Pre GE2025 Migogoro ya Ardhi Arusha yamliza Silaa

Pre GE2025 Migogoro ya Ardhi Arusha yamliza Silaa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa amejikuta akitokwa na machozi wakati akimsikiliza Makazi wa jijini Arusha ajulikanae kwa jina la Respis Brasius ambaye amekiri kwamba angekunywa Sumu kama asingesikiliza Hotuba yake ya Bajeti ya Mwaka 2024/2025 wakati akiwasilisha Bungeni Dodoma tarehe 27 Mei 2024.

Mkazi huyo alifikia hatua hiyo baada ya kuteseka kwa muda mrefu akitafuta haki yake bila mafanikio kwa kuwa alivunjiwa nyumba yake pamoja na watu wengine katika mtaa wa Unga Limited jijini Arusha.
 

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa amejikuta akitokwa na machozi wakati akimsikiliza Makazi wa jijini Arusha ajulikanae kwa jina la Respis Brasius ambaye amekiri kwamba angekunywa Sumu kama asingesikiliza Hotuba yake ya Bajeti ya Mwaka 2024/2025 wakati akiwasilisha Bungeni Dodoma tarehe 27 Mei 2024.

Mkazi huyo alifikia hatua hiyo baada ya kuteseka kwa muda mrefu akitafuta haki yake bila mafanikio kwa kuwa alivunjiwa nyumba yake pamoja na watu wengine katika mtaa wa Unga Limited jijini Arusha.
Mambo ni mengi sana nchi hii
 

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa amejikuta akitokwa na machozi wakati akimsikiliza Makazi wa jijini Arusha ajulikanae kwa jina la Respis Brasius ambaye amekiri kwamba angekunywa Sumu kama asingesikiliza Hotuba yake ya Bajeti ya Mwaka 2024/2025 wakati akiwasilisha Bungeni Dodoma tarehe 27 Mei 2024.

Mkazi huyo alifikia hatua hiyo baada ya kuteseka kwa muda mrefu akitafuta haki yake bila mafanikio kwa kuwa alivunjiwa nyumba yake pamoja na watu wengine katika mtaa wa Unga Limited jijini Arusha.
Sanaa hizi mpaka lini yarabi. Poleni sana watanzania. Najua wengi siyo makosa yenu bali ni elimu sahihi mliyonyimwa na chombo kilichostahili kuhakikisha mnaipata i.e. serikali. Mtaendelea kuchezewa n akufanywa misukule namna hii kwa muda mrefu lakini matatizo ndiyo yatazidi kuongezeka kwa sababu uongozi wetu ndivyo unavyofanya kazi. .i.e. hauzuii matatizo kabla hayajatokea bali unasubiri yatokee halafu wanachagua watu wachache sana wanajifanya kuwasikiliza ili wapate umaarufu. Hamjiulizi ni kwa nini kuna migogoro mingi? Hamjiulizi ni kwa nini vyombo vinavyostahili kuitatua havifanyi kazi? Hamjiulizi wale ambao hawapati bahati ya kusikilizwa (ambao ndiyo wengi) watakimbilia wapi? Mbwa ukitaka wakuone kama mungu wao, waache bila chakula kwa muda mrefu halafu mara moja moja, chukuwa minofu ya nyama michache watupie wagombanie... Wanasahau kuwa ni wewe ndiye unayesababisha mateso yao na kukuona kama mkombozi. Hivi ndivyo watanzania wanavyofanywa!
 
Sanaa hizi mpaka lini yarabi. Poleni sana watanzania. Najua wengi siyo makosa yenu bali ni elimu sahihi mliyonyimwa na chombo kilichostahili kuhakikisha mnaipata i.e. serikali. Mtaendelea kuchezewa n akufanywa misukule namna hii kwa muda mrefu lakini matatizo ndiyo yatazidi kuongezeka kwa sababu uongozi wetu ndivyo unavyofanya kazi. .i.e. hauzuii matatizo kabla hayajatokea bali unasubiri yatokee halafu wanachagua watu wachache sana wanajifanya kuwasikiliza ili wapate umaarufu. Hamjiulizi ni kwa nini kuna migogoro mingi? Hamjiulizi ni kwa nini vyombo vinavyostahili kuitatua havifanyi kazi? Hamjiulizi wale ambao hawapati bahati ya kusikilizwa (ambao ndiyo wengi) watakimbilia wapi?.....

Upo sahihi
CCM ktk utawala wao wa serikali wanaacha tatizo litokee baada ya kuumiza sana wananchi ndio watakuja kutatua tatizo hilo ili waonekane wanafanya kazi kumbe ni usanii tu.

mi binafsi nimeichoka CCM, hawana jipya wameitafuna sana nchi waachie na wengne
 
Jina la kiroman ( sio dini) mwanzo mwisho ivi atuwezi kurudi kwenye mizizi yetu tutumie majina ya asili yetu labda tutakombolewa kutoka kwenye haya matatizo.
 
Kulia kwa waziri maana yake n nn? Amewekwa kwenye hiyo nafasi ili alie, akilia anasaidia nini? Watz wengi akili zao wanazijua wenyewe
 

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa amejikuta akitokwa na machozi wakati akimsikiliza Makazi wa jijini Arusha ajulikanae kwa jina la Respis Brasius ambaye amekiri kwamba angekunywa Sumu kama asingesikiliza Hotuba yake ya Bajeti ya Mwaka 2024/2025 wakati akiwasilisha Bungeni Dodoma tarehe 27 Mei 2024.

Mkazi huyo alifikia hatua hiyo baada ya kuteseka kwa muda mrefu akitafuta haki yake bila mafanikio kwa kuwa alivunjiwa nyumba yake pamoja na watu wengine katika mtaa wa Unga Limited jijini Arusha.
Hiyo tunaitaga crocodile [emoji246] teas
 
Kulia kwa waziri maana yake n nn? Amewekwa kwenye hiyo nafasi ili alie, akilia anasaidia nini? Watz wengi akili zao wanazijua wenyewe
Ni wanafiki tu kama kilivyo chama chao
 
Upo sahihi
CCM ktk utawala wao wa serikali wanaacha tatizo litokee baada ya kuumiza sana wananchi ndio watakuja kutatua tatizo hilo ili waonekane wanafanya kazi kumbe ni usanii tu.

mi binafsi nimeichoka CCM, hawana jipya wameitafuna sana nchi waachie na wengne
Wametawaliwa na unafiki mkubwa
 
Kulia kwa waziri maana yake n nn? Amewekwa kwenye hiyo nafasi ili alie, akilia anasaidia nini? Watz wengi akili zao wanazijua wenyewe
Waziri hajalia,bali ametokwa tu na machozi ya hisia kwa.dhuluma walizofanyiwa wananchi ya kubomolewa makazi yao bila kosa! Hata wwe ungetokwa na machozi ya hisia ni jambo la kawaida kama una roho ya utu ndani yako, lakini kama wwe umejaa dhuluma huwezi kua na hisia za huruma kwa muathirika wa dhuluma!!
 
Waziri hajalia,bali ametokwa tu na machozi ya hisia kwa.dhuluma walizofanyiwa wananchi ya kubomolewa makazi yao bila kosa! Hata wwe ungetokwa na machozi ya hisia ni jambo la kawaida kama una roho ya utu ndani yako, lakini kama wwe umejaa dhuluma huwezi kua na hisia za huruma kwa muathirika wa dhuluma!!
Kwann ulie karibu na uchaguzi kwani wangapi wamebomolewa nyumba na taarifa anazo muda mrefu.Acheni maigizo wajomba.Tunataka kiongozi anayechukua hatua na sio kujitolesha machozi kwenye kamera.Tangu tule ubuyu na uji akili zimeanza kurudi
 
Ukiangalia tu tukio Zima unajua ni huruma iliyojaa usanii wa kisiasa. Yaani ni utapeli wa kisiasa mwanzo mwisho. Na ukisikiliza maelezo ya huyo jamaa anayesema kuvunjiwa nyumba ni maneno ya kupangwa Ili kusaka kiki za kisiasa. Nilipoona na simu inapigwa tena na kuwekwa loudspeaker, huku Kuna makamera ya waandishi wa habari, nimejua ni maigizo ya kisiasa kuhadaa wananchi kuwa Kuna utendaji serious.
 
Ukisoma comments za hawa nyumbu kwenye hii post unaona kabisa hawa watu wameshuka sana to the point of hopelessness. Inasikitisha!
 
Ukiangalia tu tukio Zima unajua ni huruma iliyojaa usanii wa kisiasa. Yaani ni utapeli wa kisiasa mwanzo mwisho. Na ukisikiliza maelezo ya huyo jamaa anayesema kuvunjiwa nyumba ni maneno ya kupangwa Ili kusaka kiki za kisiasa. Nilipoona na simu inapigwa tena na kuwekwa loudspeaker, huku Kuna makamera ya waandishi wa habari, nimejua ni maigizo ya kisiasa kuhadaa wananchi kuwa Kuna utendaji serious.
Braza pole sana,ila hujui ulisemalo,hayo ni mawazo yako tu,ukweli anao muhusika wa tukio!!
 
Back
Top Bottom