Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Acha kuleta nuksi mkuu siyo maneno mazuri yakuongea hayo unaweza kuchukuliwa hatua Kali na jamuhuri ili fundisho kwa watu wengine

Hahaha, we jamaa una hasira kama vile story umeilipia.

Bahati mbaya leo episodes hakuna, LwandaMagere anajiandaa kuangalia team yake inavyochapwa na Man City. Na akishafungwa itabidi mpaka maumivu yapoe ndo aje tena.
 
Hauko serius wewe!!! Juhudi zako pekee zitakupandisha cheo kazini. Mungu pekee ndo anaweza kukukinga na watu wabaya na wala sio nguvu za Giza. Embu kasome tena ulichoandika mzee.

Mimi ni wale vijana ambao umri wetu ni 30+ hivyo ninaelewa vizuri sana ninachokiandika alafu mkuu naomba ukae ukijua kwamba hizi ni imani na imani ni jambo pana sana na ndio maana mtoa mada kama ulimfatilia neno kwa neno amerudia rudia kwa kusema hii dunia ni pana sana kuna mengi ambayo hatuyajui na inawezekana mpk tunaingia kaburini tusiyajue sasa wewe endelea kuamini hicho unachokiamini(kwa imani yako)na mimi nitasimama kwa ninachokiamini kwa imani yangu huko kwa yesu tutakutana baadae.
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 18


Inaendelea.............


Asubuhi kulipokucha nilijianda na nilimuaga Mzee Nchibaronda na kuondoka!
Yule Mzee Nchibaronda nilimwachia shilingi laki moja ile ya kitanzania pamoja na kiasi kidogo nilichokuwa nacho cha faranga!

Mzee usiku alikuwa ameniambia kwamba siku nitakayofanikiwa inabidi nirudi kumpa shukurani maana shukurani huwa ni lazima!

Kwakuwa wakati huo nilikuwa nina uwezo wa ajabu kutokana na ile irizi niliyowekewa mkononi kuna jambo nilifanya pale si la kawaida!,Nilitamka ya kwamba "Ninataka muda huu niwe ziwa Tanganyika",na kweli nilijikuta nipo ziwani kwa upande wa kongo!.
Kiukweli nilijiona kama nina bahati kuliko binadamu wote walioko kwenye hii sayari ya dunia!
Nilitembea hapo ufukweni kuelekea kaskazini mwa Congo na muda si mrefu nilifika pale kwenye Bandari ya Kalemii!,Bado nilikuwa sielewi ule uwezo wa kutembea kwa haraka ulitoka wapi lakini yawezekana ilikuwa ile Irizi ya malikia!

Nilipofika pale Bandarini nilikuta Boti nyingi za kisasa na niliuliza pale boti inaelekea kigoma nikaonyeshwa!,nipofika kwenye hiyo boti nilipanda na kuingia ndani na hakuna aliyeweza kuniuliza kuhusu nauli maana nilikuwa ninatamka tu na inakuwa!
Huu mtindo wa kusafiri bila nauli ndo yalikuwa maisha yangu siku zote tangu nilipotoka huko chini ya maji!
Ile boti haikuchukua muda sana ilianza safari kuelekea kigoma na masaa kadhaa ikawa imetia nanga bandari ya kigoma!

Nilipofika kigoma nilijaribu kumtafuta yule jamaa wa Mwanza kwenye simu lakini alikuwa hapatikani,Baada ya kumkosa jamaa nilijaribu kumtafuta mama na alipopatikana tulisalimiana na akaniambia wao wanaendelea vizuri!,Mama aliniuliza "Kwani ukowapi wewe?,mbona hujaja nyumbani takribani wiki mbili?"
Nilimwambia mama "Nitakuja kesho maana nilikuwa bize kuna kazi nilikuwa naifanya"
Baada ya mazungumzo na mama nilielekea hapo kigoma nikatafuta hotel kwa ajili ya kupata msosi!

Baadae nilitafuta hotel maeneo ya hapo kigoma kwa ajili ya kupumzika ili kesho nianze safari ya kuelekea Mwanza!
Usiku huo nilikuwa nawaza namna nitakavyokuwa tajiri na namna ya kufanya watu wasigundue utajiri wangu kuwa niwa kishirikina!
Kulipokucha Asubuhi nilielekea kupanda basi lililokuwa linaelekea Mwanza na kama kawaida nilipanda bure sikuweza kulipa nauli!

Wakati huo mrume ndago nilikuwa nina jeuri na kiburi kisichokuwa na mfano,maana niliona mimi ndiyo mimi na kwamba hakuna mbwa yeyote wa kunibabaisha!,
Kama kawaida Mwanza tuliingia mida ya usiku!
Nilipofika hapo stendi ya Nyegezi nilipanda bodaboda mpaka Geto kwangu!,Kwakuwa ile nyumba tuliyokuwa tumepanga ilikuwa na geti niligonga na kuna jamaa mmoja alikuja kunifungulia!
"Mwanangu mambo vp",jamaa alinisalimia,nkamwambia" poa kaka"
"Ulikuwa wapi kaka maana nilijaribu kukuulizia lakini kila mtu hakuwa na jibu"jamaa aliendelea kuniuliza!
Nilimwambia "Nilisafiri kidogo kaka,siunajua tena utafutaji?"

Basi nilielekea chumbani kwa yule jamaa ambaye tulienda nae kasulu maana nilikuwa nimempa funguo zangu anitunzie!,Nilijaribu kugonga akafungua lakini ilikuwa sura ngeni machoni kwangu!
Alikuwa mwanamke na mimi nilidhani uenda angekuwa mwanamke wa jamaa lakini kumbe kulikuwa na mpangaji mpya kwenye hicho chumba!
Nilimuuliza "Vp jamaa kalala",Yule dada aliniambia "jamaa yupi"?,Aliendelea kuniambia yeye hapo kahamia ana kama wiki mbili hivi!.
Nilimuomba samahani sana maana nilijua uenda ni mwanamke wa jamaa na nkamwambia hapo mwenye chumba alichohamia kulikuwa na mpangaji ambaye nilimwachia funguo za chumbani kwangu maana mimi nilikuwa nimesafiri!

Yule dada aliniambia nijaribu kuwauliza wapangaji wengine maana yeye hafaamu kitu chochote!

Nilienda kumgongea yule jamaa aliyenifungulia nikijaribu kumuulizia labda jamaa atakuwa kamwachia funguo!,Jamaa akasema "Hapana sikuachiwa funguo"

Kuna jamaa mmoja yeye shughuli zake zilikuwa za viwandani huko Igoma na uenda nadhani jamaa ndo alimwachia funguo!
Niliona isiwe taabu sana!,Nilielekea chumbani kwangu na niligusa kile kitasa kwa mkono wa kushoto ulokuwa na ile irizi na ukafunguka nikaingia ndani!
Kiukweli sikutaka mtu yeyote lile tukio alione na ndo maana nilijaribu kuutafuta ufunguo wangu na kwakuwa ilishakuwa usiku sikuwa na namna ingawa hakuna aliyeona nafanya nini!
Asubuhi jamaa alipokuja kutoka shift huko kiwandani alishangaa kunikuta nafanya usafi ndani kwangu!

"Aisee mambo vp"?,Umerudi lini"?,yalikuwa ni maswali aliyoniuliza,Nilimjibu nimefika jana usiku!
"Ulikuwa na funguo nyingine nini!,maana jamaa aliniachia funguo zako",Nilimwambia "Ndiyo nilikuwa na funguo moja maana hii niliyompa jamaa naiachaga kama dharula"

Nilimuuliza jamaa kahamia wapi?,Jamaa aliniambia Yule mshikaji tuliyeenda naye kasulu kahamia Kahama mkoani shinyanga maana jamaa anasema alimwambia kuna chimbo la dhahabu kalipata hivyo aliona aachane na ile kampuni ya Ujenzi aelekee mgodini kutafuta mali!

Tuliendelea kupiga stori pale na jamaa na akanipatia ule ufunguo wa chumba changu mi nikaendelea na mambo mengine!
Nilipomaliza kufua nguo nilijilaza ndani nikiwa nawaza namna ya kuianza ile kazi maana niliambiwa nijitahidi ndani ya mwezi huo mwishoni damu iwe imepatikana!

Niliamka na kujianda na kuelekea nyumbani kwa Bi mkubwa na nilipitia sokoni nikanunua matunda na vyakula baadhi nikawapelekea!
Nilimkuta Bi mkubwa pale na nikamsalimia na mambo mengine yakaendelea!

Baadae niliwaaga nikaondoka zangu kurejea geto kwangu!

Siku zilizidi kuyoyoma na nilikuwa na wazo sasa la kuanza kazi rasmi!
Kumbuka niliambiwa nihakikishe kuna chumba maalumu nilichokitenga kwa ajili ya kukiweka kile kibuyu alichonipa Mzee Nchibaronda baada ya kufanya tukio na kiwe na damu!

Hiko kibuyu kilikuwa ni kidogo sana kwa muonekano wa kawaida lakini kilikuwa na uwezo wa kujaza damu kama lita 200 kwa wakati mmoja!,Na kwa kawaida ulikuwa huwezi kukinyanyua mpaka uwe na nguvu za ziada kama nilizokuwa nazo mimi!

Baada kama ya siku mbili nakumbuka ilikuwa mida ya saa tatu usiku nilielekea mitaa ya bugando na kuna ajali niliisababisha ya bodaboda ambapo waligongwa na lori mpaka vichwa vikasagika kabisa!,Nilienda pale na kibuyu changu na nikaweka damu yao wote bodaboda na abiria wake na sikubakiza hata tone la damu maana kuna dawa nilichanganya na nilipofika hapo ilivuta damu zote kwenye ile miili hakikubaki kitu!
Tukio hilo nililifanya pasipo kuonekana na mtu yeyote yule!

Wakati nafika Mwanza nilienda kuitafuta ile miti ya dawa na kuivuna na kuihifadhi ndani,pia kuna dawa nyingine nilitoka nazo kongo pia kuna miti ya dawa baadhi nilienda kununua kwenye maduka ya dawa za asili!

Basi baada ya kuwa nimeiweka ile damu kwenye kibuyu nilielekea nyumbani n nilipofika nilikiweka kile kibuyu chini ya uvungu!
Asubuhi nilipoamka nilikiangalia na sikukuta damu yoyote ndani!nikajua tayari wazee wa kazi watakuwa wamekuja wamechukua chakula chao!
Siku hiyo nilisikia sauti ikinielekeza kwamba nielekee maeneo ya Nyegezi maeneo ya hapo stendi kulikuwa na sheli(kituo cha mafuta),Nisingependa kukitaja jina!
Ile sauti iliniambia kwamba nikifika hayo maeneo kuna dada atakuwa kashika hela na nisiwe na wasiwasi nimsalimie kisha atanipa hizo hela !,Niliambiwa yeye atakuwa anaona ameshika hela kumbe kashikilia gunzi la muhindi!

Nilifanya kama nilivyoagizwa,nilipofika nilimsalimia maana nilimfahamu tu kwa kumuona!,Baada ya kumshika mkono na kumsalimia alinipa pesa zote alizokuwa nazo na yeye alikuwa kashika gunzi la muhindi akidhani pesa!
Nilipozihesabu zile hela zilikuwa kama laki tatu na hamsini!
Nikarud zangu geto kwangu!,Nilipofika ndani kwangu pia kuna hela nilizikuta kitandani zilikuwa burungutu zimefungwa na rubber bendi!
Kiukweli nilifurahi sana na nilianza kuzihesabu zilikuwa milioni 2



Itaendelea.....................
Alooooooooooooo
 
Mkuu sema tu kuwa unataka namba ya yule bibi Kasulu usiongee sana

ukimfata jamaa pm kwa kutaka msaada wa mawasiliano ya yule mama ili tupate kinga bado kuna ubaya mpaka tuogopane kiasi hicho?
Ina maana humuamini Mungu mpaka utake kinga ya shetani? 😁😁 Hufiki mbali asee afu pia hutaweza masharti.
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 19.


Inaendelea.............



Baada ya kuwa nimepata zile pesa niliona kwanza nianze ukarabati wa nyumba yetu hiyo ya Nyegezi.Mama yangu alikuwa na wasiwasi kuhusu zile pesa ya kwamba nilikuwa nimezipata wapi!,nilimwambia mama kuna mahali nilikuwa nimepata kazi ya kufundisha,hivyo nilikuwa ninalipwa vizuri,kauli ile ilimtoa mama yangu wasiwasi.

Ile nyumba nilianza kuikarabati upya na kuanzia hapo kila nilipokuwa nikipata pesa kutokana na ajali zile nilizokuwa nikisababisha hapo mjini Mwanza na miji mingine,niliendelea kuisuka upya nyumba yetu ikawa ya kisasa kabisa kama nyumba za matajiri wengine.Ulikuwa ukifika hapo nyumbani huwezi kuamini kama ile nyumba walikuwa wakikaa watu wa kawaida,maana ilibadilika sana ikawa kama nyumba za vigogo wa kiserikali.Nyumbani hawakutia shaka sana maana nilifanya usiri mkubwa sana,hivyo isingekuwa rahisi kufahamu chochote.Siku zilikuwa zikienda mbio na mimi pia niliendelea kutoa kafara!,Kuna siku niliushika mkono wangu uliyokuwa na irizi nikaanza kuongea "Mbona kafara natoa lakini bado napata pesa kidogo?".

Nilisikia sauti ikinijibu kwamba "muda wa kuwa tajiri haujawadia ila uko karibu!".

Kafara na matendo mabaya hayo nilianza kuyafanya mwaka wa 2013.Basi siku moja mwisho wa mwezi nikiwa geto kwangu nilisikia sauti ikiniambia nielekee mkoani Singida eneo la Sekenke ambako ilipaswa kuna watu wafe ili niweze kupata mali nyingi!.Asubuhi ya siku hiyo sikutaka kabisa kupoteza muda,Kuna dawa nilizichanganya hapo ndani kwangu na nilipomaliza nilitamka ya kwamba "Nahitaji kufika sekenke Singida muda huu".

Ilikuwa ni kitendo cha kufumba na kufumbua nikajikuta nipo eneo la tukio.Nilipofika maeneo hayo ya Sekenke kuna gari ambayo nilielekezwa toka mwanzo,ndani yake kulikuwa kuna abiria ambao walikuwa wakisakwa kwa udi na uvumba kutoka huko majini nilikotoka,hivyo siku hiyo ilikuwa ndiyo mwisho wao!.Basi kuna dawa niliitupa katikati ya barabara,ile gari ilipofika yale maeneo nilipoweka ile dawa,gurudumu la mbele lilipasuka ndipo ilianza kukosa uelekeo hali iliyofanya kupata ajali mbaya sana!,Kiukweli nilikuwa nina roho ya kikatili sana kwa wakati huo!,nilikuwa sina huruma hata chembe.Baada ya ile gari kuwa imepata ajali,nilisogea na kukuta wale watu niliyokuwa nimewatageti wamebanwa na viti kwa chini,Nilianza kuwachinja kichawi na kuchukua damu zao!,Pia nilichukua damu za abiria wengine waliyokuwa wamekufa kwa wakati huo,nilihakikisha nawakausha kabisa wasiwe na damu hata tone!.Nilipomaliza nilifanya haraka na kuondoka zangu hilo eneo,nilipofika geto kama kawaida kile kibuyu nilikiweka chini ya uvungu,sikutaka kushinda hapo geto,hivyo niliondoka nikaelekea Nyegezi kwa mama kuangalia maendeleo ya nyumba.Nilipojiridhisha ya kwamba mambo ni mazuri nilirudi zangu tena geto.

Safari hii niliporudi geto nilikuta kitandani kwangu kuna begi kubwa yale ya mgongoni ambayo watoto wa shule wanayowekaga madaftari nikakuta limejaa pesa,siku hiyo nilikuwa nina furaha sana maana sikuwahi kukamata pesa nyingi kiasi hicho!.Sasa nikaanza kuzihesabu pale nilipata milioni 35 pesa za kitanzania.Niliondoka hapo geto kwangu kuelekea Igoma,lengo langu ilikuwa ni kutafuta eneo ili nianze ujenzi wa nyumba,Kuna dalali nilimpata maeneo ya huko Igoma akaniambia viwanja vipo lakini kulikuwa kuna nyumba zinauzwa.Aliponiambia nyumba zipo zinauzwa,wazo la kununua uwanja nikalitoa kichwani!,nilimwambia anipeleke kwenye hizo nyumba zinazouzwa ili niangalie ambayo ningeipenda ninunue.

Jamaa alinipeleka kwenye nyumba ya kwanza ambayo ilikuwa ya kawaida!,tuliendelea kutembelea zile nyumba ambazo zilikuwa zikiuzwa huko Igoma,kuna nyumba tulifika kiukweli niliipenda sana,huyo dalali aliniambia nimwachie namba ya simu ili atakapo wasiliana na tajiri wa hiyo nyumba angenijulisha.Basi nilipoachana na yule dalali wazo lingine ambalo nilikuwa nalo ni kutafuta mwanamke wa kuishi naye ambaye niliambiwa atakuwa akibeba ujauzito ili watoto watakao zaliwa,wawe wanatolewa kafara!.Sasa akilini mwangu niliwaza kwamba nataka nimchukue yule shemeji yangu aliyekuwa na dharau na nyodo ili aifanye hiyo kazi.Lengo langu lilikuwa ni kumkomoa tu ili dharau na nyodo alizokuwa nazo zimtoke.Nilitaka kwanza nikiisha inunua hiyo nyumba na kuvuta usafiri ndiyo nifanyie kazi ilo suala!.

Nilirudi geto na kukuta tena pesa zimejaa kwenye lile lile begi ambalo mara ya kwanza nilitoa zile pesa!,japo hazikuwa nyingi kama za mara ya kwanza,safari hii nilipozihesabu ilikuwa milioni 20,hivyo ukijumlisha na zile za mara kwanza ilikuwa jumla milioni 55,Kiukweli nilipagawa sana!.Nakumbuka siku hiyo nilimpigia mama yangu simu nikamwambia "Mama nimekuagizia gari wiki hii itakuwa inaingia".

Mama aliniuliza "Mwanangu pesa unatoa wapi?".

Niliendelea kumdanganya " hapo shuleni ninapofundisha walitupatia fursa ya mkopo ndiyo nami nimechukua mkopo mama".

Ndani ya wiki hiyo nilienda kwenye Yadi ya magari iliyokuwa karibu na kamanga fery(nisingependa kuitaja) nilitoa pesa keshi nikamnunulia mama yangu gari mpya aina ya Murano.Sasa kwakuwa ilipaswa nikaonane na yule dalali wa Igoma nilimpigia simu mama nikamwambia anapelekewa gari yake.Kuna dereva wa pale Yadi nilimpa namba ya mama ili akifika maeneo ya Nyegezi ampigie.Nilipofika Igoma yule dalali alinikutanisha na mmiliki wa ile nyumba nikaongea naye,jamaa akasema nimpematie milioni 60 ili aniuzie ile nyumba,kwa wakati huo nilikuwa nimebaki na milioni 30 maana pesa nyingine nilimnunulia mama gari,siku iliyofuata nilimpelekea hiyo hela nikamwambia pesa nyingine ningempa siku si nyingi!,lile jumba lilikuwa la kisasa halafu zuri,hivyo nikaona lingenifaa kwenye mambo yangu ya kafara.

Nakumbuka mama yangu alifurahi sana baada ya kumnunulia gari maana aliishi maisha kama mtu sasa!.Kwakuwa hakujua kuendesha gari ilibidi nimtafutie dereva ambaye nilikuwa namlipa kila mwezi.

Siku ziliendelea kusonga sana,siku moja nilielekea mkoani Shinyanga kupiga tukio la kafara kama kawaida!.



Itaendelea.................
 
Back
Top Bottom