Michano/Hiphop/Freestyle

Naandika yaliyojiri hii wiki, dah! Maana ni soo/

Gwajima anasema chanjo haiaminiki, itatutoa roho/

Huku Manara kaachia kiti, japo mashabiki wanaomba poo/

Na Diamond msanii wa Muziki, kashusha Rolls Royce/

Simba imeonyesha ukaidi, Yanga imeshindwa kupiga kwenye mshono/

Matukio ya moto yamezidi, mapenzi yanatupa somo/

Mama anajitahidi, chanjo kuipigia promo/

Eti Kamanda kawa gaidi, wananchi wamelala usingizi wa pono/

Haya yote sio ya kale, ya juzi nayapanga kiufundi/

Tozo ipo pale pale, asiyeweza aende Burundi/

Corona inataka itawale, mitaani kama kaonekana Bundi/

Na Insta ni yule Mtoto mkale, na Vanny Boy wanapeana Tundi/
 
Kwa hisani ya rap nasimama juu hili beat, niongee machache juu ya hili week.../

Nuru imetoweka tumeingia gizani, uhuru hakuna wanaoteseka ni upinzani.../

Nchi ya amani ila utawala wa kichoko, soko limeungua mkabala na ofisi ya zimamoto.../

Najiuliza hivi hamjioni limbukeni kweli, soko linaungua afu maji mnayafata gomz badala ya kigamboni fery.../

Serikali kwa wananchi ipo local local ni mwiba, naskia tozo zimewekwa kuficha choko choko za katiba.../

Mtandaoni Kila napopita naskia watu wanazidi kupiga yowe, wakidai aachiwe huru maana sio gaidi freeman mbowe.../
 
Leo nalisema wazo, sio elimu ya chekechea/

Sisemi kuhusu chanjo, waliosema walipotea/

Nasema kuhusu MAWAZO, R.i.p namuombea/

Sisemi kuhusu chango, linalokuja baada ya hongo kupokea/

Nasema uje ufuate Gheto, maana tozo akili fupi/

Na ukinikuta napiga nyet*/ huenda ukanivulia chupi/

Nasema kuhusu ugaidi, ni bora tusiombe/

Nasema kuhusu kufaidi, kodi kwenye pombe/

Nasema kuhusu Amerika, wananchi kujazwa pesa/

Nasema kuhusu kushawishika, na kuchanganya madesa/


 
Hip Hop ninapo imiss, mistari nainyoosha zaidi ya sigara/

Ninachofanya sio rahisi, zaidi ya daktari maabara/

Watoto wanaponi diss, wanashangaa nipo imara/

Napambana na Taasisi, zaidi ya Haji Manara/

Wananiogopa/ zaidi ya Stopa/ wa Rhymes nipo shkopa/ natimiza malengo/

Sio kibopa/ ila nasahau ukinikopa/ juu kama Choppa/ madem makopa/ Wana show mapendo/

Siku hizi Mkulungwa nimenyuti, nadili na chapaa/

Kitambo nishabeba sana chupi, zaidi ya kunguru wa Zanzibar/
 
Nina misimamo Mvumbo, zaidi ya Gwaji Boy/

Ndio maana wachumia tumbo, nawaona kama toy,

Mtaani mikosho mikali, uso wa Bundi/

Imani za Kirasta fari, kama Baba Tundi/

Chanjo maarifa machache, hivyo ukweli tuwaambie/

Unaumia nikiwaambia waache, we mbona unawashawishi watumie/

Wenye maarifa hawataki tuyapate/

Wenye taarifa wameshapewa mkate/

Wenye sifa acha mkumbo wafate/

Wenye Taifa hawaandikii na mate/

Siandiki unielewe, wewe elewa kubet/

Maarifa unayongoja upewe, ukiyajua ni too late/

Ni dunia ya ujuzi nusu nusu, jiongeze baada ya kunakili/

Wewe tafuna Mbususu, ukishiba njoo tujadili/
 
Siasa maji ya magoti, anangoja aelekezwe/
Bora niende vituko post, kama SHIMBA YA BUYENZE/
Mbuzi ukishindwa kumpiga makofi, usimpigie ZEZE/
Hivyo sitaki nionekane mkorofi, rabda hizi ngumu wazimeze/
Hata yule anaependa magari, yaani kama pretta/
Mzee wa vieite hana hali, nae siku hizi anateseka/
Wengine hawakuweka akiba, ya kusifia kama Lokole/
Siku hizi ni Musiba, wanapaza sauti Pole pole/
 
Leo jukwaani natinga, kuwaeleza habari/

Za Jf kabla ya kina Mobimba, Enzi za Cuf ngangari/

Wajuzi mada walichimba, sio story za Diamond na Zari/

Siku hizi mtu anaandika ujinga, anamalizia na UZI TAYARI/

Mshana Jr alifafanua ulozi, mpaka wafia dini wakapiga kelele/

Pia lilikuwepo jukwaa la mamboz, mapicha live tele/

Kiranga hakuamini uokozi, wala hadithi za Mfalme Sele/

Na ukipambana unaambulia nakoz, na kumfuata ka' mfuasi wa Kibwetere/

Wengi mliishia kuwa wasomaji, kwa kuogopa kuchangia/

Siku hizi ndio wajuaji, na story za vibamia/

@maxmelo alipata kesi nyingi, maana serikali ilipigwa za kidevu/

Kuna muda ilibidi yeye aingie kingi, ili sisi tusifanyiwe uonevu/

Hii ni kabla ya magenge, yanayo andika kusifia wapewe mamlaka/

Viongozi Jf iliwakata wenge, mpaka nao wakajiunga kujibu mashtaka/

Wenzetu wengine walipotea, R.I.P Ben Saanane/

Mods siku hizi wamenywea, zamani Ban mpaka utukane/

Wakulungwa wengi wamenyuti, maana watoto wamekamata usukani/

Dakika mbili matusi, na shari kama tuko Talebani/

Sasa ni makundi, Ccm na Chadema soo/

Diamond, na Kiba mtoto wa Kariakoo/

Simba na Yanga wanatoana roho/

Mabitozi na mademu wanapigana K.O/

Wote wamejipanga, hakuna kusanda kwenye hii shughuli/

Demu unaedhani mtoto utabwaga manyanga, utapoona kiuno kina shanga kama tunguri/
 
Naongea na Naniliu, maana kuupiga mwingi sio vibaya/

Namsifu anavyopiga mbiu, Utalii ujulikane mpaka Ulaya/

Ila makesi yatamuacha 'chiu' mengine bora kugwaya/

Na Mafisadi yana 'Q' Chief Hangaya/
 
Ni bingwa kwenye michano, hata unipambanishe na Chainsaw/

Nimeshazoea mapambano, madogo hawawezi toa droo/

Ninapotimba natimiza agano, kama Izraili mtoa roho/

Unachopaswa ni kunipa tano, na kukiri mimi ni soo/

Inchaji haina ujuaji, kama madogo wa Depo/

Nina kipaji hawa wafa maji, wanatamani nisingekuwepo/

Mvumbo ndio namba, tungo ni kisanga, rabda kwa ungo wa wanga, ndio tunzo wataramba/

Na viatu nawalaza, kama usiku wa kulipa deni/

Niite Mvumbo Hamza, kwenye AK 47/
 
Kimya changu ni fumbo, ila sasa Hip hop inaendelea/

Makini kwenye tungo, bado sijapotea/

Wanajificha kama utumbo, kidume nnaposogea/

Waambie wasimchokoze Mvumbo, wamchokoze Bea/

Lazima watupe mbao, nimetanda kama ukungu/

Mimi ndio kamanda wao, vipi walete mizungu/

Ama zangu ama zao, simuachii Mungu/

Nipo juu yao, kama pembe za Kurungu/

Hii si kwa ajili ya watoto, nitawavua sketi/

Mvumbo ni Og sio photo, kipaji sio kubeti/

Na hii sio ndoto, we jaribu kutest/

Kila verse ni moto, kama nimemeza guruneti/
 
Karibu kwetu hapa ndio bongo, Huku matumizi ya mdomo yamepewa kipaumbele kuliko ubongo.../

Njoo kuna vingi vya kuvutia, ila katika hivyo vingi sio vyote tunavitumia.../

Uhuru wa kuongea ni mwingi mwamba ukija utaufaidi, ila kuongea kuhusu katiba mpya mwana huo ni ugaidi.../

Mahakama ya kwetu ni yakipee kwenye hii sayari, ambapo shahidi anapanda kizimbani akiwa na dayari.../

Sheria zipo ili haki iainishwe, lakini jaji kufanya maamuzi ni mpaka kesi iahirishwe.../

Kama jaji hafanyi haki basi kesi isitishwe, na jamhuri iliyofungua kesi iwajibishwe.../
 
Hakika umeanza vema, hivyo endeleza mkuu/
Ili wana wasije kusema, ume copy sehemu tuu/

Kwanza hiphop sio singeli, makelele ya kamatia juu
Mi Mc sio tapeli,, sijinadi na cha mtu
Sasa ushabaini ukweli,, acha kuwa panya buku
Zaire frontline Mobutu Sese Seko Ngbendu Wa Za Banga Kuku.
 

Dogo janja unamishe gani town?,, Au ndo kula kulala kwa mjomba?/
Akupi mtu usukani,, Bila leseni ya karandinga/
Unata dala mbuni sumni,, Kwanza kibyongo pinda/
Uwezi kaa pembeni,, usiku uicheze sindimba/
Nataka nikupe connection,, Uache kuvaa mitumba/
Ninanunuaga million,, kila kilo moja ya kimba/
Usiwnde kunisemea njumbani,, Kiustaalabu nakuomba/
Nikishakutia machoni,, Nitakulipa ata uki……./ yeah!
 
Jf natimba na chair dogo sogea nikukalishe, uzi wa michano we unaongea mambo ya mishe.../

Unauliza mishe, kwani uliskia mi punda.../

Au lengo unidharilishe, nikaishia kukudunda.../

Mi sio mcheza sindimba hilo napinga, kama vipi tucheze mchezo tuone yupi mjinga.../

Yani mi niwe Scar, we uwe triger.../

Mi niwe mwenye bar, afu we uwe stripper.../

Utanipaje connection wewe na hauna waya, kiuno kidogo afu trouser ya pepe si utapwaya?.../

Somesha mtoto aepukane na ujinga wa kikoloni, ili baadaye asije kuuziwa kimba milion.../
 
Sala ya mhuni kabla ya kulala

Uliumba nuru ukaumba giza, ukatupa na uhuru tumkemee adui akikatiza.../

Ukatuamuru tupae kuja kwako bila viza, tutaifika ikulu baada ya majukumu kumaliza.../

Nami bila kufuru agizo lako nalitimiza, nakuomba bila ushuru unishushie miujiza.../

Ulisema tujifunze utiifu na mipaka, Japo sio wakamilifu lakini tufanye unayotaka.../

Ukamlaani yule afanyae usiku kuwa mchana, Ukambariki msikivu zaidi ya ilivyokua jana.../

Nipe neema ya ndoto njema, nikilala nikiamka kusiwe na msoto tena.../

Nakualika uje na jopo la malaika kwa njozi, tujilipue na ma photo ya uhakika kwa pozi.../

Na yule kibaka mtaa wa tatu mpiga kareti, nakuomba umpe roho ya huruma anirudishie ile waleti.../

Ni wiki sasa tangu aibe kanivurugia bajeti, Ndani hali ngumu shibe hakuna kanikimbia aneth.../

Baba naomba utusamehe dhambi ya edeni, ndio chanzo mpaka nazongwa na haya madeni.../

Ameeen
 
unapigo za kike au we ni gay/
kazi kudis watu kila day/kamari imekumaliza pay umebaki mbupu hauna demu unapiga puchu unajifanya mgumu afu unanyoa kiduku/ usituletee ushoga huku/inaonesha umekosa dukuduku ukiona comment yangu unajishuku/ unareply utumbo coz kichwani mtupu/
 
Nikitokea kama zari kwenye beat sina wema/nashusha mistari marapa wenu wanahenya/nazidi tu kupenya/masnitch wanakenya walisema sitafika mbali saiz wananiona kwa sinema/
kitaa nawakilisha vyema nawafungua fikra wenye elimu duni
mbishi nalinda kampuni ya tamaduni/
ili wajifunze hip pop sio uhuni
 
King ndo nimefika, mitaa inaniita beast,
Ladha za uhakika, kitambo si mlisi miss,
Jishikeni patashika, naishusha kila street,
Vigagula wanatambika, naagua tu kwa hits,
Watch your back nigger, hii Vita ni jihadi simamwini even a religious figure,
Navuta mkwanja nigger, if u a little sad how am proud better smoke wider,
 
Navimba jf navimba kitaa na mistari heavy ila niko speed ka motorcar/

Sijakaa kizembe/ukizingua nakupa za chembe unakaa/sijazubaa na siishikiki kwenye miikiki niko fit niguse nikuchane na viwembe upate scars/
 
Me sio wakishua cheki sura imejaa chata, me ni rasta sili nyama ila nakula bata/ukinizingua umemchokoza paka ni ugomvi usio na mipaka nakisanua ile kimafia wananijua mpaka ma master/nikiwaka nakamua mpaka bebe zilizoungua nazichapa/
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…