Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

Mikasa ya ajabu niliyoishuhudia kwa macho yangu

MKASA WA KWANZA - Sehemu ya 3


Inaendelea.............



Basi siku ya kuwapokea wageni wa dada wa kazi iliwadia na kila mtu alikuwa na bashasha siku hiyo,nakumbuka siku hiyo lilipikwa Pilau ambalo sijawahi kulishuhudia mpaka leo hii na ukubwa wote huu,pale nyumbani kulikuwa na ratiba ya vyakula kila siku kuanzia jumatatu hadi jumapili ilikuwa na chakula chake,Kila jumapili tulishazoea ilikuwa ni siku ya kula Pilau,lakini kilichonishangaza sana ni kwamba siku hiyo pilau lilipikwa haikuwa jumapili ila kwasababu ni chakula ambacho nilikuwa nakipenda basi ilibidi nifurahi kimya kimya.Bado sijajua kama lile pilau ndiyo leo linaitwa Biriani ama vipi maana enzi hizo hata Biriani mimi silifahamu nilichokuwa nakifahamu ni Pilau tu,au wengi wetu tuliuita wali mchafu,Pilau lile lilikuwa jekundu na lilikuwa tamu hatari,kama nilivyosema hapo mwanzo sijawahi kula pilau la aina hiyo toka kipindi hicho mpaka leo hii nishakuwa mtu mzima,kumbuka mwaka huo wa 2000 mimi nilikuwa na miaka 14.

Kweli!,siku hiyo tukala vizuri kuanzia mchana mpaka jioni na kila mtu akajiandaa kuwapokea wageni,kumbukeni hapo mwanzo niliwaambia kwamba,moja ya sharti ilikuwa kwamba,ulipokuwa ukitaka kwenda kuoga ilikulazimu yule dada wa kazi akupe ile sabuni aliyokuwa akiitumia yeye ili ukaogee na hivyo ndivyo tulivyofanya!,ilipofika jioni kila mtu alikuwa yupo tayari;Ilipofika mida ya saa 1 usiku,yule dada alituita kama kawaida pale sebuleni na akatueleza namna alivyopenda tulivyoonesha utii,vinginevyo tungemuumiza yeye binafsi hata sisi pia tungeumizwa,akatuambia kwa kuwa tumejianda kikamilifu,kila mtu awe tayari kuwapokea wageni,kiukweli muda ulizidi kuyoyoma sana,mimi kama kawaida nilipata mashaka kidogo,mida ya saa 4 usiku ilipofika wageni sikuwaona na sijawahi kuwashuhudia wageni wakija pale nyumbani usiku,nilishazoea hata kama wageni wangetoka mbali basi walifika pale nyumbani mapema,ila siku hiyo ilikuwa tofauti,kitu kingine kilichonipa mashaka ni kwamba hao wageni wangefika vipi pasipo mwenyeji wao kwenda kuwapokea?,Kumbuka miaka hiyo simu za mikononi zilikuwa kwa matajiri sana,pamoja na wazee wangu kuwa na uwezo lakini hakuna aliyekuwa na simu ya mkononi au tuliita miche ya sabuni,simu iliyokuwepo ni zile simu za mezani za tu.

Yule dada wa kazi chumbani kwake kulikuwa na harufu ya marashi makali na yenye kuvutia sana!, ilipofika saa 6 usiku muda ambao nilishachukuliwa na usingizi kwenye kochi pale sebuleni,ghafla nilishitushwa na kishindo kikubwa juu ya bati!,kiukweli ndugu zangu sijawahi kuexperience hili tukio na halikuwa tukio la kawaida bali liliogopesha sana na kila mtu aliogopa,Kumbuka haya yote yanafanyika hakuna ambaye huko nje kwa majirani aliyesikia wala kuona bali ni sie humo ndani tu!.Baada ya muda yule dada alituita wote tuingie kile chumba alichokuwa akilala yeye na yule dada yangu mwingine,baada ya dakika 10 yule dada wa kazi hakuweza kuongea tena na alikauka akawa kama samaki mkavu!,kiukweli ile hali mpaka leo sitakuja kuisahau,siku hiyo ilikuwa ni mtafutano humo ndani,ndipo ghafla tulisikia sauti ya mwanamke,huyu mwanamke aliongea rafudhi kama ya watu wa pwani hasa huko Zanzibar!.

Kumbuka sauti tunaisikia ila anaye zungumza hatumuoni,hiyo sauti ilituambia tusiwe na hofu kwani wao wamekuja kumuona binti yao na anashukuru sana kwa sisi kuwa watiifu kwa mtoto wao na akatuambia hajaja peke yake bali kaja na baba yake,basi baada ya ile sauti ya kike kuzungumza ghafla ilianza kusikika sauti ya kiume iliyokuwa nzito,ndugu zangu kumbukeni mpaka huo muda huyo dada wa kazi kakauka,alikuwa hajitingishi wala haoengei,yaani alikuwa kakaushwa kama samaki mkavu!,ile sauti ya kiume ilimuita kila mtu kwa jina lake na nakumbuka aliye kuwa wa mwisho kuitwa na kutajwa jina lake alikuwa dada yangu mkubwa,kiukweli hapa labda niseme kidogo,sijawahi kuona mtu anaongea na haonekani bali mnasikia sauti tu,nilizoea kuona ni maigizo lakini siku hiyo nilishuhudia laivu(Mubashara).Dada yetu mkubwa aliitwa na akaambiwa asogee asimame katikati ya kile chumba,kumbuka tulikuwa kwenye kile chumba alichokuwa akilala dada wa kazi na yule dada yangu mwingine!,basi dada yangu alitii akasogea,ile sauti iliianza kumwambia mambo yafuatayo ambayo bado nayakumbuka,mambo hayo ni haya :-

1.Ahakikishe itakapofika ijumaa ya wiki hiyo ambayo hili tukio limetokea asifanye kama anavyofanyaga,kwani akifanya atapoteza maisha yake,dada aliitikia kwa sauti ya kwamba ameelewa.

Hapo hatukuelewa huwa anafanyaga nini,kila mtu alibaki na swali kichwani mwake.

2.Ile sauti ilimwambia kwakuwa yeye ndiye mkubwa pale nyumbani ahakikishe anamhimiza kila mtu kuwa msafi wa kila kitu kuanzia mwili,mavazi mpaka vyumba tunavyolala vinginevyo tusipofanya hayo mahimizo tutapotea na kuangamia.

3.Jambo la mwisho hiyo sauti ilisistiza ya kwamba wao hawana shida yeyote na sisi na ndiyo maana wametupenda sana kwa kuwa watiifu.

Baada ya hiyo sauti kusema na dada na kila mtu kusikia,ghafla mle ndani ya chumba kulikuwa na mtikisiko mkubwa na vicheko vya kejeli!,ndani ya dakika kama 5 kulikuwa na ukimya wa ajabu huku tukitazamana,ndipo yule dada wa kazi akajitingisha,alilejea kwenye hali yake ya kawaida,hayo yaliyoendelea humo ndani hakutaka tumsimulie kwani alisema alikuwa anayaelewa yote!.Baada ya hapo kila mtu alitaka kufahamu ile hali iliyomkuta,alituambia kuna jambo halikwenda sawa na alipaswa kufa ila kupitia sisi tuliokoa maisha yake!,nadhani hapo mwanzo mnakumbuka niliwaambia kuhusu yule mlinzi wetu mzee Mniko,yule mlinzi siku hiyo ya tukio alikuwa amekunywa pombe ili akili yake ikae sawa,sasa kwa kuwa alisha tahadharishwa na hakusikia kumbe ile adhabu ilipaswa ailipe yule dada wa kazi na ndiyo maana alikaushwa kama samaki,pona pona yake anasema ni sisi mle ndani kutii yale aliyotuambia!.

Hiyo ilikuwa mida ya saa 8 za usiku na baada ya hapo tulitaka kufahamu yule mlinzi kule nje atakuwa na hali gani,basi dada yetu mkubwa alifungua mlango akatoka nje na kumuita yule mzee Mniko lakini hakuitikia,aliendelea kuita sana lakini hakukuwa na ishara yoyote ya mwitikio kutoka kwa yule mlinzi,basi sote tuliingia ndani kulala,dada akasema uenda atakuwa katoka nje ya geti anazunguka huko nje.Kweli!,siku hiyo tulilala kwa wasiwasi sana na kwa kuwa mimi nilikuwa bado dogo dada yangu mkubwa aliniambia nikalale naye chumbani kwake.



Itaendelea ...............
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Habarini za kutwa wanajamvi ,bila shaka wote mko bìèn!.

Kwanza kabisa nianze kwa kusema ninayo mikasa miwili ambayo nimewahi kuishuhudia kwa macho yangu na kuifanya kwa mikono yangu mwenyewe,mkasa wa kwanza ulituhusu mimi na ndugu zangu ambapo wakati huo nikiwa nina miaka 14 - 15 mwaka 2000 - 2001 huko mkoani Mara,wilaya ya Tarime,nchini Tanzania.
Mkasa wa pili unanihusu mimi mwenyewe pia,huu mkasa niliufanya wakati ambapo nishakuwa mtu mzima,hii ilikuwa kuanzia mwaka 2012 - 2018,mkasa huu unahusu maisha ya kitajiri yaliyohusisha nguvu za giza.
Kuna nyuzi kadhaa humu nimekuwa nikizisoma za watu mbalimbali kusimulia visa na mikasa ya maisha yao au jamaa zao ambayo waliwahi pitia. Hivyo nami nikaona sasa ni muda muafaka wa kuleta simulizi nilizo pitia maishani ili kuwafundisha na kuwaonya vijana wenzangu wote wenye tamaa ya kutafuta mali kwa njia niliyoifanya mimi waache mara moja kwani Mwisho wake unaweza kuwa kifo mikononi mwa shetani,ingawa mimi niliponea chupuchupu.


MKASA WA KWANZA - MWAKA 2000 - 2001.


Sehemu ya 1.


Nilizaliwa mwaka 1986 wilayani Tarime,mkoa wa Mara,nchini Tanzania.Wazazi wangu walinipatia Jina ambalo nisingependa niliweke wazi,ila jina maarufu au a.k.a nafahamika kama Lwanda Magere,kwenye tumbo la mama yangu tulizaliwa watoto 4,mtoto wa kwanza ni dada yetu mkubwa,mtoto wa pili ni kaka yangu ambaye alimfuatia dada yangu kuazaliwa,mtoto wa tatu ni dada yangu mwingine ambaye ndiye niliyemfuatia katika uzao,na mwisho kabisa nilizaliwa mimi.Elimu yangu ya msingi niliipata kwenye shule mbili tofauti,kuanzia darasa la kwanza mpaka la tatu,nilisoma shule ya msingi Sabasaba,hiyo ilikuwa mwaka 1997 - 1999;Darasa la nne mpaka la saba nilisoma shule ya msingi Turwa,hiyo ilikuwa mwaka 2000 - 2003.

Mimi na ndugu zangu pamoja na wazazi wangu tulikuwa tunaishi wilaya ya Tarime,mitaa ya Bomani,(wenyeji wa Tarime wanaielewa vizuri hii mitaa) sisi hatukuwa wenyeji wa Tarime ila mama na baba walienda huko kikazi miaka ya nyuma, hivyo tukajikuta tumekuwa wenyeji wa huko,ndugu zangu walionitangulia katika uzao,wao walizaliwa mkoani Mwanza,ila mimi pekee ndiye niliyezaliwa Tarime.Wazazi wangu kikabila ni Wasukuma,mama yangu alikuwa mwenyeji wa wilaya ya Kwimba,akitokea kijiji kimoja kinaitwa Sumve;Baba yangu yeye alikuwa mwenyeji wa wilaya ya Misungwi.Baba yangu alikuwa ni mtu wa kusafiri sana kikazi na mama yangu yeye kazi alikuwa anazifanyia pale mjini,japo pia walikuwa wakitoka kikazi mikoani,anaweza kukaa hata miezi 6 hajarudi nyumbani,mama alikuwa akifanya kazi kwenye kampuni ya ujenzi,hivyo nadhani zile pilika pilika za ujenzi pia zilimfanya kuwa bize sana.Baba yangu yeye alikuwa akifanya kazi kwenye shirika lisilokuwa la kiserikali,kwa wakati huo kwakuwa nilikuwa mdogo sikuweza kufahamu hilo shirika lao lilikuwa likijihusisha na kitu gani.

Siku moja baba alipata safari ya kikazi kwenda mkoani Singida ambako alikaa kama miezi miwili, aliporudi alirudi na dada mmoja mwenye asili ya kiarabu(half cast)akiwa kama mfanyakazi wa ndani,kwa maelezo ya baba ni kwamba,yule dada alikuwa ni mfanyakazi wa ndani,nakumbuka mama yangu alimfokea sana baba akimtuhumu kwamba uenda yule mwanamke anaweza akawa mchepuko wake, ila baba anazuga kwamba ni mfanyakazi(siunajua tena mambo ya wivu).Baadae mambo yalikaa sawa,yule dada akawa mfanyakazi wa ndani pale nyumbani kwetu,Kiukweli alikuwa mzuri sana, kwasababu tulifundishwa nidhamu na heshima,tulimheshimu kama dada yetu na tukampenda pia.Siku zikasonga,hatimaye miezi nayo pia ikakata tukiishi kwa furaha,amani na upendo.
Wakati huo nakumbuka ilikuwa mwezi wa 12 mwaka 2000.Baba alihamishwa kikazi kupelekwa jijini Dar es salaam,hivyo pale nyumbani tukabaki na mama ambaye pia alianza kusafiri kikazi na kukaa hata miezi 5 au 6 hajarudi nyumbani, kilichokuwa kinafanyika ni kutumiwa pesa ya matumizi na kutupigia simu kutujulia hali.

Baada ya siku kadhaa kupita, siku moja usiku yule dada wa kazi, alituita sebuleni mimi pamoja na wale dada zangu akatueleza ya kwamba,yeye anawageni wake ambao ni ndugu zake watakuwa wanakuja kumtembelea kila mwisho wa mwezi,kwa kuwa tulifundishwa ukarimu, hivyo hatukuona taabu, ila alitueleza ya kwamba hao ndugu zake wanamashariti makali na inapaswa tuyaelewe ili watakapokuja tusipate taabu,hivyo sababu ya kutuita ilikuwa ni kutupa namna iliyo bora ya kuwapokea hao ndugu zake!.Kiukweli mimi nilipata mshituko kidogo, nilijiuliza maswaĺi kadhaa lakini sikupata majibu, tulikuwa tumezoea kuwapokea wageni mbalimbali siku zote na walikuwa wakija bila masharti!,sasa nikawa najiuliza hao ni wageni wa namna gani waliokuwa na masharti tena akasema ni makali na kila mtu anapaswa ayafuate si ombi bali ilikuwa ni lazima!.

Watu wote pale sebuleni tulikaa kimya,nilikuwa nikiziangalia sura za dada zangu zilibadilika ghafla na kuonyesha huzuni.Basi masharti yenyewe yakawekwa bayana kama ifuatavyo:-

1. Siku hiyo wote tutavaa nguo za kulalia(pajama)nyeupe.

2. Siku hiyo vyumba vya kulala vihakikishwe vinakuwa safi isionekane hata nukta ya uchafu.

3. Kabla ya kufika kwa wageni,ukihitaji kuoga basi hakikisha unaenda kuoga na sabuni ambayo alikuwa akiitumia yeye huyo dada wa kazi.

siikumbuki ile sabuni lakini ilikuwa na marashi makali sana na yenye harufu ya kupendeza.

4. Akawaambia dada zangu kwamba,siku hiyo ambayo wageni wake walikuwa wanakuja,endapo kuna mtu atakuwa kwenye siku zake za hedhi,basi hakutakiwa aonekane pale nyumbani maana angejuta!.


Hayo ndiyo yalikuwa masharti tuliyopewa siku hiyo.


Itaendelea.......................
[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Mkuu@LwandaMagere hili jina lina kisa chake ujue, nakumbuka kipindi nasoma kenya primary tulipewa hadithi za lwandamagere jinsi alivyokuwa mbabe na mpiganaji hatari wa kabila lake la wajaluo. Kilichomuondoa ni mwanamke aliyemuoa ambaye alitaka kujua siri ya nguvu zake ndipo lwanda akamwambia ukichoma kivuli changu nami ntapoteza nguvu zangu.
 
MKASA WA PILI -Sehemu ya 45.


Inaendelea.............



Sasa kuna wikiendi moja nikiwa nimepumzika nyumbani,yule jamaa aliyenipeleka Kasulu alinipigia simu akaniambia yupo njiani anakuja Mwanza,akasema atakapofika inabidi tuonane!,nilimwambia mimi nitakuwepo tu nyumbani kwangu akifika aniambie nikamchukue!.Basi baada ya masaa kadhaa jamaa alifika,nilimtuma dereva wangu aende akamchukue kule stendi.Jamaa alipofika hapo nyumbani alianza kushangaa sana namna nilivyokuwa nimepiga hatua ya kimaisha tofauti na mwanzo tulivyoachana!.

Jamaa aliniambia "Aisee kaka unatisha mzee,kaka hii yote ni mali yako?".

Jamaa aliendelea kuuliza huku akishangaa maisha yale ya kifahari niliyokuwa nikiishi.Sasa kwakuwa sikutaka kabisa mke wangu aelewe mambo yaliyokuwa yakiendelea nilimwmbia jamaa "Usijali kaka ngoja tule halafu tutoke kidogo tukapunge upepo mahali fulani".

Basi baada ya kuwa tumemaliza kula nilimchukua jamaa mpaka maeneo fulani ya Kirumba ambayo mara zote nilipendelea kwenda kupumzika.

Jamaa akaanza kuniambia "Eeh kaka nipe stori ndugu yangu mambo yaliendaje,maana baada ya kukuacha kule mimi nilirudi zangu sikufahamu kilichoendelea".

Nilimwambia "Wewe acha tu kaka mambo si mepesi kama nilivyokuwa nikidhani maana nilipitia mambo mengi sana ila namshukuru Mungu kanisimamia mpaka hatua hii".

Jamaa akaniuliza "Kwani kaka ulifanyaje mpaka kufikia hapa,tafadhali nieleze ili na mimi niangalie cha kufanya kaka".

Nilimwambia "Kaka uliponiacha Mnyegera yule mama aliniagiza kwenda Kongo na huko ndiko nilipopata dawa ya biashara na hatimaye namshukuru Mungu imenipa matokeo".

Nilimwambia huku nikifahamu kabisa ninamdanganya ila sikuwa na namna,sikutaka kabisa aelewe kilichokuwa kinanipatia pesa wakati huo.

Jamaa aliendelea kuniuliza "Kwahiyo kaka ulianzisha biashara?".

Nilimjibu "Ndiyo kaka nilianzisha biashara".

Jamaa aliniuliza "Lakini mbona imeenda fasta sana"?.

Jamaa alikuwa akiuliza maswali kana kwamba ana mashaka na wasiwasi kuhusu utajiri wangu,nilijua lazima awe na mashaka maana ule utajiri uliinuka ghafla sana.

Nilimwambia "Ndiyo ile dawa kaka imefanya haya maajabu".

Jamaa aliendelea kusema "yaani kaka ningejua na mimi tungeenda wote,mimi nilienda tu kuchukua dawa ya kinga hatimaye hata kazi yenyewe sikuendelea nayo".

Baada ya maongezi ya muda mrefu nilimwambia nitampatia pesa afanye mtaji ili aisaidie familia yake,wakati huo zile nilikuwa nikizitumia pia hata kwenye biashara,hii ni baada ya Malikia kuniambia nizifanyie maendeleo sikuwa na mashaka tena maana nilijua hata kama ingeharibika huko mbeleni mimi nisingehusika kwa wakati huo!.

Ilibidi nimuulize "kwahiyo unadhani nikikupa kiasi gani kitatosha wewe kuanzisha biashara?.

Jamaa aliniambia "Kaka kuna biashara za vipodozi nizifanye,nataka nifungue duka pale kakola maana kuna uhitaji mkubwa sana".

Nilimuuliza "Kwahiyo unadhani kiasi gani kitatosha?".

Aliendelea kuniambia "Yaani kaka mimi nikipata milioni 10 tu itanitosha,hata kama ni mahakamani tukahandikishane nitakurudishia,maana hesabu nilizo piga mpaka kufungua duka niwe nafata mzigo Uganda itanigharimu kama milioni 8,hivyo ndiyo maana nasema ningepata milioni 10 ingenisaidia sana".

Kwakuwa jamaa alinisaidia sana kunitoa Mwanza mpaka Kasulu niliona jamaa alinisaidia sana mpaka mimi kuheshimika kwa wakati huo hivyo nilimwambia kwamba nitampatia hizo pesa na sitaki anirudishie,nilitaka yeye aende akapambane na maisha ili atimize ndoto zake.Wakati huo suala la pesa lilikuwa haliniumizi akili kabisa maana kila mwezi ulikuwa unaingia mzigo wa kutosha.Basi baada ya kumpatia ile hela aliyohitaji,jamaa hakutaka kupoteza muda,alinambia inapaswa akapambane na angenijulisha kila lililoendelea kwa wakati huo,nilimwambia kama angehitaji msaada wa kifedha basi asisite kuniambia ningemsaidia!.

Sasa nakumbuka siku moja nikiwa nimelala chumbani kwangu,mke wangu alikuwa ameenda kazini,kama kawaida nilipata ndoto ambayo ilikuwa ni ileile niliyoiota siku kadhaa zilizokuwa zimepita,ile ndoto ilinitaka nielekee eneo moja ambalo nilikuwa silifahamu ili nikatoe kafara,nililiona lilelile lori la mafuta na ile costa,sasa kwakuwa ilikuwa mwisho wa mwezi sikutaka kabisa kuipuuza ile ndoto maana nisingejiongeza ilikuwa inakula kwangu.Niliamka kitandani ikabidi nielekee kule kwenye kile chumba cha siri kujiandaa kuelekea hilo eneo nililokuwa nimeonyeshwa ndotoni,niliingia ndani ya kile chumba cha siri nikachukua zana zangu za kazi,nilihakikisha pia ile pembe siku hiyo siiachi kwasababu sehemu niliyokuwa naelekea nilikuwa siifahamu vizuri,hivyo niliona ingenisaidia katika mapambano hata kama ningekuta kuna vizuizi vya kishirikina.Kabla ya kuondoka nilijaribu kuyatazama yale magari yote mawili kishirikina,yaani ile Costa pamoja na lile lori lililokuwa limebeba mafuta,lengo langu ilikuwa ni kuangalia uwezo waliyokuwa nao abiria wa magari yote mawili,nilipotazama kwa makini nikaona wote waliyokuwa kwenye hayo magari mawili walikuwa weupe na wepesi kama karatasi,hakukuwa na mtu mwenye uwezo ndani ya hayo magari ambaye angenizuia nisitoe kafara,ndipo niliushika mkono wangu wa kushoto uliyokuwa na irizi na kutamka kama kawaida ya kwamba inapaswa muda huo niwe katika hilo eneo lililokusudiwa.

Kufumba na kufumbua nilijikuta nipo kando kando ya barabara katika hilo eneo,sasa kumbe hilo eneo ilikuwa ni kijiji kimoja kinaitwa Mulowo,na barabara niliyosimama kando ilikuwa ni barabara kuu ya kutoka Mbeya kueleka Tunduma,sasa ilibidi niyatazame yale magari kishirikina ili kuona yalikuwa umbali gani,baada ya kuyatazama na kuona kwamba hayakuwa mbali sana ilibidi nisogee pembeni kuyasubiri, baada ya muda wa nusu saa kwa mbali nililiona lile lori nililoliona ndotoni likiwa linakuja kutoka Mbeya kuelekea Tunduma na ile Costa pia ilikuwa inakuja kutoka Tunduma kuelekea Mbeya,basi nilisogea kuelekea katikati ya barabara kuanza kuweka dawa za tego,safari hii nilitaka asibaki mtu hata mmoja kwenye ile kafara hata kama kungekuwa na mende au nzi kwenye hayo magari nilitaka wateketee kabisa!.

Sasa wakati nimemaliza kuweka ile dawa ya tego pale katikati ya barabara,mara ghafla niliona upepo mkali sana kama kimbunga,ule upepo ulinisomba mpaka kwenye shamba moja ambalo halikuwa mbali sana na ilipokuwa barabara,ile kutazama vizuri nikawaona wanawake wawili wakiwa uchi kama walivyozaliwa,mmoja alikuwa akining'inia angani na mwingine alikuwa amesimama kando ya barabara huku akiniangalia kwa hasira!.

Yule aliyekuwa akining'inia angani akaniuliza "Wewe umekuja kufanya nini hapa,uelewi kwamba hii si himaya yako?".

Nilinyanyuka pale chini kujaribu kuwasogelea ili nilianzishe vurumai lakini sikuweza kupiga hatua hata moja.

Yule mwenzie akaniambia "Aliyekutuma leo kakudanganya,leo tunaanza na wewe ili tukakukaange tukule nyama".

Kiukweli nilisposikia ile kauli ya kuliwa nyama,jasho likaanza kunitoka japo hakukuwa na jua!.Sasa kwa wakati huo yale magari niliyokusudia kuyatoa kafara yalikuwa yameshapita eneo la tukio nilipokuwa nimeweka lile tego,nilitambua wale wachawi walikuwa wametegua lile tego ili nisipate kitu,kiukweli wale wachawi walinizidishia hasira kiasi kwamba macho yalibadilika,nilikasirika mpaka macho yakawa mekundu kama damu,kitu kilichofanya nikasirike ni kile kitendo cha kuondoa lile tego ambalo tayari lilinikosesha damu ya kafara kwenye zile gari ukizingatia ilikuwa tarehe ya mwisho ya kutoa kafara,pia niliwaza kama ningekosa ile kafara ni nini kingenikuta maana Malikia asingenielewa kwasababu uwezo wote alikuwa amenipatia,pia alishanionya kwamba nisije rudia tena kosa nililokuwa nimelifanya kule bungu,mkoani Pwani.Nilitambua kabisa lazima ningepata adhabu maana yale magari tayari yalikuwa yameshapita lile eneo la tukio bila kupata madhara yoyote,na chanzo cha hayo yote walikuwa hao wachawi wawili.

Basi niliukamata mkono wangu uliyokuwa na irizi nikauamrisha ya kwamba nataka nipige hatua kutoka nilipokuwa nimetupwa na kile kimbunga ili niweze kusogea barabarani.Pale pale nilianza kusonga barabarani,wale wachawi baada ya kuona naelekea barabarani walianza vituko tena,walianza kutimua vumbi lile eneo kiasi kwamba kukawa kama uwanja wa vita,Kiukweli nilikuwa nimejaa sana hasira,sasa kwakuwa waliweza kutegua lile tego wakanidharau wakaona sikuwa na uwezo wa kuwafanya chochote!.Nilipoona vumbi limezidi nilichukua ile pembe nikainyoosha kwenye lile vumbi hatimaye likakoma.


Itaendelea..................
 
MKASA WA PILI -Sehemu ya 45.


Inaendelea.............



Sasa kuna wikiendi moja nikiwa nimepumzika nyumbani,yule jamaa aliyenipeleka Kasulu alinipigia simu akaniambia yupo njiani anakuja Mwanza,akasema atakapofika inabidi tuonane!,nilimwambia mimi nitakuwepo tu nyumbani kwangu akifika aniambie nikamchukue!.Basi baada ya masaa kadhaa jamaa alifika,nilimtuma dereva wangu aende akamchukue kule stendi.Jamaa alipofika hapo nyumbani alianza kushangaa sana namna nilivyokuwa nimepiga hatua ya kimaisha tofauti na mwanzo tulivyoachana!.

Jamaa aliniambia "Aisee kaka unatisha mzee,kaka hii yote ni mali yako?".

Jamaa aliendelea kuuliza huku akishangaa maisha yale ya kifahari niliyokuwa nikiishi.Sasa kwakuwa sikutaka kabisa mke wangu aelewe mambo yaliyokuwa yakiendelea nilimwmbia jamaa "Usijali kaka ngoja tule halafu tutoke kidogo tukapunge upepo mahali fulani".

Basi baada ya kuwa tumemaliza kula nilimchukua jamaa mpaka maeneo fulani ya Kirumba ambayo mara zote nilipendelea kwenda kupumzika.

Jamaa akaanza kuniambia "Eeh kaka nipe stori ndugu yangu mambo yaliendaje,maana baada ya kukuacha kule mimi nilirudi zangu sikufahamu kilichoendelea".

Nilimwambia "Wewe acha tu kaka mambo si mepesi kama nilivyokuwa nikidhani maana nilipitia mambo mengi sana ila namshukuru Mungu kanisimamia mpaka hatua hii".

Jamaa akaniuliza "Kwani kaka ulifanyaje mpaka kufikia hapa,tafadhali nieleze ili na mimi niangalie cha kufanya kaka".

Nilimwambia "Kaka uliponiacha Mnyegera yule mama aliniagiza kwenda Kongo na huko ndiko nilipopata dawa ya biashara na hatimaye namshukuru Mungu imenipa matokeo".

Nilimwambia huku nikifahamu kabisa ninamdanganya ila sikuwa na namna,sikutaka kabisa aelewe kilichokuwa kinanipatia pesa wakati huo.

Jamaa aliendelea kuniuliza "Kwahiyo kaka ulianzisha biashara?".

Nilimjibu "Ndiyo kaka nilianzisha biashara".

Jamaa aliniuliza "Lakini mbona imeenda fasta sana"?.

Jamaa alikuwa akiuliza maswali kana kwamba ana mashaka na wasiwasi kuhusu utajiri wangu,nilijua lazima awe na mashaka maana ule utajiri uliinuka ghafla sana.

Nilimwambia "Ndiyo ile dawa kaka imefanya haya maajabu".

Jamaa aliendelea kusema "yaani kaka ningejua na mimi tungeenda wote,mimi nilienda tu kuchukua dawa ya kinga hatimaye hata kazi yenyewe sikuendelea nayo".

Baada ya maongezi ya muda mrefu nilimwambia nitampatia pesa afanye mtaji ili aisaidie familia yake,wakati huo zile nilikuwa nikizitumia pia hata kwenye biashara,hii ni baada ya Malikia kuniambia nizifanyie maendeleo sikuwa na mashaka tena maana nilijua hata kama ingeharibika huko mbeleni mimi nisingehusika kwa wakati huo!.

Ilibidi nimuulize "kwahiyo unadhani nikikupa kiasi gani kitatosha wewe kuanzisha biashara?.

Jamaa aliniambia "Kaka kuna biashara za vipodozi nizifanye,nataka nifungue duka pale kakola maana kuna uhitaji mkubwa sana".

Nilimuuliza "Kwahiyo unadhani kiasi gani kitatosha?".

Aliendelea kuniambia "Yaani kaka mimi nikipata milioni 10 tu itanitosha,hata kama ni mahakamani tukahandikishane nitakurudishia,maana hesabu nilizo piga mpaka kufungua duka niwe nafata mzigo Uganda itanigharimu kama milioni 8,hivyo ndiyo maana nasema ningepata milioni 10 ingenisaidia sana".

Kwakuwa jamaa alinisaidia sana kunitoa Mwanza mpaka Kasulu niliona jamaa alinisaidia sana mpaka mimi kuheshimika kwa wakati huo hivyo nilimwambia kwamba nitampatia hizo pesa na sitaki anirudishie,nilitaka yeye aende akapambane na maisha ili atimize ndoto zake.Wakati huo suala la pesa lilikuwa haliniumizi akili kabisa maana kila mwezi ulikuwa unaingia mzigo wa kutosha.Basi baada ya kumpatia ile hela aliyohitaji,jamaa hakutaka kupoteza muda,alinambia inapaswa akapambane na angenijulisha kila lililoendelea kwa wakati huo,nilimwambia kama angehitaji msaada wa kifedha basi asisite kuniambia ningemsaidia!.

Sasa nakumbuka siku moja nikiwa nimelala chumbani kwangu,mke wangu alikuwa ameenda kazini,kama kawaida nilipata ndoto ambayo ilikuwa ni ileile niliyoiota siku kadhaa zilizokuwa zimepita,ile ndoto ilinitaka nielekee eneo moja ambalo nilikuwa silifahamu ili nikatoe kafara,nililiona lilelile lori la mafuta na ile costa,sasa kwakuwa ilikuwa mwisho wa mwezi sikutaka kabisa kuipuuza ile ndoto maana nisingejiongeza ilikuwa inakula kwangu.Niliamka kitandani ikabidi nielekee kule kwenye kile chumba cha siri kujiandaa kuelekea hilo eneo nililokuwa nimeonyeshwa ndotoni,niliingia ndani ya kile chumba cha siri nikachukua zana zangu za kazi,nilihakikisha pia ile pembe siku hiyo siiachi kwasababu sehemu niliyokuwa naelekea nilikuwa siifahamu vizuri,hivyo niliona ingenisaidia katika mapambano hata kama ningekuta kuna vizuizi vya kishirikina.Kabla ya kuondoka nilijaribu kuyatazama yale magari yote mawili kishirikina,yaani ile Costa pamoja na lile lori lililokuwa limebeba mafuta,lengo langu ilikuwa ni kuangalia uwezo waliyokuwa nao abiria wa magari yote mawili,nilipotazama kwa makini nikaona wote waliyokuwa kwenye hayo magari mawili walikuwa weupe na wepesi kama karatasi,hakukuwa na mtu mwenye uwezo ndani ya hayo magari ambaye angenizuia nisitoe kafara,ndipo niliushika mkono wangu wa kushoto uliyokuwa na irizi na kutamka kama kawaida ya kwamba inapaswa muda huo niwe katika hilo eneo lililokusudiwa.

Kufumba na kufumbua nilijikuta nipo kando kando ya barabara katika hilo eneo,sasa kumbe hilo eneo ilikuwa ni kijiji kimoja kinaitwa Mulowo,na barabara niliyosimama kando ilikuwa ni barabara kuu ya kutoka Mbeya kueleka Tunduma,sasa ilibidi niyatazame yale magari kishirikina ili kuona yalikuwa umbali gani,baada ya kuyatazama na kuona kwamba hayakuwa mbali sana ilibidi nisogee pembeni kuyasubiri, baada ya muda wa nusu saa kwa mbali nililiona lile lori nililoliona ndotoni likiwa linakuja kutoka Mbeya kuelekea Tunduma na ile Costa pia ilikuwa inakuja kutoka Tunduma kuelekea Mbeya,basi nilisogea kuelekea katikati ya barabara kuanza kuweka dawa za tego,safari hii nilitaka asibaki mtu hata mmoja kwenye ile kafara hata kama kungekuwa na mende au nzi kwenye hayo magari nilitaka wateketee kabisa!.

Sasa wakati nimemaliza kuweka ile dawa ya tego pale katikati ya barabara,mara ghafla niliona upepo mkali sana kama kimbunga,ule upepo ulinisomba mpaka kwenye shamba moja ambalo halikuwa mbali sana na ilipokuwa barabara,ile kutazama vizuri nikawaona wanawake wawili wakiwa uchi kama walivyozaliwa,mmoja alikuwa akining'inia angani na mwingine alikuwa amesimama kando ya barabara huku akiniangalia kwa hasira!.

Yule aliyekuwa akining'inia angani akaniuliza "Wewe umekuja kufanya nini hapa,uelewi kwamba hii si himaya yako?".

Nilinyanyuka pale chini kujaribu kuwasogelea ili nilianzishe vurumai lakini sikuweza kupiga hatua hata moja.

Yule mwenzie akaniambia "Aliyekutuma leo kakudanganya,leo tunaanza na wewe ili tukakukaange tukule nyama".

Kiukweli nilisposikia ile kauli ya kuliwa nyama,jasho likaanza kunitoka japo hakukuwa na jua!.Sasa kwa wakati huo yale magari niliyokusudia kuyatoa kafara yalikuwa yameshapita eneo la tukio nilipokuwa nimeweka lile tego,nilitambua wale wachawi walikuwa wametegua lile tego ili nisipate kitu,kiukweli wale wachawi walinizidishia hasira kiasi kwamba macho yalibadilika,nilikasirika mpaka macho yakawa mekundu kama damu,kitu kilichofanya nikasirike ni kile kitendo cha kuondoa lile tego ambalo tayari lilinikosesha damu ya kafara kwenye zile gari ukizingatia ilikuwa tarehe ya mwisho ya kutoa kafara,pia niliwaza kama ningekosa ile kafara ni nini kingenikuta maana Malikia asingenielewa kwasababu uwezo wote alikuwa amenipatia,pia alishanionya kwamba nisije rudia tena kosa nililokuwa nimelifanya kule bungu,mkoani Pwani.Nilitambua kabisa lazima ningepata adhabu maana yale magari tayari yalikuwa yameshapita lile eneo la tukio bila kupata madhara yoyote,na chanzo cha hayo yote walikuwa hao wachawi wawili.

Basi niliukamata mkono wangu uliyokuwa na irizi nikauamrisha ya kwamba nataka nipige hatua kutoka nilipokuwa nimetupwa na kile kimbunga ili niweze kusogea barabarani.Pale pale nilianza kusonga barabarani,wale wachawi baada ya kuona naelekea barabarani walianza vituko tena,walianza kutimua vumbi lile eneo kiasi kwamba kukawa kama uwanja wa vita,Kiukweli nilikuwa nimejaa sana hasira,sasa kwakuwa waliweza kutegua lile tego wakanidharau wakaona sikuwa na uwezo wa kuwafanya chochote!.Nilipoona vumbi limezidi nilichukua ile pembe nikainyoosha kwenye lile vumbi hatimaye likakoma.


Itaendelea..................
Aiseee[emoji134][emoji134]
Kweli ulizunguka sehemu nyingi..hadi Mlowo toka Mwanza[emoji119][emoji119][emoji119]


Hiyo pembe haikuweza kukuonyesha hali ya anga unayoenda ikoje?
 
Mkuuuu Mimi nataka kujua KWA mwezi ukiingia kwenye begi unakuta kama kiasi gani cha pesaaaa
 
hii ni stori ya kutunga tu maana kuna vitu vingi unnecesary ila unaviandika ili tu kukuza ,kulikuwa hata hakuna faida kujua kwamba mtundi ni tall.
halafu unatuambia mganga alicheka sana kwamba kazi ni rahisi wala hakuwa na ahaja ya yeye kuja wakati huohuo unasema ilikua hawezi kukutibu hadi hivyo vitu vitolewe sasa vingetolewa na nani bila yeye kuja
Mkuu umesahau waganga walivyo na mbwembwe?
 
MKASA WA PILI -Sehemu ya 45.


Inaendelea.............



Sasa kuna wikiendi moja nikiwa nimepumzika nyumbani,yule jamaa aliyenipeleka Kasulu alinipigia simu akaniambia yupo njiani anakuja Mwanza,akasema atakapofika inabidi tuonane!,nilimwambia mimi nitakuwepo tu nyumbani kwangu akifika aniambie nikamchukue!.Basi baada ya masaa kadhaa jamaa alifika,nilimtuma dereva wangu aende akamchukue kule stendi.Jamaa alipofika hapo nyumbani alianza kushangaa sana namna nilivyokuwa nimepiga hatua ya kimaisha tofauti na mwanzo tulivyoachana!.

Jamaa aliniambia "Aisee kaka unatisha mzee,kaka hii yote ni mali yako?".

Jamaa aliendelea kuuliza huku akishangaa maisha yale ya kifahari niliyokuwa nikiishi.Sasa kwakuwa sikutaka kabisa mke wangu aelewe mambo yaliyokuwa yakiendelea nilimwmbia jamaa "Usijali kaka ngoja tule halafu tutoke kidogo tukapunge upepo mahali fulani".

Basi baada ya kuwa tumemaliza kula nilimchukua jamaa mpaka maeneo fulani ya Kirumba ambayo mara zote nilipendelea kwenda kupumzika.

Jamaa akaanza kuniambia "Eeh kaka nipe stori ndugu yangu mambo yaliendaje,maana baada ya kukuacha kule mimi nilirudi zangu sikufahamu kilichoendelea".

Nilimwambia "Wewe acha tu kaka mambo si mepesi kama nilivyokuwa nikidhani maana nilipitia mambo mengi sana ila namshukuru Mungu kanisimamia mpaka hatua hii".

Jamaa akaniuliza "Kwani kaka ulifanyaje mpaka kufikia hapa,tafadhali nieleze ili na mimi niangalie cha kufanya kaka".

Nilimwambia "Kaka uliponiacha Mnyegera yule mama aliniagiza kwenda Kongo na huko ndiko nilipopata dawa ya biashara na hatimaye namshukuru Mungu imenipa matokeo".

Nilimwambia huku nikifahamu kabisa ninamdanganya ila sikuwa na namna,sikutaka kabisa aelewe kilichokuwa kinanipatia pesa wakati huo.

Jamaa aliendelea kuniuliza "Kwahiyo kaka ulianzisha biashara?".

Nilimjibu "Ndiyo kaka nilianzisha biashara".

Jamaa aliniuliza "Lakini mbona imeenda fasta sana"?.

Jamaa alikuwa akiuliza maswali kana kwamba ana mashaka na wasiwasi kuhusu utajiri wangu,nilijua lazima awe na mashaka maana ule utajiri uliinuka ghafla sana.

Nilimwambia "Ndiyo ile dawa kaka imefanya haya maajabu".

Jamaa aliendelea kusema "yaani kaka ningejua na mimi tungeenda wote,mimi nilienda tu kuchukua dawa ya kinga hatimaye hata kazi yenyewe sikuendelea nayo".

Baada ya maongezi ya muda mrefu nilimwambia nitampatia pesa afanye mtaji ili aisaidie familia yake,wakati huo zile nilikuwa nikizitumia pia hata kwenye biashara,hii ni baada ya Malikia kuniambia nizifanyie maendeleo sikuwa na mashaka tena maana nilijua hata kama ingeharibika huko mbeleni mimi nisingehusika kwa wakati huo!.

Ilibidi nimuulize "kwahiyo unadhani nikikupa kiasi gani kitatosha wewe kuanzisha biashara?.

Jamaa aliniambia "Kaka kuna biashara za vipodozi nizifanye,nataka nifungue duka pale kakola maana kuna uhitaji mkubwa sana".

Nilimuuliza "Kwahiyo unadhani kiasi gani kitatosha?".

Aliendelea kuniambia "Yaani kaka mimi nikipata milioni 10 tu itanitosha,hata kama ni mahakamani tukahandikishane nitakurudishia,maana hesabu nilizo piga mpaka kufungua duka niwe nafata mzigo Uganda itanigharimu kama milioni 8,hivyo ndiyo maana nasema ningepata milioni 10 ingenisaidia sana".

Kwakuwa jamaa alinisaidia sana kunitoa Mwanza mpaka Kasulu niliona jamaa alinisaidia sana mpaka mimi kuheshimika kwa wakati huo hivyo nilimwambia kwamba nitampatia hizo pesa na sitaki anirudishie,nilitaka yeye aende akapambane na maisha ili atimize ndoto zake.Wakati huo suala la pesa lilikuwa haliniumizi akili kabisa maana kila mwezi ulikuwa unaingia mzigo wa kutosha.Basi baada ya kumpatia ile hela aliyohitaji,jamaa hakutaka kupoteza muda,alinambia inapaswa akapambane na angenijulisha kila lililoendelea kwa wakati huo,nilimwambia kama angehitaji msaada wa kifedha basi asisite kuniambia ningemsaidia!.

Sasa nakumbuka siku moja nikiwa nimelala chumbani kwangu,mke wangu alikuwa ameenda kazini,kama kawaida nilipata ndoto ambayo ilikuwa ni ileile niliyoiota siku kadhaa zilizokuwa zimepita,ile ndoto ilinitaka nielekee eneo moja ambalo nilikuwa silifahamu ili nikatoe kafara,nililiona lilelile lori la mafuta na ile costa,sasa kwakuwa ilikuwa mwisho wa mwezi sikutaka kabisa kuipuuza ile ndoto maana nisingejiongeza ilikuwa inakula kwangu.Niliamka kitandani ikabidi nielekee kule kwenye kile chumba cha siri kujiandaa kuelekea hilo eneo nililokuwa nimeonyeshwa ndotoni,niliingia ndani ya kile chumba cha siri nikachukua zana zangu za kazi,nilihakikisha pia ile pembe siku hiyo siiachi kwasababu sehemu niliyokuwa naelekea nilikuwa siifahamu vizuri,hivyo niliona ingenisaidia katika mapambano hata kama ningekuta kuna vizuizi vya kishirikina.Kabla ya kuondoka nilijaribu kuyatazama yale magari yote mawili kishirikina,yaani ile Costa pamoja na lile lori lililokuwa limebeba mafuta,lengo langu ilikuwa ni kuangalia uwezo waliyokuwa nao abiria wa magari yote mawili,nilipotazama kwa makini nikaona wote waliyokuwa kwenye hayo magari mawili walikuwa weupe na wepesi kama karatasi,hakukuwa na mtu mwenye uwezo ndani ya hayo magari ambaye angenizuia nisitoe kafara,ndipo niliushika mkono wangu wa kushoto uliyokuwa na irizi na kutamka kama kawaida ya kwamba inapaswa muda huo niwe katika hilo eneo lililokusudiwa.

Kufumba na kufumbua nilijikuta nipo kando kando ya barabara katika hilo eneo,sasa kumbe hilo eneo ilikuwa ni kijiji kimoja kinaitwa Mulowo,na barabara niliyosimama kando ilikuwa ni barabara kuu ya kutoka Mbeya kueleka Tunduma,sasa ilibidi niyatazame yale magari kishirikina ili kuona yalikuwa umbali gani,baada ya kuyatazama na kuona kwamba hayakuwa mbali sana ilibidi nisogee pembeni kuyasubiri, baada ya muda wa nusu saa kwa mbali nililiona lile lori nililoliona ndotoni likiwa linakuja kutoka Mbeya kuelekea Tunduma na ile Costa pia ilikuwa inakuja kutoka Tunduma kuelekea Mbeya,basi nilisogea kuelekea katikati ya barabara kuanza kuweka dawa za tego,safari hii nilitaka asibaki mtu hata mmoja kwenye ile kafara hata kama kungekuwa na mende au nzi kwenye hayo magari nilitaka wateketee kabisa!.

Sasa wakati nimemaliza kuweka ile dawa ya tego pale katikati ya barabara,mara ghafla niliona upepo mkali sana kama kimbunga,ule upepo ulinisomba mpaka kwenye shamba moja ambalo halikuwa mbali sana na ilipokuwa barabara,ile kutazama vizuri nikawaona wanawake wawili wakiwa uchi kama walivyozaliwa,mmoja alikuwa akining'inia angani na mwingine alikuwa amesimama kando ya barabara huku akiniangalia kwa hasira!.

Yule aliyekuwa akining'inia angani akaniuliza "Wewe umekuja kufanya nini hapa,uelewi kwamba hii si himaya yako?".

Nilinyanyuka pale chini kujaribu kuwasogelea ili nilianzishe vurumai lakini sikuweza kupiga hatua hata moja.

Yule mwenzie akaniambia "Aliyekutuma leo kakudanganya,leo tunaanza na wewe ili tukakukaange tukule nyama".

Kiukweli nilisposikia ile kauli ya kuliwa nyama,jasho likaanza kunitoka japo hakukuwa na jua!.Sasa kwa wakati huo yale magari niliyokusudia kuyatoa kafara yalikuwa yameshapita eneo la tukio nilipokuwa nimeweka lile tego,nilitambua wale wachawi walikuwa wametegua lile tego ili nisipate kitu,kiukweli wale wachawi walinizidishia hasira kiasi kwamba macho yalibadilika,nilikasirika mpaka macho yakawa mekundu kama damu,kitu kilichofanya nikasirike ni kile kitendo cha kuondoa lile tego ambalo tayari lilinikosesha damu ya kafara kwenye zile gari ukizingatia ilikuwa tarehe ya mwisho ya kutoa kafara,pia niliwaza kama ningekosa ile kafara ni nini kingenikuta maana Malikia asingenielewa kwasababu uwezo wote alikuwa amenipatia,pia alishanionya kwamba nisije rudia tena kosa nililokuwa nimelifanya kule bungu,mkoani Pwani.Nilitambua kabisa lazima ningepata adhabu maana yale magari tayari yalikuwa yameshapita lile eneo la tukio bila kupata madhara yoyote,na chanzo cha hayo yote walikuwa hao wachawi wawili.

Basi niliukamata mkono wangu uliyokuwa na irizi nikauamrisha ya kwamba nataka nipige hatua kutoka nilipokuwa nimetupwa na kile kimbunga ili niweze kusogea barabarani.Pale pale nilianza kusonga barabarani,wale wachawi baada ya kuona naelekea barabarani walianza vituko tena,walianza kutimua vumbi lile eneo kiasi kwamba kukawa kama uwanja wa vita,Kiukweli nilikuwa nimejaa sana hasira,sasa kwakuwa waliweza kutegua lile tego wakanidharau wakaona sikuwa na uwezo wa kuwafanya chochote!.Nilipoona vumbi limezidi nilichukua ile pembe nikainyoosha kwenye lile vumbi hatimaye likakoma.


Itaendelea..................
Vyuma vimeuma .!
 
MKASA WA PILI -Sehemu ya 45.


Inaendelea.............



Sasa kuna wikiendi moja nikiwa nimepumzika nyumbani,yule jamaa aliyenipeleka Kasulu alinipigia simu akaniambia yupo njiani anakuja Mwanza,akasema atakapofika inabidi tuonane!,nilimwambia mimi nitakuwepo tu nyumbani kwangu akifika aniambie nikamchukue!.Basi baada ya masaa kadhaa jamaa alifika,nilimtuma dereva wangu aende akamchukue kule stendi.Jamaa alipofika hapo nyumbani alianza kushangaa sana namna nilivyokuwa nimepiga hatua ya kimaisha tofauti na mwanzo tulivyoachana!.

Jamaa aliniambia "Aisee kaka unatisha mzee,kaka hii yote ni mali yako?".

Jamaa aliendelea kuuliza huku akishangaa maisha yale ya kifahari niliyokuwa nikiishi.Sasa kwakuwa sikutaka kabisa mke wangu aelewe mambo yaliyokuwa yakiendelea nilimwmbia jamaa "Usijali kaka ngoja tule halafu tutoke kidogo tukapunge upepo mahali fulani".

Basi baada ya kuwa tumemaliza kula nilimchukua jamaa mpaka maeneo fulani ya Kirumba ambayo mara zote nilipendelea kwenda kupumzika.

Jamaa akaanza kuniambia "Eeh kaka nipe stori ndugu yangu mambo yaliendaje,maana baada ya kukuacha kule mimi nilirudi zangu sikufahamu kilichoendelea".

Nilimwambia "Wewe acha tu kaka mambo si mepesi kama nilivyokuwa nikidhani maana nilipitia mambo mengi sana ila namshukuru Mungu kanisimamia mpaka hatua hii".

Jamaa akaniuliza "Kwani kaka ulifanyaje mpaka kufikia hapa,tafadhali nieleze ili na mimi niangalie cha kufanya kaka".

Nilimwambia "Kaka uliponiacha Mnyegera yule mama aliniagiza kwenda Kongo na huko ndiko nilipopata dawa ya biashara na hatimaye namshukuru Mungu imenipa matokeo".

Nilimwambia huku nikifahamu kabisa ninamdanganya ila sikuwa na namna,sikutaka kabisa aelewe kilichokuwa kinanipatia pesa wakati huo.

Jamaa aliendelea kuniuliza "Kwahiyo kaka ulianzisha biashara?".

Nilimjibu "Ndiyo kaka nilianzisha biashara".

Jamaa aliniuliza "Lakini mbona imeenda fasta sana"?.

Jamaa alikuwa akiuliza maswali kana kwamba ana mashaka na wasiwasi kuhusu utajiri wangu,nilijua lazima awe na mashaka maana ule utajiri uliinuka ghafla sana.

Nilimwambia "Ndiyo ile dawa kaka imefanya haya maajabu".

Jamaa aliendelea kusema "yaani kaka ningejua na mimi tungeenda wote,mimi nilienda tu kuchukua dawa ya kinga hatimaye hata kazi yenyewe sikuendelea nayo".

Baada ya maongezi ya muda mrefu nilimwambia nitampatia pesa afanye mtaji ili aisaidie familia yake,wakati huo zile nilikuwa nikizitumia pia hata kwenye biashara,hii ni baada ya Malikia kuniambia nizifanyie maendeleo sikuwa na mashaka tena maana nilijua hata kama ingeharibika huko mbeleni mimi nisingehusika kwa wakati huo!.

Ilibidi nimuulize "kwahiyo unadhani nikikupa kiasi gani kitatosha wewe kuanzisha biashara?.

Jamaa aliniambia "Kaka kuna biashara za vipodozi nizifanye,nataka nifungue duka pale kakola maana kuna uhitaji mkubwa sana".

Nilimuuliza "Kwahiyo unadhani kiasi gani kitatosha?".

Aliendelea kuniambia "Yaani kaka mimi nikipata milioni 10 tu itanitosha,hata kama ni mahakamani tukahandikishane nitakurudishia,maana hesabu nilizo piga mpaka kufungua duka niwe nafata mzigo Uganda itanigharimu kama milioni 8,hivyo ndiyo maana nasema ningepata milioni 10 ingenisaidia sana".

Kwakuwa jamaa alinisaidia sana kunitoa Mwanza mpaka Kasulu niliona jamaa alinisaidia sana mpaka mimi kuheshimika kwa wakati huo hivyo nilimwambia kwamba nitampatia hizo pesa na sitaki anirudishie,nilitaka yeye aende akapambane na maisha ili atimize ndoto zake.Wakati huo suala la pesa lilikuwa haliniumizi akili kabisa maana kila mwezi ulikuwa unaingia mzigo wa kutosha.Basi baada ya kumpatia ile hela aliyohitaji,jamaa hakutaka kupoteza muda,alinambia inapaswa akapambane na angenijulisha kila lililoendelea kwa wakati huo,nilimwambia kama angehitaji msaada wa kifedha basi asisite kuniambia ningemsaidia!.

Sasa nakumbuka siku moja nikiwa nimelala chumbani kwangu,mke wangu alikuwa ameenda kazini,kama kawaida nilipata ndoto ambayo ilikuwa ni ileile niliyoiota siku kadhaa zilizokuwa zimepita,ile ndoto ilinitaka nielekee eneo moja ambalo nilikuwa silifahamu ili nikatoe kafara,nililiona lilelile lori la mafuta na ile costa,sasa kwakuwa ilikuwa mwisho wa mwezi sikutaka kabisa kuipuuza ile ndoto maana nisingejiongeza ilikuwa inakula kwangu.Niliamka kitandani ikabidi nielekee kule kwenye kile chumba cha siri kujiandaa kuelekea hilo eneo nililokuwa nimeonyeshwa ndotoni,niliingia ndani ya kile chumba cha siri nikachukua zana zangu za kazi,nilihakikisha pia ile pembe siku hiyo siiachi kwasababu sehemu niliyokuwa naelekea nilikuwa siifahamu vizuri,hivyo niliona ingenisaidia katika mapambano hata kama ningekuta kuna vizuizi vya kishirikina.Kabla ya kuondoka nilijaribu kuyatazama yale magari yote mawili kishirikina,yaani ile Costa pamoja na lile lori lililokuwa limebeba mafuta,lengo langu ilikuwa ni kuangalia uwezo waliyokuwa nao abiria wa magari yote mawili,nilipotazama kwa makini nikaona wote waliyokuwa kwenye hayo magari mawili walikuwa weupe na wepesi kama karatasi,hakukuwa na mtu mwenye uwezo ndani ya hayo magari ambaye angenizuia nisitoe kafara,ndipo niliushika mkono wangu wa kushoto uliyokuwa na irizi na kutamka kama kawaida ya kwamba inapaswa muda huo niwe katika hilo eneo lililokusudiwa.

Kufumba na kufumbua nilijikuta nipo kando kando ya barabara katika hilo eneo,sasa kumbe hilo eneo ilikuwa ni kijiji kimoja kinaitwa Mulowo,na barabara niliyosimama kando ilikuwa ni barabara kuu ya kutoka Mbeya kueleka Tunduma,sasa ilibidi niyatazame yale magari kishirikina ili kuona yalikuwa umbali gani,baada ya kuyatazama na kuona kwamba hayakuwa mbali sana ilibidi nisogee pembeni kuyasubiri, baada ya muda wa nusu saa kwa mbali nililiona lile lori nililoliona ndotoni likiwa linakuja kutoka Mbeya kuelekea Tunduma na ile Costa pia ilikuwa inakuja kutoka Tunduma kuelekea Mbeya,basi nilisogea kuelekea katikati ya barabara kuanza kuweka dawa za tego,safari hii nilitaka asibaki mtu hata mmoja kwenye ile kafara hata kama kungekuwa na mende au nzi kwenye hayo magari nilitaka wateketee kabisa!.

Sasa wakati nimemaliza kuweka ile dawa ya tego pale katikati ya barabara,mara ghafla niliona upepo mkali sana kama kimbunga,ule upepo ulinisomba mpaka kwenye shamba moja ambalo halikuwa mbali sana na ilipokuwa barabara,ile kutazama vizuri nikawaona wanawake wawili wakiwa uchi kama walivyozaliwa,mmoja alikuwa akining'inia angani na mwingine alikuwa amesimama kando ya barabara huku akiniangalia kwa hasira!.

Yule aliyekuwa akining'inia angani akaniuliza "Wewe umekuja kufanya nini hapa,uelewi kwamba hii si himaya yako?".

Nilinyanyuka pale chini kujaribu kuwasogelea ili nilianzishe vurumai lakini sikuweza kupiga hatua hata moja.

Yule mwenzie akaniambia "Aliyekutuma leo kakudanganya,leo tunaanza na wewe ili tukakukaange tukule nyama".

Kiukweli nilisposikia ile kauli ya kuliwa nyama,jasho likaanza kunitoka japo hakukuwa na jua!.Sasa kwa wakati huo yale magari niliyokusudia kuyatoa kafara yalikuwa yameshapita eneo la tukio nilipokuwa nimeweka lile tego,nilitambua wale wachawi walikuwa wametegua lile tego ili nisipate kitu,kiukweli wale wachawi walinizidishia hasira kiasi kwamba macho yalibadilika,nilikasirika mpaka macho yakawa mekundu kama damu,kitu kilichofanya nikasirike ni kile kitendo cha kuondoa lile tego ambalo tayari lilinikosesha damu ya kafara kwenye zile gari ukizingatia ilikuwa tarehe ya mwisho ya kutoa kafara,pia niliwaza kama ningekosa ile kafara ni nini kingenikuta maana Malikia asingenielewa kwasababu uwezo wote alikuwa amenipatia,pia alishanionya kwamba nisije rudia tena kosa nililokuwa nimelifanya kule bungu,mkoani Pwani.Nilitambua kabisa lazima ningepata adhabu maana yale magari tayari yalikuwa yameshapita lile eneo la tukio bila kupata madhara yoyote,na chanzo cha hayo yote walikuwa hao wachawi wawili.

Basi niliukamata mkono wangu uliyokuwa na irizi nikauamrisha ya kwamba nataka nipige hatua kutoka nilipokuwa nimetupwa na kile kimbunga ili niweze kusogea barabarani.Pale pale nilianza kusonga barabarani,wale wachawi baada ya kuona naelekea barabarani walianza vituko tena,walianza kutimua vumbi lile eneo kiasi kwamba kukawa kama uwanja wa vita,Kiukweli nilikuwa nimejaa sana hasira,sasa kwakuwa waliweza kutegua lile tego wakanidharau wakaona sikuwa na uwezo wa kuwafanya chochote!.Nilipoona vumbi limezidi nilichukua ile pembe nikainyoosha kwenye lile vumbi hatimaye likakoma.


Itaendelea..................
Hapa lazima patakuwa Iwambi kama unaenda Mbalizi au Senjele kutoka Tunduma kuja Mbeya
 
Back
Top Bottom