Michakato na vikao vya CCM vinapokaa hufuatiliwa kwa karibu na Mamilioni ya Watanzania

Ninachokukubali ni kuwa una ujasiri wa kujifunika shuka moja na nyoka.. hongera ndugu yangu, maisha ya Watanzania wote ni safi na ccm idumu milele
 
maamuzi yote ya kukandamiza watz hufanyika kwenye vikao vya chama tawala, ni lazima vifuatiliwe
CCM ndio chama chenye Sera na ajenda zinazogusa maisha ya watanzania Ndio sababu ya kufuatilia na watanzania wengi
 
Utafiti hupingwa kwa utafiti, Kama unautafiti wako unaopingana na huu waweza uleta hapa, kwani wewe huoni hata taarifa za vikao vyake CCM namna ambavyo huteka vyombo vya habari na mitandao ya kijamii
Una upeo mdogo sana wa kufikiri. Nisamehe tu kwa kukuambia huu ukweli mchungu.
Ila nahisi hata baadhi ya makada wenzako, watakuwa wanajisikia aibu sana kusoma haya maandishi yako.
 

Kuna na yule alisema robo ya Dunia walifuatilia mazishi ya shujaa wetu. Ngoja arejee kuwapa mwongozo.
 
ni bora nifuatilie Mandoga ulingoni 'cause at the end of the day nitafurahi kuona uso wake umetapakaa minundu huku akijitapa kwamba next game anakwenda kuua mtu.
 
ni bora nifuatilie Mandoga ulingoni 'cause at the end of the day nitafurahi kuona uso wake umetapakaa minundu huku akijitapa kwamba next game anakwenda kuua mtu.
CCM Ni Kama maji usipoyanywa utayaoga tu, kila kitu ifanyacho CCM lazima kiguse maisha yako, Hata ukiichukia CCM mwisho wa siku itakulazimu usipende tu maana Ni chama chenye Sera na ajenda nzuri za kugusa maisha yetu
 
Nina swali kdg!!

Eti MKULIMA anaelilia Bei ya mbolea ishuke, au machinga anaomba apate mtaji, au mfanyakazi apataye mshahara usiokidhi mahitaji......

Watu hao maskini wamepata wapi pesa za kuwanunulia mav8 mliyopaki nje ya kikao Cha CCM Dodoma????
 
Ni kweli CCM inafuatiliwa, ila inafuatiliwa na mamilioni ya wazee.
Inafuatiliwa na Watanzania wa Rika zote maana Sera na ajenda zake zinagusa maisha ya Watanzania wa Rika zote ,kwa kuwa pia ndani ya CCM watu wote Ni sawa na Wana nafasi sawa bila ubaguzi wowote, Ndani ya CCM yeyote unaweza ukawa kiongozi wa ngazi yoyote bila kujari Hali yako ya kiuchumi au familia uliyotokea ikiwa tu unazo sifa na uwezo wa kiuongozi wa kuwatumikia watu kwa weledi na ufanisi, Hii ndio sababu ya CCM kupendwa na kuungwa mkono na mamillion ya watanzania wa Rika zote
 
Ni suala la muda tu, mbona malengo yako yasipotimia utakuja humu na Id nyingine ukiponda mbaya kabisa.

Sio wewe tu wapo wengi kabla yako na tunawajua tangu enzi za Kikwete humu. Kwa ushauri hebu mtafute bro Pasikali akupe moja na mbili kuhusu hao viwavi jeshi.
 

Hamna mtu anapenda chama cha zamani hivyo, ndio maana mbeleko ya dola imekuwa nguvu kuu ya kubaki madarakani kwa shuruti.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…