambao ndio engine ya taasisi husika hapo kutakuwa na kosa la kiweledi
 
Back
Top Bottom