Miili ya watu wawili na kichwa kimoja vyakutwa hifadhi ya Ruaha

Miili ya watu wawili na kichwa kimoja vyakutwa hifadhi ya Ruaha

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Miili ya watu wawili na kichwa kimoja vimekutwa kwenye eneo la hifadhi ya Taifa ya Ruaha Wilayani Mbarali mkoani Mbeya jana Jumatatu Aprili 27, 2021 huku vikiwa vimeharibika.

Taarifa za vifo hivyo zilitolewa na baadhi ya wanavijiji waliodai kukimbia askari wa wanyamapori waliokuwa wakiwafukuza katika hifadhi hiyo juzi.

Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Urlich Matei amethibitisha kukutwa kwa miili na kichwa hicho jana Jumatatu April 26, 2021 na kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi.

Akizungumza na Mwananchi leo April 27,2021 Matei amesema kuwa kwa sasa bado polisi wanandelea na ufuatiliaji wa tukio hilo ili kujua sababu ya vifo hivyo kama ni kutokana na maji ya mvua au mauaji.

"Polisi tangu jana wako huko tunaendelea kufuatilia sababu vya vifo hivyo kwani mvua zinaendelea kunyesha pamoja na kuendelea kutafuta watu wengine wanaosadikika kutoweka kwenye familia zao," amesema RPC Matei.

Awali Mwenyekiti wa CCM, Kata ya Isisi ya kichama wilayani humo, Thobias Mjengwa ameiambia Mwanachi kwa njia ya simu kuwa mbali ya kupatikana kwa miili hiyo na kichwa bado kuna familia zinadai ndugu zao wanne kutoonekana kwa muda wa siku kadhaa.

"Mimi nimekwenda kushuhudia tukio hilo ni nilishiriki kuwatafuta watu ambao wanasadikika kupoteza maisha na tulianza kuwatafuta baada ya kupata taarifa za watu kukamatwa eneo la hifadhi nawaliofanikiwa kukimbia kutoka eneo la hifadhini,” amsema Mjengwa.
 
Akizungumza na Mwananchi leo April 27,2021 Matei amesema kuwa kwa sasa bado polisi wanandelea na ufuatiliaji wa tukio hilo ili kujua sababu ya vifo hivyo kama ni kutokana na maji ya mvua au mauaji.

"Polisi tangu jana wako huko tunaendelea kufuatilia sababu vya vifo hivyo kwani mvua zinaendelea kunyesha pamoja na kuendelea kutafuta watu wengine wanaosadikika kutoweka kwenye familia zao," amesema RPC Matei.
Majibu wa polisi wetu siku zote yapo shallow sana, mvua za siku hizi zinakata watu shingo
 
Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Urlich Matei amethibitisha kukutwa kwa miili na kichwa hicho jana Jumatatu April 26, 2021 na kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi.

Akizungumza na Mwananchi leo April 27,2021 Matei amesema kuwa kwa sasa bado polisi wanandelea na ufuatiliaji wa tukio hilo ili kujua sababu ya vifo hivyo kama ni kutokana na maji ya mvua au mauaji.
 
Makauzu sana
Wako vile maana
Na wao wanafanyiwa
Kichizi

Ova
Hahahaaa kuna siku nilikua nalewa na jamaa zangu kadhaa vitalu vya kuwinda huko mara simu upepo msako ukaanza na kadrone

Walimkamata mtu ana kindoo cha Lita 20 kimejaa risasi na mjegejo wa haja

Wakawa wananiambia ndomaana inabidi tuwe kauzu humu yani majangiri wamejizira sana usipowafanyia unyama wanakufanyia unyama(Rules of the jungle ndo zinatawala)
 
Hahahaha wale askari walinda mbuga usiombe ukutane nao porini kwenye mazingira ya kijangiri. Ni heri ukutane na simba
Maliasili wale jamaa ni wauwaji. Kuliko uingie anga zao ni kweli mkuu bora ukutane na mkubwa wa pori tu unaweza ukajitetea.

Kuna jamaa walipigwa kwa kukutwa na nyama ya pofu wakala kichapo kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 2 usiku halafu wakaachiwa wakaambiwa ondokeni.

Hawakuweza kuondoka hata kusimama hawawezi maana jamaa waliwapiga na vikwata (miba fulani ya porini) kwenye unyayo. Kuna mzee mmoja alikuwa mwiongoni mwao alipigwa mpaka nerves za harufu zikafa yani yeye huwa nahusi harufu yoyote mpaka leo.

Jamaa mwingi alikamatwa amewinda kanga wakamwambia awale na manyoya yake hivyo hivyo jamaa alikula ila alikufa.

Kuna siku niko pori moja Simanjiro jamaa wakawa wametega kanga tukawa tunapika kwenye camp tuliona gari inakuja kwa mbali kuelekea camp yetu aseee tulikimbia maporini yani speed hatari kumbe hawakuwa maliasili ilikuwa jamaa wa kambi ya jirani katoka town.

Yani mimi nikiwa mahali halafu kuna nyara hizi za hata mfupa wa mnyama pori sikai hapo maana jamaa hata wakikuta mfupa wa mwaka juzi lazima wakufanye vibaya. Yani hata wakute manyoya ya njiwa pori au hata ndege utaisoma namba.

Hao watu sio binadamu wakawaida.
 
Maliasili wale jamaa ni wauwaji. Kuliko uingie anga zao ni kweli mkuu bora ukutane na mkubwa wa pori tu unaweza ukajitetea.

Kuna jamaa walipigwa kwa kukutwa na nyama ya pofu wakala kichapo kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 2 usiku halafu wakaachiwa wakaambiwa ondokeni.

Hawakuweza kuondoka hata kusimama hawawezi maana jamaa waliwapiga na vikwata (miba fulani ya porini) kwenye unyayo. Kuna mzee mmoja alikuwa mwiongoni mwao alipigwa mpaka nerves za harufu zikafa yani yeye huwa nahusi harufu yoyote mpaka leo.

Jamaa mwingi alikamatwa amewinda kanga wakamwambia awale na manyoya yake hivyo hivyo jamaa alikula ila alikufa.

Kuna siku niko pori moja Simanjiro jamaa wakawa wametega kanga tukawa tunapika kwenye camp tuliona gari inakuja kwa mbali kuelekea camp yetu aseee tulikimbia maporini yani speed hatari kumbe hawakuwa maliasili ilikuwa jamaa wa kambi ya jirani katoka town.

Yani mimi nikiwa mahali halafu kuna nyara hizi za hata mfupa wa mnyama pori sikai hapo maana jamaa hata wakikuta mfupa wa mwaka juzi lazima wakufanye vibaya. Yani hata wakute manyoya ya njiwa pori au hata ndege utaisoma namba.

Hao watu sio binadamu wakawaida.
Duuh nimeshindwa kumaliza kusoma, huu ni zaidi ya unyama[emoji24][emoji24][emoji24]
 
Back
Top Bottom