Mazuri yake kiaina;
Ameiwezesha Taifa Stars kufuzu Afcon baada ya miaka 39, ameongeza timu za ligi kuu kutoka 16 mpaka 20, ameimarisha soka la wanawake na mfano mzuri ni hao Tanzanite, Ameanzisha ligi ya wanawake, ameboresha/kuanzisha mashindano ya vijana ya umri tofauti tofauti kwa lengo la kuvumbua vipaji, nk.
Madudu yake sasa;
Ligi kukosa mdhamini kwa mara ya kwanza tangu enzi za FAT, Kujipendekeza kwa watawala na kushindwa kuficha mahaba yake kwa ccm, ligi kuwa na waamuzi wengi walio lalamikiwa kwa kuboronga kuliko awamu nyingine, kuteua baadhi ya watendaji kwa kujuana au kwa kubebana kama ilivyokua kwa mtangulizi wake Malinzi; mfano uteuzi wa Amunike, Oscar Mirambo na Amy Ninje, kupenda kuzurura huku kukiwa hakuna mpango wowote wa kujenga viwanja vipya mfano kwenye eneo lao la Tanga, kujenga vitega uchumi vya TFF mfano ofisi nzuri za kisasa, hotel, hostel, nk.
Hitimisho: Ikiwezekana uchaguzi ujao, wachaguliwe watu wenye uchungu na mpira wa Tanzania na siyo hao makada na wanachama wa ccm ambao mwisho wa siku wanaifanya timu ya Taifa kama vile ni timu ya ccm.