Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

MKASA WA PILI - Sehemu ya 18


Inaendelea.............


Asubuhi kulipokucha nilijianda na nilimuaga Mzee Nchibaronda na kuondoka!
Yule Mzee Nchibaronda nilimwachia shilingi laki moja ile ya kitanzania pamoja na kiasi kidogo nilichokuwa nacho cha faranga!

Mzee usiku alikuwa ameniambia kwamba siku nitakayofanikiwa inabidi nirudi kumpa shukurani maana shukurani huwa ni lazima!

Kwakuwa wakati huo nilikuwa nina uwezo wa ajabu kutokana na ile irizi niliyowekewa mkononi kuna jambo nilifanya pale si la kawaida!,Nilitamka ya kwamba "Ninataka muda huu niwe ziwa Tanganyika",na kweli nilijikuta nipo ziwani kwa upande wa kongo!.
Kiukweli nilijiona kama nina bahati kuliko binadamu wote walioko kwenye hii sayari ya dunia!
Nilitembea hapo ufukweni kuelekea kaskazini mwa Congo na muda si mrefu nilifika pale kwenye Bandari ya Kalemii!,Bado nilikuwa sielewi ule uwezo wa kutembea kwa haraka ulitoka wapi lakini yawezekana ilikuwa ile Irizi ya malikia!

Nilipofika pale Bandarini nilikuta Boti nyingi za kisasa na niliuliza pale boti inaelekea kigoma nikaonyeshwa!,nipofika kwenye hiyo boti nilipanda na kuingia ndani na hakuna aliyeweza kuniuliza kuhusu nauli maana nilikuwa ninatamka tu na inakuwa!
Huu mtindo wa kusafiri bila nauli ndo yalikuwa maisha yangu siku zote tangu nilipotoka huko chini ya maji!
Ile boti haikuchukua muda sana ilianza safari kuelekea kigoma na masaa kadhaa ikawa imetia nanga bandari ya kigoma!

Nilipofika kigoma nilijaribu kumtafuta yule jamaa wa Mwanza kwenye simu lakini alikuwa hapatikani,Baada ya kumkosa jamaa nilijaribu kumtafuta mama na alipopatikana tulisalimiana na akaniambia wao wanaendelea vizuri!,Mama aliniuliza "Kwani ukowapi wewe?,mbona hujaja nyumbani takribani wiki mbili?"
Nilimwambia mama "Nitakuja kesho maana nilikuwa bize kuna kazi nilikuwa naifanya"
Baada ya mazungumzo na mama nilielekea hapo kigoma nikatafuta hotel kwa ajili ya kupata msosi!

Baadae nilitafuta hotel maeneo ya hapo kigoma kwa ajili ya kupumzika ili kesho nianze safari ya kuelekea Mwanza!
Usiku huo nilikuwa nawaza namna nitakavyokuwa tajiri na namna ya kufanya watu wasigundue utajiri wangu kuwa niwa kishirikina!
Kulipokucha Asubuhi nilielekea kupanda basi lililokuwa linaelekea Mwanza na kama kawaida nilipanda bure sikuweza kulipa nauli!

Wakati huo mrume ndago nilikuwa nina jeuri na kiburi kisichokuwa na mfano,maana niliona mimi ndiyo mimi na kwamba hakuna mbwa yeyote wa kunibabaisha!,
Kama kawaida Mwanza tuliingia mida ya usiku!
Nilipofika hapo stendi ya Nyegezi nilipanda bodaboda mpaka Geto kwangu!,Kwakuwa ile nyumba tuliyokuwa tumepanga ilikuwa na geti niligonga na kuna jamaa mmoja alikuja kunifungulia!
"Mwanangu mambo vp",jamaa alinisalimia,nkamwambia" poa kaka"
"Ulikuwa wapi kaka maana nilijaribu kukuulizia lakini kila mtu hakuwa na jibu"jamaa aliendelea kuniuliza!
Nilimwambia "Nilisafiri kidogo kaka,siunajua tena utafutaji?"

Basi nilielekea chumbani kwa yule jamaa ambaye tulienda nae kasulu maana nilikuwa nimempa funguo zangu anitunzie!,Nilijaribu kugonga akafungua lakini ilikuwa sura ngeni machoni kwangu!
Alikuwa mwanamke na mimi nilidhani uenda angekuwa mwanamke wa jamaa lakini kumbe kulikuwa na mpangaji mpya kwenye hicho chumba!
Nilimuuliza "Vp jamaa kalala",Yule dada aliniambia "jamaa yupi"?,Aliendelea kuniambia yeye hapo kahamia ana kama wiki mbili hivi!.
Nilimuomba samahani sana maana nilijua uenda ni mwanamke wa jamaa na nkamwambia hapo mwenye chumba alichohamia kulikuwa na mpangaji ambaye nilimwachia funguo za chumbani kwangu maana mimi nilikuwa nimesafiri!

Yule dada aliniambia nijaribu kuwauliza wapangaji wengine maana yeye hafaamu kitu chochote!

Nilienda kumgongea yule jamaa aliyenifungulia nikijaribu kumuulizia labda jamaa atakuwa kamwachia funguo!,Jamaa akasema "Hapana sikuachiwa funguo"

Kuna jamaa mmoja yeye shughuli zake zilikuwa za viwandani huko Igoma na uenda nadhani jamaa ndo alimwachia funguo!
Niliona isiwe taabu sana!,Nilielekea chumbani kwangu na niligusa kile kitasa kwa mkono wa kushoto ulokuwa na ile irizi na ukafunguka nikaingia ndani!
Kiukweli sikutaka mtu yeyote lile tukio alione na ndo maana nilijaribu kuutafuta ufunguo wangu na kwakuwa ilishakuwa usiku sikuwa na namna ingawa hakuna aliyeona nafanya nini!
Asubuhi jamaa alipokuja kutoka shift huko kiwandani alishangaa kunikuta nafanya usafi ndani kwangu!

"Aisee mambo vp"?,Umerudi lini"?,yalikuwa ni maswali aliyoniuliza,Nilimjibu nimefika jana usiku!
"Ulikuwa na funguo nyingine nini!,maana jamaa aliniachia funguo zako",Nilimwambia "Ndiyo nilikuwa na funguo moja maana hii niliyompa jamaa naiachaga kama dharula"

Nilimuuliza jamaa kahamia wapi?,Jamaa aliniambia Yule mshikaji tuliyeenda naye kasulu kahamia Kahama mkoani shinyanga maana jamaa anasema alimwambia kuna chimbo la dhahabu kalipata hivyo aliona aachane na ile kampuni ya Ujenzi aelekee mgodini kutafuta mali!

Tuliendelea kupiga stori pale na jamaa na akanipatia ule ufunguo wa chumba changu mi nikaendelea na mambo mengine!
Nilipomaliza kufua nguo nilijilaza ndani nikiwa nawaza namna ya kuianza ile kazi maana niliambiwa nijitahidi ndani ya mwezi huo mwishoni damu iwe imepatikana!

Niliamka na kujianda na kuelekea nyumbani kwa Bi mkubwa na nilipitia sokoni nikanunua matunda na vyakula baadhi nikawapelekea!
Nilimkuta Bi mkubwa pale na nikamsalimia na mambo mengine yakaendelea!

Baadae niliwaaga nikaondoka zangu kurejea geto kwangu!

Siku zilizidi kuyoyoma na nilikuwa na wazo sasa la kuanza kazi rasmi!
Kumbuka niliambiwa nihakikishe kuna chumba maalumu nilichokitenga kwa ajili ya kukiweka kile kibuyu alichonipa Mzee Nchibaronda baada ya kufanya tukio na kiwe na damu!

Hiko kibuyu kilikuwa ni kidogo sana kwa muonekano wa kawaida lakini kilikuwa na uwezo wa kujaza damu kama lita 200 kwa wakati mmoja!,Na kwa kawaida ulikuwa huwezi kukinyanyua mpaka uwe na nguvu za ziada kama nilizokuwa nazo mimi!

Baada kama ya siku mbili nakumbuka ilikuwa mida ya saa tatu usiku nilielekea mitaa ya bugando na kuna ajali niliisababisha ya bodaboda ambapo waligongwa na lori mpaka vichwa vikasagika kabisa!,Nilienda pale na kibuyu changu na nikaweka damu yao wote bodaboda na abiria wake na sikubakiza hata tone la damu maana kuna dawa nilichanganya na nilipofika hapo ilivuta damu zote kwenye ile miili hakikubaki kitu!
Tukio hilo nililifanya pasipo kuonekana na mtu yeyote yule!

Wakati nafika Mwanza nilienda kuitafuta ile miti ya dawa na kuivuna na kuihifadhi ndani,pia kuna dawa nyingine nilitoka nazo kongo pia kuna miti ya dawa baadhi nilienda kununua kwenye maduka ya dawa za asili!

Basi baada ya kuwa nimeiweka ile damu kwenye kibuyu nilielekea nyumbani n nilipofika nilikiweka kile kibuyu chini ya uvungu!
Asubuhi nilipoamka nilikiangalia na sikukuta damu yoyote ndani!nikajua tayari wazee wa kazi watakuwa wamekuja wamechukua chakula chao!
Siku hiyo nilisikia sauti ikinielekeza kwamba nielekee maeneo ya Nyegezi maeneo ya hapo stendi kulikuwa na sheli(kituo cha mafuta),Nisingependa kukitaja jina!
Ile sauti iliniambia kwamba nikifika hayo maeneo kuna dada atakuwa kashika hela na nisiwe na wasiwasi nimsalimie kisha atanipa hizo hela !,Niliambiwa yeye atakuwa anaona ameshika hela kumbe kashikilia gunzi la muhindi!

Nilifanya kama nilivyoagizwa,nilipofika nilimsalimia maana nilimfahamu tu kwa kumuona!,Baada ya kumshika mkono na kumsalimia alinipa pesa zote alizokuwa nazo na yeye alikuwa kashika gunzi la muhindi akidhani pesa!
Nilipozihesabu zile hela zilikuwa kama laki tatu na hamsini!
Nikarud zangu geto kwangu!,Nilipofika ndani kwangu pia kuna hela nilizikuta kitandani zilikuwa burungutu zimefungwa na rubber bendi!
Kiukweli nilifurahi sana na nilianza kuzihesabu zilikuwa milioni 2



Itaendelea.....................

Hii story nilivyokuwa na hamu ya kuendelea kuisoma natamani kama ni cd basi ningehakikisha nanunua episode zoooooooote[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mkuu LwandaMagere zingatia sana huu ushauri👇👇

Block pm yako watu wasikupate
Kuna watu watakufuata huko Kama watu wema lakini huwezi jua Wana malengo gani
Kumbuka hapo umeelezea ulipewa unga kumbe ulikuwa mifupa ya albino

Ndugu unaweza kujikuta matatani

Pia ujue Kuna Siri unazitoa Sasa kwa watu ambao Bado wanamtumikia shetani hawapendi Siri zao zitolewe hvyo wanaweza kukutafuta kwa malengo mabaya kuwa makini sana

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Block pm yako watu wasikupate
Kuna watu watakufuata huko Kama watu wema lakini huwezi jua Wana malengo gani
Kumbuka hapo umeelezea ulipewa unga kumbe ulikuwa mifupa ya albino

Ndugu unaweza kujikuta matatani

Pia ujue Kuna Siri unazitoa Sasa kwa watu ambao Bado wanamtumikia shetani hawapendi Siri zao zitolewe hvyo wanaweza kukutafuta kwa malengo mabaya kuwa makini sana

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app

Namimi naomba kuunga mkono hoja lakni kwa kukazia tu ni kwamba si wote na sitegemei kuwa wote wanaomfata pm wanalengo hilo rahasha inawezekana mwingine akavutiwa na mshikaji kwakuwa ameweza kuruka vihunzi vingi hivyo kwa uzoefu wake akapenda wawekaribu katika kubadilishana nae mawazo kulingana na experiences alizokuwanazo

Mfano mzuri ni yule rafiki yake aliyempeleka kigoma kumbuka yule rafiki yake alikwenda kwa mambo yake binafsi yaani apate kinga dhidi ya watu wabaya na mafanikio kazini na sasa yupo migodini sasa ukimfata jamaa pm kwa kutaka msaada wa mawasiliano ya yule mama ili tupate kinga bado kuna ubaya mpaka tuogopane kiasi hicho?

Jaman haya maisha ni magumu na yanasiri ndefu tuache kumtisha jamaaa hata hivyo mkuu na wewe tambua katika safari yako ya kutafuta mafanikio kama uto rafiki yako angesema akufiche au awe mchoyo wa fadhira sidhani kama leo ungetoa ushuhuda huu sasa hapo ndio utambue umuhimu wa kuwa na marafiki na watu tofauti tofauti ingawa si kila rafiki ni rafiki utakuwa ukiwachuja mwenyewe
 
Aiseeeeh haya maisha watu wanapitia mengi sana ambayo wengine hatuyajui; kuna siri nyingi sana zimefichwa kwenye maisha ya watu zikihusisha mafanikio au kufeli kwao maisha; Mungu azidi kutujaalia mioyo ya kutafuta mali kwa njia halali na kuridhika na tulichonacho.....!
Twende kazi mkuu....!
 
Wakuu habarini za mida

Kuna watu wananifata inbox wanataka niwaambie namna ya kufikia kama mimi nilivyokuwa na wanaenda mbali sana wanasema wamechoka na maisha ya umasikini!

Labda tu niwaambie kwamba ni heri kufa masikini kuliko kuwa tajiri wa mali za kishirikina!,Maskini wanamaisha ya raha sana na kuwa na amani japo kwa akili ya kawaida unaweza kudhani wao ndo wanaopata taabu!

Muogopeni sana Ibilisi,hafai hata kwa sekunde moja!

Nilipompokea Yesu japo kuna wakati nalala na njaa lakini nimesharizika kuliko ambavyo nilikuwa kwa Ibilisi.
Hivyo niwaombe sana vijana muacheni tamaa za muda mfupi!

............................................................


Leo kwa muda kadhaa nitakaribisha maswali kabla ya kuendelea na niliyo yafanya nikiwa huku duniani!

Karibuni!
Hongera kwa kutoka kifungoni mwa shetani.. [emoji122]

Kwa Yesu kuzuri, kwa Yesu raha... [emoji4]
 
Namimi naomba kuunga mkono hoja lakni kwa kukazia tu ni kwamba si wote na sitegemei kuwa wote wanaomfata pm wanalengo hilo rahasha inawezekana mwingine akavutiwa na mshikaji kwakuwa ameweza kuruka vihunzi vingi hivyo kwa uzoefu wake akapenda wawekaribu katika kubadilishana nae mawazo kulingana na experiences alizokuwanazo

Mfano mzuri ni yule rafiki yake aliyempeleka kigoma kumbuka yule rafiki yake alikwenda kwa mambo yake binafsi yaani apate kinga dhidi ya watu wabaya na mafanikio kazini na sasa yupo migodini sasa ukimfata jamaa pm kwa kutaka msaada wa mawasiliano ya yule mama ili tupate kinga bado kuna ubaya mpaka tuogopane kiasi hicho?

Jaman haya maisha ni magumu na yanasiri ndefu tuache kumtisha jamaaa hata hivyo mkuu na wewe tambua katika safari yako ya kutafuta mafanikio kama uto rafiki yako angesema akufiche au awe mchoyo wa fadhira sidhani kama leo ungetoa ushuhuda huu sasa hapo ndio utambue umuhimu wa kuwa na marafiki na watu tofauti tofauti ingawa si kila rafiki ni rafiki utakuwa ukiwachuja mwenyewe
Wee utakuwa ulienda pm weweeee
Sio kwa msisitizo huo hahaaa

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
Namimi naomba kuunga mkono hoja lakni kwa kukazia tu ni kwamba si wote na sitegemei kuwa wote wanaomfata pm wanalengo hilo rahasha inawezekana mwingine akavutiwa na mshikaji kwakuwa ameweza kuruka vihunzi vingi hivyo kwa uzoefu wake akapenda wawekaribu katika kubadilishana nae mawazo kulingana na experiences alizokuwanazo

Mfano mzuri ni yule rafiki yake aliyempeleka kigoma kumbuka yule rafiki yake alikwenda kwa mambo yake binafsi yaani apate kinga dhidi ya watu wabaya na mafanikio kazini na sasa yupo migodini sasa ukimfata jamaa pm kwa kutaka msaada wa mawasiliano ya yule mama ili tupate kinga bado kuna ubaya mpaka tuogopane kiasi hicho?

Jaman haya maisha ni magumu na yanasiri ndefu tuache kumtisha jamaaa hata hivyo mkuu na wewe tambua katika safari yako ya kutafuta mafanikio kama uto rafiki yako angesema akufiche au awe mchoyo wa fadhira sidhani kama leo ungetoa ushuhuda huu sasa hapo ndio utambue umuhimu wa kuwa na marafiki na watu tofauti tofauti ingawa si kila rafiki ni rafiki utakuwa ukiwachuja mwenyewe
Mkuu kinga ipo huko Lupatu, au hukuusoma ule uzi wa mkuu Kitoabu yani ni nomaaa
 
Namimi naomba kuunga mkono hoja lakni kwa kukazia tu ni kwamba si wote na sitegemei kuwa wote wanaomfata pm wanalengo hilo rahasha inawezekana mwingine akavutiwa na mshikaji kwakuwa ameweza kuruka vihunzi vingi hivyo kwa uzoefu wake akapenda wawekaribu katika kubadilishana nae mawazo kulingana na experiences alizokuwanazo

Mfano mzuri ni yule rafiki yake aliyempeleka kigoma kumbuka yule rafiki yake alikwenda kwa mambo yake binafsi yaani apate kinga dhidi ya watu wabaya na mafanikio kazini na sasa yupo migodini sasa ukimfata jamaa pm kwa kutaka msaada wa mawasiliano ya yule mama ili tupate kinga bado kuna ubaya mpaka tuogopane kiasi hicho?

Jaman haya maisha ni magumu na yanasiri ndefu tuache kumtisha jamaaa hata hivyo mkuu na wewe tambua katika safari yako ya kutafuta mafanikio kama uto rafiki yako angesema akufiche au awe mchoyo wa fadhira sidhani kama leo ungetoa ushuhuda huu sasa hapo ndio utambue umuhimu wa kuwa na marafiki na watu tofauti tofauti ingawa si kila rafiki ni rafiki utakuwa ukiwachuja mwenyewe
Hauko serius wewe!!! Juhudi zako pekee zitakupandisha cheo kazini. Mungu pekee ndo anaweza kukukinga na watu wabaya na wala sio nguvu za Giza. Embu kasome tena ulichoandika mzee.
 
Back
Top Bottom