Michael Macharia Njiri (Dj Brownskin) aliyemrekodi mkewe akijiua ashtakiwa kwa kusaidia kujiua

Michael Macharia Njiri (Dj Brownskin) aliyemrekodi mkewe akijiua ashtakiwa kwa kusaidia kujiua

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Screenshot 2023-06-12 132701.png


Michael Macharia Njiri maarufu kwa jina la Dj Brownskin ameshtakiwa kwa kusaidia kujiua kinyume na kifungu cha 225 (b) cha kanuni ya adhabu.

Inadaiwa kuwa tarehe 29 Julai 2022, eneo la Kariobangi South, kata ya Buruburu, alitoa usaidizi kwa Sharon Njeri Mwangi ili ajiue.

Kwa kosa la pili, Brownskin anashtakiwa kwa uzembe wa kushindwa kuzuia kosa la jinai, ambapo alishindwa kutumia njia zote za busara kuzuia kujiua.
DJ huyo pia anashtakiwa kwa kuharibu ushahidi, ambapo inadaiwa kuwa

"kwa kujua kuwa simu yake ya mkononi yenye nambari ya kadi ya simu 07**** iliyokuwa mikononi mwake inaweza kuhitajika kama ushahidi katika kesi ya kisheria, aliiondoa kwa nia ya kuzuia kutumika kama ushahidi."
Brownskin alikana mashtaka hayo na amezuiliwa kwa siku tatu, akisubiri ripoti ya uangalizi wa utimamu wa akili.

Mshtakiwa alikamatwa tarehe 1 Juni 2023, kuhusiana na kifo cha mkewe.
Tarehe 4 Juni, DCI ilisema DJ huyo alikamatwa baada ya kukaidi wito wa polisi kurekodi taarifa kuhusiana na kifo cha mkewe.

"Katika kanda ya video yenye kuumiza moyo iliyotolewa na bloga maarufu tarehe 1 Aprili, miezi 9 baada ya mabaki ya Njeri kuzikwa, Dakika zake za mwisho zilirekodiwa na DJ huyo alipokuwa akiweka kitu chenye sumu ndani ya kikombe na kunywa bila kusita. Kisha alianguka kutoka kwenye kochi na kuwaita watoto wake wawili kuwajulisha juu ya kifo chake kinachokuja," DCI ilisema katika taarifa yake na kuongeza kuwa mtuhumiwa alituma video hiyo kwa mpenzi wake mwingine anayeishi nje ya nchi.

Pia soma: DJ aliyerekodi Video wakati mkewe akinywa Sumu hadi kufa, akamatwa na Polisi

Citizen Digital
 
Watu wafupi akili zao sijui zipogi wapi!!!

Yaani akaacha mke aliyemzalia watoto ajiue huku aki-record tukio halafu akaenda kupiga picha mbele ya kaburi lake kisha akatuma kwa mpenzi wake aliye ng'ambo?
 
Na bado anaishi kabisaaa😡😡😡 ndugu wa mke bado wapo hai?

Nahisi sababu nina dada mmoja ndio maana nipo hai NINGEUA MTU
 
Na bado anaishi kabisaaa😡😡😡 ndugu wa mke bado wapo hai?

Nahisi sababu nina dada mmoja ndio maana nipo hai NINGEUA MTU
Mkuu, uliona lakini video ya marehemu anavyojiwekea dawa na kunywa sumu? Alidhamiria kwelikweli kujiua
 
Watu wafupi akili zao sijui zipogi wapi!!!

Yaani akaacha mke aliyemzalia watoto ajiue huku aki-record tukio halafu akaenda kupiga picha mbele ya kaburi lake kisha akatuma kwa mpenzi wake aliye ng'ambo?
Ningeua mtu mapemaaaa😡😡😠🤬🤬
 

Angalia video ipo katika huu uzi
Halafu kidooogo jina la mdada lifanane na la Mwanangu "Charlotte" ndio nazidi kupata moto
 
Ni kama mwanamke alikuwa amemcheat sana masta na jamaa alijua hilo, kwa hiyo mke alipoamua kujiua jamaa akaona poa tu

Mzee hata kama sio kurekodi tukio zima.fikiria hao watoto wanavokua na kuona hio video unazan watamchukuliaje baba yao.je ndugu wa upande wa mke nao?
 
Mkuu, uliona lakini video ya marehemu anavyojiwekea dawa na kunywa sumu? Alidhamiria kwelikweli kujiua
Alidhamiria baada ya mateso ya huyu fala. Na kwa ukatili akamrecord
 
Back
Top Bottom