Mikasa ya ndege kubwa kubwa

Mikasa ya ndege kubwa kubwa

Ni kweli kabisa, upande huo huo unaofikiria ni sawa. Kwa kuwa ndege husafiri kwa mwendo wa kasi, na juu sana, huhitaji umbali mrefu kugeuka na kanza kushuka kidogo kidogo huku ikipunguza mwendo. Kama angetokea upande wa Holili KIA angeiona kwanza hivyo isingekuwa tatizo. Mawasiliano kati ya nchi kavu na ndege yanajulikana kwa masafa ya redio, hivyo yanajulikana kwa kuwa ukiweka masafa Fulani ni ya uwanja Fulani kama redio za kawaida Cluods, Radio Uhuru nk. Pamoja na hayo bado atajitambulisha kuwa yeye ni wa KIA na rubani naye atasema jina la mruko wake kwa wakati ule. Kwa hiyo ni kweli yule alikuwa na bahati tu pale Arusha hapakuwa na kizuizi barabarani maana alishuka bila ruhusa. Alikuwa anawasiliana na KIA ila akatua Arusha.
Asante Kiongozi.
 
Subiri baada ya miaka 50 CIA watakapotoa misiri yao utaelewa kila kitu
Unajaribu kusema haikua ni ajali ya kawaida?

But hebu tuyajenge vizuri, kwa technology ilivyokubwa sasa inawezekana ni kweli baada ya kuzima transponder ndege ikapotea kabisa Mkuu?
 
Ha ha haaaa.. Hii walipotea njia nadhani, badala ya kutua KIA wakatua kisongo(hapo sina uhakika sana)

Ila ni kwamba ndege ilitua kwenye uwanja mdogo kuliko size yake, shughuli ikaja jinsi ya kuirusha, ilibidi run way ianzie offroad lakini iliruka, alierusha alikua Mwanajeshi... Ipo Youtube pia.
Hebu nisaidie hilo tukio nilitafute vipi u_tube limeandikwa kiswahili au??
 
Hebu nisaidie hilo tukio nilitafute vipi u_tube limeandikwa kiswahili au??
Andika "For the love of avition... Ethiopian airline takeoff-short field.. Boeng 767" utakuja, au check post #63, Kuna link.
 
Napingana na wewe kuhusu hili. Nitaweza kuitolea maelezo kufuatana na ukweli kuhusiana na safari za anga zinazotumika. Kuna aina nyingi zinazowezesha ndege kutua katika kiwanja/viwanja duniani, na hili linategemeana na aina ya kiwanja (matumizi), hali ya hewa wakati wa kutua, aina ya ndege, sheria za nchi zinazoongoza ndege na aina za leseni walizonazo marubani. Sasa inavyoonekana kwa tukio la Ethiopian Arusha, rubani ama aliomba au alilazimika kutumia utaratibu wa VFR(Visual Flight Rules) yaani kuruka kwa kuangalia nje, kama gari ili kuona unapokwenda. Hivyo basi, wakati wa kutua wanaomba kutumia pia Visual approaches (Ushukaji kwa kuangalia kwa macho). Huu huwa ni mawasiliano njia mbili, mwongozaji ndege toka uwanjani na rubani ndani ya ndege.
Tukiangalia ramani ya TZ, kutokea Ethiopia kuingia anga la Tanzania unatokea kaskazini upande wa Kenya. Hapa kwa utaratibu wa kuruka kwa kuangalia(ambao hutumika tu pale hali ya hewa ikiwa shwari Zaidi-isiyo na mawingu mengi),rubani huulizwa kama amekiona kiwanja (barabara ya kurukia) na akisema amekiona basi hupewa ruhusa kutua. Changamoto iliyopo kati ya Arusha na KIA ni kuwa viwanja vyote viwili vina uelekeo sawa 09/27, hii ni kufuatana na nyuzi za uelekeo wa dunia. Yaani barabara za kurukia ndege zinaanzia nyuzi 90, upande mmoja na nyuzi 270 upande wa pili. Hivyo kufanya makosa ya kibinaadam ni rahisi Zaidi hapo.
Ethiopian aliomba kutua KIA kutokea magharibi ya Arusha kwa hiyo alikuwa atue kwenye barabara kutokea nyuzi 270, alipoangalia akiwa ameelekea nyuzi 270 akaona barabara ya Kisongo akasema nimeona akaruhusiwa, akatua. Nadhani umenielewa. Swala na mafuta kwa rubani siyo rahisi kutokea kihivyo ulivyoelezea.
Asante mkuu kwa kuelezea kitaalam zaidi! Nasi tumepata kitu kwa maelezo yako.
 
Kwa matukio haya bombadia bado ni ndege bora!!
Inategemea na safari Mkuu, acha kufanisha vitu vya ajabu na Boeng, airbus, imagine Concorde ulikua na uwezo wa kuvuka Antlantic for only 3.5hrs, sasa hilo panga boy lilivuka kwa masaa mangapi?
 
Napingana na wewe kuhusu hili. Nitaweza kuitolea maelezo kufuatana na ukweli kuhusiana na safari za anga zinazotumika. Kuna aina nyingi zinazowezesha ndege kutua katika kiwanja/viwanja duniani, na hili linategemeana na aina ya kiwanja (matumizi), hali ya hewa wakati wa kutua, aina ya ndege, sheria za nchi zinazoongoza ndege na aina za leseni walizonazo marubani. Sasa inavyoonekana kwa tukio la Ethiopian Arusha, rubani ama aliomba au alilazimika kutumia utaratibu wa VFR(Visual Flight Rules) yaani kuruka kwa kuangalia nje, kama gari ili kuona unapokwenda. Hivyo basi, wakati wa kutua wanaomba kutumia pia Visual approaches (Ushukaji kwa kuangalia kwa macho). Huu huwa ni mawasiliano njia mbili, mwongozaji ndege toka uwanjani na rubani ndani ya ndege.
Tukiangalia ramani ya TZ, kutokea Ethiopia kuingia anga la Tanzania unatokea kaskazini upande wa Kenya. Hapa kwa utaratibu wa kuruka kwa kuangalia(ambao hutumika tu pale hali ya hewa ikiwa shwari Zaidi-isiyo na mawingu mengi),rubani huulizwa kama amekiona kiwanja (barabara ya kurukia) na akisema amekiona basi hupewa ruhusa kutua. Changamoto iliyopo kati ya Arusha na KIA ni kuwa viwanja vyote viwili vina uelekeo sawa 09/27, hii ni kufuatana na nyuzi za uelekeo wa dunia. Yaani barabara za kurukia ndege zinaanzia nyuzi 90, upande mmoja na nyuzi 270 upande wa pili. Hivyo kufanya makosa ya kibinaadam ni rahisi Zaidi hapo.
Ethiopian aliomba kutua KIA kutokea magharibi ya Arusha kwa hiyo alikuwa atue kwenye barabara kutokea nyuzi 270, alipoangalia akiwa ameelekea nyuzi 270 akaona barabara ya Kisongo akasema nimeona akaruhusiwa, akatua. Nadhani umenielewa. Swala na mafuta kwa rubani siyo rahisi kutokea kihivyo ulivyoelezea.
Bado sijakuelewa kitu flani, unavosema aliomba kutua kia akitokea magharib mwa arusha sijaelewa hapo maana mimi nilikuwa arusha pale mianzini siku ya tukio la hiyo ndege na tuliiona ikiwa chini sana watu wakawa wanasema inaenda dondoka hiyooo....
Alafu pia kwa jinsi matairi yalivokuwa yamezama kweny ardhi ilikuwa inajionyesha ile ndege ilitua kutokea mashariki mwa arusha kwa jinsi ilivokuwa
 
Mm leo ndio nimeanza kuangalia ile Malaysia airline 370
 
Hizi ndege bwana watu tunazifurahia sana lakini siku ikiwa yako haupatikani hata nyama

Katika pita pita zangu ajali mbaya zaidi ya ndege ni ile ya "Tenerife Airport Disaster" ya 1997 ilitokea wakati wa mwisho kabisa Spain.

Pata picha ile speed ya Runway halafu zitokee ndege mbili zinazokaribina ukubwa zikavaana zaidi ya watu 500+ walipoteza maisha pale pale.

Ndege zote zilikua Boeing 747 moja ikitokea Netherland nyingine ikitokea Los Angeles baadaye chumba cha kuongoza ndege pale Spain kilidai makosa yalikuwa ya marubani wote wawili ila upande wa Los Angels wakakataa na kusema makosa yalikuwa chumba cha kuongoza marubani pale Tenerife.

Baadaye ilibidi nchi zote zitume wapelelezi maalumu wakagundua makosa yalikuwa kwa rubani wa KLM-Boeing 747 ya Netherland ikabidi nchi na shirika hili la ndege liwajibike kuwalipa waliofiwa na waloliojeruhiwa.

Lakini pia ajali hii ilifanya pande zote mbili kukaa na kuangalia upya mifumo ya mawasiliano viwanjani na kuleta mabadiliko makubwa sana katika mawasiliano pamoja na crew za kuongoza ndege kuanzia kwa marubani mpaka viwanjani

natamani sana kuielezea kwa undani hii ajali sema leo weekend inabidi vingine viendelee-wengine wataendelea nilipoishia
 
Back
Top Bottom