Ralph Tyler
JF-Expert Member
- Jul 31, 2015
- 2,828
- 3,579
Msingi wa mafundisho ya Padre Dr Martin Luther ulikuwa mambo mawili:
1. Sola gratia. Maana yake "kwa neema tu". Kwamba hakuna namna binadamu anaweza kununua wokovu ila tu kwa neema ya Mungu, na ndio uliokuwa msingi wake wa kupinga lile fundisho lililokuwepo wakati ule la watu kutakiwa kulipia toba ama kununua ondoleo la dhambi.
2. Sola scriptura. Maana yake "kwa maandiko tu". Kwamba jambo lolote ndani ya kanisa ni lazima liwe na msingi wake katika maandiko matakatifu ya Biblia. Na aliamini kuwa kulipia toba ilikuwa kinyume na maandiko.
Natamani angefufuka leo aje ashuhudie jinsi kanisa aliloasisi linavyokiuka misingi yake. Sakramenti zinauzwa. Aje amuulize Mch Daniel Mgogo anahubiri Biblia gani katika zile comedy zake kama za Masanja Mkandamizaji. Aulize kama maaskofu wanaongoza ibada za ndoa za maskini au hata maziko ya masikini.
Naongezea yafuatayo kuhusu mada hii:
1. Haikuwa dhamira ya Padre Dr Martin Luther kujitenga na kanisa katoliki. Akiwa Profesa wa Moral Theology katika chuo kikuu cha Wittenberg, Fr Luther aliandika zile 95 theses kuamsha mjadala wa kitaaluma, akiwa na lengo la kupata sauti za wengine pia ili kurekebisha kasoro za kiteolojia alizoziona.
2. Kama zilivyo taaluma nyingine, Theology nayo ina wabobezi wake ambao ni kawaida kukinzana kifikra miongoni mwao. Kulikuwa na different school of thoughts kuhusu hizi 95 theses, wapo waliomuunga mkono Fr Luther, na wapo waliompinga kwa hoja za kitaalamu. Miongoni wa waliompiga ni Fr Konrad Wimpina ambaye aliandika theses 106 kupinga zile 95 za Fr Luther. Mwingine ni Johann Eck ambaye pia alikuwa rafiki na mwanataaluma mwenzake Fr Luther; huyu aliandika majibu dhidi ya zile 95 theses kwa namna iliyosababisha wafarakane na rafiki yake.
3. Hata hiyo misingi ya 'sola gratia' na 'sola scriptura' inatafsirika kitofauti sana miongoni mwa wataalamu, wakianzia na definitions: neema ni nini? Maandiko ni nini? Kumbukeni vitabu vya Biblia vilikusanywa na hawa hawa ambao Fr Luther alikuwa anawa-challenge, lakini yeye akiongozwa zaidi na fani yake ya Moral Theology. Hata moral theologians wenzie alipishana nao katika tafsiri za mambo mbalimbali.
4. Mwisho, kitendo cha kutengwa kwa Fr Luther nadhani kilitokana na a failed dialogue. Palikosena an unbiased moderator wa kusimamia hii dialogue bila mihemuko. Hata hivyo, matokeo yake bado yamekuwa afya kwa kanisa (kwa maana ya Mwili wa Kristo) kwa kiasi fulani, na changamoto zilizobaki tunaishi nazo.
1. Sola gratia. Maana yake "kwa neema tu". Kwamba hakuna namna binadamu anaweza kununua wokovu ila tu kwa neema ya Mungu, na ndio uliokuwa msingi wake wa kupinga lile fundisho lililokuwepo wakati ule la watu kutakiwa kulipia toba ama kununua ondoleo la dhambi.
2. Sola scriptura. Maana yake "kwa maandiko tu". Kwamba jambo lolote ndani ya kanisa ni lazima liwe na msingi wake katika maandiko matakatifu ya Biblia. Na aliamini kuwa kulipia toba ilikuwa kinyume na maandiko.
Natamani angefufuka leo aje ashuhudie jinsi kanisa aliloasisi linavyokiuka misingi yake. Sakramenti zinauzwa. Aje amuulize Mch Daniel Mgogo anahubiri Biblia gani katika zile comedy zake kama za Masanja Mkandamizaji. Aulize kama maaskofu wanaongoza ibada za ndoa za maskini au hata maziko ya masikini.
Naongezea yafuatayo kuhusu mada hii:
1. Haikuwa dhamira ya Padre Dr Martin Luther kujitenga na kanisa katoliki. Akiwa Profesa wa Moral Theology katika chuo kikuu cha Wittenberg, Fr Luther aliandika zile 95 theses kuamsha mjadala wa kitaaluma, akiwa na lengo la kupata sauti za wengine pia ili kurekebisha kasoro za kiteolojia alizoziona.
2. Kama zilivyo taaluma nyingine, Theology nayo ina wabobezi wake ambao ni kawaida kukinzana kifikra miongoni mwao. Kulikuwa na different school of thoughts kuhusu hizi 95 theses, wapo waliomuunga mkono Fr Luther, na wapo waliompinga kwa hoja za kitaalamu. Miongoni wa waliompiga ni Fr Konrad Wimpina ambaye aliandika theses 106 kupinga zile 95 za Fr Luther. Mwingine ni Johann Eck ambaye pia alikuwa rafiki na mwanataaluma mwenzake Fr Luther; huyu aliandika majibu dhidi ya zile 95 theses kwa namna iliyosababisha wafarakane na rafiki yake.
3. Hata hiyo misingi ya 'sola gratia' na 'sola scriptura' inatafsirika kitofauti sana miongoni mwa wataalamu, wakianzia na definitions: neema ni nini? Maandiko ni nini? Kumbukeni vitabu vya Biblia vilikusanywa na hawa hawa ambao Fr Luther alikuwa anawa-challenge, lakini yeye akiongozwa zaidi na fani yake ya Moral Theology. Hata moral theologians wenzie alipishana nao katika tafsiri za mambo mbalimbali.
4. Mwisho, kitendo cha kutengwa kwa Fr Luther nadhani kilitokana na a failed dialogue. Palikosena an unbiased moderator wa kusimamia hii dialogue bila mihemuko. Hata hivyo, matokeo yake bado yamekuwa afya kwa kanisa (kwa maana ya Mwili wa Kristo) kwa kiasi fulani, na changamoto zilizobaki tunaishi nazo.