onlyalvira
JF-Expert Member
- Dec 9, 2013
- 1,499
- 3,113
Hata mm nahisi hvyoChizi Maarifa ndiyo LwandaMagere
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata mm nahisi hvyoChizi Maarifa ndiyo LwandaMagere
Kabla hajanunua nyumba mpya kibuyu alikihifadhi Wap kama sio getoni mwake? Tens chini ya uvungu!Ngoja nikujibu Mimi ambae nimeelewa mana mkuu we ulisoma fasta na auku elewa ni ivi alinunua nyumba mpya aka karabati ikakamilika fresh na akahama kule geto, ile nyumba mpya katika vyumba vinne akatenga kchumba kimoja akaweka kile kibuyu cha damu nkwa jili ya mungu kibonge na hats pesa alikua anazikuta humo, yusta na zainat aliwaleta kwenye hii nyumba yake mpya na kila mmoja akamuweka kwenye chumba chake so akawa anapga shipa zamu kwa zamu anatoka chumba hiki anahamia chumba hiki pasipo wao kufahamu. Bila shaka jibu swaafiiiiii na umeelewa mkuu bila shaka kuuliza si ujinga Bali nikutaka kujua.
Yote hiyo ni mitego tu mkuu,ni kipimo pia cha uvumilivu wako. Ndio maana vijana wengi wana-fail katika mambo mengi. Unakutana na mtihani kidogo tu umeterereka. Katika 100 wanapass 3Ungetoroka na huyo binti wa mganga mkuu...unafeli wapi
Sorry hata ukinijibu baadae niulize hili swali. Muda wote wa haya mambo,tangu kule polini,kupaa,mpaka huko chini ya maji ulikuwa unajihisi kama vile ulivyotoka Tarime?. Yaani bado ulikuwa una akili zako timamu 100%?MKASA WA PILI - Sehemu ya 16
Inaendelea.............
Tulipofika hapo Ziwani tulianza kushangaa hatukujua cha kufanya,lakini mi nkakumbuka kwamba yule Mzee Nchibaronda aliniambia kuna usafiri ungekuja kutuchukua pale na utakapofika sikutakiwa kupoteza muda!
Mpaka wakati huo hatukuwa na kitu chochote zaidi ya zile ngozi tulizovikwa kuficha nyeti zetu na vifaa vya kazi ambavyo kila mtu alipewa maelekezo kivyake!
Nguo nilizoenda nimevaa pamoja na pesa vyote niliviacha kwa babu Nchibaronda na alisema nitakapokamilisha kupewa utajiri huko nilipotakiwa kwenda ningevirudia hapo nyumbani kwake!
Kiukweli nilianza sasa kuwa na roho ya kikatili sana na kumbuka kwamba aliyenifanya mimi kwenda kuusaka utajiri ni yule shemeji aliyekuwa dada yake na Mme wa sista yangu mdogo!,Kiukweli yule shemeji nilikuwa nina hasira nae sana!
Basi baada ya muda kama wa nusu saa ulitokea upepo mkali hapo ziwani na kuangalia juu tuliona Ungo mkubwa(Huu ungo ni kama ule tunaopetea mchele majumbani)ukiwa unashuka,ulipofika katikati ya ziwa uliganda kwa juu,Nilikumbuka maneno ya Mzee Nchibaronda kwamba "Kabla ya yote nichukue ule unga wa albino nimwage ziwani"
Nilifanya kama nilivyoelekezwa,Ule unga niliumwaga kwenye maji ya ziwa na ndipo ule ungo uli shuka zaidi chini na ukatusogelea jirani tulipokuwepo lakini haukugusa maji.
Yule jamaa aliyekuwa na ile shilingi yenye tobo aliirusha kwenye Ungo na akawa wa kwanza yeye kupanda kisha nikafata mimi halafu wa mwisho alikuwa yule jamaa aliyekuwa na ile irizi ambayo tuliambiwa ni pasipoti huko tunakoenda!
Safari ikaanza kuelekea ziwani,Mambo yote hayo yanafanyika hapo ziwani tulikuwa tukiona sisi tu,watu wengine waliokuwa kando ya ziwa hawakuelewa chochote maana niliona wakiendelea na shughuli zao kama kawaida!
Safari ilisonga sana kuelekea katikati ya ziwa tanganyika,Tulipofika katikati ya lile ziwa kwa maana kwamba tulikuwa hatuoni eneo lolote la nchi kavu kaskazini,kusini,magharibi wala mashariki!.
Ule ungo ulianza kushuka chini hapo katikati ya ziwa na maji yakawa yanajitenga kama kutupisha!,Tuliposonga sana kwenda chini ya maji hatimaye tulifika nchi kavu chini ya maji na tukashuka hatimaye ule Ungo ulipotea!
Nilibaki nimeduwaa maana nikiangalia huko tulipo palikuwa ni nchi kavu na nikiangalia juu kulikuwa na maji,hilo eneo tuliloshuka lilikuwa ni Kubwa mno na lilikuwa kama uwanda!
Basi yule jamaa mwenye ile Irizi tuliyoambiwa ni pasipoti kuna maneno aliyatamka pale na akairusha ile Irizi kuelekea juu na ikapotelea juu kwa juu!,Kufumba na kufumbua ghafla tuliona majumba mengi ya kifahari na watu wengi wakiwa uchi wa mnyama na kila mtu aliendelea na shughuli zake!
Kumbuka hapo mimi kwa upande wangu nimefata utajiri na wenzangu wao walikuwa wameenda kufata nguvu za uchawi!
Wengi wa watu niliowaona huko walikuwa wanawake,japo wanaume pia walikuwepo lakini hawakuwa wengi sana!,Basi kwa mbali walikuja mabinti fulani kutupokea na walipofika hapo kila mtu walimsalimia kwa lugha yake!,Wale jamaa kwa kuwa walikuwa wanatoka Sumbawanga nadhani walisalimiwa kwa lugha yao maana sikuifahamu na mimi pia kuna mdada alinisalimia kisukuma!
Baadae mimi na wale jamaa tulitenganishwa,Wao waliekea nji yao na wale wadada wawili na mimi nilichukuliwa na yule dada mwingine aliyenisalimia kisukuma!
Niliendelea kushangaa sana kule chini ya maji namna kulivyojengeka na kulikuwa kuzuri sana,Naweza sema kwa uzuri ule hata Mwanza haikuona ndani!
Ndugu zangu hii dunia ina mambo sana na usije ukaona unaishi tu ukachukulia poa,Kila muda usiache kumshukuru Mungu kwa kila jambo na endelea kumshukuru sana Mungu kukuficha mambo mengi usiyaone!,kwa hali niliyoiona duniani huko kiukweli ni roho wa Mungu tu aliyenifanya mpaka sasa naandika hapa!,na ndo maana baadae niliamua kumtafuta Mungu kwa nguvu zote na kuachana na mambo ya ulimwengu ambayo muda si mrefu yatafikia tamati!
Basi yule dada alinichukua mpaka kwenye jumba moja ambalo nilikuta kuna jamaa wanasex hadharani na hawakuona taabu kabisa wala aibu yeyote!,Baadae nilikuja kufahamu kwamba wale jamaa walienda mle majini kama sisi na walienda kwa shughuli za kusaka kilichowapeleka lakini baada ya kufika huko walishindwa kujizuia na tamaa za ngono hatimaye walipofanya tu ngono ndipo hiyo kazi ya kufanya sex ikawa kazi yao masaa 24 usiku na mchana!,Yaani wanawake wote wa humo ndani walikuwa wanapewa huduma na hao jamaa usiku na mchana na hayo ndo yalikuwa maisha yao huko na wasingweza kutoka huko mpaka mwisho wa maisha yao!
Nilipofikishwa hapo yule dada aliondoka na walikuja madada wengine waliokuwa wazuri kama half - cast hivi,mmoja alinivua ile ngozi niliyokuwa nimevikwa kuficha nyeti na mmoja alinishika kuniingiza kwenye bwawa la maji yaliyokuwa na uvuguvugu na wakaanza kuniosha!
Nilioshwa na kupapaswa kila sehemu ya mwili wangu!,nililambwa kila sehemu ya mwili wangu na wakati huo uume ukiwa umesimama kama msumari!,Kiukweli ni rehema za Mungu tu sikuweza kufanya lile tendo maana wale wadada walikuwa na kila sifa ya kuitwa mwanamke!,wakati wakiwa wanaendelea kuniosha na kunipapasa kila mahali na kuzichezea zile nyeti zangu,nilisikia sauti ya Mzee Nchibaronda ikiniambia "Usithubutu kufanya ngono,ukifanya nao tu ngono umekwisha"
Ile sauti iliendelea kunisihi sana na sikuwa na namna ilibidi niitii ile sauti!,Baada ya muda kidogo walimaliza kuniosha na walinibeba kunitoa mle ndani ya maji na nilichukuliwa na mwanamke mwingine kupelekwa chumba kingine na wale waliishia pale!
Nilipoingizwa mle chumbani kulikuwa kuzuri ajabu na kulikuwa kukinukia marashi yenye harufu kali sana!
Yule dada aliyekuwa mzuri kama wenzie alinisogelea na kuanza kunipaka mafuta ambayo baada tu ya kugusa ngozi nilianza kuwashwa sana na aliniambia nisijikune,aliendelea kunipaka yale mafuta sehemu zote za mwili wangu,wakati huo kila mtu akiwa uchi wa kuzaliwa!
Baada kama ya dakika 2 niliachwa kuwashwa na nilijiona mwepesi sana na nilikuwa na ufahamu wa kupita maelezo!,Kuna mambo niliyafahamu ambayo yalipita uwezo wangu wa kawaida wa akili ya kibinadamu na ndipo nilifahamu kwamba hata ule unga niliopewa na mzee Nchibaronda kumbe ilikuwa mifupa ya Albino iliyokuwa imesagwa!,Kwa ufahamu na uelewa niliyokuwa nao huko ilibidi nimzuie mama asiwe na akili ya kunitafuta wala kuniulizia kwa wakati huo wote mpaka ntakaporudi Mwanza,na nilifanya na ikawezekana!
Basi baada ya hapo yule dada alinichukua akaanza kunitembeza na kunionyesha viunga mbalimbali vilivyohusika na vitengo mbali mbali!
Alinichukua mpaka kwenye mjengo ambao kuna watu kama mimi walienda kuusaka utajiri,Humo ndani kulikuwa na watu mbalimbali ambao yule dada aliniambia walikuwa wameenda kuusaka utajiri na akaniambia chochote ukionacho humo ndani nitakapofanikiwa kuondoka basi ikawe siri yangu vinginevyo nitapata taabu sana!
Kuna jamaa wawili ambao mpaka leo ninawafahamu na wapo hapa mjini Dar es salaam wakiendelea kutesa na kula maisha wakifurahia utajiri wao!,Mmoja yupo hapo mbezi beach ni tajiri mkubwa tu na mwingine anaishi maeneo ya Tegeta!
Siku moja namuona mmoja wapo kwenye TV anaenda kutoa misaada nikawa nacheka tu!
Nilipoingizwa mle ndani wote tulikuwa uchi wa mnyama na kulikuwa na baadhi ya wanawake lakini wanaume ndo tulikuwa wengi!,Basi nilikuta wenzangu wanaendelea kupewa mikakati ya namna ya kufanya!
Baada ya muda kidogo walitoka hivyo nilibaki mimi na mshikaji mmoja ambao tuliingia muda si mrefu!
Yule mwanamke alianza kusema "Sasa umekuwa mwanaume,na muda si mrefu utaelekea kwa Mungu wa ulimwengu huu ambaye atakupa masharti na ukiayaweza utakuwa tajiri mkubwa sana"!,Niliitikia "sawa"
Kiukweli toka nimeingia humo ndani ya maji sikuwahi kuuona usiku na sikuelewa hiyo ilikuwa siku ya ngapi mimi kuwa pale lakini baada ya kutoka nilielewa siku nilizokaa mle ndani!,na kwa wakati wote huo nilikuwa sihisi njaa!
Baada ya muda kadhaa ya siku hizo nilizokuwa humo ndani,tulichukuliwa mimi na wale wenzangu wote niliowakuta mle ndani,tulikuwa grupu la watu kama hamsini hivi ukijumlisha na wanawake waliokuwa kama 6 hivi!
Tuliambiwa tuelekee kwa Mungu aliyekuwa kwenye jumba moja la kifahari sana!
Tulifanikiwa kuingia mle ndani na tuliambiwa tusujudu mbele ya huyo Mungu,Kiukweli ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona mtu mnene kwa kiwango kile!,Yule Mungu alikuwa mnene sana mpaka kiti alichokuwa amekalia kilikuwa kimefunikwa na nyama zake!
Baada ya kusujudu pale kila mtu alianza kwenda kwake na kuanza kuelezea shida yake na kupewa maelekezo na baada ya hayo maelekezo aliondoka hapo ndani!
Mimi nilikuwa mtu wa nilikuwa mtu wa 49 maana walianza wale tuliowakuta kwanza na baada yangu kuna jamaa aliyenifuatia!
Itaendelea..................
Ngoja nikujibu Mimi ambae nimeelewa mana mkuu we ulisoma fasta na auku elewa ni ivi alinunua nyumba mpya aka karabati ikakamilika fresh na akahama kule geto, ile nyumba mpya katika vyumba vinne akatenga kchumba kimoja akaweka kile kibuyu cha damu nkwa jili ya mungu kibonge na hats pesa alikua anazikuta humo, yusta na zainat aliwaleta kwenye hii nyumba yake mpya na kila mmoja akamuweka kwenye chumba chake so akawa anapga shipa zamu kwa zamu anatoka chumba hiki anahamia chumba hiki pasipo wao kufahamu. Bila shaka jibu swaafiiiiii na umeelewa mkuu bila shaka kuuliza si ujinga Bali nikutaka kujua.
Ilipofikia mm nataka niache kuisoma jamaa kaanza kuua ndugu zakeEm nipe link ya Telegram
Sorry hata ukinijibu baadae niulize hili swali. Muda wote wa haya mambo,tangu kule polini,kupaa,mpaka huko chini ya maji ulikuwa unajihisi kama vile ulivyotoka Tarime?. Yaani bado ulikuwa una akili zako timamu 100%?
@Carleen muda mwingine wa moto,muda mwingine wa baridi. Sikunyaki sana. Unaweza kukuta hapa ukanishushia rundo la maneno magumu. Muda mwingine maneno kama unaishi jirani na YESUAiseeeh..!!
Kwa wanaoamini katika Mungu wa mbinguni, Muumba mbingu na nchi, kila mtokapo na muingiapo hakikisheni mmejifunika kwa damu ya Yesu, Ombeeni safari zenu, Ombeeni wapendwa wenu hakikisheni mnawaweka chini ya ulinzi wa Mungu siku zote, Maan' this sh** is so real..!
Inapatikana wapi mkuu?Nimeshaanza nayo hii ya Zabron leo niko episode ya tatu
Huwa sipendi ujinga
Eti..Chizi Maarifa limejichanganya[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nilisema hiyo stori ya kutunga, vichwa maji wakajiita watetezi
Mkuu nimecheka sana ulivyomuuliza maswali ghafla akafuta comment yake..... sema bado sijajua je Chizi maarifa ndio Lwanda au Chizi maarifa kafanya kusudi kumharibia pesa Lwanda [emoji23][emoji23][emoji23]We ndo ulisusia uzi kisa Mods wameuhamisha? Vip ulikuwa na LwandaMagere kipindi hayo yote yanatokea au yule Dada muuza phamarcy ndo alikuwa anakuhadithia kupitia wale viumbe wake?
Au wewe ndiye LwandaMagere mwenyew una ID mbili, maana umeandika as if we ndo unaisimulia huo mkasa wa Lwanda
Kweli aisee alitaka afanye mchezo kama huuNdio maana alichukia sana uzi wake kuhamishwa, lengo lake lilivurugwa
Chizi maarifa ndio lwandamagere,kama unakumbuka kuna story yake ilihamishwa jukwaaa,aliwaka sana na akasusa kuendelea akidai ni story ya kweli kwann iwekwe kwenye jukwaa la burudan,alitaka kufanya kama hvMkuu nimecheka sana ulivyomuuliza maswali ghafla akafuta comment yake..... sema bado sijajua je Chizi maarifa ndio Lwanda au Chizi maarifa kafanya kusudi kumharibia pesa Lwanda [emoji23][emoji23][emoji23]
Nakumbuka vizuri aligoma kumalizia......hajatenda haki ni bora angesema tu story ya kutunga kuliko kuaminishana sana story ya kweli hadi watu wameenda kulipia na kudownload telegramChizi maarifa ndio lwandamagere,kama unakumbuka kuna story yake ilihamishwa jukwaaa,aliwaka sana na akasusa kuendelea akidai ni story ya kweli kwann iwekwe kwenye jukwaa la burudan,alitaka kufanya kama hv
Kwani chizimaarifa kafanyyaje maana mm niliachana na huu uziMkuu nimecheka sana ulivyomuuliza maswali ghafla akafuta comment yake..... sema bado sijajua je Chizi maarifa ndio Lwanda au Chizi maarifa kafanya kusudi kumharibia pesa Lwanda [emoji23][emoji23][emoji23]
Duuh Sasa nimeelewaWe ndo ulisusia uzi kisa Mods wameuhamisha? Vip ulikuwa na LwandaMagere kipindi hayo yote yanatokea au yule Dada muuza phamarcy ndo alikuwa anakuhadithia kupitia wale viumbe wake?
Au wewe ndiye LwandaMagere mwenyew una ID mbili, maana umeandika as if we ndo unaisimulia huo mkasa wa Lwanda