Migomo Kariakoo: Serikali kuendelea kulea utamaduni wa kulinda wahalifu utakutokea puani

Migomo Kariakoo: Serikali kuendelea kulea utamaduni wa kulinda wahalifu utakutokea puani

Mapato ya idara ya forodha yanaweza kuwa mara 10 ya yanayopatikana sasa..

Kuna mizigo mingi inaingizwa na syndicate na kuonyesha inapita kwenda nchi jirani na kutolipa kodi (Transit imports) inaishia kubaki humu Kwa maafisa wachache kupewa sehemu ya kodi..Nyaraka kugongwa mipakani kuonyesha mizigo imevuka..

Mtandao ni mkubwa mnoo na unajulikana..Taarifa zipo..Kodi zinaliwa na kutafuna na wachache..
 
Hao ni kucheza nao hivyo hivyo, wakigoma serikali wanakaa nao chini, wanarudi kufunguwa maduka, simply wapo "bored" tu.

Chalamila kawaambia maneno mazuri sana leo, kawaambia wanogoma watalindwa na serikali na wasiwaingilie wasiogoma nao pia wanalindwa na serikali. Kwa ufuipi kawaambia wanaogoma wagome, wasiogoma wasigome, hasara ni kwa wenye kugoma, watagoma na kodi watalipa.

Tatizo nini, hata mama aingilie haki za watu za kugoma? Wagome tu lakini wasitishe au kulazimisha wasiotaka kugoma.

Kwa mama, ukitaka kugoma, goma, utasikiliswa, ukitaka kufanya maandamano fanya utasikilizwa.

Hivi maandamano yua chadomo yameishia wapi? Si unaona falsafa ya maa ya kuwawachia wafanye maandamano, kila mtu kabaki shwari.

Mama Samia apewe hongera sana kwa mageuzi ya uongozi anayoyafanya.
Aisee umerudi! sasa uko na mama wakati ule alikuwa na Magu! Hivi umeshajiuliza kodi kubwa kubwa na mikopo mingi kuliko mapato ya kodi vinaendaga wapi? Unafuatilia suala na Mpina - Bashe saga? Au wewe ni team praises tu? Ulisema lolote kuhusu bandari zetu? Mbuga zetu je? misitu ya blue carbon je?
Ulimuunga mkono yule muovu JPM Allah akamuwahi sasa huyu Bi kzmkz wamtakiani wewe mdada?
 
Aisee umerudi! sasa uko na mama wakati ule alikuwa na Magu! Hivi umeshajiuliza kodi kubwa kubwa na mikopo mingi kuliko mapato ya kodi vinaendaga wapi? Unafuatilia suala na Mpina - Bashe saga? Au wewe ni team praises tu? Ulisema lolote kuhusu bandari zetu? Mbuga zetu je? misitu ya blue carbon je?
Ulimuunga mkono yule muovu JPM Allah akamuwahi sasa huyu Bi kzmkz wamtakiani wewe mdada?
Kama huzioni hpspitali mpya, huzioni barabra mpya, huioni reli mpya, huoni madarasa mapya, huoni ndege mpya, huoni viwanja vipya vya michezo, huoni mikopo mipya ya wanafunzi wa vyuo vikuu, huoni maandamano mapya ya chadomo? Huoni masoko mapya? Huoni viwanda vipya? Huoni umeme mpya?

Kama huyaoni yote hayo basi hata kusikia husikii?
 
Kwa mabadilishano na raslimali zetu kuu? Bandari zetu zote!, Misitu yetu yote, mbuga zetu kwa kiasi cha kufurusha raia kama digdig? Na matozo juu pamoja na hongo za pikipiki zenye gharama ya 54000,000,000 TAS? Na kuwalinda majambazi kama bashe? Na kashfa zote za repoti za CAG? Tunaongozwa na majambazi! jambazi mkuu akitokea kizmkaz! ATAFURUSHWA tu kama tukishindwa Allah atafanya yake tu!
Kama huzioni hpspitali mpya, huzioni barabra mpya, huioni reli mpya, huoni madarasa mapya, huoni ndege mpya, huoni viwanja vipya vya michezo, huoni mikopo mipya ya wanafunzi wa vyuo vikuu, huoni maandamano mapya ya chadomo? Huoni masoko mapya? Huoni viwanda vipya? Huoni umeme mpya?

Kama huyaoni yote hayo basi hata kusikia husikii
 
Kwa Mtazamo wangu

TATIZO LA KARIAKOO NI ZAIDI YA WAFANYABIASHARA,WACHUUZI..LETS BE SERIOUS.

Tatizo la kariakoo haliwezi Kwisha ikiwa total supply chain ya mizigo inayouzwa kariakoo isiporekebishwa au kudhibitiwa kupitia maamuzi magumu na kutooneana haya wala aibu..

Bidhaa nyingi zinazouzwa kkoo zinaingizwa (Imported) toka China,India,Uturuki,Thailand,Vietnam,Zambia,Uganda,etc..Mfumo wa uingizaji na ulipiaji kodi wa mizigo husika ndio mzizi wa shida na tatizo lililopo na litakalokuwepo..

Cartel inayoratibu Logistics na supply chain ya mizigo ya wafanyabiashara wa karikoo isipodhibitiwa kila nyakati tutaona fukuto na migomo isiyohitaji siasa Bali utashi wa maamuzi magumu kudhibiti wahujumu uchumi tunaowalinda..

Mathalani,Mfanyabiashara akiagiza mzigo wa viatu Kwa kontena na kulipa ushuru stahiki kisha kuwa na nyaraka zote Za kikodi (Import duties,Port charges,Wharfage,VAT) inamgharimu milioni 45….NOTE:- Ila akiagiza mzigo huo huo kwa kutumia Logistics Cartels inamgharimu Milioni 15 tu pasipo nyaraka zozote lakini Ana uhakika wa kufikishiwa mzigo dukani au warehouse kwake pasipo usumbufu..

Sasa wale wafanyabiashara waliokuwa wakikomaa na kufuata taratibu stahiki wamejikuta wakishindwa kushindana ktk soko na kufirisika ama kufa kibiashara sababu ya ughali wa bidhaa dhidi ya wale wanaotumia Logistics Mafia..

On the other hand wanaotumia huduma za logistics cartel au mafia inawawia Vigumu sana kufanya compliance za kikodi sababu ya kukosa nyaraka muhimu kussuport mapana ya stock zao..Mauzo yao,returns zao..Hapa ndio kwenye shidaa haswaa…Wengi wana stock kubwa kuliko vielelezo vya manunuzi ya stock husika..Wamegeuka wachuuzi..Wanaouza ambacho hawana nyaraka Za wametoa wapi..SHIDA.

Logistics Cartel/Supply chain Mafia:-Ni kundi hatari lenye nguvu kupitia wanasiasa wakubwa waliopo na wastaafu..Wana ukwasi mkubwa na umaarufu mkubwa ktk Kiwango cha kuogopeka na Wakubwa wa TRA,Polisi,Etc..Wana nguvu mnooo ya kufanya wakubwa ktk mamlaka Za kodi watumbuliwe,Wafanyakazi wahamishwe,Wawe demoted..Wapate Stroke..Nina hakika hata CG wa TRA anawaogopa..Hana la kuwafanya..Inasemekana baadhi ya viongozi ni marafiki wakubwa..

Cartels hizi zimehodhi Supply chain Za uagizaji bidhaa,usafirishaji,Ulipaji kodi,Udanganyifu (under declaration&Falsa Declarations),Uzungushaji mizigo (Taarifa Za kampuni Za tracking devices Za mizigo ya transit zina mengi)..Wanamiriki makampuni ya uagizaji,Usafirishaji,Bonded Warehouses,ICD’s,CFS..yaani acha tu..

Kwa hakika tunapoteza kodi nyingi sana zinazoingia mifukoni mwa wachache tunaowaimbia mapambio ya utajiri na ubilionea huku wachache wakikamuliwa hata kuzirai kibiashara..Bila maamuzi magumu na dhabiti tutaendelea kukwama na kuumiza wasiostahili..

Tukiamua Tunaweza..Viongozi wenye dhamana Simameni kwenye haki na ukweli..
Silent Ocean
 
Serikali imeendelea kupuuza hoja za wafanya biashara walizo zitoa na hii itapelekea mgomo mwezi ujao kua mkali zaidi kuliko hivi sasa
 
Back
Top Bottom