Miezi mitatu kabla ya kuandamana Wenyeviti wa vijiji 80 vya Ngorongoro walikwenda kumsihi RC Makonda awarudishie huduma za kijamii

Makonda angekuwa Rais angewafyeka Masai wote huku akijiita mtetezi wa wanyonge. πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Ku retreat ndio usikivu wenyewe.Zoezi la kuwahamisha Kwa hiari linaendelea huku Huduma zikiendelea.
 
Makonda alikuwa off kwenye shughuli za serikali msimsingizie

..umeangalia hiyo video?

..viongozi wa vijiji walikwenda kumuona Makonda miezi mitatu kabla ya maandamano. Wakati huo Makonda hakuwa likizo.

..maandamano yametokea baada ya Wamaasai kujaribu njia zote za amani na kushindwa.
 

..vijiji vilifutwa kwasababu Serikali ilishaondoa huduma kwa Wamaasai miaka 3 nyuma.

..Huwezi kufuta vijiji bila kwanza kuwa umefuta huduma.

..Tunapaswa kujiuliza vyombo vya habari vilikuwa wapi wakati mambo yote haya yanatokea?
 
ila serikali yake sio sikivu kabisa!. Nimeshauri waliotufikisha hapa kwenye hili la Ngorongoro wawajibishwe
Hapa itakuwa ni kutaka kutafuta mbuzi wa kafara tu.

Kwa mujibu wa hii katiba yetu mbovu, maamuzi mazito kama haya kwa vyovyote vile yametoka kwenye kichwa na kinywa cha rais.

Kama kuna anayepswa kuwajibika/kuwajibishwa basi rais awe ndiye nambari one.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…