Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

MKASA WA PILI - Sehemu ya 22.


Inaendelea.............



Nilipofika nyumbani kwa mama nilimkuta akiwa na wageni,hizi pesa acheni ziitwe pesa maana wakati hatuna hela yaani hata wageni kututembelea ilikuwa nadra sana.Ile nyumba nilikuwa nimeikarabati sana,nilipiga fensi ya ukuta kuzunguka nyumba nzima,kiukweli ulikuwa ukifika hapo nyumbani kipindi hicho,ulikuwa unashangaa sana.

Basi baada ya muda nilipomaliza kupata chakula nilimuaga mama nikarudi zangu geto kwangu.Nilipofika geto niliyatupa macho kitandani,ndipo nilikuta lile begi limejaa pesa ,safari hii zilikuwa nyingi maana nilianza kuzihesabu nilitumia muda kidogo,nilipata jumla yake milioni 38 zile noti zilikuwa mpya sana!.Kiukweli wakati huo nilikuwa nawaona watu wote wanaotafuta pesa kwa jasho ni wajinga wanaopaswa kuuawa na dunia yote niimiliki mimi!,nilikuwa nina kiburi sana,kwakuwa niliishazoea sasa kukamata hela nyingi kwa mkupuo hata kiwewe kiliniondoka!.Nilizichukua zile hela nikaziweka kwenye begi kubwa na kile kibegi cha mgongoni nikakirudisha chini ya uvungu,Kitu ambacho nakumbuka niliambiwa nisije kufanya ni kuziweka zile pesa kwenye akaunti benki!,Yaani niliambiwa nisije thubutu katu kuweka hizo pesa benki.

Baada ya kupata hizo pesa niliondoka hapo nyumbani kuelekea mjini,lengo langu ilikuwa ni kwenda kununua kila kitu cha ndani,sasa kabla sijanunua,Kuna dada mmoja aliyekuwa hapo dukani aliniambia kuna kampuni ya upambaji wa majumba (decorations) wanafanya nayo kazi,kama nitaweza awapigie simu waje niwapeleke kwenye nyumba yangu na wao watanishauri namna ya kuipamba ile nyumba ili iwe na muonekano mzuri kwa ndani,Kwakuwa sikutaka kuonekana mshamba kwa yule dada ilibidi nimwambie awaite twende Igoma.Wale jamaa hakika walikuwa wamesomea hiyo kazi maana walinishauri kila kitu na aina ya mapazia yanavyopaswa kuendana na masofa.Baada ya kunipatia hayo maelekezo niliwauliza wao kuipendezesha nyumba nzima ingegharimu kiasi gani?,kuna mwanamke aliyekuwa mwarabu,na ndiye alikuwa mmiliki wa ile taasisi aliniambia wao kuweka kila kitu humo ndani mpaka kufikia kuhamia,ilikuwa inagharimu Tsh milioni 25.Basi nilimwambia yule mwanamke wa kiarabu kwamba,turudi mpaka kwenye lile la duka la samani(furniture),wakanisubiri nikawaletee pesa.Tuliondoka huko Igoma kuelekea mjini,tulipofika kwenye lile duka,wao niliwaacha nikawaambia wanisubiri nikawaletee pesa waliyoitaka,ndipo mimi nikaelekea geto kuwachukulia zile pesa.

Baada ya kurudi na zile pesa,kila mtu alishangaa kijana mdogo nawezaje kuwa na pesa nyingi kiasi hicho.

Niilimuuliza yule mwanamke "itachukua siku ngapi mpaka mimi kuhamia kwenye nyumba yangu?".

Aliniambia "Tupatie wiki moja bosi wangu".

Nilimkabidhi ufunguo na ile nyumba nikamwambia awe makini!.Nilipotoka hapo dukani nilielekea mtaa mmoja kuna duka walikuwa wanauza vito vya thamani kama heleni,pete na cheni za dhahabu.Kuna dada mmoja alikuwa mwarabu ambaye wakati huo alikuwa kafunga ushungi ndiye nilimkuta kama muuzaji wa lile duka,pia kuna wauzaji wengine niliwakuta humo ndani lakini mimi nilitaka nihudumiwe na yule mrembo,kilichonipeleka hapo dukani,ni kwamba nilikuwa nataka nimchukulie yule mwanamke wangu mwalimu mkufu na pete ya dhahabu!.Kiukweli yule mwalimu licha ya kutaka kumkomoa lakini nilianza kumpenda sana.Basi nilimsalimia yule mtoto mzuri wa kiarabu aliyekuwa akiuza,bahati nzuri alinisalimia kama tunajuana.Baada ya kuwa nimemaliza kufanya manunuzi,nilimuomba yule dada anipatie namba yake,nilimwambia nilikuwa nina maongezi naye baadae!.

Yule dada aliniambia "Maongezi gani kaka?".

Nilimwambia "ni maongezi ya kawaida tu mrembo".

Aliniambia "Kwani huwezi kuniambia hapa mpaka nikupatie namba yangu ya simu?".

Nilimuuliza "Kwani umeolewa?".

Akaniambia "Hapana".

Nikamuuliza "Sasa kama bado hujaolewa kwanini unaninyima namba?".

Alishindwa kunijibu akawa anaendelea na shughuli zake.

Nilimuuliza "Unaitwa nani?".

Akajibu "Naitwa Zainati".

Nilimsihi sana Zainati anipatie namba yake lakini akasema hawezi kutoa namba na endapo nikiendelea kumsumbua angemuita mlinzi!,basi nikaona isiwe kesi sana maana kuna wateja wengine walianza kuingia mle dukani.

Nilimwambia "Yaani Zainati pamoja na kutumia gharama kubwa kukuchangia lakini bado unaniona kama kibaka?".

Niliachana naye nikawa nimeondoka zangu lakini niliapa nikasema "lazima anitambue mimi ni nani,hawezi kuniletea dharau kiasi hiki wakati uwezo wote ninao".

Jioni nilimpigia simu yule mwalimu akaja geto kwangu nikampa zile zawadi zake,kiukweli alifurahi sana na alinishukuru sana.Basi siku hiyo alilala hapo kwangu na asubuhi kulivyokucha alielekea shuleni kama kawaida,mimi nilimwambia kuna mahala nilikuwa naelekea hivyo nisingeenda huko shuleni siku hiyo.Nilikaa nikawaza nikasema sasa ilipaswa nirudi kwa mzee Nchibaronda kumrudishia shukurani kama alivyoniambia,Pia kuna dawa kadhaa pale ndani zilianza kuniishia,hivyo nilitaka nikaongeze nyingine.Siku hiyo nilishinda hapo nyumbani lakini alfajiri ya siku iliyofuata niliondoka kuelekea Kigoma,Nilipofika kigoma sikutaka itumia ile njia ya mkato ya kutamka,maana mzee aliwahi kuniambia hilo ziwa Tanganyika lina nguvu za ajabu hivyo niwe makini,nilifahamu ningetumia ile njia ya kuukamata mkono na kutamka ingekuwa ni hatari kwenye lile ziwa,hivyo nilitumia boti kama kawaida mpaka Kalemii na nilipofika Kalemii niliunganisha kwenda mpaka Moba kisha nikachukua usafiri mpaka kijiji cha Kirungu.Wakati huo sikuwa na pasipoti ila hakuna aliyeniuliza kwasababu nilikuwa nikitumia ushirikina.

Nilimkuta mzee Nchibaronda na aliponiona aliniambia "Wewe kijana ni mwaminifu sana".Tulipiga stori sana akawa ananiuliza namna nilivyoweza kufanikiwa!.Nilitoa kiasi cha milioni 2 nikampatia mzee na akaniambia huo ni mwanzo tu bali mambo mazuri yanakuja.Nilimweleza kilichonipeleka kwake mbali ya kutoa pesa ya shukurani lakini pia kuna dawa zilianza kuisha.

Mzee aliniambia "Ondoa shaka mwanangu hapa umefika".

Aliniambia "Kesho tutaongozana wote msituni tukachume dawa!".

Asubuhi kulipokucha tulielekea msituni tukaanza kuchuma dawa kwenye ile miti aliyoifahamu yeye na mingine pia niliifahamu.Basi kuna mti mmoja alinionyesha pale akanimbia kwamba "Unauona huu mti?".

Nilimjibu "ndiyo nauona mzee".

Akanimbia "huu mti kuna dawa unaichanganya halafu unaitengeneza kama chai na ukiinywa unaweza kulala na wanawake hata watano kwa pamoja na ukawashughulikia kisawasawa,wasipo zimia basi wanaweza kabisa kupoteza maisha maana wewe utakuwa huchoki ila wao cha moto watakiona!".

Huo mti nakumbuka wakati nikiwa Tabora kwenye pilika zangu za ushirikina niliwahi kuuona.

Basi mzee akaanza kunielekeza namna ya kutengeneza ulikuwa unachanganya na majani fulani hivi ya mti fulani halafu unaukausha!.Nilikuwa najisemea kimoyo moyo kwamba nikirudi Mwanza nataka Zainati anitambue vizuri kwamba mimi ni nani!,mzee alinichumia dawa nyingi za kutosha,kwakuwa nilikuwa ninafahamu sasa namna ya kuzichanganya sikupata shida sana!.Tuliondoka msituni kurudi kwa mzee Nchibaronda na mimi sikutaka kupoteza muda nilimuaga mzee akaniambia ananitakia mafanikio mema.Niliondoka zangu kurejea Kigoma ili nirudi Mwanza!.Nilifika kigoma muda ulikuwa umekwenda sana hivyo nililazimika kulala hotelini na asubuhi nilidamka kuelekea kwenye magari ya Mwanza kwa ajili ya safari.





Itaendelea....................
 
MKASA WA PILI - Sehemu ya 20

Inaendelea.............

Niliondoka hapo geto kwangu nikiwa nimejianda kikamilifu kwa ajili ya kuelekea Shinyanga,Nilifika maeneo fulani hv panaitwa Tinde,pale Tinde kuna njia moja ilikuwa ikielekea Kahama.
Sasa kabla hujafika kahama hapo katikati huwa kuna ka mji kanaitwa Isaka,Tukio nililoenda kupiga siku hiyo ilikuwa katikati ya Tinde na Isaka!

Nilipofila pale nilianza kuangalia magari yanayopita pale!,Nilikuwa nina uwezo wa kuliona gari lote na uwezo wa abiria waliokuwemo!,Kama hilo gari lilikuwa limebeba watu waliokuwa wamejizindika nilikuwa nina achana nalo!

Sasa hapa labda nieleze kidogo!,Iko hivi,Mara nyingi mshirikina yeyote au mchawi akimuona mtu hata kama analindwa na Mungu yeye kwa akili yake anajua huyo mtu atakuwa na dawa kali kuliko zake!
Hiyo hali na mimi nilikutana nayo kwenye baadhi ya magari na kiukweli nilikuwa ninaachana nao maana nilijua naweza kupata majanga!
Nilipokaa kwa muda mrefu kidogo yale maeneo niliona kuna Gari aina ya Noah lilikuwa linakuja kwa kasi sana!,nilipopiga darubini yangu niliona waliokuwa ndani ya hilo gari walikuwa emptiness(Hawakuwa na chochote ambacho kingenizuia mimi kufanya tukio).

Basi kuna tego nililiweka pale Barabarani na gari ilipofika yale maeneo ilikula mzinga wa maana na palepale walikufa watu 3,Ndani ya lile gari kulikuwa na Mwanaume na mwanamke wamekaa mbele na nyuma kulikuwa na abiria kama 5 hivi,kwa muonekano wa lile gari nadhani wale wa Mbele walikuwa ni mke na mume ambao walionekana kabisa ndiyo wamiliki wa lile gari wale wengine nadhani walikuwa tu abiria ambao walikuwa wamewachukua njiani ili kupata hela kidogo!
Nililisogelea lile gari na nikachukua kibuyu kile na kuanza kuweka damu!,Nilihakikisha siachi hata tone la damu na wale ambao niliwakuta hai nilihakikisha nawanyonya damu yote kiasi kwamba hata wangepelekwa hospitali wasingefika kabla hawajafa!,Na hivyo ndivyo ilivyokuwa!

Nilipomaliza zangu kufanya kilichonipeleka niliondoka yale maeneo pasipo kuonekana na yeyote!
Nilipofika geto kama kawaida nilichukua kile kibuyu nikakiweka chini ya uvungu na mimi nikaondoka zangu kupiga mishemishe zangu za ualimu!
Kwa wakati huo nilikuwa ninapiga pamba kali na nilikuwa nina pendeza sana na isingekuwa rahisi kwa mtu yeyote kujua ninachokifanya!

Sasa pale shuleni nilipokuwa nikifundisha kama kuzuga ili nionekane nina kazi,kuna demu mmoja alikuwa Mwalimu ameajiriwa,kumbuka mimi nilikuwa mwalimu temporary mpaka wakati huo!
Yule Maalimu alikuwa mzuri sana na alikuwa na maringo sana,kuna wakati unaweza kumsalimia na asikuitikie kisa tu alikuwa mzuri na wengine tulionekana vibaka tu,Kwa wakati huo alikuwa na gari ambayo inasemekana alinunuliwa na jamaa yake ambaye tuliambiwa alikuwa na mshiko!
Alikuwa na kigari fulani hivi kinaitwa Duet,nadhani kalikuwa kametengeneza na kampuni ya Toyota kama sikosei!

Nilijiapiza ya kwamba wikiendi itakayofuata,yaani ndani ya wiki hiyo lazima atanitambua maana nilisema lazima nimkung'ute shipa la maana!
Basi baada ya vipindi nilirudi zangu nyumbani na nilipofika nilikuta kama kawaida begi lile limejaa pesa na nkaanza kuzihesabu mara hii zilikuwa kama milioni 15,Nilizitoa kwenye Begi na nikaziweka kwenye sanduku moja ambalo ndo nilikuwa natunzia hela na lile begi nikalirudisha uvunguni!
Wakati huo kwakuwa ndo kwanza mwezi ulikuwa umeanza nilikuwa nimelipwa vi-hela vya kazi yangu hiyo niliyokuwa naifanya!

Kiukweli nilikuwa sioni faida yeyote ya ile hela kwa wakati huo maana nilijiona kama ni pesa ninayo ya kutosha hivyo kule nilienda tu kufanya kazi kama geresha tu!
Sasa niliamua kulivalia njuga suala la yule Maalimu aliyekuwa na maringo,Kuna dawa nilitengeneza hapo ndani na nikaiweka mfukoni nikaondoka zangu!

Ndugu zangu kwa ile dawa hakukuwa na kiumbe yeyote anayeitwa mwanamke ambaye alikuwa anachomoa,sema mimi na wanawake ilikuwa ni mbalimbali ila nilikuwa na dili na wale tu waliokuwa na nyodo na dharau!
Nilipofika shuleni niliendelea na shughuli zangu kama kawaida na nilipopata wasaa wa mapumziko nilimfata yule demu aliyekuwa kaumbika kila idara,nikamsalimia na aliitikia siku hiyo kwa uchangamfu kama wote!
Nilimuomba baadae atakapotoka taka kuondoka anipe lift na akakubali akasema "Ondoa shaka".
Sikuwa na wasiwasi maana nilijua huyu tayari ni wa kwangu!
Baadae nilipomaliza kufundisha kama kawa ilibidi nimsubiri na alipomaliza tuliondoka zetu akanibeba kwenye hicho kigari chake!

Tukiwa ndani ya gari sikutaka kupoteza muda nilimgusa mkono na palepale alisema "leo naenda kulala kwako", Nilimuuliza "Kwanini"?,Akaendelea kusema "Huwa nakupendaga muda mrefu sema hujuagi tu",nilitambua tayari kitu kimeshatiki! Kwa maana alikuwaga hanaga muda na mtu hasa ukizingatia kipindi kile nilikuwa nimechoka na isingekuwa rahisi kupendwa na mtoto mzuri kama yule!
Kwakuwa hapo kwenye hiyo nyumba niliyopanga kulikuwa na geti hivyo kuliwezesha lile gari lake kupata nafasi ya kupaki!
Ilikuwa mida ya jioni na wapangaji wenzangu walikuwa wakishangaa namna nilivyokuja na yule demu mkali,wengi walishangaa maana hawakuwahi kuniona pale nyumbani na demu yeyote!
Tulipofika nyumbani nilimwacha mi nikaelekea zangu kununua nyama ya kuchoma na viazi vilivyokaangwa(chips)nikamletea!
Mle ndani kwangu nilikuwa najitahidi kupaweka safi maana sikutaka yeyote afahamu kilichokuwa kinaendelea na nilihakikisha kile kibuyu nimekificha kimazingara hakuna yeyote aliyekiona ila mimi tu!

Kiukweli usiku huo yule mwanamke hatokuja kuusahau maana nilimkung'uta shipa la ki-mkakati na namna alivyokuwa mzuri nilihakikisha hatonisahau!
Asubuhi kulivyokucha alikataa kuamka kabisa na akasema kama nikufukuzwa kazi basi afukuzwe ila pale aondoki maana hajawahi kukutana na mwanaume kama mimi!,Nilimsihi sana tuende kazini lakini aligoma katakata!
Basi siku hiyo nzima tulichapana mle ndani bakora za hali ya juu na kiukweli nilikuwa sichoki maana nilikuwa nina uwezo huo!,Nilimchapa bakora sana na alishindwa kuamka kabisa akawa kama mgonjwa siku nzima hiyo!

Kuanzia hapo nilimtengenezea dawa yaani amsahau yule jamaa yake na aniwaze mimi tu lakini baadae nilikuja kuona anaweza kuwa mwendawazimu maana alikuwa kama kachanganyikiwa kwa ajili yangu!,Nililegeza kidogo na akawa anaenda kwake kama kawaida ila nilipomuhitaji nilimpata kwa wakati niliotaka mimi!

Yule jamaa wa Igoma mwenye nyumba alinipigia simu na akawa ananikumbushia kuhusu kile kiasi kilichokuwa kimebaki na nilimwambia ndani ya siku mbili hizo nitampa!
Kwenye begi nilikuwa nina milioni 15 hivyo pungufu ya kumpa mzee ilibaki milioni kumi na tano nyingine!,Na kwa wakati huo haukuwa mwisho wa Mwezi ambapo niingeenda kufanya tukio!
Basi nilimshawishi yule demu ticha amwambie mumewe ampe milioni kumi na tano,Kuna kitu nilitamka pale kwenye mkono wangu wa kushoto uliokuwa na ile Irizi ya kwamba amuombe yule bwana yake hiyo milioni kumi na tano aniletee na asihoji chochote!
Hivyo ndivyo ilivyokuwa!,Yule mwanamke alionekana sana kuchizika na mimi laki sikutaka iwe hivyo sana maana niliona ntampoteza!
Baada ya siku hizo nilizomuahidi mzee kweli nilimpelekea ile hela na kutakaandikishiana pale na nkakabidhiwa ile nyumba rasmi!

Kiukweli lilikuwa bonge la nyumba la kisasa na nikaona litanifaa sana kwenye shughuli zangu!
Hivyo nilijisema kwamba ikifika mwisho wa mwezi nikienda kupiga tukio pesa nitakayo ipata nitanunua kila kitu cha ndani na kuhamia huko Igoma.



Itaendelea...................
Aloo mkuu hii episode ya 20 imenifanya nitafute nyumba ya ibada nikaswali.
 
Jana wakati naisoma hii sehemu ya 19 ulikuwa saa kumi na mbili hivi! Ghafla kuna jamaa akaja pale kijiweni akasema kuna ajali imetoke huko mgodini(Rashi wanaita) Bodaboda zimegongana ila mmoja amekufa hapohapo lakini hana hata TONE DAMU! Nikajisemea moyoni Teyari kafala imeshafanyika hapo!
Unasema kweli??
 
Nilikuwa nashauri pia hizi contacts uziweke mwisho wa kila post yako, ili namba zako ziwe rahisi kuwa traced...!!

We're together in this one usijali.!
Carleen mpnz. Sevu Ile namba kwenye hiyo iPhone yako, Kisha kabla ya kufanya shopping ya Xmas kwa vitu visivyo vya muhimu. Mtumbukizie mRume ka hamsini au hata ka laki..
 
Ni youtube mama sio uzi wa humu

Ila kwa humu kuna uzi wa Bilionea Bazoka ndio nilikua napotezea mawazo naposubiri hii sema yule mwandishi mnyanyasaji sana
Niite huko basi, ila huko youtube pia ntaenda[emoji28][emoji28][emoji28]
 
Back
Top Bottom