Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Stori ishaanza kukosa Radha Haina hata uzuri wowte yaani ,kisa huko chini itaendelea nachokushauri usilete huo mwendelezo badala ya kusema itaendelea andika hata siku mbili au tano kabisa ikisha kamilika ndo uilete hapo hakuna hata Cha kukielewa ,smart people always doing smart thing
Nitakutoa nje sasa hivi choko ww🙄🙄🙄 endelea kuchonga tu....
 
mwenye link ya stori ya msitu wa nairoto plz naomba msaada
 
MKASA WA PILI -sehemu ya 10.

Inaendelea.............



Wakati tukiwa kwenye lile lori nilikuwa nikipiga stori na dogo nilimuuliza endapo tungefanikiwa kupata hela yeye angefanyia nini,ndipo nikagundua dogo anapenda sana maisha ya starehe,maana alikuwa akiniambia angeipata hiyo hela kitu cha kwanza ni kununua gari la kifahari na kutafuta mwanamke mzuri wa kuishi naye.Kiukweli mimi nilikuwa nawaza namna ya kumkwamua mama yangu kutoka kwenye umasikini hasa ukizingatia baada tu ya kutoka Tarime na kuhamia Mwanza maisha yalibadilika na kuwa ya Hovyo sana.
Baada ya muda kupita aliniambia "Hawa jamaa inabidi tuwashitue watuache shule ya sekondari ya Bunda".

Baada ya kufika Bunda tuliwashitua wale jamaa wakatuacha karibu na Bunda Sekondari,dogo akaniambia kutoka hayo maeneo tulipoachwa mpaka kilipo chuo cha ualimu si mbali hivyo tutembee taratibu tutafika.Kiukweli wakati huo nilikuwa nanuka harufu ya mbuzi kwasababu ya kukaa nyuma ya lile lori lakini sikujali sana,tulianza kutembea taratibu kuelekea hayo maeneo ya chuo ambayo jamaa alituambia kwamba ndipo kuna ile sarafu ya 100 ya mwaka 1993.
Nilimtafuta yule jamaa wa Ukerewe akatuelekeza hayo maeneo,sasa kwakuwa dogo yeye alikuwa mwenyeji wa Bunda alikuwa akielewa maeneo mengi ya huko chuoni,lakini jamaa akasisitiza ya kwamba tuhakikishe kweli kama tunataka kuichukua hiyo sarafu,inapaswa tumuachie huyo mke wake tutakaye mkuta hapo nyumbani kwake shilingi laki 3 kama tulivyokuwa tumekubaliana.

Tulipofika hapo nyumbani kwa jamaa tulifanikiwa kumkuta huyo mwanamke na kwakuwa jamaa alikuwa amempa maelekezo haikuwa ngumu sana kujieleza,aliingia ndani akatoka na sarafu za shilingi 100 kama tatu hivi,akaanza kuangalia ya mwaka 1993 na ndipo akaipata.Alituonyesha ile sarafu ili kujihakikishia kama ndiyo yenyewe,baada ya kuishika ile sarafu na kujihakikishia ya kwamba ni yenyewe,nilianza kuingiwa na kitete kisichokuwa cha kawaida.Nilikuwa nina furaha isiyokuwa na kifani,yule mwanamke alisema amepewa maelekezo na mumewe ya kwamba inapaswa tulipe ile laki tatu ndiyo tutaruhusiwa kuondoka na hiyo sarafu.Kwakuwa hatukuwa na laki tatu wakati huo,niliamua kumpigia simu yule Mkenya nikamueleza kwamba tushaipata ile sarafu,ikiwezekana atume hiyo laki tatu halafu wao wangetukata kwenye ile milioni 100 ambayo aliahidi tungelipwa,sasa nilipokuwa naongea naye ilionekana yeye pia kapagawa.

Aliniambia"Subiri kidogo nakupigia".

Baada ya dakika 5 alinipigia simu akaniuliza kwa wakati huo tupo maeneo gani?,nilimwambia tupo maeneo fulani hapo Bunda.

Jamaa akaendelea kuniambia"Subirini hapo hapo kuna watu wanakuja na hiyo laki 3 ya kumpa huyo mama!”.

Nilianza kuingiwa na wasiwasi,ilibidi nimuulize kuhusu hela yetu inakuwaje?,jamaa akasema kwamba wakishachukua hiyo sarafu tutaongozana nao kuelekea Mwanza maana hata tajiri aliyekuwa katoka
Kenya bado alikuwa hapo Mwanza na tungefika tulikuwa tunalipwa hiyo pesa bila wasiwasi wowote.Nilimkumbushia kwamba,mwanzo kabla hatujaanza kazi alisema hiyo pesa wangetuwekea kwenye akaunti, sasa inakuwaje wakatupe mkononi?.

Jamaa alisema"Nitumie namba ya akaunti yako ya benki”.

Kwa kipindi hicho sikuwa na akaunti ya benki,hivyo nilimwambia jamaa anitumie vocha nimwambie mama yangu anitumie namba ya akaunti ya kwake ili hiyo hela itumwe huko.Ndani ya dakika kadhaa jamaa aliponitumia vocha,nilimpigia simu mama na kumueleza kila kitu,ndipo akanitumia namba ya akaunti nikamtumia jamaa yule mkenya.

Jamaa baada ya kuipata ile akaunti alisema "sawa tutaingiza hiyo pesa muda si mrefu lakini kuna vijana wanakuja hapo kuichukua hiyo 100 wapeni".

Baada ya mazungumzo kwenye simu nilimuita yule dogo tukaanza kujadiliana,Yule dogo alikuwa na akili sana,alianza kuniambia kwamba hao jamaa tusipokuwa makini wanataka kututapeli,endapo tungewaelekeza maeneo tuliyokuwepo wangefika na kuichukua hiyo sarafu tusingepata kitu.Maelezo ya yule dogo ni kama sasa yalianza kunifungua akili,kwa ujasiri nilimpigia simu yule mkenya kumueleza ya kwamba pasipo hiyo hela kutumwa kwenye akaunti niliyomtumia nisingemuelekeza tulipo na nisingempa ushirikiano wa aina yeyote,jamaa aliendelea kusisitiza kwamba pesa ingewekwa muda si mrefu kwenye akaunti.Baadae nilimpigia mama simu nikamwambia aende benki akaangalie kama ile hela ishawekwa;Baada ya muda mama yangu akasema “hakuna hela yoyote iliyoingia mwanangu”.

Nilimwambia dogo tuelekee nyumbani maana hatukuwa na shaka yeyote kwakuwa hiyo sarafu tayari tushaipata.Kabla hata hatujafika nyumbani kwa mama mdogo jamaa akawa amepiga simu akaanza kusema kwamba hao jamaa wapo maeneo ya hapo stendi Bunda tuwaelekeze maeneo tulipo ili waje,nilimwambia yule jamaa siwezi kuwaelekeza wale jamaa bila hela kuingizwa kwenye akaunti.

Nilimwambia "kwanini usinitumie hiyo laki tatu nikatoe nimlipe yule mama?".

Yule jamaa mkenya inaonekana alianza kuchukia akaanza kuongea kwa ukali sana.Alikata simu kwa muda kidogo,aliponipigia tena aliniambia "Wewe mjinga si unajifanya mjanja?,sasa itakula kwako,mtake msitake tutawatafuta popote mlipo na kuhakikisha hiyo sarafu tunaipata,vinginevyo lazima mfe".

Jamaa akakata simu,nilimueleza dogo namna jamaa alivyoniambia,dogo akasema "Mimi nilijua tu maana ishu za pesa kama hizi mara nyingi huwa si salama sana".

Nilipatwa na uoga ambao sikuwahi kukutana nao kwa kipindi chote ambacho tuko huko,ilibidi nimpigie simu mama nikamueleza kila kitu,aliniambia nihakikishe kesho narudi Mwanza haraka iwezekanavyo hao jamaa wasije nifanyia kitu kibaya.Yule jamaa alikuwa akinipigia simu sana lakini sikuweza kupokea,jamaa alianza kutuma sms za vitisho na matusi makali,alisema lazima watupate tu hata kama tungeenda wapi maana wao wanakikosi kazi ambacho kisingeshindwa kazi ya kutusaka.Tulipofika nyumbani ilibidi tumsimulie mama mdogo namna hali ilivyokuwa tangu siku tunaondoka mpaka kupatikana kwa hiyo hela,niliendelea kumwambia mama mdogo kuhusu huyo mkenya na sms zake alizokuwa akituma,mama mdogo alituambia hao jamaa wangetudhulumu na isingekuwa ajabu kutuua ili wapate wanachokitaka.
Baadae kidogo nikiwa nyumbani kuna simu ilipigwa nikaipokea,jamaa alijitambulisha kama askari akasema kwa usalama wetu tujisalimishe pale kituo cha polisi cha wilaya ya Bunda maana hatutaweza kukimbia mahali popote bila kukamatwa,nilibaki najiuliza maswali mengi sana kichwani,wanataka watukamate kwa kosa gani tulilokuwa tumefanya?,nilijua kabisa kutakuwa na askari ambao hawakuwa waaminifu walikuwa wakishirikiana na lile genge la waharifu,sasa walidhani kupitia vitisho vyao tungeogopa,niliamua kuitoa ile line kwenye simu na kuitupa.


Itaendelea.......................



............................................................





MKASA WA PILI - Sehemu ya 11.


Inaendelea................


Baada ya kuitupa ile line ya simu nilikaa kwa kutulia nikiwaza na kuwazua," Ina maana kuhangaika kote siku kadhaa za kuitafuta hiyo hela leo hawa majinga wanataka kututoa uhai kisa sarafu ya 100?",kiukweli niliwaza bila kupata majibu.


Nilimwambia dogo ahakikishe anakaa kwa kutulia mpaka hali itakapokuwa shwari maana nilijua wale jamaa wangeendelea kumtafuta pale Bunda hasa ukizingatia mji wenyewe haukuwa mkubwa sana.Kesho yake nilimuomba mama mdogo nauli ili niondoke kurudi Mwanza maana niliona kila kitu kilikuwa kimeshaharibika!,Niliona ni heri nikaishi masikini kuliko kuendelea kukaa hapo kwa wasiwasi huku maisha yangu yakiwa rehani!.Niliondoka Bunda na sikutaka dogo anisindikize maana nilijua anaweza kukamatwa na wale mafia hatimaye mambo yakaharibika.Niliingia Mwanza mida ya saa 8 mchana na nilimweleza mama kila tukio lililo kuwa limetokea kwa siku hizo.

Basi kwakuwa sikuwa na kazi ya kufanya kwa wakati huo niliamua niende nikaendelee na ile kazi yangu ya ualimu wa temporary niliyokuwa nikiufanya baada ya kumaliza elimu yangu ya sekondari,Kwahiyo nilikuwa nikitoka kwenye vipindi mchana jioni nilikuwa naenda kuwafundisha wanafunzi niliyokuwa nao kwa wakati ule kabla sijaenda Geita na walikuwa wakinilipa elfu 3 kwa kila topic tuliyokuwa tunamaliza.Baada ya kukaa pale nyumbani kwa muda mrefu,nilimwambia mama ya kwamba,ulifika wakati sasa na mimi niende kupanga chumba changu ili nijitegemee!,mama yangu alikaataa kabisa akasema nyumba bado ni kubwa na mimi sipaswi kuondoka hapo nyumbani,niliona kama kanibana maana kuna mambo yangu niliona kama hayataenda,niliendelea kumsihi mama aniruhusu nikapange lakini ningekuwa narejea nyumbani kuwasalimia,baada ya kumsihi sana mama alikubali na akanitaka endapo maisha yakinishinda nirudi nyumbani!.

Nilikuwa namuhurumia sana mama yangu kiukweli na nilimpenda sana japo sikuwa na kitu!.Kwakuwa kuna vihela vyangu nilikuwa nimevikusanya kwa wakati huo nilienda kutafuta chumba nikalipia miezi 3 na nikanunua godoro na vyombo kadhaa vya kupikia,nilinunua pia na vitu kadhaa vya ndani na kadri siku zilivyoenda nilipokuwa nikilipwa nilikuwa nikinunua vitu taratibu!.

Maisha yalisonga na muda nao ukazidi kuyoyoma,siku moja wakati nikiwa geto kwangu,mama alinipigia simu akataka niende kule nyumbani maana kulikuwa kuna maongezi ya kifamilia.Basi nikajianda nikaondoka zangu mpaka nyumbani,nilipofika nilimkuta dada yangu mkubwa,mama,shangazi,pamoja na wale mabinti waliokuwa wakikaa hapo nyumbani ambao walikuwa watoto wa Shangazi.Mama alisema ametuita hapo kwasababu kuna jambo kalisikia ambalo halikuwa zuri.

Nilimuuliza mama "ni jambo gani hilo?"

Ndipo binti mmoja wa Shangazi aliyekuwa mkubwa akawa nasema alikutana na Shemeji yangu mmoja ambaye kwa upande wa dada zangu alikuwa ni wifi yao,kuna maneno aliyaongea ambayo hayakuwa mazuri!,Yule mtoto wa shangazi akawa anasema alikutana na shemeji kanisani akawa anamwambia kwamba sisi hapo nyumbani ni Masikini na alikuwa anajuta kaka yao kuoa hapo nyumbani kwenye ukoo masikini!,Yule shemeji aliendelea kusema kwamba anaogopaga hata kuwapeleka rafiki zake ukweni kwasababu tulikuwa tunanuka umasikini!.Yule binti akawa anasema yule shemeji alikuwa anasema kwamba hizo taarifa zimfikie mama yangu maana hatukuwa nala kumfanya kwasababu sisi ni masikini wa kutupa,alikuwa akilaani sana kwanini kaka yake asingeenda kuoa kwenye familia ya kitajiri akaenda kuoa kwetu kwenye familia masikini.

Hayo ndiyo yalikuwa maelezo ya yule binti mtoto wa shangazi.

Sasa huyo shemeji tuliyekuwa tukimjadili hapo kwenye kikao labda nimuelezee kidogo.Huyo shemeji kaka yake ndiye alikuwa amemuoa dada yangu niliyekuwa nikimfuatia katika uzao ambaye kwa wakati huo walikuwa wakiishi mkoani Arusha,huyu shemeji alikuwa anafanya kazi kwenye benki fulani hapo mjini na alikuwa amekaa sana Afrika kusini,Kwahiyo dharau na nyodo zote alikuwa anazifanya kwakuwa alikuwa na ajira benki na kukaa tu hapo Afrika Kusini!.

Baada ya hayo maelezo nilikuwa najiuliza maswali mengi kichwani yasiyokuwa na majibu.
Nilijikuta namwambia mama "kwani umasikini ni nini?,maana sisi kama ni kula mbona tunakula vizuri?,kama ni nyumba mbona tuna nyumba?,huyo malaya anataka maisha gani?,au kwakuwa yeye ana gari na kufanya kazi benki ndiyo anadharau watu?".

Toka wakati huo nilimwambia mama "sitokaa niimtambue yule mume wa dada kama shemeji maana dada yake anatudharirisha na kutuahibisha".

Tulipomaliza yale mazungumzo niliondoka zangu pale nyumbani kuelekea Geto kwangu kulala,siku hiyo nilikosa raha sana na nilikuwa nimechukia sana,nilijiona bado nilikuwa nina safari ndefu sana ya kuwa tajiri.Pale nyumbani nilipokuwa nimepanga kuna jamaa mmoja tulikuwa tumepakana vyumba na alikuwa rafiki yangu sana maana hata alipokuwa akielekea kwenye shughuli zake ambazo zilimchukua hata mwezi alikuwa akiniachia funguo!.Sasa baada ya kuona sikuwa na raha,jamaa aliniuliza "Mwanangu mbona leo huna raha?,una shida gani?".

Nilimwambia nilikuwa sijisikii vizuri tu!,huyu jamaa alikuwa akifanya kazi kampuni ya ujenzi ya Nyanza,usiku ule nilimfuata jamaa nikamwambia kwa ujasiri mkubwa "Nataka kuwa tajiri".

Jamaa alioneshaa kushituka sana na kuniuliza "Mwanangu leo umepatwa na nini?,tafadhali nieleze ukweli".

Basi nilimsimulia yaliyonisibu na kiukweli alihuzunika sana,akaniambia nisijali niende nikapumzike halafu kesho tungeongea.Siku iliyofuata baada ya kutoka kwenye shughuli zangu za kushika chaki ilibidi nimueleze jamaa adhma yangu ya kuutafuta utajiri.

Nilimwambia jamaa "Mimi ninachotaka ni utajiri,haijalishi ni utajiri wa namna gani"

Dhumuni la mimi kutaka kuwa tajiri ni kumuonyeshea uwezo yule shemeji yangu na watu wengine waliyokuwa wanatuona sisi masikini!,Kiukweli kwa wakati huo nilikuwa nipo tayari kufanya jambo lolote ili niweze kuwa tajiri.

Jamaa aliniambia "tafuta nauli twende zetu kigoma maana kuna kipindi tulienda kufanya kazi ya ujenzi wa barabara kule,kuna bibi tuliwahi kwenda kwake alikuwa ni balaa!,kipindi hicho mimi nilienda kwake kufata dawa ya kinga dhidi ya watu wabaya pale kazini hivyo sikufata utajiri,lakini safari hii nataka na mimi nikatafute dawa ya kupanda cheo na kupata pesa!".

Basi hayo mazungumzo ya jamaa yalinipa faraja kidogo na yakaniondolea upweke wa nafsi.Niliendelea kutafuta pesa za nauli maana jamaa aliniambia nikipata kama laki 2 nimshitue ili tuondoke maana yeye alikuwa yuko tayari muda wote.Mwezi uliofuatia ulikuwa mwezi wa 6 mwaka 2012 ambao tulipanga tuondoke,sikutaka kumwambia mtu yeyote,hata mama pia sikutaka kumuaga,mtu aliyekuwa akifahamu ni huyo jamaa tuliyekuwa tukikaa naye hapo nyumbani vyumba jiarani.

Basi tulipanga safari ya kwenda kigoma na tuliondoka Mwanza siku iliyofuata!




Itaendelea..............
 
MKASA WA PILI -sehemu ya 11

Inaendelea................


Baada ya kuitupa ile line ya simu nilikaa kwa kutulia nikiwaza na kuwazua!," Ina maana kuhangaika kote siku kadhaa za kuitafuta hiyo hela leo hawa majinga wanataka kututoa uhai kisa shilingi 100"?,Nilijisemea!

Basi nilimwambia dogo ahakikishe Anakaa kwa kutulia mpaka hali itakapokuwa shwari maana nilijua wale jamaa wangeendelea kumtafuta pale Bunda hasa ukizingatia mji wenyewe haukuwa mkubwa hivyo!

Kesho yake ilibidi mimi niondoke Pale kwa Mama mdogo kurudi Mwanza maana niliona kila kitu kilikuwa kimeshaharibika!,Nikajisemea ni heri nkaishi masikini kuliko kuendelea kukaa hapo kwa wasiwasi huku maisha yangu yakiwa rehani!
Niliondoka hapo nyumbani Bunda na sikutaka dogo anisindikize maana nilijua anaweza kukamatwa na wale mafia hatimaye mambo yakaharibika!

Niliingia Mwanza mnamo mida ya saa 8 mchana na nilimweleza Bi mkubwa kila tukio lililo kuwa limetokea kwa siku hizo!

Basi kwakuwa siku na kazi ya kufanya kwa wakati huo nilitafuta shule kadhaa pale mjini wa kufundisha tuition,kwa bahati nzuri kuna shule fulani niliipata pale Mjini ambayo nilipewa ajira temporary ya kuwa mwalimu wa History na Geography na nilikuwa nalipwa kila Mwezi 150000/=Nilimshukuru Mungu sana hasa ukizingatia sikuwa na chochote!,Kwahiyo nilikuwa nikitoka kwenye vipindi mchana jioni nilikuwa naenda kuwafundisha wanafunzi niliokuwa nao kwa wakati ule kabla sijaenda Geita na walikuwa wakinilipa 3000 kwa kila topic tunayomaliza!

Baada ya kukaa pale nyumbani kwa muda nilimwambia Bi mkubwa ni wakati sasa na mimi niende kupanga chumba changu ili nijitegemee!,Bi mkubwa alikaataa na akasema nyumba bado ni kubwa na mimi sipaswi kuondoka hapo nyumbani!,Niliona kama Bi mkubwa kanibana maana kuna mitikasi yangu niliona kama haitaenda!,Niliendelea kumsihi Bi mkubwa kwamba ntaenda kupanga ila ntakuwa sikauki pale nyumbani,Baada ya kumsihi sana Bi mkubwa alikubali na akanitaka endapo maisha yakinishinda basi nirudi nyumbani!

Nilikuwa namuhurumia sana Mama yangu kiukweli na nilimpenda sana japo sikuwa na kitu!
Kwakuwa kuna vihela vyangu nilikuwa nimevikusanya kwa wakati huo nilienda kutafuta chumba nkalipia miezi 3 na nkanunua godoro na vyombo kadhaa vya kupikia,nilinunua pia na vitu kadhaa vya ndani na kadri siku zilivyoenda nilipokuwa nikilipwa nilikuwa nikinunua vitu taratibu!

Maisha yalisonga na muda ukayoyoma!,Hatimaye Mungu akasaidia nikauona Mwaka 2011.

Sasa siku moja wakati nikiwa homu Bi mkubwa alinipigia simu akataka niende kule nyumbani maana kuna maongezi!
Basi nkajianda nkasepa zangu mpaka nyumbani,Nilipofika nilimkuta Yule sista mkubwa kaja,Bi mkubwa pia alikuwepo pamoja na wale mabinti waliokuwa wakikaa hapo kwa Bi mkubwa watoto wa Shangazi!
Bi mkubwa alisema ametuita hapo kwasababu kuna jambo kalisikia si zuri!,Nilimuuliza bi mkubwa ni jambo gani hilo?

Ndipo binti mmoja wa Shangazi aliyekuwa mkubwa kuliko yule Mwenzake akawa nasema alikutana na Shemeji yangu mmoja hivi ambaye kwa upande wa Ma sista alikuwa ni wifi yao,kuna maneno aliongea ambayo hayakuwa mazuri!,Yule binti akawa anasema alikutana na Yule shemeji kanisani akawa anamwambia kwamba sisi hapo nyumbani ni Masikini na anajuta hata kaka yao kuuoa hapo nyumbani kwenye ukoo masikini!,Yule shemeji aliendelea kusema kwamba anaogopaga hata kuwapeleka rafiki zake ukweni kwasababu tunanuka umasikini!

Yule Binti akawa anasema tena yule Shemeji alikuwa anasema kwamba hizo taarifa zimfikie mama maana hatuna la kumfanya kwasababu sisi ni masikini wa kutupa,Alikuwa akilaani sana kwanini kaka yake asingeenda kuoa kwenye familia ya kitajiri akaenda kuoa kwetu kwenye familia masikini!

Hayo ndiyo yalikuwa maelezo ya yule Binti mtoto wa Shangazi!

Labda tu niseme hapa kitu ndugu zanguni

Huyu shemeji kaka yake ndo kamuoa dada yetu yule mdogo ambae wanaishi Arusha,Huyu shemeji alikuwa kaajiriwa Benki fulani hapo Mjini na amekaa sana Africa kusini,Kwahiyo hizi mbwembwe zote Alikuwa anazifanya kwakuwa alikuwa na Ajira benki na kukaa tu hapo afrika kusini!.

Baada ya hayo maelezo nilikuwa najiuliza maswali mengi sana,nilikuwa namuuliza mama kwani umasikini ni nini?,Maana sisi kama ni kula mbona tunakula?,kama ni nyumba mbona tuna nyumba?,Huyo malaya anataka maisha gani ?,au kwakuwa yeye ana gari na kufanya kazi benki ndo anadharau watu?
Toka wakati huo nilimwambia Bi mkubwa kwamba sitokaa niimtambue yule Mume wa sista kama shemeji maana dada yake alikuwa akituahibisha na kutusimanga!

Tulipomaliza yale mazungumzo niliondoka zangu pale nyumbani kuelekea Geto kwangu kulala!,Siku hiyo nzima nilikosa raha sana na kutafakari haya maisha,Nilijiona bado nina safari ndefu sana ya kuwa tajiri!

Pale nyumbani kuna jamaa mmoja tulikuwa tumepakana vyumba na alikuwa Rafiki yangu sana maana hata alipokuwa akielekea kwenye shughuli zake ambazo zilimchukua hata mwezi alikuwa akiniachia funguo!
"Mwanangu mbona leo huna raha?,una shida gani"?,Jamaa aliniuliza.

Nilimwambia nilikuwa sijisikii vizuri tu!,Huyu jamaa alikuwa akifanya kazi kampuni ya ujenzi ya Nyanza,Usiku ule nilimfuata jamaa nikamwambia kwa ujasiri mkubwa "NATAKA KUWA TAJIRI",Jamaa alioneshaa kushituka kidogo na kuniuliza "Mwanangu leo umepatwa na nini?,tafadhali nieleze ukweli"
Basi nilimsimulia yaliyonisibu na kiukweli alihuzunika sana na akanambia nisijali niende nikapumzike halafu kesho tutaongea!

Siku iliyofuata baada ya kutoka kwenye shughuli zangu za kushika chaki ilibidi nimueleze jamaa adhma yangu ya kuutafuta utajiri!
Nilimwambia jamaa "Mimi ninachotaka ni utajiri,haijalishi ni utajiri wa namna gani"

Dhumuni la mimi kutaka kuwa tajiri ni kumuonyeshea uwezo yule shemeji yangu na watu wengine waliokuwa wanatuona sisi masikini!,Kiukweli kwa wakati huo nilikuwa tayari kufanya jambo lolote!

Jamaa aliniambia tafuta nauli twende zetu kigoma maana kuna kipindi tulienda kufanya kazi ya ujenzi wa Barabara kule na kuna Bibi tuliwahi kwenda kwake alikuwa ni balaa!,Jamaa akawa anasema kipindi hicho mimi nilienda kwake kufata dawa ya kinga dhidi ya watu wabaya pale kazini hivyo sikufata utajiri,lakini safari hii nataka na mimi nikatafute dawa ya kupanda cheo na kupata pesa!,

Basi hayo mazungumzo ya jamaa yalinipa faraja kidogo nkajiona siko mpweke!

Niliendelea kutafuta pesa za nauli maana jamaa alinambia nikipata kama laki 200000/= nimshitue ili tuondoke maana yeye alikuwa tayari muda wote!
Mwezi uliofata nakumbuka ulikuwa mwezi wa 4 mwaka 2011 sikutaka kumwambia mtu yeyote na sikutaka kumuaga hata Bi mkubwa naelekea wapi!,Mtu aliyekuwa akifahamu ni huyo jamaa tuliyekuwa tukikaa nae hapo nyumbani vyumba jiarani!

Basi tulipanga safari ya kwenda kigoma na tuliondoka Mwanza siku iliyofuata!




Itaendelea..............
Tupia nyingine mkuu, tupo hapa wazee wa kasulu, kibondo!
 
Mimi nataka kujua issue ya baiskeli ya mshkaji iliishia wapi.??


Halafu tafadhali acha kuwasikiliza baadhi ya hawa maandazi wa humu, ona kipande cha mwisho kilivyo hakina ladha kama chips zilizolala kisa tu kufupisha story,

LwandaMagere wewe tuwekee details zote ikiwezekana hata ratiba za msosi wa week nzima, tunaotaka tutasoma wasotaka waende jukwaa la siasa, hatuwezi kosa utamu kisa mafurushi machache..!!
kweli kabisa kuna mijitu kazi yao ku criticize tu....wewe kama una hadith yako ya ukweli iweke hapa ubaoni...sio kuanza kukosoa tu kila kitu...kuna vitu vya kujifunza humu...ona sasa mdada wa kazi alivyoiletea shida hii familia.
 
Back
Top Bottom