Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
- Thread starter
- #3,281
Yanga malumbano
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 19th January 2011 @ 23:55
YANGA bado hapakaliki na wala hakunogi baada ya baadhi ya wanachama wa klabu hiyo na wazee kuja juu na kuhoji mahali inapopelekwa timu yao wakidai kuwa wanaingizwa kwenye siasa.
Kwa muda mrefu sasa, ndani ya Yanga mambo yamekuwa hayaeleweki kutokana na sababu mbalimbali ndani ya uongozi wa klabu hiyo kongwe yenye maskani yake mtaa wa Twiga na Jangwani Kariakoo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili kwa sharti la kutoandikwa majina yao gazetini baadhi ya wanachama hao na wazee wa Yanga walisema kuwa klabu yao sasa inaingizwa kwenye masuala ya siasa kitu ambacho wao hawakitaki kwa vile si malengo ya klabu hiyo.
"Klabu yetu inaenda wapi, tumesikia kwamba mfadhili (Yusuf Manji) amemteua Mtemvu (Abbas) kuwa mmoja wa wadhamini, hilo limepitishwa na nani?"
"Mbali na hilo, lakini pia tunasikia kwamba kuna wanasiasa wengine anataka kuwaingiza kwenye safu ya udhamini ya Yanga, jamani tumefikia hatua hiyo kweli,"alisema mwanachama mmoja ambaye aliwahi kuwa kiongozi wa Yanga.
Alisema kwa anavyofahamu, suala la mdhamini wa Yanga ni lazima achaguliwe na Kamati ya Utendaji na pia mkutano mkuu ulipitishe jina lake lakini mambo si kama yanavyokwenda sasa Yanga.
"Huyo Manji mwenyewe mpaka sasa mkutano mkuu haujampitisha bado, halafu yeye analeta watu wengine, tena bila Kamati ya Utendaji kuamua wala mkutano mkuu, hapana hili sasa halikubaliki,"alisema.
Akizungumza na gazeti hili jana, mjumbe mmoja wa Kamati ya Utendaji ya Yanga alikiri kuwa uamuzi wa kumpatia Mtemvu udhamini haukufikishwa katika Kamati yao na wao pia wanashangaa kitendo cha mdhamini wao huyo.
"Ni kweli wanavyosema hao wanachama wala si uongo, tunatakiwa tuamue Kamati ya Utendaji, kisha tupeleke jina hilo kwenye mkutano mkuu wa wanachama nao walipitishe, hivi ninavyokwambia hata wenyewe hatuelewi hali inakuwa vipi".
"Kwanza hata yeye mwenyewe, ( Manji) uteuzi wake haukupitishwa kwenye mkutano wa wanachama bali kiongozi mmoja tu katika uongozi uliopita (anamtaja jina) alimteua basi,"alisema.
Habari zaidi zilizopatikana Dar es Salaam jana, zilidai kuwa jana kulikuwa na kikao kati ya wazee na Manji kikao ambacho kilichukua muda mrefu na kilikuwa na mabishano ya hapa na pale.
"Lakini sisi Kamati ya Utendaji tutakutana leo jioni (jana), hapo ndipo zitakapojulikana mbichi na mbivu, tunataka tujue mustakabali wa klabu, haiwezekani watu wengine waingie watuendeshe wanavyotaka wao, kama ni hivyo kusiwe na uongozi basi, kama kila kitu anafanya mdhamini,"alisema.
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 19th January 2011 @ 23:55
YANGA bado hapakaliki na wala hakunogi baada ya baadhi ya wanachama wa klabu hiyo na wazee kuja juu na kuhoji mahali inapopelekwa timu yao wakidai kuwa wanaingizwa kwenye siasa.
Kwa muda mrefu sasa, ndani ya Yanga mambo yamekuwa hayaeleweki kutokana na sababu mbalimbali ndani ya uongozi wa klabu hiyo kongwe yenye maskani yake mtaa wa Twiga na Jangwani Kariakoo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili kwa sharti la kutoandikwa majina yao gazetini baadhi ya wanachama hao na wazee wa Yanga walisema kuwa klabu yao sasa inaingizwa kwenye masuala ya siasa kitu ambacho wao hawakitaki kwa vile si malengo ya klabu hiyo.
"Klabu yetu inaenda wapi, tumesikia kwamba mfadhili (Yusuf Manji) amemteua Mtemvu (Abbas) kuwa mmoja wa wadhamini, hilo limepitishwa na nani?"
"Mbali na hilo, lakini pia tunasikia kwamba kuna wanasiasa wengine anataka kuwaingiza kwenye safu ya udhamini ya Yanga, jamani tumefikia hatua hiyo kweli,"alisema mwanachama mmoja ambaye aliwahi kuwa kiongozi wa Yanga.
Alisema kwa anavyofahamu, suala la mdhamini wa Yanga ni lazima achaguliwe na Kamati ya Utendaji na pia mkutano mkuu ulipitishe jina lake lakini mambo si kama yanavyokwenda sasa Yanga.
"Huyo Manji mwenyewe mpaka sasa mkutano mkuu haujampitisha bado, halafu yeye analeta watu wengine, tena bila Kamati ya Utendaji kuamua wala mkutano mkuu, hapana hili sasa halikubaliki,"alisema.
Akizungumza na gazeti hili jana, mjumbe mmoja wa Kamati ya Utendaji ya Yanga alikiri kuwa uamuzi wa kumpatia Mtemvu udhamini haukufikishwa katika Kamati yao na wao pia wanashangaa kitendo cha mdhamini wao huyo.
"Ni kweli wanavyosema hao wanachama wala si uongo, tunatakiwa tuamue Kamati ya Utendaji, kisha tupeleke jina hilo kwenye mkutano mkuu wa wanachama nao walipitishe, hivi ninavyokwambia hata wenyewe hatuelewi hali inakuwa vipi".
"Kwanza hata yeye mwenyewe, ( Manji) uteuzi wake haukupitishwa kwenye mkutano wa wanachama bali kiongozi mmoja tu katika uongozi uliopita (anamtaja jina) alimteua basi,"alisema.
Habari zaidi zilizopatikana Dar es Salaam jana, zilidai kuwa jana kulikuwa na kikao kati ya wazee na Manji kikao ambacho kilichukua muda mrefu na kilikuwa na mabishano ya hapa na pale.
"Lakini sisi Kamati ya Utendaji tutakutana leo jioni (jana), hapo ndipo zitakapojulikana mbichi na mbivu, tunataka tujue mustakabali wa klabu, haiwezekani watu wengine waingie watuendeshe wanavyotaka wao, kama ni hivyo kusiwe na uongozi basi, kama kila kitu anafanya mdhamini,"alisema.