Mwanongwa
JF-Expert Member
- Feb 15, 2023
- 611
- 567
Nilianza kufanya mchakato wa maombi ya kupata Pasi ya Kusafiria kwa kufuata njia halali, awali nilienda Kibaha Mkoani Pwani, kuna staff mmoja wa pale akanishauri kuwa kama nina haraka nifanye mambi yangu mtandaoni kisha nielekeze nikachukue Passport yangu hiyo Dar es Salaam
Nikafanya hivyo, baada ya kukamilisha kila kitu baadaye nikaanza mchakato wa kufuatilia, kila nikienda nikaanza kuwa nazungushwa naambiwa hivi mara vile.
Kila walichokuwa wakihitaji nikakifanya na kutimiza, ofisa mmoja ambaye jina na vithibitisho vyote ninavyo akaniambia “Niongee vizuri ili niweze kupata Passport yangu ndani ya muda mfupi” sikulifanya hilo kwa kuwa sikuwa na haraka na Pasi yenyewe, nimeamua kuchukua kwa kuwa ni haki yangu na ninaweza kuitumia siku za mbeleni.
Ningekuwa Mdada ningesema labda jamaa anataka kutumia njia hiyo kunitongoza lakini mazingira yanaonesha wazi kuwa bila kutumia mlango wa nyuma ni vigumu kupata huduma haraka kama Viongozi wa Uhamiaji wanavyojinadi.
Huu sasa ni mwezi wa tatu sijapata Passport yangu licha ya kukamilisha kila kitu, kila nikifuatilia naambiwa “njoo wiki ijayo”, kibaya zaidi kuna watu nawajua na tunajuana wao wamekuja mbele yangu wamepata Passport ndani ya muda mfupi.
Mimi nikiuliza naambiwa ipo kwenye mchakato wa kuprintiwa, mbona za wengine zinaprintiwa fasta?
Kamishna Dr. Anna P. Makakala hivi unajua kinachoendelea, je ni kweli kuna watu ambao wao ni maalum Nchini ndio wanapata Pasi mapema au ni kweli kuwa UHAMIAJI mmeishiwa material ya kuprinti Passport mpya?
Nimesoma uzi sehemu jamaa anasema kule Kibaha kuna ambao wameomba Passport huu ni mwezi wa Sita sasa hawajapata.
Pia soma
~ Upatikanaji wa Passport kwenye ofisi ya Uhamiaji pale Kibaha Mjini bado ni changamoto
~ Paul Mselle: Wenye changamoto ya kucheleweshewa “Passport” wafike ofisini watapata majibu
Nikafanya hivyo, baada ya kukamilisha kila kitu baadaye nikaanza mchakato wa kufuatilia, kila nikienda nikaanza kuwa nazungushwa naambiwa hivi mara vile.
Kila walichokuwa wakihitaji nikakifanya na kutimiza, ofisa mmoja ambaye jina na vithibitisho vyote ninavyo akaniambia “Niongee vizuri ili niweze kupata Passport yangu ndani ya muda mfupi” sikulifanya hilo kwa kuwa sikuwa na haraka na Pasi yenyewe, nimeamua kuchukua kwa kuwa ni haki yangu na ninaweza kuitumia siku za mbeleni.
Ningekuwa Mdada ningesema labda jamaa anataka kutumia njia hiyo kunitongoza lakini mazingira yanaonesha wazi kuwa bila kutumia mlango wa nyuma ni vigumu kupata huduma haraka kama Viongozi wa Uhamiaji wanavyojinadi.
Huu sasa ni mwezi wa tatu sijapata Passport yangu licha ya kukamilisha kila kitu, kila nikifuatilia naambiwa “njoo wiki ijayo”, kibaya zaidi kuna watu nawajua na tunajuana wao wamekuja mbele yangu wamepata Passport ndani ya muda mfupi.
Mimi nikiuliza naambiwa ipo kwenye mchakato wa kuprintiwa, mbona za wengine zinaprintiwa fasta?
Kamishna Dr. Anna P. Makakala hivi unajua kinachoendelea, je ni kweli kuna watu ambao wao ni maalum Nchini ndio wanapata Pasi mapema au ni kweli kuwa UHAMIAJI mmeishiwa material ya kuprinti Passport mpya?
Nimesoma uzi sehemu jamaa anasema kule Kibaha kuna ambao wameomba Passport huu ni mwezi wa Sita sasa hawajapata.
Pia soma
~ Upatikanaji wa Passport kwenye ofisi ya Uhamiaji pale Kibaha Mjini bado ni changamoto
~ Paul Mselle: Wenye changamoto ya kucheleweshewa “Passport” wafike ofisini watapata majibu