Michuano ipi ya World Cup ilikuwa bora sana kuitazama?

Kwangu ni Mwaka 1994...enzi zile Temeke Mikoroshini ,wenye TV UNAWAHESABU😀😀 hata Mzee Uruguay hakuwa nayo! Tulikuwa tunaenda Stereo...ile Nyomi haikuwa ya nchi hii!
Siku ya Fainali umeme ukakatika pale Stirio,tulihaha!ikabidi kwenda kwa Mzee mmoja wa Kihaya ..pale karibu na Lusaka kama una enda Yombo ,just opposite na kwa Said Mwamba,...tulibanana humo ...hadi leo ni siri yangu kuwa dakika za mwisho mpir asikuuona ,nilikuwa nashangilia tu! Kulikuwa na house boy wa yule mzee alikuwa na roho mbaya sana!
Tumetoka mbali ...!
 
Bonge ya game ilikuwa.
Ila nakusahihisha Magoli yalifungwa na Fabio Groso na Del Piero na si Iaquinta.
 
1988 aisee,wachezaji wengi sana walionyesha viwango,kina davo Suka,Mari selo salali,mwanko kanu,zizu ,Luis Figo,Devi's bekhamp,Patric cruvet,n.k
Nadhani unamaana 1998. Karembeu,petit,desairy,ronaldo mwenyewe , zidane, salas, D sukar, rivaldo, colombia,romania,chile..
Fire fire
 
Hiyo 90 game zilikuwa zinapigwa mda mbaya. Nakumbuka nilikuwa doga sana. Niongozana na mshua wangu kwenda kuangalia mpIra pale chuo cha polisi CCP, Kwenye moja ya bwalo la maafisa wa polisi.

Argentina ikitokea kuchukua kombe kule mexico 86. Walikuwa na kikosi kizuri chini ya kocha Carlos Bilado.

Wachezaji ninao wakumbuka. Maradona, Caniggia, Burruchaga, Neri Pompidou, Sergio Goicochea, dah kitambo sana ila kama juzi tu.

Ujerumani mabingwa wa 90. Holland ya kina Gulitt, England ya Liniker. Romania ya Marius Lacatus, brazili ya careca na Cameroon ya Rodger Milla.

Africa tuliwakilishwa na nchi mbili. Misri na Cameroon.
 
Personally 2006 na 2010 pure football, pure drama, pure talents, class countries.

Na sababu kubwa tuwe wakweli Shakira na partnership ya RedOne ndio huchagiza kupendezesha michuano.

2018 Diplo na wavuta Bangi wenzao FIFA walifanya michuano kuwa takataka, Ilizidiwa hadi na Euro 16 na Copa America.

Nilikuwa bado na maziwa by the way. Na hii ni opinion yangu.
 
Kama sijakosea Mali walifika robo au nusu fainali kwenye hizi fainali
 
Jamaa hauko makini na usahihi wa majina ya wachezaji!
Davor Suker
Nwankwo Kanu
Kluvert
Beckham

Kuwa makini
1998 aisee,wachezaji wengi sana walionyesha viwango,kina davo Suka,Mari selo salali,mwanko kanu,zizu ,Luis Figo,Devi's bekhamp,Patric cruvet,n.k
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…