Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Kuna mdogo angu akikosa kuvuta bangi for 2 days anasema Nina alolo!

Na Mimi nasema Nina alolo na epsod 12
 
Sio nyingine tu ni nyingi tu ,nimeagiza mzinga hapa nasukutua na hadithi murua kabisa
 
Mhmm what next??? sacrifice on my mind never do it brother, wacha tuendelee kunywa mchuzi nyama tutazikuta chini........
 
Ushasoma ya msiti wa Nairoto ya mzee baba Kitoabu ?? Bila shaka kwangu ni #1
Kuna stori inaitwa Siri za Utajiri wa Bazoka sijui

Nzuri sema yule mtunzi kama The Bold tu

Akiweka leo anasubiri wiki mbili
 
MKASA WA PILI -sehemu ya 11

Inaendelea................


Baada ya kuitupa ile line ya simu nilikaa kwa kutulia nikiwaza na kuwazua!," Ina maana kuhangaika kote siku kadhaa za kuitafuta hiyo hela leo hawa majinga wanataka kututoa uhai kisa shilingi 100"?,Nilijisemea!

Basi nilimwambia dogo ahakikishe Anakaa kwa kutulia mpaka hali itakapokuwa shwari maana nilijua wale jamaa wangeendelea kumtafuta pale Bunda hasa ukizingatia mji wenyewe haukuwa mkubwa hivyo!

Kesho yake ilibidi mimi niondoke Pale kwa Mama mdogo kurudi Mwanza maana niliona kila kitu kilikuwa kimeshaharibika!,Nikajisemea ni heri nkaishi masikini kuliko kuendelea kukaa hapo kwa wasiwasi huku maisha yangu yakiwa rehani!
Niliondoka hapo nyumbani Bunda na sikutaka dogo anisindikize maana nilijua anaweza kukamatwa na wale mafia hatimaye mambo yakaharibika!

Niliingia Mwanza mnamo mida ya saa 8 mchana na nilimweleza Bi mkubwa kila tukio lililo kuwa limetokea kwa siku hizo!

Basi kwakuwa siku na kazi ya kufanya kwa wakati huo nilitafuta shule kadhaa pale mjini wa kufundisha tuition,kwa bahati nzuri kuna shule fulani niliipata pale Mjini ambayo nilipewa ajira temporary ya kuwa mwalimu wa History na Geography na nilikuwa nalipwa kila Mwezi 150000/=Nilimshukuru Mungu sana hasa ukizingatia sikuwa na chochote!,Kwahiyo nilikuwa nikitoka kwenye vipindi mchana jioni nilikuwa naenda kuwafundisha wanafunzi niliokuwa nao kwa wakati ule kabla sijaenda Geita na walikuwa wakinilipa 3000 kwa kila topic tunayomaliza!

Baada ya kukaa pale nyumbani kwa muda nilimwambia Bi mkubwa ni wakati sasa na mimi niende kupanga chumba changu ili nijitegemee!,Bi mkubwa alikaataa na akasema nyumba bado ni kubwa na mimi sipaswi kuondoka hapo nyumbani!,Niliona kama Bi mkubwa kanibana maana kuna mitikasi yangu niliona kama haitaenda!,Niliendelea kumsihi Bi mkubwa kwamba ntaenda kupanga ila ntakuwa sikauki pale nyumbani,Baada ya kumsihi sana Bi mkubwa alikubali na akanitaka endapo maisha yakinishinda basi nirudi nyumbani!

Nilikuwa namuhurumia sana Mama yangu kiukweli na nilimpenda sana japo sikuwa na kitu!
Kwakuwa kuna vihela vyangu nilikuwa nimevikusanya kwa wakati huo nilienda kutafuta chumba nkalipia miezi 3 na nkanunua godoro na vyombo kadhaa vya kupikia,nilinunua pia na vitu kadhaa vya ndani na kadri siku zilivyoenda nilipokuwa nikilipwa nilikuwa nikinunua vitu taratibu!

Maisha yalisonga na muda ukayoyoma!,Hatimaye Mungu akasaidia nikauona Mwaka 2011.

Sasa siku moja wakati nikiwa homu Bi mkubwa alinipigia simu akataka niende kule nyumbani maana kuna maongezi!
Basi nkajianda nkasepa zangu mpaka nyumbani,Nilipofika nilimkuta Yule sista mkubwa kaja,Bi mkubwa pia alikuwepo pamoja na wale mabinti waliokuwa wakikaa hapo kwa Bi mkubwa watoto wa Shangazi!
Bi mkubwa alisema ametuita hapo kwasababu kuna jambo kalisikia si zuri!,Nilimuuliza bi mkubwa ni jambo gani hilo?

Ndipo binti mmoja wa Shangazi aliyekuwa mkubwa kuliko yule Mwenzake akawa nasema alikutana na Shemeji yangu mmoja hivi ambaye kwa upande wa Ma sista alikuwa ni wifi yao,kuna maneno aliongea ambayo hayakuwa mazuri!,Yule binti akawa anasema alikutana na Yule shemeji kanisani akawa anamwambia kwamba sisi hapo nyumbani ni Masikini na anajuta hata kaka yao kuuoa hapo nyumbani kwenye ukoo masikini!,Yule shemeji aliendelea kusema kwamba anaogopaga hata kuwapeleka rafiki zake ukweni kwasababu tunanuka umasikini!

Yule Binti akawa anasema tena yule Shemeji alikuwa anasema kwamba hizo taarifa zimfikie mama maana hatuna la kumfanya kwasababu sisi ni masikini wa kutupa,Alikuwa akilaani sana kwanini kaka yake asingeenda kuoa kwenye familia ya kitajiri akaenda kuoa kwetu kwenye familia masikini!

Hayo ndiyo yalikuwa maelezo ya yule Binti mtoto wa Shangazi!

Labda tu niseme hapa kitu ndugu zanguni

Huyu shemeji kaka yake ndo kamuoa dada yetu yule mdogo ambae wanaishi Arusha,Huyu shemeji alikuwa kaajiriwa Benki fulani hapo Mjini na amekaa sana Africa kusini,Kwahiyo hizi mbwembwe zote Alikuwa anazifanya kwakuwa alikuwa na Ajira benki na kukaa tu hapo afrika kusini!.

Baada ya hayo maelezo nilikuwa najiuliza maswali mengi sana,nilikuwa namuuliza mama kwani umasikini ni nini?,Maana sisi kama ni kula mbona tunakula?,kama ni nyumba mbona tuna nyumba?,Huyo malaya anataka maisha gani ?,au kwakuwa yeye ana gari na kufanya kazi benki ndo anadharau watu?
Toka wakati huo nilimwambia Bi mkubwa kwamba sitokaa niimtambue yule Mume wa sista kama shemeji maana dada yake alikuwa akituahibisha na kutusimanga!

Tulipomaliza yale mazungumzo niliondoka zangu pale nyumbani kuelekea Geto kwangu kulala!,Siku hiyo nzima nilikosa raha sana na kutafakari haya maisha,Nilijiona bado nina safari ndefu sana ya kuwa tajiri!

Pale nyumbani kuna jamaa mmoja tulikuwa tumepakana vyumba na alikuwa Rafiki yangu sana maana hata alipokuwa akielekea kwenye shughuli zake ambazo zilimchukua hata mwezi alikuwa akiniachia funguo!
"Mwanangu mbona leo huna raha?,una shida gani"?,Jamaa aliniuliza.

Nilimwambia nilikuwa sijisikii vizuri tu!,Huyu jamaa alikuwa akifanya kazi kampuni ya ujenzi ya Nyanza,Usiku ule nilimfuata jamaa nikamwambia kwa ujasiri mkubwa "NATAKA KUWA TAJIRI",Jamaa alioneshaa kushituka kidogo na kuniuliza "Mwanangu leo umepatwa na nini?,tafadhali nieleze ukweli"
Basi nilimsimulia yaliyonisibu na kiukweli alihuzunika sana na akanambia nisijali niende nikapumzike halafu kesho tutaongea!

Siku iliyofuata baada ya kutoka kwenye shughuli zangu za kushika chaki ilibidi nimueleze jamaa adhma yangu ya kuutafuta utajiri!
Nilimwambia jamaa "Mimi ninachotaka ni utajiri,haijalishi ni utajiri wa namna gani"

Dhumuni la mimi kutaka kuwa tajiri ni kumuonyeshea uwezo yule shemeji yangu na watu wengine waliokuwa wanatuona sisi masikini!,Kiukweli kwa wakati huo nilikuwa tayari kufanya jambo lolote!

Jamaa aliniambia tafuta nauli twende zetu kigoma maana kuna kipindi tulienda kufanya kazi ya ujenzi wa Barabara kule na kuna Bibi tuliwahi kwenda kwake alikuwa ni balaa!,Jamaa akawa anasema kipindi hicho mimi nilienda kwake kufata dawa ya kinga dhidi ya watu wabaya pale kazini hivyo sikufata utajiri,lakini safari hii nataka na mimi nikatafute dawa ya kupanda cheo na kupata pesa!,

Basi hayo mazungumzo ya jamaa yalinipa faraja kidogo nkajiona siko mpweke!

Niliendelea kutafuta pesa za nauli maana jamaa alinambia nikipata kama laki 200000/= nimshitue ili tuondoke maana yeye alikuwa tayari muda wote!
Mwezi uliofata nakumbuka ulikuwa mwezi wa 4 mwaka 2011 sikutaka kumwambia mtu yeyote na sikutaka kumuaga hata Bi mkubwa naelekea wapi!,Mtu aliyekuwa akifahamu ni huyo jamaa tuliyekuwa tukikaa nae hapo nyumbani vyumba jiarani!

Basi tulipanga safari ya kwenda kigoma na tuliondoka Mwanza siku iliyofuata!




Itaendelea..............
Aloo umejilipua.. Ila acheni ukiwa maskini una dharaulika sana.
 
kweli kabisa kuna mijitu kazi yao ku criticize tu....wewe kama una hadith yako ya ukweli iweke hapa ubaoni...sio kuanza kukosoa tu kila kitu...kuna vitu vya kujifunza humu...ona sasa mdada wa kazi alivyoiletea shida hii familia.
Wabongo huwawezi mkuu,
 
Hata kama wana kamati watachukia lakini lazima tukubali maelezo yamekuwa mengi yasiyo na maana yoyote[emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125][emoji125]
Si uache kusoma, kwan lazima uisome hii hadithi??? Ina meneno mengi unaona sio matakwa yako. Tunga yako yenye maneno nachache kisha uisome mwenyewe!!!
 
Si uache kusoma, kwan lazima uisome hii hadithi??? Ina meneno mengi unaona sio matakwa yako. Tunga yako yenye maneno nachache kisha uisome mwenyewe!!!
Tulishamaliza hii
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 5


Inaendelea.............


Asubuhi kulipokucha ilitubidi tuamke Asubuhi ya saa 12 maana tuliambiwa kupata magari ya huko Bukima ni mpaka tupitie Musoma,Tulifanikiwa kuondoka mimi na Huyo dogo Mtoto wa Ma mdogo!,ilibidi tukae barabarani kusubiri Hiace zinazoenda Musoma,Kiukweli mimi mpaka wakati huo nilibaki na 48000/= tu,Nauli ya kutoka Bunda kwenda Musoma kwa wakati huo ilikuwa 3000 hivyo nilivyolipia naulia ya watu wawili nilibakiwa na 42000/=,Basi safari ikaanza na ilituchukua kama lisaa kufika Musoma,Hiyo ilikuwa yapata kama saa 2 kasoro dakika kadhaa!
Tulipofika pale stendi ya Musoma hatukutaka kupoteza Muda maana tuliambiwa hapo huwa kuna gari moja la kuelekea Huko Bukima na endapo tungelikosa ingetubidi tulale!,Kweli!,kuna basi moja tulikukuta pale stendi likiwa limechoka sana!,ilikuwa ni aina fulani ya magari ya zamani!,ilibidi niulizie nauli!,Konda akasema nauli ya kutoka Musoma Mpaka huko tunakoenda ni 5000 maana barabara si nzuri!,Ila akatuambia ili gari lenyewe linaitishia njiani na akasema kuna kijiji kinaitwa MRANGI ndo wao wataishia hapo!,Ilibidi nimuulize kwani kutoka hapo nyinyi mnapoishia na huko Bukima kuna umbali gani?,Jamaa alisema si mbali ila tungefika hapo angefanya namna ili sisi tuendelee na safari!,Jamaa alisisitiza sana kwamba kwa wakati huo pale stendi hakukuwa na gari lingine la kuelekea huko!

Sasa kwasababu sisi hatukuwa wenyeji nilimwambia dogo ngoja nilipe nauli twende zetu maana tunachoenda kukifata ni kikubwa sana kuliko kitu chochote!,Basi nilitoa elfu 10000/= nkampa yule konda,Baa ya kumpa akasema gari itaanza safari mida ya saa 5 Asubuhi hivyo kama mnazunguka nyie zungukeni ila msiende mbali sana!
Kwakuwa tulitoka homu Bunda Bila kupata chochote kitu nilimwambia dogo twende tukatafute sehemu wanauza chai tunywe!

Kwa bahati nzuri tulipozunguka tu nyuma kidogo ya stendi kuna mama tulimkuta akichoma vitumbua,hivyo tulikaa hapo tukaagiza na chai tukaanza kunywa!,mpaka hapo mfukoni nilibaki kama 30000/= maana hapo kwenye chai tulitumia kama 2000/=,Basi baada ya kupata chai na vitumbua nikamwambia dogo tusikae sana mbali maana hatukuwa wenyeji hapo Musoma,Hiyo ilikuwa mida ya saa 3 Asubuhi hivyo tulikuwa kama na masaa 2 mbele!,Masaa yaliposogea ilibidi na sisi tusogee kwenye gari na baada ya muda ule alotuambia konda kufika!,kweli! gari lilianza kuondoka,watu walikuwa wengi kwenye gari na wengine walisimama na kiukweli nilisema yawezekana gari lilikuwa lile tu maana yangekuwepo mengi basi watu wasingesimama!

Ilikuwa ni safari ya muda mrefu kidogo,Kuna jamaa nilimuuliza hiyo safari huwa inachukua muda gani hadi kufika,Jamaa alisema kutokana na gari kusimama simama njiani ni Takribani kama Masaa 2 : 30,Baada kama ya masaa 3 na ushee gari lilifika mwisho na baada ya kuuliza tuliambiwa hapo ni sehemu moja ambayo bado naikumbuka jina ilikuwa inaitwa Mrangi!,Basi tulitelemka pale na nkamfata dereva nkamueleza kwamba sisi tulikuwa tunaenda Bukima na yule jamaa aliyekuwa anakata tiketi alituambia tukifika hapa angetufanyia namna ya kufika huko Bukima!
Yule dereva alisikitika sana "Yule jamaa ni mpumbavu,kwanini hakuwaambia kwamba kuna Hiace ya Bukima?",Jamaa akaendelea kusema kwamba "Maana kutoka hapa mpaka Bukima bado kuna umbali,lakini subirini kuna watu hapa niongee nao huwa wanakodisha baiskeli kama vipi wawapeleke,japo itachukua muda maana ni mbali"
Ilibidi tuwe wapole maana tayari tulishaingizwa cha kike na yule Mpiga debe tuliyemkuta akikata tiketi,Kumbe nia yake ni sisi tulipe ili yeye apate posho!,Tufike au tusifike hilo lilikuwa halimihusu tena!

Jamaa alituitia vijana wawili pale na akaanza kuongea nao kwa Lugha ya kwao,nadhani ilikuwa ni Wajita,Basi wale jamaa wakamwambia jamaa kwa ki-lugha kwamba tuwalipe 5000 wote wawili!,Hatukuwa na namna ilibidi niwape ile hela na wakatuchukua mimi na dogo kila mmoja kwenye baiskeli yake na safari ikaanza,Hiyo ilikuwa yapata kama saa 9 Alasiri!,Basi safari ilikuwa ndefu kidogo na tuliingia Hapo Bukima mnamo saa 10 kasoro kuelekea 11!

Tulivyofika hapo Bukima hatukupoteza Muda ilibidi sasa tuanze kumuulizia yule Mganga tuliyeelekezwa na yule Dingi wa Bunda!,Kwa bahati nzuri hakuwa mgeni sana pale Bukima maana ule mji haukuwa mkubwa bali ilikuwa kama ki-center fulani hivi!,Basi tukianza safari ya kuelekea kwake tukiongozwa na dogo mmoja tuliyemkuta pale center ya Bukima!,Kwa kuwa tulikuwa wageni watu walikuwa wakitushangaa,nadhani kwakuwa ilikuwa center ndogo hivyo watu au wenyeji wengi wanafahamiana!Hivyo ukiwa mgeni ilikuwa ni rahisi sana kufahamika!,yule Mzee(Mganga),Tulifika kwake na alikuwa akiishi nje kidogo ya center na ilikuwa karibu na ziwani,maana ulikuwa ukikaa nje ya nyumba ya Huyo mzee ziwa lilikuwa kama mita 300 hivi!
Tulimsalimia Mzee na tukajitambulisha kwake!,tulimweleza ya Kwamba tuliagizwa kwake na Mzee yule wa Bunda,kiukweli alionyesha kumfahamu yule mzee na alikuwa akituuliza hali yake vipi!

Basi baada ya mazungumzo kadhaa hapo ilibidi tumueleze kilichotupeleka hapo kwake!

Baada ya kutusikiliza kwa muda mrefu alituambia ya kwamba kuna watu fulani waliwahi kwenda hapo kama miaka 2 iliyopita na wao walikuwa wakitafuta zile pesa zilizokuwa na tundu katikati,kwakuwa kwa wakati huo alikuwa nazo ilibidi awape na walimpa pesa!,Sasa sisi alituuliza endapo hiyo shilingi 100 ya Mwaka 1993 ingepatikana tungempa kiasi gani?,Kiukweli Moyo ulipiga Paaah!mawazoni nilikuwa naamini ya kwamba sasa naenda kuuaga Umasikini na utajiri ulikuwa ushafika mlangoni,kazi iliyokuwepo ni kufungua tu mlango uingie ndani!
Nilimwambia mzee endapo tungekipata hicho ki hela basi tungempa laki 200000/=,Yeye alituuliza "Nyinyi mkikipata mnaenda kupata bei gani"?,Ilibidi nimdanganye Yule Mzee ya kwamba sisi tumeambiwa tukikipeleka tunalipwa milioni moja hivyo endapo tungekuwa wewe hiyo laki 200000/=,sisi tungebaki na laki 800000/=ambayo tutagawana na mwenzangu maana kuna gharama pia zimetumika mpaka kufika hapo!

Basi yule mzee alisema funguo za Sanduku ambamo zime hela mbalimbali za miaka ya nyuma anazo mke wake ambaye kwa wakati ule hakuwepo,Alituambia tumsubiri na akatusihi ya kwamba kwakuwa jioni ilishaingia hatuna budi tulale pale!,Basi mimi na dogo ilibidi twende ziwani tukashangae shangae huku tukibadilisha mawazo!,Ilipofika saa 12 jioni tulirudi hapo nyumbani kwa huyo mzee na siku hiyo yule mzee alichinja Bata kwa ajili ya kitoweo!
Yule mzee kiukweli sikuona uganga wowote alokuwa nao maana hata pale kwake hatukukuta watu bali walikuwa watu wa familia yake!,Nadhani kama alikuwa mganga basi ni wale wasiyokuwa na mbwembwe nyingi!

Jioni ile Mkewe alirudi akiwa na baiskeli kafunga mzigo nyuma na alipokewa na kijana wake mmoja tulimkuta pale!,Kwakuwa sasa usiku ulishaingia Mzee alituambia zoezi litafanyika kesho Asubuhi!,Basi usiku ule tulipata zetu ugali wa muhogo na Bata,kiukweli Msosi ule ulikuwa umeenda skuli kwa namna ulivyokuwa na kiwango!,Baada ya chakula ilibidi kile chumba alichokuwa kuwa analala yule kijana wa yule mzee tulale sisi na yeye nadhani alienda kulala kwa jirani au rafiki!,Siunajua tena mambo ya vijijini suala la wapi pa kulala huwaga halisumbui!Siyo kama mjini!

Itaendelea...................
Nimeona umezungumzia Ile pesa yenye Tundu katikati ninayo hyo!
 
Mkuu mkuu mkuu

Fanya kudondosha episode moja chap nshaagiza castle lager apa nakusubiri wewe tu badae niangalie mpira wa manchester united nisogezee mda kidogo

[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom