LwandaMagere
JF-Expert Member
- Mar 15, 2020
- 264
- 2,484
- Thread starter
- #501
MKASA WA PILI - Sehemu ya 5
Inaendelea.............
Kulipokucha ilitubidi tuamke mapem maana tuliambiwa kupata magari ya huko Bukima ilikuwa inatupasa tupitie Musoma mjini ambako ndiko tungepata usafiri,ilibidi tukae barabarani kusubiri Hiace zilizokuwa zinaelekea Musoma,kiukweli mpaka wakati huo mfukoni nilikuwa nina Tsh elfu 48 tu,nauli ya kutoka Bunda kwenda Musoma kwa wakati huo ilikuwa elfu 3 hivyo nilivyolipia naulia ya watu wawili nilibakiwa na elfu 42,basi safari ikaanza na ilituchukua kama saa 1 hadi kufika Musoma.Tulipofika pale stendi ya Musoma hatukutaka kupoteza muda maana tuliambiwa huwa kuna gari moja la kuelekea huko Bukima,endapo tungelikosa hilo gari ingetubidi tulale!,kuna basi moja tulilikuta stendi likiwa limechoka sana!,ilikuwa ni aina fulani ya magari ya zamani,ilibidi sasa nikaulizie nauli ya kuelekea huko Bukima ilikuwa ni kiasi gani,tulimkuta mtu mmoja ambaye alijinasibu kwamba ndiye Konda wa lile gari,akatuambia nauli ya kutoka Musoma mpaka huko tulipo kuwa tunaenda ni elfu 5,ila huyo konda akatuambia hilo gari litaishia njiani,akasema kuna kijiji kinaitwa Mrangi ndiyo wao wangeishia hapo,ilibidi nimuulize kutoka hapo Mrangi mpaka Bukima kulikuwa na umbali gani?.
Jamaa alisema hakukuwa mbali sana,alituambia tungefika Mrangi angefanya namna ili sisi tuendelee na safari,jamaa alisisitiza sana kwamba kwa wakati huo pale stendi hakukuwa na gari lingine la kuelekea huko Bukima,hivyo tupande lile gari kisha tungefika Mrangi angetutafutia usafiri wa kuelekea Bukima.Basi nilitoa elfu 10 nikampa yule konda,baada ya kumpa akasema" Gari itaanza safari saa 5 asubuhi hivyo kama mnzunguka nyie zungukeni ila msiende mbali sana!".
Kwakuwa tulitoka Bunda bila kupata chochote kitu nilimwambia dogo twende tukatafute sehemu wanauza chai tunywe.Kwa bahati nzuri tulipozunguka nyuma ya stendi kulikuwa na mama akichoma vitumbua,hivyo tulikaa hapo tukaagiza na chai tukaanza kunywa!,wakati huo mfukoni nilibaki na elfu 30.Hapo kwenye chai tulitumia elfu 2,baada ya kupata chai na vitumbua nikamwambia dogo tusikae sana mbali maana hatukuwa wenyeji hapo Musoma,Masaa yaliposogea ilibidi na sisi tusogee kwenye gari na baada ya muda ule aliyotuambia konda kufika gari lilianza kuondoka,watu walikuwa wengi kwenye gari na wengine walisimama,yawezekana uenda gari lilikuwa lile tu maana yangekuwepo mengi watu wasingesimama na kubanana kiasi kile.Ilikuwa ni safari ya muda mrefu sana,Kuna jamaa alikuwa amesimama kando yangu nilimuuliza hiyo safari huwa inachukua muda gani hadi kufika,jamaa aliniambia kwamba,kwasababu lile gari lilikuwa likisimama simama sana njiani,ingetuchukua takribani saa 2 : 30 hadi kufika hapo Murangi.Baada ya saa 3 njiani,hatimaye lile gari lilifika hapo Murangi,tuliteremka nikamfuata dereva nikamueleza kwamba sisi tulikuwa tunaenda Bukima na yule jamaa aliyekuwa anakata tikiti alituambia tukifika hapo angetufanyia namna ya kufika huko Bukima.
Yule dereva alisikitika sana akawa anasema"Yule jamaa ni mpumbavu,kwanini akuwaambia kwamba kulikuwa na Hiace ya Bukima?".
Jamaa akaendelea kusema "Maana kutoka hapa mpaka Bukima bado kuna umbali,lakini subirini kuna watu hapa niongee nao huwa wanakodisha baiskeli kama vipi wawapeleke,japo itachukua muda kwasababu ni mbali".
Jamaa alituitia vijana wawili akaanza kuongea nao kwa lugha ya kwao,wale jamaa wakamwambia yule dereva kwa kilugha kwamba tuwalipe elfu 5 wote wawili!,hatukuwa na namna ilibidi niwape ile hela wakatuchukua mimi na dogo kila mmoja kwenye baiskeli yake na safari ikaanza,hiyo ilikuwa yapata saa 9 alasiri,safari ilikuwa ndefu kidogo na tuliingia hapo Bukima mnamo saa 10 kasoro.Tulivyofika hapo Bukima hatukupoteza muda,ilibidi sasa tuanze kumuulizia yule mganga tuliyeelekezwa na yule mzee wa Bunda,Kwa bahati nzuri huyo mganga hakuwa mgeni sana hapo Bukima,tulianza safari ya kuelekea kwake tukiongozwa na dogo mmoja tuliyemkuta pale center ya Bukima,Kwa kuwa tulikuwa wageni watu walikuwa wakitushangaa sana,nadhani kwakuwa ilikuwa mji mdogo hivyo watu au wenyeji wengi walikuwa wakifahamiana,hivyo kwa wageni ilikuwa ni rahisi sana kufahamika!.Tulifanikiwa kufika kwa huyo mganga,alikuwa akiishi nje ya mji na ilikuwa karibu na ziwa Victoria,ulikuwa ukikaa nje ya nyumba ya huyo mzee,ziwa lilionekana umbali wa mita 300 hivi!,tulimsalimia mzee na tukajitambulisha kwake,tulimueleza ya kwamba tuliagizwa kwake na mzee yule wa Bunda,kiukweli alionyesha kumfahamu yule mzee na alikuwa akituuliza hali ya maisha yake na familia yake.
Baada ya mazungumzo kadhaa ilibidi tumueleze kilichokuwa kimetupeleka hapo kwake.Baada ya kutusikiliza kwa muda mrefu alituambia ya kwamba kuna watu fulani waliwahi kwenda hapo kwake miaka 2 iliyopita na wao walikuwa wakitafuta zile pesa zilizokuwa na tundu katikati,kwakuwa kwa wakati huo alikuwa nazo ilibidi awape na walimpa pesa,alituuliza endapo hiyo sarafu ya 100 ya mwaka 1993 ingepatikana tungempa kiasi gani?,kiukweli moyo ulipiga Paaah!,kichwani mwangu nilikuwa naamini ya kwamba sasa naenda kuuaga umasikini na utajiri ulikuwa ushafika mlangoni,kazi iliyokuwepo ni kufungua tu mlango uingie ndani!.
Nilimwambia mzee endapo tungeipata ile sarafu,basi tungempa laki 2,Yeye alituuliza "Nyinyi mkiipata mnaenda kupata bei gani?".
Ilibidi nimdanganye Yule mzee kwamba "Sisi tumeambiwa tukiipeleka hiyo sarafu tunalipwa milioni 1, hivyo endapo tukikup wewe hiyo laki 2,sisi tungebaki na laki 8 ambayo tutagawana na mwenzangu maana kuna gharama pia zimetumika mpaka kufika hapa kwako".
Basi yule mzee alisema funguo za Sanduku ambamo zimo hela mbalimbali za miaka ya nyuma anazo mke wake ambaye kwa wakati ule hakuwepo,alituambia tumsubiri mpaka atakareje na akatusihi ya kwamba kwakuwa jioni ilishaingia hatuna budi tulale pale,basi mimi na dogo ilibidi twende ziwani tukashangae huku tukibadilisha mawazo,ilipofika saa 12 jioni tulirudi hapo nyumbani kwa huyo mzee,siku hiyo yule mzee alichinja Bata kwa ajili ya kitoweo!.Yule mzee kiukweli sikuona uganga wowote aliyokuwa nao maana hata pale kwake hatukukuta watu bali walikuwa watu wa familia yake!,nadhani kama alikuwa mganga basi ni wale wasiyokuwa na mbwembwe nyingi.Jioni ile mkewe alirudi akiwa na baiskeli kafunga mzigo nyuma,alipokewa na kijana wake mmoja tuliyemkuta pale,Kwakuwa sasa usiku ulishaingia mzee alituambia zoezi lingefanyika kesho yake asubuhi.
Usiku ule tulikula ugali wa muhogo na nyama ya Bata,kiukweli chakula kile kilikuwa kitamu sana!,baada ya chakula ilibidi kile chumba alichokuwa analala yule kijana wa yule mzee tulale sisi na yeye nadhani alienda kulala kwa jirani au marafiki zake,Kama mjuavyo tena mambo ya vijijini,suala la wapi pa kulala huwaga halisumbui,Siyo kama mjini.
Itaendelea...................
Inaendelea.............
Kulipokucha ilitubidi tuamke mapem maana tuliambiwa kupata magari ya huko Bukima ilikuwa inatupasa tupitie Musoma mjini ambako ndiko tungepata usafiri,ilibidi tukae barabarani kusubiri Hiace zilizokuwa zinaelekea Musoma,kiukweli mpaka wakati huo mfukoni nilikuwa nina Tsh elfu 48 tu,nauli ya kutoka Bunda kwenda Musoma kwa wakati huo ilikuwa elfu 3 hivyo nilivyolipia naulia ya watu wawili nilibakiwa na elfu 42,basi safari ikaanza na ilituchukua kama saa 1 hadi kufika Musoma.Tulipofika pale stendi ya Musoma hatukutaka kupoteza muda maana tuliambiwa huwa kuna gari moja la kuelekea huko Bukima,endapo tungelikosa hilo gari ingetubidi tulale!,kuna basi moja tulilikuta stendi likiwa limechoka sana!,ilikuwa ni aina fulani ya magari ya zamani,ilibidi sasa nikaulizie nauli ya kuelekea huko Bukima ilikuwa ni kiasi gani,tulimkuta mtu mmoja ambaye alijinasibu kwamba ndiye Konda wa lile gari,akatuambia nauli ya kutoka Musoma mpaka huko tulipo kuwa tunaenda ni elfu 5,ila huyo konda akatuambia hilo gari litaishia njiani,akasema kuna kijiji kinaitwa Mrangi ndiyo wao wangeishia hapo,ilibidi nimuulize kutoka hapo Mrangi mpaka Bukima kulikuwa na umbali gani?.
Jamaa alisema hakukuwa mbali sana,alituambia tungefika Mrangi angefanya namna ili sisi tuendelee na safari,jamaa alisisitiza sana kwamba kwa wakati huo pale stendi hakukuwa na gari lingine la kuelekea huko Bukima,hivyo tupande lile gari kisha tungefika Mrangi angetutafutia usafiri wa kuelekea Bukima.Basi nilitoa elfu 10 nikampa yule konda,baada ya kumpa akasema" Gari itaanza safari saa 5 asubuhi hivyo kama mnzunguka nyie zungukeni ila msiende mbali sana!".
Kwakuwa tulitoka Bunda bila kupata chochote kitu nilimwambia dogo twende tukatafute sehemu wanauza chai tunywe.Kwa bahati nzuri tulipozunguka nyuma ya stendi kulikuwa na mama akichoma vitumbua,hivyo tulikaa hapo tukaagiza na chai tukaanza kunywa!,wakati huo mfukoni nilibaki na elfu 30.Hapo kwenye chai tulitumia elfu 2,baada ya kupata chai na vitumbua nikamwambia dogo tusikae sana mbali maana hatukuwa wenyeji hapo Musoma,Masaa yaliposogea ilibidi na sisi tusogee kwenye gari na baada ya muda ule aliyotuambia konda kufika gari lilianza kuondoka,watu walikuwa wengi kwenye gari na wengine walisimama,yawezekana uenda gari lilikuwa lile tu maana yangekuwepo mengi watu wasingesimama na kubanana kiasi kile.Ilikuwa ni safari ya muda mrefu sana,Kuna jamaa alikuwa amesimama kando yangu nilimuuliza hiyo safari huwa inachukua muda gani hadi kufika,jamaa aliniambia kwamba,kwasababu lile gari lilikuwa likisimama simama sana njiani,ingetuchukua takribani saa 2 : 30 hadi kufika hapo Murangi.Baada ya saa 3 njiani,hatimaye lile gari lilifika hapo Murangi,tuliteremka nikamfuata dereva nikamueleza kwamba sisi tulikuwa tunaenda Bukima na yule jamaa aliyekuwa anakata tikiti alituambia tukifika hapo angetufanyia namna ya kufika huko Bukima.
Yule dereva alisikitika sana akawa anasema"Yule jamaa ni mpumbavu,kwanini akuwaambia kwamba kulikuwa na Hiace ya Bukima?".
Jamaa akaendelea kusema "Maana kutoka hapa mpaka Bukima bado kuna umbali,lakini subirini kuna watu hapa niongee nao huwa wanakodisha baiskeli kama vipi wawapeleke,japo itachukua muda kwasababu ni mbali".
Jamaa alituitia vijana wawili akaanza kuongea nao kwa lugha ya kwao,wale jamaa wakamwambia yule dereva kwa kilugha kwamba tuwalipe elfu 5 wote wawili!,hatukuwa na namna ilibidi niwape ile hela wakatuchukua mimi na dogo kila mmoja kwenye baiskeli yake na safari ikaanza,hiyo ilikuwa yapata saa 9 alasiri,safari ilikuwa ndefu kidogo na tuliingia hapo Bukima mnamo saa 10 kasoro.Tulivyofika hapo Bukima hatukupoteza muda,ilibidi sasa tuanze kumuulizia yule mganga tuliyeelekezwa na yule mzee wa Bunda,Kwa bahati nzuri huyo mganga hakuwa mgeni sana hapo Bukima,tulianza safari ya kuelekea kwake tukiongozwa na dogo mmoja tuliyemkuta pale center ya Bukima,Kwa kuwa tulikuwa wageni watu walikuwa wakitushangaa sana,nadhani kwakuwa ilikuwa mji mdogo hivyo watu au wenyeji wengi walikuwa wakifahamiana,hivyo kwa wageni ilikuwa ni rahisi sana kufahamika!.Tulifanikiwa kufika kwa huyo mganga,alikuwa akiishi nje ya mji na ilikuwa karibu na ziwa Victoria,ulikuwa ukikaa nje ya nyumba ya huyo mzee,ziwa lilionekana umbali wa mita 300 hivi!,tulimsalimia mzee na tukajitambulisha kwake,tulimueleza ya kwamba tuliagizwa kwake na mzee yule wa Bunda,kiukweli alionyesha kumfahamu yule mzee na alikuwa akituuliza hali ya maisha yake na familia yake.
Baada ya mazungumzo kadhaa ilibidi tumueleze kilichokuwa kimetupeleka hapo kwake.Baada ya kutusikiliza kwa muda mrefu alituambia ya kwamba kuna watu fulani waliwahi kwenda hapo kwake miaka 2 iliyopita na wao walikuwa wakitafuta zile pesa zilizokuwa na tundu katikati,kwakuwa kwa wakati huo alikuwa nazo ilibidi awape na walimpa pesa,alituuliza endapo hiyo sarafu ya 100 ya mwaka 1993 ingepatikana tungempa kiasi gani?,kiukweli moyo ulipiga Paaah!,kichwani mwangu nilikuwa naamini ya kwamba sasa naenda kuuaga umasikini na utajiri ulikuwa ushafika mlangoni,kazi iliyokuwepo ni kufungua tu mlango uingie ndani!.
Nilimwambia mzee endapo tungeipata ile sarafu,basi tungempa laki 2,Yeye alituuliza "Nyinyi mkiipata mnaenda kupata bei gani?".
Ilibidi nimdanganye Yule mzee kwamba "Sisi tumeambiwa tukiipeleka hiyo sarafu tunalipwa milioni 1, hivyo endapo tukikup wewe hiyo laki 2,sisi tungebaki na laki 8 ambayo tutagawana na mwenzangu maana kuna gharama pia zimetumika mpaka kufika hapa kwako".
Basi yule mzee alisema funguo za Sanduku ambamo zimo hela mbalimbali za miaka ya nyuma anazo mke wake ambaye kwa wakati ule hakuwepo,alituambia tumsubiri mpaka atakareje na akatusihi ya kwamba kwakuwa jioni ilishaingia hatuna budi tulale pale,basi mimi na dogo ilibidi twende ziwani tukashangae huku tukibadilisha mawazo,ilipofika saa 12 jioni tulirudi hapo nyumbani kwa huyo mzee,siku hiyo yule mzee alichinja Bata kwa ajili ya kitoweo!.Yule mzee kiukweli sikuona uganga wowote aliyokuwa nao maana hata pale kwake hatukukuta watu bali walikuwa watu wa familia yake!,nadhani kama alikuwa mganga basi ni wale wasiyokuwa na mbwembwe nyingi.Jioni ile mkewe alirudi akiwa na baiskeli kafunga mzigo nyuma,alipokewa na kijana wake mmoja tuliyemkuta pale,Kwakuwa sasa usiku ulishaingia mzee alituambia zoezi lingefanyika kesho yake asubuhi.
Usiku ule tulikula ugali wa muhogo na nyama ya Bata,kiukweli chakula kile kilikuwa kitamu sana!,baada ya chakula ilibidi kile chumba alichokuwa analala yule kijana wa yule mzee tulale sisi na yeye nadhani alienda kulala kwa jirani au marafiki zake,Kama mjuavyo tena mambo ya vijijini,suala la wapi pa kulala huwaga halisumbui,Siyo kama mjini.
Itaendelea...................