Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mimi ni mtumiaji wa telegram mzuri tu shida kwanini asingezichangisha hapa hapa?? Sababu telegram ameweka kwenye private group au channel angefanya hivyo hapa pia ukituma iyo buku unatupiwa episode pm. Mambo ni yale yale sema ana agenda ya siri
Sasa kama angefanya ya kulipwa na kumtumia mtu PM. Hiyo si biashara kichaa... yaan aandike na kuanza kutupia PM za watu zaid ya 100 mmoja mmoja... watu wana mawazo balaa!!!
 
Stori ishaanza kukosa Radha Haina hata uzuri wowte yaani ,kisa huko chini itaendelea nachokushauri usilete huo mwendelezo badala ya kusema itaendelea andika hata siku mbili au tano kabisa ikisha kamilika ndo uilete hapo hakuna hata Cha kukielewa ,smart people always doing smart thing
Mpu.mbavu
 
Hata MI siwezi
Buku mkuu unadhan nashindwa??tatizo kuwepa ma app mengi kwenye simu huo mda sina,ila najua nitaisoma tu [emoji23][emoji23] ,afe kipa afe beki
Majukumu ya familia chungu nzima bado kwenye siku mtu uje na. Ma apps kama yote kisa?
 
Sasa kama angefanya ya kulipwa na kumtumia mtu PM. Hiyo si biashara kichaa... yaan aandike na kuanza kutupia PM za watu zaid ya 100 mmoja mmoja... watu wana mawazo balaa!!!
Kwani kukopi na kupest shida inakuwa nini? Au ww mgeni na simu?
 
Hii story nmeshaikosa ingawaje nmetuma buku ya mb,masimu ya kichina yakshajaa vitu vingi huwa hayaruhusu kudownload ktu,n bora utumie WhatsApp maana kila mtu anayo
ikishajaa nini?

kuna simu ikishajaa storage yake
inaruhusu kudownload vitu?

whatsapp ina limit ya watu, telegram hailimit watu
katika group..
 
watu mnapenda vya bure[emoji2][emoji2].
Hata Yesu alisema asiefanya kazi na asile
 
Inaendelea.............MWISHO


Wakuu habarini za Asubuhi,Bila shaka mko vyema mkiendelea na majuku kama kawaida!

Nimepitia comment nyingi na wengi wanalaumu mimi kurefusha uzi na kuandika kwenye stori yasiyotakiwa,Labda niseme niliamua kuandika hivi ili nieleweke wapi nilipotoka na mikasa niliyokutana nayo kwenye maisha!,Lengo la kuandika kila nilililokutana nalo kwenye huu mkasa wa kwanza ni kutoa picha na uelekeo wa mkasa wa pili ambao ni Maisha ya Yangu ya kutafuta Utajiri ambao ndani yake kuna safari ya kutisha na kugopesha!,hivyo niliona nifanye hivi ili huko mbele kwenye mkasa wa pili maswali yapungue!

Sasa kwakuwa watu wanaona kama narefusha stori ngoja niikatishe ili ikiwezekana leo leo au kesho niianze kusimulia mkasa wa pili wa Maisha yangu dhidi ya utafutaji wa maisha mazuri uliogeuka shubiri!(HAKUNA SHOTI KATI YA MAISHA,MAISHA NI KUPAMBANA KIUHALISIA)

Inaendelea...........

Japo hamkutaka nimalizie story yote lakini humo katikati niliwahi kuitwa mwizi na ilikuwa ni vurumai!


Basi bana nadhani mnakumbuka niliwaambia kwamba mauza uza pale nyumbani "YALIKUWA LIKIZO KWA MUDA",Siku moja Mzee alirudi kutoka Dar es salaam alipokuwa amehamishiwa kikazi na hatukujua ni nini kirimrudisha hapo homu ghfla hivyo!
Nadhani niliiwaambia kuna siku aliaga akasema anaelekea kwa rafiki yake mmoja Utegi!,Kumbe kule UTegi hakwenda kwa rafiki yake wala nini bali alikuwa kaenda kwa Mganga wa kienyeji,Kwa taarifa tulizozipata pale nyumbani ni kwamba,kipindi kile alipo enda kwa huyo mganga hakumkuta na ikabidi amsubiri pale nyumbani kwa mganga ambako muda huo kulikuwa na wasaidizi wake tu!

Kwahivyo Mzee ilibidi Amsubiri yule Mganga kwa muda kama wiki nzima lakini halikuwa hakurudi maana alikuwa kaenda kuagua mahala pengine, ndipo Mzee ilibidi arudi nyumbani kujiandaa na Safari ya Dar es salaam!
Sasa kumbe ule ujio wa mzee inaonekana aliwasiliana na huyo Mganga na akamwambia safari hii aende atamkuta!,Basi Mzee baada kama ya siku tatu akaondoka na kauli yake ile ile ya anaenda kuonana na rafiki yake kule Utegi!,Kweli tumekaa pale nyumbani siku hiyo ikapita na siku iliyofuata nakumbuka ilikuwa kama mida ya 10 jioni mi narudi zangu maskani kutoka Shule naingia Ndani nakutana na kikao hapo sebuleni,Alikuwepo Yule mama mdogo pamoja na Masista wakizungumza!,Ndipo nilipoambiwa Muda si mrefu Yule kiumbe wa Ajabu Ashura alikuwa hapo na katoka kuwaambia kila kitu alichokuwa anakifanya Mzee na safari ya yeye kwenda Utegi,sasa kabla ya Ashura kuondoka aliwaambia wajiandae kufanya msiba maana Mzee Atarudi na hatomaliza siku pale nyumbani!

Kiukweli mimi nilidhani ni kama maigizo lakini ndivyo ilivyokuwa,Maana Ashura aliwahi kusema yeyote atakayejifanya kwenda kwa mganga kwa ajili yake ina maana alikuwa anataka kumuua yeye au kumsababishia matatizo kutoka kwa ndugu zake ikiwemo kuuliwa!,Akasema sasa kabla ya yeye hayo hayajamkuta inapaswa huyo anayetekeleza huo ujinga afe yeye kwanza!,Pia aliwahi kusema ni marufuku kuomba au kusoma vitabu Vitakatifu,Hili agizo walitoa wale waliokuwa wanafahamika kama wazazi wake!

Basi bhana baada ya siku kadhaa mzee alireje a pale nyumbani na Masista walimsimulia yote yaliyosema na Ashura na Mzee akawaambia" nilienda huko kwa ajili yenu wanangu,na kwa ajili ya kazini kwangu"!
Mzee akimaliza siku hiyo bali damu zilianza kumtoka puani kama maji,Sista mkubwa ilibidi ampigie simu Mama na kumuleza hali namna ilivyokuwa!
Lakini ndugu zangu mpaka Bi mkubwa anarudi nyumbani ndipo alikuta tayari kuna Msiba wa Mzee (R.I.P),Mzee alizikwa kwenye makaburi ya Ronsoti(Wenyeji wa Tarime watakuwa wanayafamu),Kiukweli hali ilikuwa mbaya sana na ukizingatia mzee tena ndo alikuwa nguzo ya familia na Mzee wetu kidogo alikuwa na vipesa vya hapa na pale maana kwa wakati huo kukaa maeneo hayo ya Bomani haikuwa kazi nyepesi sana!,wakazi wa Tarime nadhani watakuwa wanaelewa vizuri hayo maeneo!

Basi baada ya Msiba wa mzee ni kama familia nzima ilikumbwa ni mikosi maana Maza nae ile kampuni yao ya ujenzi aliyokuwa akifanyia kazi ni kama ilifilisika,sikujua ilikumbwa na nini maana kipindi kile sina ufahamu sana wa haya mambo ya kufilisika,Lakini Bi mkubwa alisimama kwenda kazini!

Maisha yalivyozidi kuwa magumu kuna yule Shangazi yetu aliyekuwa akikaa mwanza alimshauri Bi Mkubwa atafute pesa na akafanye biashara huko Mwanza!,Bi mkubwa wazo la kuuiuza ile nyumba yetu lilimjia na ndipo alipotuita wanae wote pamoja na yule aliyekuwa kwa Shangazi Mwanza na akatushirikisha na sote tulikubaliana ukizingatia Nyumba yenyewe ilikuwa na Mauza uza,mpaka wakati huo hakuna ambaye alielewa mauza uza ya pale nyumbani ila ilikuwa ni siri ya familia!

Ndani ya siku kadhaa mwaka huohuo ilibidi mimi sasa nitafutiwe uamisho wa kuelekea kusoma Mwanza na kiukweli sote tulihamia Mwanza,sikutaka kufahamu ile nyumba aliuziwa nani na ilikuwaje,mi nilichojua ni kwamba Tumehamia Mwanza na maisha ya Mwanza yakaanza kama kawaida!

Ninapoandika hiki kisa Bi mkubwa Tayari pia ni Marehemu,Mimi ninaishi Dar es salaam now,Dada yangu Mkubwa yupo hapo Mwanza kaolewa na Yule Sista Mdogo nae yupo Arusha kaolewa!


............................................................


Sasa kabla ya kuuanza Mkasa wa pili wa mimi kwenda kuusaka utajiri na chanzo chake kikiwa ni dharau na maisha magumu,naomba niruhusu maswali kama yapo ili nikianza kisa cha pili ni kupepea tu!

Karibuni kama kuna maswali
Baada ya kuambiwa kuwa Ashura ana vitu ameviacha kwenye nyumba kwa nini msingeisafisha nyumba yoote kila mtu ashike chake ili kujua ambavyo haviwahusu vichomwe moto.
 
Swali moja nauliza, moja ya masharti muhimu na kuu kabisa aliambiwa ahakikishe anakua na chumba kimoja ambacho ataingia peke yake.

Ilikuaje akawa anaingia na wanawake kwenye geto lake kuwapiga kimkakati na chumba hichohicho ndio ameweka mitambo yake?

Tokea mwanzo ningeshangaa sana hizi chengachenga zisingetokea, nilivyoona tu nimeokoka na kumpokea Yesu huku kuna baadhi ya maneno anaandika hadi Carleen anaenda madhabahuni kutubu, nikajua tunatengenezwa tujae vizuri...kisha akapima upepo kwa kusema watu wamemwendea PM asitishe wanunue stori...nikajua maandiko yametimia kama ilivyonenwa na manabii.

Hata hivyo kuna mengi nimejifunza. Tunashukuru kwa yote hadi kufikia hapa.

Kitoabu anaendelea kubaki Mlume Ndago wa ukwelikweliiii. Akianza, anamaliza hakuna vumbi vumbi.
 
Back
Top Bottom