Mifumo ya Uendeshaji wa Serikali ya Awamu ya Tano, iangaliwe upya! Watanzania "tutachoka" vibaya sana ndani ya hii miaka 10 ya Mhe. Rais Magufuli

Aisee....nimekuelewa vizuri!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
WAPIGA DILI ambao leo wamevaa koti la UZALENDO hawataki taarifa za CAG aliyepita Prof.Musa Assad,hawataki manunuzi kama ya Ndege yafuate sheria za manunuzi na wala hawataki idhini ya Bunge!

Hao wazalendo mkuu wanataka nchi iende mbele, tumenunua ndege wenyewe halafu utukague ili iweje mbona wengine hawakununua baadala yake waliuza scraper zote alizoacha JKN.. Mkuu kuwa Mzalendo chagua JPM 2020 ushindi 99.9%
 
Aisee umenena Mkuu...!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunyweni bia tusheherekee Christmas nchi iko kwenye mikono salama ya jembe Dr JPM chini ya askari wake wa miavuli RC Makonda, RC Mnyeti, Kangi Lugola, DC Jokate, RC Dr pale Mbeya, DC Sabaya, Mh Jafo, Mh Karemani, Mh Biteko, Polepole, Dr Bashiru nk..

Chrismass tamu haijawahi kutokea ng'ombe, mbuzi, kondoo na kuku wamechinjwa balaa maduka ya nguo yako bize mpaka jana usiku wa manane, kariakoo imekesha wiki hizi mbili... 2020 chagua Dr JPM ushindi wa kishindo 99.9%..
 
Aisee hebu tuliza akili soma kwa utulivu,utamuelewa vizuri Mkuu.....!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Nimekuelewa chief🀣
 
Halafu wenye takataka kichwani humu wanakalia kuimba sifa!!
Inachofanya serkali ni uharamia dhidi ya jamii. Maelfu tayari wako vijiweni kwa jina la Machinga, na kama haitoshi bado secta binafsi inayoweza kukomboa watu nayo inatazamwa kwa jicho la husuda na watawala ambao wanapaswa kuisaidia ili iajiri zaidi.
Nafikiri kuna kitu si sawa kichwani kwa watawala hawa wa awamu ya tano japo tunajua CCM ni ile ile tangu kale!!!
 
Hao wazalendo mkuu wanataka nchi iende mbele, tumenunua ndege wenyewe halafu utukague ili iweje mbona wengine hawakununua baadala yake waliuza scraper zote alizoacha JKN.. Mkuu kuwa Mzalendo chagua JPM 2020 ushindi 99.9%
2020 hakutakuwa na mgombea anaitwa JPM kwenye kinyan'ganyiro cha urais.
 
U
Tulia basi mavyama ya nn mbona unanongwa jamani amekosea kwa hekima tu hapo no tusi unaanza kubwabwaja kwan ni dhambi kumkosoa raisi? Sis ndo mabosi zake wananchi anawajibika kwetu
 
Swali fikiri je una uhakika ya kuishi miaka 10 au 5 ijayo ''you have to think out side the box with this question before you give an answer''
 
U
Tulia basi mavyama ya nn mbona unanongwa jamani amekosea kwa hekima tu hapo no tusi unaanza kubwabwaja kwan ni dhambi kumkosoa raisi? Sis ndo mabosi zake wananchi anawajibika kwetu

Mkuu hizo ni hadithi za kufurahishia genge, kwamba wananchi ndio maboss wa rais? Una uhakika rais anapatikana kwa kura za hao wananchi?
 
Mkuu upo sahihi sana, hii ni nchi ya wanyonge.
Hahaaa
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kibwengo anakusanya pesa na kuzigawa mwenyewe ajuavyo. Kwenye Taasisi za chini hazifiki kabisa.

Ndio maana kila kitaasisi sasa ili kiishi, kimeamua na chenyewe kukusanya fedha zake chenyewe:

- TARURA
- NEMC
- TRA
- SERIKALI ZA MITAA
- HALMASHAURI
- FIRE
- TRAFFIC POLICE
Na hapo wanaoumia kwa kuwa bombarded na michango yote hiyo ni wale wale, WANANCHI.
 

Onyeaha kwanza wewe umekosoa vipi na ukatafutwa au ukalaumiwa?
 
😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭
 
Hilo la Wakurugenzi wa Halmashauri kukopa hapana aisee?!

Hata mimi binafsi siliungi mkono!

Tena sikuwahi kuwaza kama kitu cha namna hiyo kinaweza kufanyika kwenye Halmashauri zetu nchini.

Wao waimarishe ukusanyi wa mapato, wabuni vyanzo vya mapato visivyoumiza watu.

Ruzuku na OCs wanazipewa wachanganye pamoja kisha watekeleze miradi ya maendeleo kwa ufanisi mkubwa


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Umeongea vizuri sana.....

Lakini kwa kuongezea tu kwenye hoja yako ni kuwa ishu si kutekelezwa ama kutotekelezwa kwa mega development projects kama vile mradi wa umeme wa Stiglers Gorge, ujenzi wa Reli ya kisasa (SGR), ufufuaji Airline Charter ya nchi (ATCL) nk nk....

Na nadhani tuwaambie wote watoa sifa na serikali kwa ujumla kuwa, hakuna anayepinga nchi kuwekeza kwenye miradi mikubwa ya maendeleo kama inavyotajwa....

Sisi wakosoaji (na nadhani ndiyo lengo na mantiki ya makala hii ya Fumadilu Kalimanzila), pamoja na nia njema ya miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa na nchi yetu, lakini tunataka mambo yafuatayo yaende sambamba na hayo;

βˆšβ€’ MOSI, kuwe na uwiano ulio sawa kati ya maendeleo ya vitu na wakati huo huo tukiwaangalia watu kwa kuhakikisha kuwa wana uwezo wa kuuza na kununua, wana uwezo wa kumudu kupata mahitaji yao muhimu ya kila siku nk. Wengine wanasema tuangalie maendeleo ya watu zaidi kuliko vitu....!!!

Ukichunguza sana utagundua kuwa popote palipo na mitafaruku na migongano ya kijamii, chanzo chake ni watu kuchoka kwa kushindwa kumudu kupata mahitaji yao ya kila siku....

Kwa lugha rahisi na ya kueleweka, ni kuwa, fedha kuwa mikononi mwa wachache hususani tabaka la watawala huku wananchi wanyonge walio mengi kwa zaidi ya 95% wakiachwa bila kitu....!!

βˆšβ€’ MBILI, tabaka la WATAWALA na WATOA MAAMUZI liache kuhodhi nguvu ya uhuru wa watu kutoa maoni yao, hisia zao na grievances zao kwa mujibu wa sheria....

Mfano wanafunzi wa vyuo vikuu juzi kati hapa kufukuzwa chuo eti tu waliamua kudai haki yao ya kupata mikopo.....

Kwa lugha rahisi kabisa, tuachilie demokrasia ishike mkondo wake sawasawa na katiba na sheria zetu zinavyotuongoza.....

βˆšβ€’ TATU, tuachilie mifumo ya kiutawala na kisheria ifanye kazi kwa uhuru na kwa mujibu wa majukumu yao ya kikatiba na kisheria pasipo kuingiliwa......

Mwandishi wa makala tunayoijadili ameeleza vizuri sana kuhusu hili....

Kwamba, ilivyo sasa Binge, Mahakama na vyombo vingine vyote vinavyosimamia mwenendo wa kijamii kama polisi, TISS, ofisi ya CAG, msajili wa vyama vya siasa viko compromised na Executive (kwa maana ya Rais).....

Kwamba mifumo na vyombo hivi kwa sasa, ingalau kwa miaka hii minne zaidi (2015 - 2019), imejikita kufanya kazi kumlinda mtu mmoja zaidi aitwaye RAIS kuliko kulinda maslahi mapana ya nchi na watu wake.....!!

Bunge haliko huru kabisa kutekeleza wajibu wake wa kikatiba. Vivyo hivyo mahakama ukiachilia mbali Jaji na Hakimu mmoja mmoja....

Executive hujiamulia tu mambo ikiwemo kupanga matumizi ya fedha za umma huku kazi hiyo kikatiba na kisheria ikiwa ni ya Binge la wananchi na hakuna wa kuuliza....!!

MWISHO, namalizia tena kwa kusema, hakuna mwenye ishu na miradi mikubwa ya maendeleo. Na in fact, hakuna asemaye miradi hii ni mibaya na kwamba, haina faida yoyote kwa nchi na watu wake wa sasa na wa vizazi vijavyo vya miaka inayokuja....

The problem ni namna inavyotekelezwa kwa maamuzi ya mtu mmoja aitwaye RAIS......

Na yeyote anayejaribu kuhoji, kukosoa au kushauri anaweza kujikuta amepoteza maisha ama kupotea kusikojulikana....

Ndipo hapo watu tunajiuliza, kulikoni? Kuna nia njema kweli kwenye hii miradi? Na je, ni miradi ya wananchi kweli au ni ya viongozi tu kupigia fedha za umma? Kwanini CAG anaposema kinyume na matarajio yao kuhusu projects hizi wahusika wanang'aka na kutaka hata kuua? Kulikoni????

Na mara nyingi sana miradi inayoanzishwa kwa njia za ulaghai laghai na ujanja ujanja wa wizi siku zote huwa siyo sustainable na hata ukamilikaji huwa ni wa taabu sana....

Mfano halisi ni mradi wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo.....

Kwa kuwa ulianzishwa kilaghai, ndo hivyo tena umeishia njiani....

Who knows, kwamba, miradi kama ya SGR na Bwawa la uzalishaji umeme la Stiglers Gorge haitakuja kukumbwa na dhahama kama ulivyoikumba Bandari ya Bagamoyo??

Are we sure kuwa aliyeanzisha projects hizi Bwana Pombe Magufuli atakuwepo kesho au keshokutwa?

Anaweza kufa ama asiwe Rais tena in a just a near future. Who knows??

Na akiondoka kwa namna yoyote ile, maana yake atakuwa ameondoka na SGR yake kama Kikwete alivyoondoka Bandari ya Bagamoyo, Atakuwa aneondoka na Chato International Airport kama ile ya Mobutu Seseseko wa Zaire....!!

Inakuwa ni nini hiyo?

Ni matumizi mabaya na ya hovyo ya fedha za umma and in fact lazima waliohusika wawe answerable in future....

Tuache mifumo itende kazi yake. Maamuzi ya mtu mmoja tu katika nchi bila kuwa CHECKED and BALANCED ni janga kwa taifa....

Ndivyo ilivyo katika TZ yetu leo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…