Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

DAAH hii dunia kuna watu wanapitia magumu
Sio Kama wewe
School bus
English medium school
Chuo Cha magumashi
Kazi ya kutaftiwa NSSF
Kuozeshwa mtoto wa bestie wa mum
Kukabidhiwa gari ....siku ya send off
Kukabidhiwa nyumba..harusi
Halafu unaboa wafanya kazi wenzio na kusumbua wastaafu.
Kifupi huna mchango wowote hapa duniani....
 
Sio Kama wewe
School bus
English medium school
Chuo Cha magumashi
Kazi ya kutaftiwa NSSF
Kuozeshwa mtoto wa bestie wa mum
Kukabidhiwa gari ....siku ya send off
Kukabidhiwa nyumba..harusi
Halafu unaboa wafanya kazi wenzio na kusumbua wastaafu.
Kifupi huna mchango wowote hapa duniani....
🤣🤣🤣Hivi mtu huyu anawezaje kuelewa harakati za kupigania ukombozi toka kwa mkoloni mweusi? Nimecheka sana asee heb chukua 🍺🍺
 
MKASA WA PILI -sehemu ya 6


Inaendelea.............


Asubuhi tuliamka tukaanza kusalimia wenyeji,Mzee alipoamka kumbe alidamka asubuhi na mapema kwenda ziwani kwenye samaki,Kumbe licha ya kuwa mganga kama tulivyoambiwa lakini biashara au kazi nyingine aliyokuwa akiifanya yule mzee ni kulangua samaki na kuwauza kwa wateja mbalimbali!.Kwahiyo ilibidi tumsubiri mpaka atakaporejea kutoka ziwani,asubuhi hiyo tulipoamka tulielekea ziwani kuoga kisha tulirudi hapo nyumbani kwa mzee,kuna binti mmoja wa yule mzee alikuja kutukaribisha twende tukale,mimi nilijua uenda ingekuwa uji maana nilijua watu wa vijijini wao na chai ilikuwa ni mbalimbali!.Baada ya kuingia mle ndani tukakutana na bonge la ugali,Samaki na vipande vya bata kwenye bakuli,yule bata alikuwa ni yule tuliyemla usiku akabaki sasa tulipakuliwa ili tummalizie kabisa!.

Kwanza nilibaki nimeshangaa maana sikuwahi kula Ugali asububi,katika maisha yangu yote nilishazoea kunywa chai au uji,ilibidi nimuulize yule dogo kama alishawahi kula Ugali asubuhi.

Dogo akaniambia "Mbona bro haya mambo ya kawaida sana".

Basi sikuwa na namna ilibidi tulianzishe,kiukweli ule Ugali ulikuwa mtamu sana,japo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza kula ugali asubuhi,nilitamani niendelee kubaki huko ili niwe napikiwa kila asubuhi,kiukweli nilipenda sana maisha ya wale watu.Baada ya kuwa tumemaliza kula tukiwa hapo nje tunapunga upepo,yule mzee alirejea kutoka huko ziwani kwenye biashara zake za samaki,na yeye kama kawaida alitengewa chakula akaanza kula,alipo maliza kula alileta lile sanduku lililokuwa na zile fedha za zamani pale,akalifungua na kuanza kusaka ile sarafu ya 100 ya mwaka 1993,mzee aliendelea kutafuta kwa makini sana,Kuna shilingi ishirini ya zamani ambayo sikuwahi kuiona kabla lakini siku hiyo niliiona hapo kwa huyo mzee,mzee aliendelea kutafuta lakini hakukuwa na mafanikio yeyote,sarafu zilikuwemo nyingi lakini ya 1993 haikuwemo.

Baada ya kutafuta sana na kwa umakini mkubwa Mzee akatuambia hiyo hela tuliyokuwa tunaitafuta haikuwepo!,kiukweli moyo wangu uliuma sana lakini nikajipa moyo maana ilikuwa bado ni mapema sana kukata tamaa,ndio kwanza hata wiki ilikuwa haijaisha.Basi yule Mzee akatuambia ili tusiendele kupoteza muda kuna mtu alikuwa anafahamiana naye,naye alikuwa anafanya kazi za kuagua kama yeye,akatutaka twende kwa huyo mtu,lakini kabla ya kutupatia maelekezo ya huyo mtu na anakopatikana aliniomba simu yangu akaingiza namba za huyo mtu akaanza Kumpigia,alipompata walikuwa wanaongea kwa kilugha,Baada ya maongezi mzee akatuambia yule mzee mwenzie amesema twende na yeye pia anazo hela za zamani tukaangalie uenda anaweza akawa nayo!.Mzee alituambia huyo mzee mwenzie anapatikana kijiji kimoja kinaitwa Saragana,alituambia tukifika hapo kijijini tutampigia simu,kwakuwa namba yake alikuwa keshamaliza kuongea naye muda si mrefu akanitaka niisevu ili iwe rahisi kumtafuta.

Nikamuuliza yule mzee "tutafikaje huko kijiji cha Saragana?".

Mzee alisema "kuna baiskeli hapa kijijini za kukodi,ngoja niwaite vijana 2 ili muelewane nao wawapeleke".

Yule Mzee alituitia kijana mmoja tukaongea naye akasema "ngoja nikamuite mwenzangu ili tuelewane kwa pamoja tuwapeleke!"

Wale jamaa wakasema kutupeleka kijiji cha Saragana kwa kuwa ni mbali tuwape elfu 10 kwa wote wawili,basi kwakuwa mpaka muda huo nilikuwa nina elfu 25,ilibidi niwape hiyo elfu 10 nikabaki na elfu 15,ilibidi tuanze safari ikiwa mida ya saa 5 asubuhi,Kiukweli ile safari ya kuelekea kijijini Saragana ilinichosha sana maana palikuwa mbali sana!,Kuna muda niliona kama wale vijana kuwapa ile elfu 10 ni kama nilikuwa nimewadhurumu!,sikuwa na namna maana sikuwa na hela nyingine zaidi ya ile elfu 15.Tulipokuwa tukifika kwenye milima ilitubidi tushuke tusukume baiskeli mpaka sehemu tambarare ndiyo tuendelee na safari.Ile safari ilituchukua kama masaa 6,Kuna njia jamaa walikuwa wanatupitisha za porini ambazo walidai wao ndiyo njia za karibu,walikuwa wanasema tungefuata barabara moja kwa moja ingetuwia vigumu kufika mapema.

Tuliingia hapo Kijiji cha Saragana mida ya saa 11 jioni,tulikuta kulikuwa na mnada na kuna baadhi ya wafanyabiashara walikuwa wameanza kufungasha mizigo maana sasa jioni ishaanza kuingia,tulivyofika hayo maeneo ilibidi nimpigie yule mzee na bahati nzuri alipokea simu,baada ya kupokea simu nilianza kusikia sauti ya kilevi,ilionyesha yule mzee alikuwa amekunywa pombe!,baada ya kumulekeza tulipokuwa tumesimama alikuja akatuchukua kuelekea kwenye vibanda vya hapo mnadani!,Mzee akaanza kuongea mambo mengi nikajua tu tayari atakuwa amelewa pombe!,inavyoonekana alikuwa hapo mnadani muda mrefu akilewa pombe,basi nikamwambia dogo "hapa hakuna kitu maana huyu mzee mwenyewe kalewa hatotuelewa!".

Yule Mzee akaanza kututambulisha kwa wazee wenzie waliyokuwa hapo kwamba sisi ni wanaye!,Kumbe mzee wakati sisi tukiwa pale tunashangaa alikuwa kaagiza pombe fulani hivi walikuwa wanawekewa kwenye makopo makubwa,kibaya zaidi akaagizia na wenzie waliyokuwa watatu halafu akamwambia mama muuzaji kwamba "Yule kijana wangu aliyesimama pale atakupa hela".

Kiukweli nilighafirika sana hasa ukizingatia kilichotupeleka hapo ni kitu kingine halafu yeye analeta habari za pombe tena!,basi baadae yule mama muuza pombe alinifata akasema nimpe hela yake maana wao wanataka kufunga,sikuwa na namna ilibidi nilipe,nilimpa elfu 5 akiniletea chenji ya elfu 2,kwa maana hiyo yule mzee na wenzie walikunywa pombe ya elfu 3,ile elfu 2 ilibidi nimpe dogo nikamwambia akanunue miwa alete tutafune wakati huo tunaangalia cha kufanya!,basi haukupita muda dogo akaja na miwa miwili iliyogharimu elfu 1,ile elfu 1 nyingine iliyobaki ikabidi niirudishe mfukoni.Baadae wazo likanijia ya kwamba nimpigie simu Yule mzee wa Bukima nimweleze hali halisi ya mzee mwenzie,nilipomueleza mzee alisikitika sana akasema kwamba nimpe simu aongee naye,inavyoonekana yule mzee wa Bukima alimgombeza sana yule mzee mlevi,maana alikuwa amekaa kimya hata kujibu hajibu!.Baada ya mazungumzo yale nilimwambia mzee wa Bukima kwamba inabidi turudi Bunda maana mzee ambaye ilibidi atusaidie ndiye huyo kalewa chakari,wazo lilikuja kwamba hayo magari ya minadani ndiyo ambayo tutarudi nayo,nilimwambia dogo tuanze kuzungukia yale magari tuulize yalikuwa yakienda wapi ili kama tukipata la Bunda tuongee nao tuwalipe tujiandae kwa safari!.

Kiukweli tulizungukia yale magari na yote baada ya huo mnada wa hapo kijijini Saragana yalikuwa yakielekea sehemu moja inaitwa Kiabakari maana siku iliyofuata kulikuwa na mnada huko,nikamuuliza dogo hapo Kiabakari na Bunda kulikuwa na umbali gani?,dogo akasema ilikuwa ni mbali sana ila akasema kuna unafuu maana ni njiani hivyo kupata Hiace ilikuwa simpo!,ikabidi nimfate tena dereva wa lori moja lililokuwa hapo jirani nikamuuliza kutoka hapo Kijiji cha Saragana mpaka Bunda kulikuwa na umbali gani?,jamaa akasema si chini ya km 30!,Kiukweli nilichoka sana maana nilitaka endapo ingekuwa karibu tutembee kwa miguu!,ikabidi nimuulize dogo tunafanyaje?.Dogo kuna wazo alitoa nikaona kama lilikuwa na mantiki.

Dogo alisema "Tupande gari zinazoenda kiabakari tukifika huko kwakuwa pia ni vijijini tutaendelea kuitafuta ile shilingi sarafu uenda tungefanikiwa kuipata".

Nimuulize dogo "Usiku huu tulala wapi?".

Dogo akasema "haya magari moja wapo tutakalo panda tutalala humohumo kwenye mizigo".

Ilibidi iwe hivyo kama dogo alivyoshauri!,Kuna muda nilikuwa ninachoka lakini najipa moyo nikiamini siku si nyingi naenda kuwa tajiri!,kuna gari tuliipata na dereva akasema tutampa elfu 6 kwa wote wawili mpaka huko Kiabakari,mfukoni nilibaki na balansi ya elfu5 ,baada ya kuwa wamemaliza kukusanya mizigo tulifanikiwa kuondoka hapo mida ya saa 1 usiku kuelekea Kiabakari!.


Itaendelea.....................
 
Ahahahahahaa!!!,Mkuu mwezio enzi hizo za miaka 14 -15 nilikuwa hata sijui habari za wanawake,Wanawake nimekutana nao ukubwani Mkuu nikiwa sekondari
Mwenzieo nilikuwa natembea na vioo..alafu nawawekea kwa chini hivi..na vile visketi vyao basi ni mwendo wa kutazama tu episode mbalimbali za vyupi..
 
Back
Top Bottom