LwandaMagere
JF-Expert Member
- Mar 15, 2020
- 264
- 2,484
- Thread starter
- #661
MKASA WA PILI - sehemu ya 12.
Inaendelea.............
Tuliondoka Mwanza majira ya saa 12 asubuhi,ile njia kuipita mwisho wangu ulikuwa Katoro Geita,lakini kuelekea huko mbele sikuwahi kufika na hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza,nilibeba kibegi kidogo nikaweka nguo za kubadilisha,jamaa yangu yeye alienda akiwa amevaa nguo alizokuwa nazo tu,nikasema uenda safari kama zile yeye alikuwa ni mzoefu!.Ile safari ilikuwa ndefu sana,jamaa aliniambia tukifika Kasulu tungeshuka maana baada ya kufika hapo Kasulu ingetubidi tuelekee kijiji kimoja kinaitwa Munyegera.Ilituchukua masaa 9 mpaka kufika Kasulu mjini,kwakuwa bado ilikuwa mapema jamaa aliniambia tutafute kwanza sehemu wanayouza chakula tule.
Baada ya kumaliza kupata chakula jamaa aliniambia tutafute usafiri wa kuelekea huko kijijini Munyegera,Kwa kuwa mimi ndo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika hapo kasulu nilikuwa nikishangaa yale mazingira ya mji wa Kasulu yalivyokuwa.Nchi ya Tanzania ni kubwa sana,sikuwahi kudhani kama ipo siku ningefika Kasulu,jamaa akaniambia inabidi tuchukue bodaboda mpaka huko kijiji cha Munyegera,Kwakuwa jamaa alikuwa mwenyeji mimi sikuwa na shaka yeyote.
Tulimuita muendesha boda mmoja akawa amekuja kutusikiliza,jamaa alioongea naye akakubali kutupeleka Munyegera kwa elfu 15 kwa wote wawili.Tulianza safari ya kuelekea huko Munyegera na ilituchukua saa 1:30 mpaka kufika,baada ya kufika tulimpa hela yake jamaa akaondoka zake na sisi kuianza safari ya kutembea kwa miguu kuelekea maporini!.Ilikuwa tayari ishaingia giza lakini hatukujali tuliendelea kuchanja mbuga!,mfukoni wakati huo mimi nilikuwa nina laki tatu,jumla ya pesa niliyobeba ilikuwa laki tatu na sabini(370000/=),hivyo ukijumlisha nauli pamoja na mambo mengine humo njiani nilibaki na laki tatu,sikutaka kupata shida kama niliyoipata hapo nyuma wakati tunaitafuta ile sarafu,japo wakati tuko Mwanza jamaa aliniambia nitafute laki mbili lakini mimi niliamua kujiongeza.
Basi baada ya kutembea kwa muda mrefu hatimaye tulifika hapo nyumbani kwa huyo mama mganga na tulipokelewa na mabinti wawili waliyokuwa hapo,Kuna watu tuliwakuta pale ilibidi nimuulize jamaa mwenyeji wangu akaniambia hao pia walikuwa pale wamefata tiba!,akili yangu mara zote nilipokuwa ugenini,ilikuwa ni mawazo ya namna ya kupata mahali pa kulala tu!.Kwakuwa ilikuwa ishafika usiku tulikuta umekokwa moto,kuna raia wengine walikuwa wakiota moto pale huku wakiendelea kupiga stori za hapa na pale kwa kiswahili chenye lafudhi ya Kiha!.
Jamaa aliniambia "ngoja niende kumuona mama mganga kama yupo halafu narudi".
Baada ya dakika kadhaa alirudi na kuniambia msaidizi wa yule mama kamwambia yule mama hayupo ila angerudi asubuhi,hata hao watu tuliowakuta walikuwa wakimsubiri yeye!,Kwakuwa baridi ishaanza kuwa kali ilibidi mimi na jamaa tusogee kwenye moto,tulikaa hapo chini ya mkeka mpaka mimi usingizi ukanipitia,nilishituka nikakuta bado jamaa wako macho wakiendelea kupiga stori,niliendelea na hiyo hali ya kulala na kushituka mpaka kulipo pambazuka!,Kuna jamaa tulimkuta pale kazi yake ilikuwa ni kuongeza magogo tu kwenye ule moto kila ulipoonyesha hali ya kufifia!.
Asubuhi kila mtu alikuwa na ishu zake,niliona kila mtu alikuwa amekaa na mtu ambaye walikuwa wakifahamiana naye!,Yule mama mganga tuliambiwa alikuwa amerudi,nilijiuliza alirudi vipi wakati usiku huo wote hakukuwa na mtu mwingine aliyeingia hapo? nikakosa majibu!.Watu tuliowakuta hapo ndiyo walioanza kuingia ndani kwenye nyumba ya mganga na kuelezwa walichoelezwa,kuna wengine walikuwa wakitoka wanaondoka jumla na kuna wengine walikuwa wakitoka wanarudi tena nje kukaa nadhani waliambiwa wasubiri!.Tulikaa kwa muda mrefu ndipo zamu yetu ilipofika tuliitwa na msaidizi wa yule mama,tuliambiwa tunaingia mmoja mmoja ndani,ndipo mimi nikamwambia yule jamaa yangu aanze yeye!.Jamaa alikaa humo ndani kama nusu saa halafu akatoka akaniambia na mimi niende ndani.Nilipofika ndani nilimsalimia Yule mama ambaye hakuwa mzee sana kama nilivyofikiria,kabla sijaanza kuongea naye aliniambia ninyamaze maana maisha yangu yote toka tukiwa Tarime mpaka nimefika hapo kwake alikuwa anayafahamu hivyo akaniambia nimwambie kilichokuwa kimenipeleka kwake!,kiukweli aliponiambia anayafahamu maisha yangu Tangu nikiwa Tarime nilishangaa sana!.Hivyo ilibidi nimueleze kwamba ninataka kuwa tajiri,aliniangalia akawa anatikisa kichwa tu,kisha akaniambia "Mbona mwanangu umeharibiwa sana"!,huwezi kuwa tajiri mpaka usafishwe kisawa sawa!".
Akaendelea kuniambia kwamba "nyota ya marehemu baba yako unayo wewe,ila kuna kitu kimekuzuia usiipate,kitu hicho ndicho kinafanya nyota ya baba yako ising'ae kwako ili uwe tajiri".
Akaniambia yeye atanisafisha na kunipa dawa ya kinga ili chochote kibaya kitakachonisogelea basi kiende na maji!,akaniambia baada ya kunisafisha itanipaswa niende mpaka Kigoma halafu nivuke ng'ambo ya pili upande niingie upande wa Kongo sehemu moja inaitwa Kalemii,huko kuna mtu ambaye angeniondolea hilo tatizo hatimaye nyota ya baba yangu niipate mimi ili niwe tajiri.Kiukweli nilivuta pumzi sana maana nilifahamu nilikuwa nimemaliza kazi kumbe ndiyo kwanza kazi ilikuwa haijaanza!,aliniambia itanibidi nikae pale kwake siku tatu ili akimaliza kuwashughulikia wale wagonjwa wengine niliyowakuta ndipo nianze dozi!.Nilipomaliza kuongea na yule mama ilibidi nitoke nje kuongea na yule jamaa aliyenipeleka,baada ya kumsimulia kila kitu jamaa kashangaa sana!.
Jamaa akaniambia "Mwanangu jipe moyo,kwakuwa umeamua pasipo kulazimishwa inakupasa uwe na uvumilivu".
Yule mama alitoka nje na kuanza kuongea na wateja wake,alipofika kwetu alimwambia yule jamaa yangu kwamba "huyu mwenzio bado nina kazi naye!,Wewe kama utamsubiri endelea kumsubiri,lakini akimaliza hapa bado anasafari nyingine!".
Jamaa tuliongea naye na hakuwa na namna ilibidi aondoke akawahi kazi zake lakini akaniambia mimi ni mwanaume nijipe moyo!.Nilimwambia jamaa endapo nisingerudi nyumbani kwa chochote ambacho kingenipata basi anichukulie vile vyombo vyangu anipelekee nyumbani kwetu Nyegezi,jamaa alikubali!,jamaa aliniaga na akaniongezea laki moja tena ila nilimwambia ningerudi ningemrudishia hiyo hela.Wakati jamaa anaondoka nilijikuta nalia kama mtoto maana sasa nilijiona bado nilikuwa nina safari ndefu ukizingatia nilikuwa mgeni hayo maeneo.Nilijipa moyo sana maana niliona ningekata tamaa hakuna ambacho ningefanikisha!.
Itaendelea..............
Inaendelea.............
Tuliondoka Mwanza majira ya saa 12 asubuhi,ile njia kuipita mwisho wangu ulikuwa Katoro Geita,lakini kuelekea huko mbele sikuwahi kufika na hiyo ndiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza,nilibeba kibegi kidogo nikaweka nguo za kubadilisha,jamaa yangu yeye alienda akiwa amevaa nguo alizokuwa nazo tu,nikasema uenda safari kama zile yeye alikuwa ni mzoefu!.Ile safari ilikuwa ndefu sana,jamaa aliniambia tukifika Kasulu tungeshuka maana baada ya kufika hapo Kasulu ingetubidi tuelekee kijiji kimoja kinaitwa Munyegera.Ilituchukua masaa 9 mpaka kufika Kasulu mjini,kwakuwa bado ilikuwa mapema jamaa aliniambia tutafute kwanza sehemu wanayouza chakula tule.
Baada ya kumaliza kupata chakula jamaa aliniambia tutafute usafiri wa kuelekea huko kijijini Munyegera,Kwa kuwa mimi ndo ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika hapo kasulu nilikuwa nikishangaa yale mazingira ya mji wa Kasulu yalivyokuwa.Nchi ya Tanzania ni kubwa sana,sikuwahi kudhani kama ipo siku ningefika Kasulu,jamaa akaniambia inabidi tuchukue bodaboda mpaka huko kijiji cha Munyegera,Kwakuwa jamaa alikuwa mwenyeji mimi sikuwa na shaka yeyote.
Tulimuita muendesha boda mmoja akawa amekuja kutusikiliza,jamaa alioongea naye akakubali kutupeleka Munyegera kwa elfu 15 kwa wote wawili.Tulianza safari ya kuelekea huko Munyegera na ilituchukua saa 1:30 mpaka kufika,baada ya kufika tulimpa hela yake jamaa akaondoka zake na sisi kuianza safari ya kutembea kwa miguu kuelekea maporini!.Ilikuwa tayari ishaingia giza lakini hatukujali tuliendelea kuchanja mbuga!,mfukoni wakati huo mimi nilikuwa nina laki tatu,jumla ya pesa niliyobeba ilikuwa laki tatu na sabini(370000/=),hivyo ukijumlisha nauli pamoja na mambo mengine humo njiani nilibaki na laki tatu,sikutaka kupata shida kama niliyoipata hapo nyuma wakati tunaitafuta ile sarafu,japo wakati tuko Mwanza jamaa aliniambia nitafute laki mbili lakini mimi niliamua kujiongeza.
Basi baada ya kutembea kwa muda mrefu hatimaye tulifika hapo nyumbani kwa huyo mama mganga na tulipokelewa na mabinti wawili waliyokuwa hapo,Kuna watu tuliwakuta pale ilibidi nimuulize jamaa mwenyeji wangu akaniambia hao pia walikuwa pale wamefata tiba!,akili yangu mara zote nilipokuwa ugenini,ilikuwa ni mawazo ya namna ya kupata mahali pa kulala tu!.Kwakuwa ilikuwa ishafika usiku tulikuta umekokwa moto,kuna raia wengine walikuwa wakiota moto pale huku wakiendelea kupiga stori za hapa na pale kwa kiswahili chenye lafudhi ya Kiha!.
Jamaa aliniambia "ngoja niende kumuona mama mganga kama yupo halafu narudi".
Baada ya dakika kadhaa alirudi na kuniambia msaidizi wa yule mama kamwambia yule mama hayupo ila angerudi asubuhi,hata hao watu tuliowakuta walikuwa wakimsubiri yeye!,Kwakuwa baridi ishaanza kuwa kali ilibidi mimi na jamaa tusogee kwenye moto,tulikaa hapo chini ya mkeka mpaka mimi usingizi ukanipitia,nilishituka nikakuta bado jamaa wako macho wakiendelea kupiga stori,niliendelea na hiyo hali ya kulala na kushituka mpaka kulipo pambazuka!,Kuna jamaa tulimkuta pale kazi yake ilikuwa ni kuongeza magogo tu kwenye ule moto kila ulipoonyesha hali ya kufifia!.
Asubuhi kila mtu alikuwa na ishu zake,niliona kila mtu alikuwa amekaa na mtu ambaye walikuwa wakifahamiana naye!,Yule mama mganga tuliambiwa alikuwa amerudi,nilijiuliza alirudi vipi wakati usiku huo wote hakukuwa na mtu mwingine aliyeingia hapo? nikakosa majibu!.Watu tuliowakuta hapo ndiyo walioanza kuingia ndani kwenye nyumba ya mganga na kuelezwa walichoelezwa,kuna wengine walikuwa wakitoka wanaondoka jumla na kuna wengine walikuwa wakitoka wanarudi tena nje kukaa nadhani waliambiwa wasubiri!.Tulikaa kwa muda mrefu ndipo zamu yetu ilipofika tuliitwa na msaidizi wa yule mama,tuliambiwa tunaingia mmoja mmoja ndani,ndipo mimi nikamwambia yule jamaa yangu aanze yeye!.Jamaa alikaa humo ndani kama nusu saa halafu akatoka akaniambia na mimi niende ndani.Nilipofika ndani nilimsalimia Yule mama ambaye hakuwa mzee sana kama nilivyofikiria,kabla sijaanza kuongea naye aliniambia ninyamaze maana maisha yangu yote toka tukiwa Tarime mpaka nimefika hapo kwake alikuwa anayafahamu hivyo akaniambia nimwambie kilichokuwa kimenipeleka kwake!,kiukweli aliponiambia anayafahamu maisha yangu Tangu nikiwa Tarime nilishangaa sana!.Hivyo ilibidi nimueleze kwamba ninataka kuwa tajiri,aliniangalia akawa anatikisa kichwa tu,kisha akaniambia "Mbona mwanangu umeharibiwa sana"!,huwezi kuwa tajiri mpaka usafishwe kisawa sawa!".
Akaendelea kuniambia kwamba "nyota ya marehemu baba yako unayo wewe,ila kuna kitu kimekuzuia usiipate,kitu hicho ndicho kinafanya nyota ya baba yako ising'ae kwako ili uwe tajiri".
Akaniambia yeye atanisafisha na kunipa dawa ya kinga ili chochote kibaya kitakachonisogelea basi kiende na maji!,akaniambia baada ya kunisafisha itanipaswa niende mpaka Kigoma halafu nivuke ng'ambo ya pili upande niingie upande wa Kongo sehemu moja inaitwa Kalemii,huko kuna mtu ambaye angeniondolea hilo tatizo hatimaye nyota ya baba yangu niipate mimi ili niwe tajiri.Kiukweli nilivuta pumzi sana maana nilifahamu nilikuwa nimemaliza kazi kumbe ndiyo kwanza kazi ilikuwa haijaanza!,aliniambia itanibidi nikae pale kwake siku tatu ili akimaliza kuwashughulikia wale wagonjwa wengine niliyowakuta ndipo nianze dozi!.Nilipomaliza kuongea na yule mama ilibidi nitoke nje kuongea na yule jamaa aliyenipeleka,baada ya kumsimulia kila kitu jamaa kashangaa sana!.
Jamaa akaniambia "Mwanangu jipe moyo,kwakuwa umeamua pasipo kulazimishwa inakupasa uwe na uvumilivu".
Yule mama alitoka nje na kuanza kuongea na wateja wake,alipofika kwetu alimwambia yule jamaa yangu kwamba "huyu mwenzio bado nina kazi naye!,Wewe kama utamsubiri endelea kumsubiri,lakini akimaliza hapa bado anasafari nyingine!".
Jamaa tuliongea naye na hakuwa na namna ilibidi aondoke akawahi kazi zake lakini akaniambia mimi ni mwanaume nijipe moyo!.Nilimwambia jamaa endapo nisingerudi nyumbani kwa chochote ambacho kingenipata basi anichukulie vile vyombo vyangu anipelekee nyumbani kwetu Nyegezi,jamaa alikubali!,jamaa aliniaga na akaniongezea laki moja tena ila nilimwambia ningerudi ningemrudishia hiyo hela.Wakati jamaa anaondoka nilijikuta nalia kama mtoto maana sasa nilijiona bado nilikuwa nina safari ndefu ukizingatia nilikuwa mgeni hayo maeneo.Nilijipa moyo sana maana niliona ningekata tamaa hakuna ambacho ningefanikisha!.
Itaendelea..............