Mikanganyiko katika Biblia ni kigezo kinachowapa watu uhalali wa kusema hakuna Mungu

Mikanganyiko katika Biblia ni kigezo kinachowapa watu uhalali wa kusema hakuna Mungu

Bado haujajibu swali ulitaka dunia iweje na binadamu tuweje ili ndo uamini kuwa mungu yupo
Unaamini vipi kitu hakipo, na hicho ambacho ngozi nyeupe kakuletea kina mashaka na kinajichanganya Sana, yaani ni kiumbe Fulani katili sana
 
Nimekujibu ndugu yangu, labda Kama sijaeleweka nimesema hivi mimi na wewe tunaimani tofauti, sasa siwezi zungumzia kwa upande wako, ila kwangu Mungu ninayemwabudu Mimi ni mkamilifu(perfect) ila wako siwezi mjibia wewe ndiye unayemjua ni perfect au siyo perfect. Kwahiyo si kweli kwamba Mungu perfect hayupo
Ndio maana nilikuuliza unakubali mungu wako ni perfect ila hajaumba viumbe perfect? Yaani kitu unachokiita perfect kimeshindwa kuunda kitu perfect huo uperfect unatokea wapi?
 
Swali zuri.

Kwa sababu, kwanza, maendeleo yanaendana na utashi wa watu. Hutakiwi kujichukulia wewe unachoona ni maendeleo kuwa ndicho maendeleo.

Kwa mfano, maendeleo ni lazima yaje na uhuru wa kujichagulia. Maendeleo bila uhuru wa kujichagulia ni utumwa. Sasa utawaleteaje maendeleo, kwa mfano uwajengee majumba ya maghorofa na viwanda, watu ambao nia yao ni kukaa kwenye vibanda vyao vya asili na kilimo chao cha asili?

Mwalimu Nyerere alienda Umoja wa Mataifa mwaka 1959 katika harakati za kudai uhuru. Akawa anahojiwa katika TV show moja, show ya Mama Roosevelt New York City. Video ipo Youtube. Katika ile show, Nyerere aliulizwa, wewe unataka watu wako wapewe uhuru mjitawale, lakini mbona nyie watu kama hamjafikia uwezo wa kujiendesha nchi bado? Hamna wasomi wa kutosha, hamna ujuzi wa kuendesha nchi kisasa etc. Nyerere akawajibu kifalsafa sana, kwa mfano. Akasema, ukimkuta mtu kavaa koti lake, ukamnyang'anya, ukasema hili koti hujui kuvaa, kwanza kubwa halikutoshi, nipe mimi. Baada ya muda yule mtu akaja kudai koti lake, akisema sijali kama koti kubwa, sijali kama koti halinitoshi, najali kwamba koti ni langu, nipe mwenyewe koti langu nivae.

Nyerere alikuwa anaongelea haki ya self determination, kwamba, whether mtu anajua kuutumia uhuru wake si hoja, hoja ni kwamba uhuru ni wake apewe.

Wewe unachosema ni kama kile alichoulizwa Nyerere, unasema hawa watu wanyang'anywe makoti, kwa sababu si size yao, hawajui kuvaa. Tuwafundishe. Lakini labda unavyopenda wewe si wanavyooenda wao.

The transcripts and video of the Nyerere Interview are available here

Kwa mantiki hiyo ya uhuru wa kujichagulia. Kwanini basi uchawi , uganga wa jadi, kupiga ramli,arbotion kunakatazwa na dini ndo ionekane ni spesho,kwamba watu wana uhuru wa kujichagulia na si hivo vingine?
 
Kama ana uwezo wa kuona dhambi utakazofanya ukiwa duniani na bado akakuumba halafu baada kifo ukaenda motoni, maana yake Mungu/Allah alimuumba ili akuchome Moto, maana toka anakuumba alijua mwisho wako ni motoni
Mungu alituumba ili tuje TUMUABUDU.na si vinginevyo
 
Kwa hyo unataka kusema hakuna binadamu wa kwanza?
Binadamu wa kwanza Hayupo.

Ndio maana Duniani kuna binadamu wenye rangi tofauti na DNA 🧬 tofauti.

Binadamu tuna Genes tofauti.

Kuna waafrika weusi, wazungu weupe, wahindi weusi, wahindi weupe n.k na tuko na utofauti mkubwa sana wa miili yetu kwenye ku adapt mazingira na mifumo yake.

Sasa huwezi kusema kwamba kuna binadamu wa kwanza kwenye dunia iliyo jaa binadamu wengi wenye utofauti.

Kama binadamu wa kwanza angekuwepo, Binadamu wote tungekuwa wa aina moja tu kufuata Genes za huyo Binadamu wa kwanza.
 
Kama Mungu aliumba binadamu wote tuje tumwabudu na si vinginevyo, Mbona sisi Atheists hatumwabudu?

Au Mungu huyo haku tuumba?

Au sisi Atheists au mimi infropreneur sio binadamu?
Sasa kama unakaza future unataka akushikie bakora?si utakufa utakwenda kuonana nae
 
Binadamu wa kwanza Hayupo.

Ndio maana Duniani kuna binadamu wenye rangi tofauti na DNA 🧬 tofauti.

Binadamu tuna Genes tofauti.

Kuna waafrika weusi, wazungu weupe, wahindi weusi, wahindi weupe n.k na tuko na utofauti mkubwa sana wa miili yetu kwenye ku adapt mazingira na mifumo yake.

Sasa huwezi kusema kwamba kuna binadamu wa kwanza kwenye dunia iliyo jaa binadamu wengi wenye utofauti.

Kama binadamu wa kwanza angekuwepo, Binadamu wote tungekuwa wa aina moja tu kufuata Genes za huyo Binadamu wa kwanza.
Sasa binadamu tumetoka wapi?
 
Kama Mungu aliumba binadamu wote tuje tumwabudu na si vinginevyo, Mbona sisi Atheists hatumwabudu?

Au Mungu huyo haku tuumba?

Au sisi Atheists au mimi infropreneur sio binadamu?
Ukishakubali wewe ni binadamu afu ukapinga uwepo wa abrahamac god unakuwa unafanya contradiction. Nje ya propaganda za abrahamac god hakuna binadamu bali kuna watu.According to abrahamac fairy tales Adamu ni binadamu wa kwanza na waliofuata nyuma yake wanaitwa binadamu.
 
Kwa mantiki hiyo ya uhuru wa kujichagulia. Kwanini basi uchawi , uganga wa jadi, kupiga ramli kunakatazwa na dini ndo ionekane ni spesho,kwamba watu wana uhuru wa kujichagulia na si hivo vingine?
Wewe unaipinga dini, kwa nini unaifanya dini bado iwe dira yako? Kwa nini unaiga inachofanya dini wakati wewe unataka kutoka kwenye dunia ya dini?

Kwa nini unaicopy dini kwamba dini inapinga wasioamini, na wewe ambaye huamini unapinga dini?

Huoni mpaka hapo unakuwa bado unaifanya dini ikupangie maisha yako, badala ya kujitungia mfumo mwingine wa maisha?

Watu wengine tuliotoka kwenye dini hatusumbuliwi na waamini dini. Tunawaachia uhuru wao kwenye imani, ingawa tukija kwenye facts tuna wa set straight.

Kuhusu swali lako, wachawi, waganga wa jadi, kupiga ramli zote hizo ni imani tu, na as long as hawamdhuru mtu, waachiwe tu watimize imani zao, na hivyo ndivyo mtu asiyeamini dini kama mimi anatimiza uhuru wa kuamini wa kila mtu.

Watu wa dini wana haki ya kusema kwamba dini zao haziruhusu mambo hayo, and that is OK. There is nothing special in that. Ila, wewe ukianza kuwaonea gele watu wa dini kwa nini wanaweka mipango yao hivyo, wewe ndiye unawapa u special.

Wewe unaweza kuanzisha jamii yako ya wasioamini, ikasema kwamba waganga wa kienyeji ni watu muhimu katika research za madawa ya asili, hatuwabagui. Tutawa upgrade wafanye mambo kileo na kisayansi zaidi. Umeondoa ubspecial wa watu wa dini hapo. Waganga wa kienyeji kibao watasema hebu tumsikilize huyu mtu hatubagui kama dini zinavyotubagua.
 
Sasa kama huyo Mungu muweza na mwenye nguvu tulieaminishwa kuwa ana nguvu kumbe nae anafanya makosa kama ya kibinadamu, yaani Neno lake alilotuaminisha ni takatifu kumbe limejawa uongo na mikanganyiko, tunawezaje kuthibitisha au kuamini hata uwepo wake sio Uongo?

Ni sawa na kulazimisha maji kupanda mlima, ndivyo hivyo kulazimisha Mungu wa biblia/quran kuwepo wakati hawana vithibitisho.

Biblia/quran sio kithibitisho cha uwepo wa huyo Mungu maana hivyo vitabu havina logic wala ushahidi wa stories zake, pia huwezi kumthibitisha Mungu kupitia hizo ngonjera zake za uongo za vitabu vya dini.

Kuna wale wanaosingizia masuala ya Uumbaji, nipende tu kuwaambia ukweli mchungu, Mungu hausiki na uumbaji wa dunia wala kiumbe chochote dunian wala nje ya dunia, maana kiuhalisia Mungu nae ni kiumbe, je inawezekana kiumbe kuumba kiumbe mwingine?

Someni vizuri hizo ngonjera za vitabu vya dini zenu mtagundua kuwa kumbe hata binadamu akiwa na nguvu ktk jamii yake nae ni Mungu, kiumbe cha kiroho chochote ni Mungu, hata huyo Mungu wa Mbinguni nae ni kiumbe maana anaishi ktk ulimwengu, na sifa kuu ya kiumbe ni kuishi au kuwa covered/kupatikana/existence ktk ulimwengu wa Mwili au Roho.

Haiwezekani muumbaji aishi ktk kitu/ulimwengu aliouumba yeye mwenyewe je kabla hajazifanya hizo mbingu alikuwa wapi? Someni vizuri na mzielewe hizo stories zenu za uongo mtayajua madhaifu mengi ya huyo mnaemuita Mungu.

Narudia tena wanaopinga uwepo wa Mungu wako sahihi na wanaolazimisha uwepo wa Mungu wako sahihi pia maana hata sisi binadamu ni waungu kwa baadhi ya viumbe dhaifu hivyo tunavitawala, na wanaopinga uwepo wa Mungu wako sahihi maana huyo Mungu tulieaminishwa hayuko na wala hatowai kuwepo zaidi ya ngonjera za vitisho.
Dini ni wizi mtupu!!
 
Mimi najua wasio na imani ndo wanaenda motoni. Swali hilo nimekuuliza kutokana na wewe kusema imani haikupeleki mbinguni kwaio nataka nisikie upande wako,Labda una sifa zingine unazozijua ambazo mimi sizijui
na hakuna sehemu nimesema najua kila kitu.
Miongoni mwa sifa soma waebrania 12:14

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
 
Sasa binadamu tumetoka wapi?
Binafsi naweza kusema kwamba,

Binadamu hatuja tokea popote pale.

Binadamu tulikuwepo, tupo na tutaendelea kuwepo.

Kama binadamu hatukuwepo duniani halafu ghafla bin vuuh! tukawepo,
Je huko tulipokuwepo kabla ya kuwepo duniani Kulitoka wapi?

Au kabla ya Mungu kuumba mbingu na Dunia alikuwa wapi?
Na huko alikokuwa kulitoka wapi?

Mkuu hapo kutakuwa na mtiririko wa maswali yasiyo na mwisho wa kila kitu kilitoka wapi?

Hata chanzo, cha chanzo, cha chanzo cha chanzo, cha ulimwengu either ni mungu au anything else, kitakuwa kimetoka wapi?

Hatuwezi kujua tusicho kijua, ila tuna punguza tusivyo vijua kwa kujifunza kadiri muda unavyokwenda.
 
Back
Top Bottom