Miaka 500 yatimia tangu Kanisa Katoliki kumtenga Martin Luther, mwanzilishi wa Kanisa la Kilutheri

Miaka 500 yatimia tangu Kanisa Katoliki kumtenga Martin Luther, mwanzilishi wa Kanisa la Kilutheri

Msingi wa mafundisho ya Padre Dr Martin Luther ulikuwa mambo mawili:
1. Sola gratia. Maana yake "kwa neema tu". Kwamba hakuna namna binadamu anaweza kununua wokovu ila tu kwa neema ya Mungu, na ndio uliokuwa msingi wake wa kupinga lile fundisho lililokuwepo wakati ule la watu kutakiwa kulipia toba ama kununua ondoleo la dhambi.
2. Sola scriptura. Maana yake "kwa maandiko tu". Kwamba jambo lolote ndani ya kanisa ni lazima liwe na msingi wake katika maandiko matakatifu ya Biblia. Na aliamini kuwa kulipia toba ilikuwa kinyume na maandiko.

Natamani angefufuka leo aje ashuhudie jinsi kanisa aliloasisi linavyokiuka misingi yake. Sakramenti zinauzwa. Aje amuulize Mch Daniel Mgogo anahubiri Biblia gani katika zile comedy zake kama za Masanja Mkandamizaji. Aulize kama maaskofu wanaongoza ibada za ndoa za maskini au hata maziko ya masikini.

Naongezea yafuatayo kuhusu mada hii:
1. Haikuwa dhamira ya Padre Dr Martin Luther kujitenga na kanisa katoliki. Akiwa Profesa wa Moral Theology katika chuo kikuu cha Wittenberg, Fr Luther aliandika zile 95 theses kuamsha mjadala wa kitaaluma, akiwa na lengo la kupata sauti za wengine pia ili kurekebisha kasoro za kiteolojia alizoziona.
2. Kama zilivyo taaluma nyingine, Theology nayo ina wabobezi wake ambao ni kawaida kukinzana kifikra miongoni mwao. Kulikuwa na different school of thoughts kuhusu hizi 95 theses, wapo waliomuunga mkono Fr Luther, na wapo waliompinga kwa hoja za kitaalamu. Miongoni wa waliompiga ni Fr Konrad Wimpina ambaye aliandika theses 106 kupinga zile 95 za Fr Luther. Mwingine ni Johann Eck ambaye pia alikuwa rafiki na mwanataaluma mwenzake Fr Luther; huyu aliandika majibu dhidi ya zile 95 theses kwa namna iliyosababisha wafarakane na rafiki yake.
3. Hata hiyo misingi ya 'sola gratia' na 'sola scriptura' inatafsirika kitofauti sana miongoni mwa wataalamu, wakianzia na definitions: neema ni nini? Maandiko ni nini? Kumbukeni vitabu vya Biblia vilikusanywa na hawa hawa ambao Fr Luther alikuwa anawa-challenge, lakini yeye akiongozwa zaidi na fani yake ya Moral Theology. Hata moral theologians wenzie alipishana nao katika tafsiri za mambo mbalimbali.
4. Mwisho, kitendo cha kutengwa kwa Fr Luther nadhani kilitokana na a failed dialogue. Palikosena an unbiased moderator wa kusimamia hii dialogue bila mihemuko. Hata hivyo, matokeo yake bado yamekuwa afya kwa kanisa (kwa maana ya Mwili wa Kristo) kwa kiasi fulani, na changamoto zilizobaki tunaishi nazo.
 
Martin Luther alikuwa kidume kweli. Nchi ya Germany in deserve kuitwa HE.
1. Martin Luther
2. Adolf Hitler na wengine wengi wameuoa Ujerumani heshima ya kipekee kabisa duniani
Wajerumani ni akili kubwa na wachapa kazi. Waliishi Tanganyika miaka 20 tu lakini walijenga miundo mbinu ambayo mingine tunaitumia mpaka leo.
 
Martin Luther alikuwa kidume kweli. Nchi ya Germany in deserve kuitwa HE.
1. Martin Luther
2. Adolf Hitler na wengine wengi wameuoa Ujerumani heshima ya kipekee kabisa duniani
Helmoth Kol,Angella Merkel,Willy Brandt,Oliver Khan,Jurgen Klop ,Dietmer Hamman nk
 
Naona umepanic kama vile masirahi yako yameguswa..
Mengi manayofanya mme CTRL +V kutoka RC halafu mkaongezea mambo kidogo..ndio maana hadi kuimba mnaimba kama sisi..Ubarikiwa kama sisi.

RC ina miaka 2000+ sasa na itaendelea kuwepo milele na milele. Hoja ya kuoa au kutokuoa si hoja maana ni taratibu binafsi
Nyie mnaimba,,,,neeendeeeni naaa amaaaniiii,kwanini msiseme tu,nendeni na amani? Mbung'o wa Kawe anasema,Ukimuona hivi na lifimbo lake hivi na likanzu jeupe ujue Ni......
 
Leo tunatimiza miaka 500 tangu Kanisa Katoliki lilipotoa waraka wa Kipapa wa kumfukuza aliyekuwa padre wake Martin Luther Januari 3, 1521. Papa alifikia uamuzi huo baada ya miaka minne ya minyukano kati ya kanisa na Luther. Luther alikuwa padre na mtawa wa kanisa katoliki kupitia shirika la Waagustino aliyepadrishwa mwaka 1507.

Alikuwa msomi na mhadhiri wa Taalimungu. Mwandishi mahiri. Mtunzi wa muziki na mtu maarufu wa mabadiliko. Amri hiyo iliyotolewa na papa hujulikana kwa lugha ya kilatin kama “Decet Romanum Pontificem” (It Pleases the Roman Pontiff) ndiyo iliyomfukuzisha Martin.

Chanzo cha kutengwa kwake
Kanisa katoliki katika kupitia kipindi kigumu cha uchumi wake, kilimfanya kiongozi wa wakati huo Papa Leo X kuendelea kutafuta vyanzo vipya vya kuongeza mapato ya kanisa. Kulikuwa na mambo kadhaa yaliyopelekea kuhitajika kwa fedha katika utawala wa papa huyu, mojawapo ikiwa ni hitaji kubwa la kuendelea kujenga kanisa la Mt Petro pale Roma achilia mbali hoja ya Wafaransa kuitawala Italia. Chanzo kimojawapo muhimu kilikuwa ni kulipia ondoleo la dhambi.

Wakati wa utawala wa papa Julius wa Pili, dhambi zilikuwa zinaondolewa kwa kulipia malipizi ya fedha zilizosaidia kujenga kanisa la Mt Petro. Papa Leo X ambaye alikuwa na haja kubwa ya kuendelea kwa ujenzi wa kanisa hilo, nae aliendeleza kile kilichoanzishwa na mtangulizi wake,ili kukusanya fedha zaidi za kujenga kanisa hilo. Kwa sababu za kutokufahamika sana ulaya magharibi kwa jambo hilo, iliyotokana na hoja za kiuchumi, hadi ilipofikia mwaka 1517 ndipo mhubiri aliyefahamika kama Johann Tetzel, mtawa wa shirika la Kidominikani alipoanza kuhubiri kuhusu malipizi hayo katika Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mainz na Magdeburg nchini Ujerumani mwaka 1516.

Tayari alikuwa na uzoefu mkubwa katika kupigia chapuo la kuuzwa kwa malipizi kama ondoleo la dhambi kwenye kiti cha kitubio kati ya miaka 1503 hadi 1510 katika miji mingine ya Ujerumani. Wengi waliona ni matumizi mabaya ya sakramenti ya Kitubio. Hii ndio hasa iliamsha hasira za Martin Luther, akiwa ameyasikia mahubiri hayo ya Tetzel akiwa Juterbog, karibu na mji wake wa Wittenberg mwaka 1517. Johann Tetzel hakuwa mtaalamu wa kutosha kuhusu Taalimungu (Theology) kama ilivyokuwa kwa Dr Martin Luther.

Katika kujibu mahubiri hayo, ndipo padre Martin Luther alipopinga vikali kwa kuandika hoja 95 zinazojulikana sana kama hoja 95 (95 Theses). Hoja hizo zilibandikwa mlangoni mwa kanisa alilokuwa anahudumu, huko Wittenberg Ujerumani tarehe 31 October 1517 akishutumu na kupinga mtindo mpya wa kuuza malipizi. Watu wengi walisoma na kukukubaliana na hoja zake na hoja hizo zilisambaa kwa kasi nchini Ujerumani kama moto wa kifuu. Mwaka 1518 hoja za Luther zilimfikia Papa Leo mjini Roma, na papa alitoa amri kwa mkuu wa shirika la Waagustino, ambako Martin alikuwa ndilo shirika lake, kumnyamazisha. Baada ya kushindikana kupitia mkuu wake wa shirika, Papa alifanya kile kilichoshindwa pia kumnyamazisha kupitia kwa Frederick wa Saxony, huyu alikwa Mfalme wakati huo.

Hatimaye ilipofika June 15 1518, papa alitoa amri kwenye (Exsurge Domini) kwa Martin kuzikana hadharani, akiorodhesha sentensi 41 alizoonyesha kuwa Martin alikuwa anapindisha mafundisho ya kanisa na utaratibu wake, hivyo akimtaka ndani ya siku sitini kukana au akabiliane na adhabu ya kutengwa na kanisa.

Hofu ya papa ilikuwa hoja hizo zingewapotosha waamini. Martin Luther kwa wakati huo tayari alikwisha pata uungwaji mkono sana na watu maarufu nchini Ujerumani, alimjia juu papa na kugoma kukana hoja zake. Licha ya mikutano kadhaa kufanyika za kumtisha Martin azifute hoja hizo lakini alishikilia msimamo wake hadi mwisho. "Sumu" ya Luther ilianza kuenea nje ya Ujerumani, na kupata wafuasi wengi Ulaya Magharibi. Papa Leo X hakuwa na namna nyingine baada ya hapo zaidi ya kutoa amri ya kutengwa kwake Januari 3, 1521.

Papa Leo X kwa mtazamo wa wasomi wengi wa mambo ya kanisa, hakujua na hakupima madhara ya hoja za Martin namna zilivyoenea na kuleta mabadiliko makubwa nchini Ujerumani na duniani kote, kitu ambacho kilikuja kuonekana baadae. Yeye aliamini tu kuwa Martin alikuwa ni sehemu tu ya wapinga kanisa kama wengine waliokwisha tangulia, akijua kuwa kanisa la ukweli litapata ushindi tu. Papa Leo X alikufa ghafla Desemba 1521, akiacha mtanziko mkubwa wa kisiasa na kidini nchini Italia na kuenea kwa kasi Ulaya Magharibi.

Mabadiliko katika kanisa
Baada ya vuguvugu la mabadiliko kushika kasi, kanisa lilifanya mabadiliko kwenye yale yaliyoandikwa na Martin. Hadi leo kanisa linafuata kile kilichopingwa na Martin kutokuuza misamaha ya dhambi kama ilivyotokea nyakati hizo.

Kuzaliwa na Kifo
Martin Luther alizaliwa November 10, 1483 katika mji wa Eisleben, Ujerumani na na kufariki Februari 18, 1546. Katika kuishi kwake nje ya kanisa, alifanya kazi kubwa ya kutafsiri biblia katika lugha ya Kijerumani kutoka Kiebrania, Kigiriki na Kilatini kutokana na umahiri wake wa kuzijua vizuri lugha hizo, ingawa yeye hakuwa wa kwanza kufanya hivyo maana alitanguliwa na Mtakatifi Jerome.

Utofauti ni kuwa wakati wa kutafsiri na namna ya kutumia Biblia. Kwa kutumia wasaidizi kwenye kazi hii, alimaliza Agano zote mbili mwaka 1534. Lakini Martin alileta mapinduzi mapya kwenye kulimiliki neno la Mungu kwani ndiye aliyeleta mawazo mapya kuwa biblia imilikiwe kokote na watu wote iwe kanisani, shuleni au nyumbani. Sio suala la makuhani tu.
Yaliyosemwa ni sawa. Mie siyo PhD wa theology lakini katika kusomasoma tungo za USSR, kuna haya ya kuongenzLa:
G
MOSI
Sapoti kubwa ya ML ndani ya Ujerumani ilikuwa ni ya Mfalme (Chancellor) aliyemuona Papa kama msh8ndani waje Kisiasa. The whole thing was politically motivated "na sisi tuwe nao uhuru wetu. ilijitokeza tena England pale Papa alipokataa kumpa talaka King wa Uingereza ili avmuoe hawara yake. King akaachana na Papa on sovereignty grounds, mpaka leo MYPHITYO.

PILI
ML anaheshimiwa kwa kAufunya Bible iwe ya watu, hapo zamani ilikuwani Kilatini tu. Alichokosea (kama ni kukosea) ni pale alipoikataa Sabato isiwe Jumamosi. Ili kumng'ong'aPapa, ML aliamua KKKT kuwatumie Bible ya Kiebrania tu, si ile ya Kigiriki ilivyokwa mapokeo ya Katoliki. Hadi leo Biblia Katoliki ina vitabu 46 Agano la kale, ya KKKT ina vitabu 39 Agano la Kale, pungufu 7. Alifyanya hivyo kupoza Wasabato, KKKT bado husali Jumapili.

TATU
Enzi za ML kulikuwa na utitiri wa dini, kama vile Mbeya kulivy,o. Kulikuwa na Jan Hus wa Moravia, Czechoslovakia (Moravians), Anglikana England, na Methodists wa Scotland, Austria na USA. Katoliki hawakustuka, walijua ni kuwa .history repeats itself.

Kupama kuna nikichosahau ongezeni,
Regard:
LGF
 
Back
Top Bottom