Miguel Gamond ni kocha aliyekuja kuvuruga maana halisi ya "kikosi kipana"

Miguel Gamond ni kocha aliyekuja kuvuruga maana halisi ya "kikosi kipana"

Mashabiki siku zote hawaeleweki wanataka nini

Kipindi mnapigwa na Ihefu unakumbuka lawama zilikuwa kuhusu nini?

Wengi mlimshukia Kocha kwa kufanya rotation ya kikosi kwa kuwaweka benchi wachezaji wenu mnao wapenda.

Leo kocha anaweka hao wachezaji wenu mnao wapenda ambao mna amini ndio mhimili wa timu lakini bado mnakuja tena kumpa lawama kwanini hachezeshi wale wachezaji ambao hamkuwataka kwenye mechi ya Ihefu.

Hao ndio Gongowazi
Nakumbuka na sifa akapewa kwamba kwa Gamond kila mchezaji atapata nafasi uwanjani. Wakawahesabu wachezaji wote wameshacheza kasoro Msheri tu. Sifa akapewa za kutosha kuwa kikosi ni kipana Gamond ni bingwa wa rotation. Mechi ya Ihefu ikabadili upepo, Yanga alipofungwa mashabiki wakalalamikia uwepo wa akina Mauya na Sureboy, nk kuwa kocha alikosea kufanya rotation katika mechi ngumu kama ile ya away. Mashabiki wakalalamika, kocha akajifunza kutumia silaha zake zile zile anazoamini ili apate matokeo.

Kocha inawezekana akawa ni muumini mzuri wa rotation, na akili yake pengine ilikuwa inadhani wachezaji wote wa Yanga wanashabihiana kwa uwezo na ubora ila aliyaona kwenye ile mechi akapata funzo.
 
Game ya Medeama Gamondi alitutoa sadaka Max alikua kasha choka pia ana yellow card, kakomaa nae wakati Mudathir yupo bench, Job hii mechi ya tatu ana chomemesha Fred yupo pale bench , Moloko tutamsahau wakati kipindi Nabi yupo hadi Nkane alikua anacheza
Moloko hajakaa sawa kiafya, Moloko umesahau kuwa ndiye super Sub ya Gamond? Aliingia kwenye mechi ya Coastal union na Namungo akaipa Yanga ushindi. Kuhusu Mudathir sijui imekuaje maana moja ya mfumo wake ni Aucho na Mudathir
 
Game ya Yanga na Coastal Union final ya FA alimuingiza Nkane kila mtu akatukana kilicho tokea hakuna alie amini
Nabi alishakaa na wachezaji kwa muda mrefu alishawajua wachezaji wake nje ndani, Gamond alianza kwa fikra za kuamini kuwa wachezaji wote waliopo Yanga ni wazuri na wenye ubora sawa. Kitu ambacho kilimjengea kujiamini kupita kiasi na kuamua leo anaanza na fulani, kesho ana wapanga wengine kabisa. Kilichotokea kwa Ihefu kimemtia uoga kabisa. Kwasasa kocha kawa muoga hakuna kingine zaidi ya hilo.
 
Game ya Medeama Gamondi alitutoa sadaka Max alikua kasha choka pia ana yellow card, kakomaa nae wakati Mudathir yupo bench, Job hii mechi ya tatu ana chomemesha Fred yupo pale bench , Moloko tutamsahau wakati kipindi Nabi yupo hadi Nkane alikua anacheza
Denis nkane saivi kawa kichekesho Cha Yanga so sad.
 
Game ya Medeama Gamondi alitutoa sadaka Max alikua kasha choka pia ana yellow card, kakomaa nae wakati Mudathir yupo bench, Job hii mechi ya tatu ana chomemesha Fred yupo pale bench , Moloko tutamsahau wakati kipindi Nabi yupo hadi Nkane alikua anacheza
Nafikiri Mudathir atarudi kikosini nikwakua kwenye hizi mechi 2 za caf amebadili mfumo kwa kuanza na back 3 lakini akirudi kwenye mfumo wake wa kawaida Muda anarudi kikosini, nafikiri kwenye ligi atarudi kwenye 4,2,3,1
 
Ndiyoo! Kocha Gamondi kaja na Falsafa yake lakini Falsafa yake ni sumu iliyokuja kubomoa/ kuharibu kikosi kipana kilichotengenezwa na Fundi wa mpira Prof Nabi.

Nabi alitengeneza kitu kinachoitwa "HAKUNA STAR KWENYE TIMU YANGU" na kweli Hilo liliwezekana kila mchezaji aliyepewa nafasi alicheza mpira Kama hatocheza Tena.

Nabi alitengeneza kikosi kipana ikapatikana Rotation ya wachezaji na kweli wachezaji walipumnzika na waliopata nafasi ya kucheza timu ilipata matokeo.

Lakini ujio wa Gamondi umekuja kuchuja na kuchukua wachezaji wake "First eleven" Hii ni sumu kubwa sana maana waliopo benchi hawapati match fitness siku wakipewa namba tutawakataa. Wapo wapi Abubakari Salumu (sureboy), Faridi Musa, Kibwana Shomari n.k

Yanga ya saivi akiumia mchezaji mmoja tu benchi la ufundi linaanza kuumiza kichwa huu ni mfano mzuri alipoumia Lomalisa Mutambala mawazo yalikua mengi lakini enzi za Nabi Faridi Musa na kitasa Kibwana Shomari walicheza vizuri tu.

Maoni Yangu: Gamondi aambiwe ukweli kuwa afanye Rotation ili kunusuru talanta za wachezaji.
Ikifanyika Yanga inaitwa rotation, ila ikifanywa na simba Kocha hana first eleven. Mpaka mseme!
 
Tatizo la Yanga ni kujisahaulisha kwamba timu ilikua ikibebwa na Mayele, yule mwamba mara zote alikua akiibeba Yanga mabegani mwake. Na mara nyingi alipokosekana mayele timu ili-struggle kupata matokeo hivyo jukumu la kuamua mechi lilibakia kwa Feisal feitoto, kwa lugha nyepesi mayele alikuwa akificha madhaifu ya wachezaji wenzie. Now that he's gone, hiyo mnayoita rotation hata ikifanyika itakua ni bure tu kwakuwa Yanga haina kikosi kipana bali imejaza wachezaji wengi ambao ni average.

Ukitaka uelewe nini namaanisha angalia margin ya magoli ambayo yanga ilikuwa ikifunga kipindi cha mayele, karibia kila mechi yanga inashinda goli 1 au 2 na mfungaji mayele itokee sana afunge mtu mwengine.

Kwa sasa kidogo wanajitahidi kugawanya magoli akina Azizi ki, Nzengeli,Pacome wanajaribu kufunga funga magoli. Sasa ukisema uwatoe hao wanao kufungia magoli aingie sureboy na mauya mnataka timu ishuke daraja ?.
 
Mmesahau yule kipa metacha alivyo changia kutupoteza kwenye haya mashindano? Mmesahau kukosekana kwa mwamnyeto siku hiyo kulivyotucost? Mmesahau mechi ya ihefu hao akina mauya na sure boy walivopwaya na kusababisha kipigo? Alafu huyo mudathiri haendani na falsafa ya GAMOND yeye akiwa golini huwa anapiga mashuti hovyo hovyo ambayo huwa yanaenda juu usawa wa paa la mkapa stadium pia huwa anaenda mbele anasahau kurudi kwa wakati kwenye nafasi yake
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mmesahau yule kipa metacha alivyo changia kutupoteza kwenye haya mashindano? Mmesahau kukosekana kwa mwamnyeto siku hiyo kulivyotucost? Mmesahau mechi ya ihefu hao akina mauya na sure boy walivopwaya na kusababisha kipigo? Alafu huyo mudathiri haendani na falsafa ya GAMOND yeye akiwa golini huwa anapiga mashuti hovyo hovyo ambayo huwa yanaenda juu usawa wa paa la mkapa stadium pia huwa anaenda mbele anasahau kurudi kwa wakati kwenye nafasi yake
Wamepwaya kitokana na nini zaidi ya kukosa match Fitness. Anatakiwa arotate watu aache uoga wa kufukuzwa.
 
Winning team never change Guardiola ndio kocha bora duniani kwa sasa ila kwenye team yake akikosekana rodri tu basi inakuwa shida Manchester city hajashinda mechi yoyote ambayo amekosekana uwanjani kachezea kichapa so rodri is a foundation of Manchester city na kila kocha ana foundation yake.
 
Hata ningekuwa mimi Gamondi ningewapiga benchi hivi hivi tu. Tuwe wakweli wachezaji ambao wanapigwa sana benchi hawana uwezo huo wa kuongeza kitu timu inapokuwa inataka matokeo.

Kuendesha timu kwa huruma ndio mwanzo wa kufeli.

Nimshauri tu Hersi atafute masoko ya hawa wakina Mauya,Nkane, Sureboy, Kibwana, Farid,Musonda na Skudu. Mudathir nimemweka kiporo kwa sasa ila nae uwezo wake hauridhishi.

Yanga ya Nabi haikuwahi kucheza vizuri kama hii ya Gamondi, tuache kujisahaulisha.
 
Gamond kweli anakosea, mchezaji kama Mudathir alipaswa awe anacheza mara kwa mara lakini inashangaza hatumiki
 
Kila Mwalimu na falsafa yake gamondi apewe muda tatizo lililopo Hana striker wa kumalizia mchezo nabi alikuwa na striker na karibu asilimia 96 ya mechi zote za nabi ,mayele hakupumzika .
Yanga inatengeneza nafasi nyingi sana za kufunga lakini kina mzize ,Musonda hawazitumii ipasavyo .
Na kumbuka msimu wa kwanza champions league Nabi alitolewa mwanzoni kabisa .
Yaani wewe nae lipumbavu kweli, striker wa nini na hapa tunaongelea rotation ya wachezaji, kocha analeta matabaka kwenye team, watu hata sub hawapewi, wewe na kocha wote wapumbavu.
 
Back
Top Bottom