Mheshimiwa Rais sidhani kama kupenda Kwako kila mara ' Kumtajataja ' hadharani TISS DG Dkt. Kipilimba ni sawa Kiuweledi

Mheshimiwa Rais sidhani kama kupenda Kwako kila mara ' Kumtajataja ' hadharani TISS DG Dkt. Kipilimba ni sawa Kiuweledi

Kuna watu wa ajabu sana humu bora wewe umetishwa hadharani mtu ka inbox kabisa na vitisho uchwara.

Wamesahau kwamba wengine ' Makabila ' yetu tu ni ya ' Kikatili ' na ya ' Kiuwaji ' vile vile halafu ' Umafia ' ndiyo asili yetu tukuka.
 
ANGALIZO

Naomba kama unajijua kabisa kuwa uwezo wako wa kuona vitu vya umbali / unyeti / umuhimu wake basi katika huu ' Uzi ' kaa nao mbali kabisa na waachie wenye ' akili ' zao na ' Wachambuzi ' wa masuala haya ya Kijasusi ambao wapo ( tunao ) wengi humu na Sisi Mangumbaru na Mapopoma wengine tuwe watazamaji tu kuliko Kuchangia halafu ukajikuta umevapa / umekosea.

HOJA KUU

Nashukuru sana Mwenyezi Mungu kwamba karibia awamu zote za nchi hii nilikuwepo japo ya Hayati Baba wa Taifa ilinikutia nikiwa bado katika Ndoo ya Kuogea na nalilia Uji wa Buruga ( namaanisha nikiwa bado Kichanga kabisa ) ila kwa awamu ya Mzee Mwinyi niliishuhudia bila kusahau ya Mzee Mkapa na ya Mzee Kikwete na sasa nipo hii ya Mheshimiwa Dkt. Magufuli natiririka na naserereka nayo.

Katika Awamu zote hizo sikuwahi hata Siku moja kuwasikia hao Watangulizi wake Rais Dkt. Magufuli wakiwa na tabia ya kupenda ' Kumtajataja ' au hata kupenda kuonyesha kwamba Mkurugenzi Mkuu wa Idara Nyeti nchini ya Usalama wa Taifa ( TISS ) yupo eneo ambalo Wao wapo ila ilikuwa ni mpaka tu labda Mtu akutonye / akuambie.

Nimejuiuliza maswali mengi sana kwani Marais wote Wastaafu walikuwa hawapendi kuwatajataja Wakuregenzi wao Usalama wa Taifa ( TISS DG ) lakini kwa Awamu hii ya Gwala / Tano Rais Dkt. Magufuli anapenda mno ' Kumtaja ' na hata kupenda ' Kumuinua ' Kitini Mkurugenzi wa sasa Dkt. Modestus Kipilimba na bado sijapata jawabu / jibu ila najua kupitia ' Majiniasi ' waliotukuka wa Jamvi hili la JamiiForums leo nitayapata.

Sikuishia tu hapo kama kawaida yangu huwa napenda kwenda ' deep ' zaidi kufanya ' references ' na Mataifa mengine mbalimbali kuanzia na haya Jirani ( tunaofanana kwa Vingi ) kisha hupenda pia kuangalia na yale Mataifa makubwa ambayo yana uwezo mkubwa wa Kuanzia Uchumi, Kijeshi na Kiusalama kuliko Tanzania yetu hii na sijaona mahala ambapo Marais wao huwa wanawataja hovyo tena hadharani Wakurugenzi Wakuu wa Idara zao ' Nyeti ' za Usalama wa Taifa ila kwa Tanzania naona hii tabia inaanza Kuzoeleka.

Kwa maoni au mtazamo wangu mdogo tu ( mnaojua zaidi mtanisaidia ) kwa asili ya hizi nchi zetu tena ambazo zina ' Majaribu ' na ' Matatizo ' mengi ya Kimsingi huku kukiwa na ' Maadui ' wengi wa ndani na nje sidhani na siafiki kabisa tena kwa 100% kwa Wakurugenzi wetu hawa wa hii Idara / Taasisi muhimu kama si nyeti ya Usalama wa Taifa ( TISS ) kutajwatajwa hovyo kwa Watu na hata kujulikana kwakuwa Tanzania ya sasa imejaa Watu wa ajabu ajabu wenye ' maslahi ' yao ' hasi ' na nchi hii hivyo kuna uwezekano na Wao wakaanza Kumjua na Kumzoea kisha hali ikaja kuwa mbaya zaidi huko mbeleni.

Na sidhani pia kama hata ' Kiuweledi ' hivi anavyofanya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano Dkt. Magufuli la kupenda ' Kumtajataja ' Mkurugenzi Mkuu wa Idara / Taasisi ya Usalama wa Taifa ( TISS DG ) Dkt. Kipilimba ni sahihi na kama itapendeza nadhani Watu wa ' Itifaki ' ambao nina uhakika kuwa wengi wenu tunatiririka na kuserereka pamoja 24/7 hapa JamiiForums hili mtaliangalia kwa hayo mapana yake ili utaratibu ule ule uliozoeleka wa zamani wa hawa Wakurugenzi kutojulikana sana au kutajwatajwa hovyo uendelee kwani Kwangu Mimi kwa ' Mazingira ' ya nchi yetu ulikuwa ni utaratibu murua / mujarab / sahihi kabisa kuliko huu wa sasa aliouanzisha Amiri Jeshi Mkuu na Rais Dkt. Magufuli.

Huu ulikuwa ni mtizamo wangu Mimi kama GENTAMYCINE ila nitashukuru na Watu wengine nao wakija hapa wakichangia huku wale ambao ' watanikosoa ' basi wanikosoe ha ' Hoja ' nzito nzito kwani hata Mimi nataka Kujifunza jambo hapa kutokana na kwamba yawezekana huu utaratibu wa sasa ukawa ndiyo sahihi kuliko ule ambalo nimeukariri / nimeuzoea. Nia na madhamuni tupate afya ya Kimjadala na ya Kimantiki juu ya hili ' Suala ' kusudi mwisho wa Siku wote tupate ' maarifa ' na ' ufahamu ' zaidi.

Karibuni!

Nawasilisha.
UNATAKA KUJUA NA UKIJUA UNAFANYAJE SASA MAADA ZINGINE PELEKENI HUKO KWA WATOTO FACEBOOK
 
Lazima amtajetaje kwa sababu anamfurahishaga sana kwa shughuli za utekaji
 
Kulikoni leo HUJANITISHIA MAISHA ( kuwa my days are numbered ) KAMA AMBAVYO ULINITISHIA KATIKA ' POSTS ' ZAKO MBILI ZA JUMAPILI NA JUMATATU?
Haikuwa na maana mbaya kama ulivyofikiria.......kusema 'Days are numbered' na wala sikusema 'Your Days are numbered'
 
Haikuwa na maana mbaya kama ulivyofikiria.......kusema 'Days are numbered' na wala sikusema 'Your Days are numbered'

Mimi napenda na nitapenda Mimi na Wewe ' tutishiane ' na ikibidi ' tuviziane ' ili mmoja Wetu amtangulize Mwenzake mapema Makaburini. Watutsi hii michezo huwa tunaipenda halafu tunaimudu mno tu!
 
Hivi ww unafikiri kila kitu unakiazishia maada eee? Kuna taasisi zingine hazijadiliwi hovyo hovyo si kila sehem unaingiza siasa

Kama Idara / Taasisi wana Mtumishi wake ' Popoma / Pumbavu ' hivi kama Wewe basi nawashauri waangalie upya aina yao ya ' recruitment ' bila kusahau na kufanya ' thorough vetting ' kwa ' Candidate ' wake kwani Wewe tayari umesha ' prove failure ' tena ya hali ya juu / kutukuka.
 
Kama Idara / Taasisi wana Mtumishi wake ' Popoma / Pumbavu ' hivi kama Wewe basi nawashauri waangalie upya aina yao ya ' recruitment ' bila kusahau na kufanya ' thorough vetting ' kwa ' Candidate ' wake kwani Wewe tayari umesha ' prove failure ' tena ya hali ya juu / kutukuka.
Kwahyo unataka kuniambia hayo unayoyasema hapa ndiyo katiba ya jamhur ya muungano wa Tanzanià inaelekeza hivyo?
 
Mimi napenda na nitapenda Mimi na Wewe ' tutishiane ' na ikibidi ' tuviziane ' ili mmoja Wetu amtangulize Mwenzake mapema Makaburini. Watutsi hii michezo huwa tunaipenda halafu tunaimudu mno tu!
ntangorane
 
Sijawahi Kuanzisha ' Threads ' fupi hapa JamiiForums Mkuu ( pitia threads zangu zote za mambo sensitive zilivyo ) na nashukuru zote zimekuwa zikisomwa na kupata mrejesho wake hivyo labda hili ni tatizo lako tu. Hata hivyo asante kwa kuja na kuchangia hivyo nikuombe tu kaa pembeni waachie ' Great Thinkers ' waje waweze kunipa ' Madini ' tafadhali.
Wavivu wa kusoma utawajua tu mkuu. Hata mimi mkuu nimekuwapo katika awamu zote sikuwahi kusikia mkuu huyo akitajwa tajwa hadharani tena hata mashushu wenyewe ilikuwa ni vigumu sana kuwajua. Siku hizi wanapenda sifa hata wao wenyewe wanajitambulisha. Zamani hata mke au mume angeweza asijue.
 
Kwahyo unataka kuniambia hayo unayoyasema hapa ndiyo katiba ya jamhur ya muungano wa Tanzanià inaelekeza hivyo?

Hapana ni Katiba ya ' Matakoni ' Kwako ndiyo inaelekeza hivyo.
 
Wavivu wa kusoma utawajua tu mkuu. Hata mimi mkuu nimekuwapo katika awamu zote sikuwahi kusikia mkuu huyo akitajwa tajwa hadharani tena hata mashushu wenyewe ilikuwa ni vigumu sana kuwajua. Siku hizi wanapenda sifa hata wao wenyewe wanajitambulisha. Zamani hata mke au mume angeweza asijue.

Kuna mmoja namfahamu alikuwa ni Bosi mkubwa sana huko ameishi na Mkewe akiwa ni Mtumishi wa huko kwa miaka yake 15 akiwa ' Mkubwa ' lakini Mkewe kaja Kujua baada ya Yeye Kustaafu Kiutendaji ( japo Kustaafu Kwao kabisa ni mpaka pale Makaburi yao yatakapofukiwa kabisa na Udongo ) na huyo Mkewe baada ya Kujua alimuogopa mno Mumewe japo baadae Mumewe alijitahidi kumuweka sawa na akamwelewa.

Hii siku sitaisahau Mkuu kuna Siku moja nakumbuka tena mwaka huu huu tu mwanzoni hapo kuna ' Demu ' mmoja nilimbahatisha kama kawaida yangu ' nikamdanganya ' na akanivulia na tulipokuwa Chumbani tukawa tunazungumza mambo mbalimbali na ' interest ' yangu kubwa ilikuwa ni Kumjua vyema Mumewe cha Kushangaza ' Demu ' alianza pale pale Kutiririka na Kuserereka kuwa Mumewe yupo Idarani / Taasisini huko hadi Majina yake yote akanitajia na kunielekeza anapoishi kwani walikuwa hawakai pamoko / pamoja.

Nakumbuka nilimuuliza je imekuwaje Yeye alijua kuwa Mpenziwe yuko huko jibu alilonipa Mkuu hadi ' Mtalimbo / Mpingo / Uume / Mkuyenge ' wangu huu ' tukuka ' uligoma kabisa Kusimama kwa ' mshtuko ' baada ya kuniambia kuwa ' Jamaa ' alimwambia walipokuwa Chumbani ' wanatinduana / wanangonoka ' na kama haitoshi alimtolea hadi Kitambulisho chake na kumuonyesha na ' Pistol ' yake huku akimwambia kwamba ' asitishike ' na Mwanaume mwingine yeyote yule kwani Yeye ndiyo nchi na anaogopwa.

Mkuu nisiende mbali zaidi ila naomba tu niishie hapa tafadhali.
 
Hapana ni Katiba ya ' Matakoni ' Kwako ndiyo inaelekeza hivyo.
Ww toa maneno yako yote machafu ukichoka utaniambia, hili jukwaa kuna watu kama wewe wachache wanalivunjia heshima ila endelea
 
Back
Top Bottom