Mi mgeni humu na huu mtandao nimeupenda naomba utaratibu tuende sawa

Mi mgeni humu na huu mtandao nimeupenda naomba utaratibu tuende sawa

Humu kazi ya moyo kusukuma damu tu na si vinginevyo,usilete habari za moyo wangu umemdondokea!
 
We siio mgeni unapost 239 unaugeni gani?
Hata kama zingekua 10000 c kila mtu na spid yake ya kupost post zake so hilo lisikupe shida angalia details
 
Huku mkuu kwanza kila mtu ni mkuu, Usipomuita mtu mkuu utaitwa mpenda makuu.

Kingine penda uongo, pia kujisifia. Huku hakuna masikini wala hatujui bei ya dagaa, wala soko lake liko wapi? Ukiwa huku usizungumzie daladala, bodaboda achilia mbali vigari vidogo. mkuu Tuko pamoja?

Huku kupanda ndege ni jambo la kawaida sana, kuibiwa kwa njia ya mtandao tumilioni kadhaa ndio majanga yetu. Huwa hatuibiwi tecno, hapa tunaibiwa Iphone, samasung za bei kubwa na vito vya dhahabu. tecno yako naomba uibatize jina kuanzia leo uiite iphone seven.

Watu wote humu wana majumba yao, usitoe mifano ya mpangaji mwenzako, sema jirani yangu inatosha.

wanawake wa humu wooote ni warembo sana,...mengine utajifunza taratiiibu...

UMENIFAHAMU SANA??
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Back
Top Bottom