Mhubiri Paul MacKenzie alianzaje safari tata ya kuwashawishi watu kufunga hadi kufa?

Mhubiri Paul MacKenzie alianzaje safari tata ya kuwashawishi watu kufunga hadi kufa?

jastertz

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2020
Posts
407
Reaction score
768
Ulianza kama ufichuzi ambao ungeyeyuka baada ya muda mfupi wa mihemko na lalama.

Lakini kilichoanzia kati kati ya msitu eneo la Malindi Pwani ya Kenya wiki moja iliyopita sasa kinageuka kuwa donda ambalo kumbukumbu zake hazitafifia hivi karibuni.

Kufukuliwa kwa makaburi ya kina kifupi ambayo yametoa miili ya makumi ya watu na kufikisha hadi takriban watu 70 ambao walikufa kwa kuamrishwa kufunga ili kukutana na Yesu.

Mengi kumhusu yanaendelea kujitokeza pindi siku zinavyosonga mbele lakini kuna ya msingi hadi sasa tunayofahamu kumhusu mhubiri huyu tata.

Paul Makenzi alianza maisha katika mji wa Malindi kama dereva wa teksi.
Wengi waliomfahamu wakati huo hawakuweza kutabiri kitakachotokea miaka mingi baadaye ambapo simulizi zao ni kama za filamu inayotumbukia kuwa ya kutisha.

Mwaka wa 2003 wakati kanisa lake lilipoanza kuwavutia wengi , anadaiwa kubadilisha mafunzo na akaanza kuwataka waumini kuchoma vyeti vyao vya utambulisho na hata vya elimu.

Pia wengi waliowahi kuhudhuria kanisa lake wanasema alianza kuhubiri chuki dhidi ya dini nyingine na hapo aliwapoteza baadhi ya waumini wake ambao waliondoka. Hata hivyo wengi waliwaacha jamaa zao-mume aliondoka na kuwaacha mkewe na watoto katika kanisa hilo.

Wengine waliwatoroka jamaa zao na kujiunga na kanisa hilo kisiri wakisakwa kwa miaka bila kujulikana waliko hadi ufichuzi huu ulivyolipuka.

Katika kanisa lake ,watoto hawakuruhusiwa kwenda shule wala kutibiwa hospitalini.

STORY NI NDEFU.

Maswali mengi kuliko majibu, unahisi tatizo ni nini hasa kwenye haya masuala ya kidini na nini kifanyike?
 
Namshukuru Allah kwa neema ya uislamu niliyo nayo.
Mind you.

Ukisoma kwa utulivu huku ukishirikisha ubongo wako vizuri utagundua hata wale wanaofanyiwa brain wash kwamba ukimuuwa mtu wa tofauti na dini yao wanaenda moja kwa moja peponi kufaidi neema za Allah hawana tofauti na hawa.

Tofauti ni hawa wamedanganywa wamejiuwa wao wakati wale wanadanganywa (au sijui kama ni kweli) kwenda kuuwa wengine.
 
Mind you.

Ukisoma kwa utulivu huku ukishirikisha ubongo wako vizuri utagundua hata wale wanaofanyiwa brain wash kwamba ukimuuwa mtu wa tofauti na dini yao wanaenda moja kwa moja peponi kufaidi neema za Allah hawana tofauti na hawa.

Tofauti ni hawa wamedanganywa wamejiuwa wao wakati wale wanadanganywa (au sijui kama ni kweli) kwenda kuuwa wengine.
Mungu atulinde.
 
Alianza hivihivi kama Gwajima na Mwamposa!


Unadhani Gwajima akiiambia ile misukule yake ifunge mpaka kufa itakataa?
hata pia nawaza hivo. japo usiwaite misukule wale ni ndugu zetu. wanatakiwa wapate elimu.
 
Namshukuru Allah kwa neema ya uislamu niliyo nayo.

Uislamu nawapa credit kwenye internal regulation ya dini. Huwezi kuamka asubuhi ukafungua msikiti ila kwenye Ukristo mtu anaweza kuamka asubuhi akaanzisha kanisa na asiulizwe kitu.
 
Namshukuru Allah kwa neema ya uislamu niliyo nayo.
 
Alianza hivihivi kama Gwajima na Mwamposa!


Unadhani Gwajima akiiambia ile misukule yake ifunge mpaka kufa itakataa?

Sifa kuu ya wafuasi wa cult ni kuwa na kiburi na kutokuambiwa mpaka wanakufa.
 
Matatizo ya akili yakichanganywa na hali ngumu ya maisha matokeo yake ni makubwa Sana.
 
Back
Top Bottom