MKASA WA PILI - Sehemu ya 7.
Inaendelea.............
Safari ilianza hiyo mida ya 1 Usiku kama kawaida na sisi tulikaa nyuma ya lile lori kwenye mizigo,lile lori lilikuwa halijabeba watu wengi maana jamaa walisema askari wa barabarani walikuwa wakiwasumbua sana endapo wakibeba mizigo na abiria kwa pamoja,hivyo magari ya abiria yalikuwa yametangulia halafu hayo ya mizigo yalikuwa ya mwisho,hivyo yule dereva alituambia tuhakikishe tunapata upenyo wa kukaa ambako si rahisi kuonekana kirahisi.Mimi na dogo tuliendelea kutafuna miwa yetu tuliyoinunua hapo mnadani maana tulifahamu kwa usiku huo tusingekula na hiyo miwa ndiyo ingekuwa chakula chetu!.Safari ilisonga kwa muda sana na tuliingia pale Kiabakari yapata saa 6 usiku,kwakuwa hatukuwa napa kwenda ilibidi tulale mle kwenye lori,mimi kichwani niliwaza ya kwamba pakipambazuka tu,ni kutafuta usafiri na kurudi Bunda maana hata hela ilikuwa imetuishia,mfukoni nilikuwa nimebaki na elfu 5 tu.
Asubuhi kulipokucha mida ya saa 12 asubuhi ilibidi tushuke kwenye lori maana jamaa walisema muda si mrefu wao walikuwa wakielekea mnadani.Nilimwambia dogo tukae hapo barabarani tusubirie garu zilizokuwa zinatoka Musoma tupande twende Bunda.
Dogo alianza kuniambia "Inamaana bro umekata tamaa?".
Nilimgeukia dogo nikamwambia "Hapana".
Dogo aliniuliza "Sasa kama hujakata tamaa tunarudi Bunda kufanya nini?,jana tulikubaliana kwamba tukifika hapa Kiabakari tuanze kuitafuta ile hela maana huku ni vijijini uenda tukaipata".
Kiukweli ilibidi nimwambie dogo pesa niliyokuwa nayo imeisha na hata nguo hatukuwa naza kubalisha,Yule dogo ilionekana anatamani sana kuipata ile sarafu maana alisema "Nguo kitu gani bro,mbona tutanunua nyingi tu endapo tukifanikiwa kuipata hiyo hela!".
Kuna muda nilikuwa nakata tamaa lakini dogo alikuwa akinipa morali na hali ya kuendelea kuisaka ile sarafu ya 100 ya mwaka 1993,basi nilimwambia dogo "Hapa mfukoni nina elfu 5 tu,twende tutafute sehemu tunywe chai na nyingine niweke vocha nimpigie mama Mwanza maana nina muda sijaongea naye!".
Yale maeneo ya hapo Kiabakari kulikuwa kuna wafanyabiashara wa mazao mbalimbali na hasa ndizi na nyanya.Dogo aliniambia "Bro tununue ndizi mbivu tule maana hapa ni nyingi sana na bei ni chee,kisha tukishushia na maji ya kunywa naamini itatusaidia maana chai inawahi kuisha tumboni".
Kuna mama mmoja alikuwa akiuza ndizi hayo maeneo tulimuita aje atuuzie,tulimsalimia kisha nikamuuliza "ndizi unauza bei gani?".
Yule mama alisema "Hiki kibeseni chote nipeni elfu 2500 wanangu".
Kiukweli zile ndizi zilikuwa ni nyingi sana halafu zilikuwa kubwa!,ilibidi nimuulize vizuri ni kweli ni 2500 au kakosea kutamka?,Yule mama alisisitiza hiyo ndiyo bei,nilichomoa ile elfu 5 mfukoni nikampa yule mama kisha akaturudishia chenji,ilibidi nimwambie dogo akanunue mfuko wa rambo wa 500 ili tuweke zile ndizi kwa maana zilikuwa nyingi,nikamwambia aniletee na vocha ya Zain (Airtel) ya 500.Wakati dogo akiwa kaenda dukani nilimuita yule mama aliyetuuzia ndizi nikawa namuuliza yale maeneo kama tungeweza kumpata mganga.
Yule mama aliniuliza "Kwani mlikuwa na shida gani wanangu?".
Kwa wakati ule sikutaka kumficha kitu yule mama ilibidi nimueleze kila kitu kuhusu ile sarafu,Mama aliniambia kwamba kwa waganga wa hapo Kiabakari hakuona kama tungeweza kuipata hiyo sarafu,Yule mama aliniambia kuna mganga ambaye yeye huwa anamsaidia kwenye mambo yake ikiwemo biashara zake na hakuwa hapo bali alikuwa anapatikana maeneo ya Ikizu,mama akasema uenda anaweza akawa nazo!,nilimuuliza yule mama kutoka hapo Kiabakari mpaka huko Ikizu kulikuwa na umbali gani?.
Yule mama aliniuliza "Kwani haya maeneo wewe ni mgeni mwanangu?".
Nilimjibu "Ndiyo".
Wakati tunaongea na yule mama bahati nzuri dogo naye akawa kafika,akachukua zile ndizi akaziweka kwenye mfuko,nilimsimulia yule dogo jinsi yule mama alivyokuwa ameniambiania.Dogo akasema "Huko Ikizu mpaka turudi tena Bunda ndiyo tunapanda gari za kuelekea huko".
Yule mama alisema "Huko Bunda ni mbali sana,ukiwa hapa kwenda Ikizu mbona ni jirani tu wanangu?".
Alituambia kuna njia moja ambayo tungeipita kisha tungetokezea kijiji cha Butiama halafu tungeikuta njia kubwa ambayo inaelekea Ikizu.Basi yule mama alitoa simu yake aliyokuwa ameiweka kwenye matiti akawa anaitafuta namba ya yule mganga aliyesema yupo huko Ikizu,alipoipata alinitajia namba akaniambia kama nina salio nimpigie yeye aongee naye,niliichukua ile vocha aliyonunua dogo nikajiunga dakika za kutosha kisha nikaanza kumpigia yule mganga,Simu ilipokuwa ikiita nilimpa yule mama nikamwambia "Inaita,Ongea naye".
Yule mama alianza kuongea naye kwa kilugha na alimueleza kila kitu kuhusu sisi.Yule mganga alimwambia yule mama anipatie simu niongee naye,mganga aliniambia endapo kama hiyo sarafu ingepatikana hapo kwake tungempatia shilingi ngapi?,ilibidi nimwambie dau kama nililomwambia yule mzee wa Bukima lakini yule mganga akasema hilo dau ni dogo sana tuongeze dau,baada ya kusikia ile kauli ya mganga nilijipa moyo sana,nilijua uenda yule mganga angekuwa na ile sarafu maana kama asingekuwa nayo asingeniambia kwamba lile dau lilikuwa dogo.Nilimuuliza yule mganga aseme yeye alikuwa anataka shilingi ngapi?,yule mganga alitamka kwamba tumpatie laki tatu.Nilicheka kimoyomoyo nikajisemea "laki tatu kitu gani wakati sisi tunapata milioni 100!".
Basi tulikubaliana na nikamwambia tunaanza safari ya kuelekea huko kwake na muda wote apatikane hewani,baada ya kuwa tumekubaliana tukamshukuru sana yule mama,alitueleza ya kwamba tulikuwa waungwana ndiyo maana na yeye alionyesha ushirikiano kwetu,alituambia ngoja kwanza akachukue ndizi nyingine ili aje atuonyeshe njia fupi ambayo isingekuwa rahisi kupotea.Wakati huo dogo alishauri tuanze kula zile ndizi ili tutakapoianza safari iwe rahisi kutembea,tulikula zile ndizi na kwa namna zilivyokuwa nyingi nyingine zilibaki nikamwambia dogo tutakula mbele ya safari!,tulipomaliza kula ndizi kuna kibanda kilikuwa maeneo ya hapo jirani walikuwa wanauza chai tuliingia kuomba maji ya kunywa tukapewa kwenye jagi.Kiukweli nilishiba sana kwa wakati ule maana zile ndizi hazikuwa za mchezo hata kidogo.
Namshukuru sana Mungu maana hii safari ya kutafuta maisha ilinifanya nikayafahamu maeneo mengi ya nchi hii ya Tanzania pamoja na nchi jirani,basi baada ya yule mama kurejea,alituchukua mpaka kwenye njia ya vumbi akatuambia "Fuateni hili barabara hamtapotea na huko mbele mtakuwa mnauliza watu njia ya kuelekea Butiama watawaonyesheni".
Yule mama aliendelea kusisitiza ya kwamba hatutoweza kupotea,alituambia kwamba tukifika hapo Butiama tutauliza njia ya kwenda Ikizu tutaelekezwa na wenyeji wa hapo.Safari ikaanza kama kawaida,muda huu kwa kuwa hatukuwa na hela ilibidi tuanze kupiga kwato taratibu!.
Itaendelea............