Mikataba anayoingia Waziri Makamba ina mkono wa mkuu wa nchi? Kwanini hatusikii akiikemea? Wananchi wanabakia kunung'unika Taifa lao kufisadiwa

Tueleweshane kwanza. Transaction advisor ni nani?
Transaction advisor kwenye hatua ya ujenzi wa mradi wa gesi asilia mkoani Lindi (exploration stage) ni kampuni ya Baker Botts ya Uingereza.

Nimeweka bold hapo juu kwa makusudi kabisa.

Tuwekane sawa kidogo:
Katika sekta ya madini, gesi na mafuta, kutafiti na kuvuna (exploration) ni vitu viwili tofauti kabisa. Kila kimoja kina leseni yake na kina taratibu zake.
Kampuni A inaweza kufanya utafiti wa gesi eneo X na kugundua ipo. Ili waweze kuivuna gesi hiyo, ni lazima waombe leseni upya ya uvunaji. Au kampuni nyingine B ndio inaweza kupewa leseni ya kuvuna gesi kwenye eneo X.
Hapa kunakua na mikataba tofauti maana hizi ni shughuli mbili tofauti.

Kutokana na hilo, ndio maana nikasema Transaction advisor katika hatua hii ya exploration (sio hatua ya awali ya utafiti) ni hiyo kampuni ya Uingereza unayoilalamikia.
Soma hii hapa chini...


Ili kujiridhisha na maelezo yangu, upatapo muda jaribu kutembelea Tanzanian mining cadastre portal kupitia Tanzania Mining Cadastre eGov Portal - Home - FlexiCadastre utaona aina tofauti za leseni za uchimbaji wa madini, mafuta na gesi kwa maana ya zile za "uchimbaji kwa maana ya uvunaji" pamoja na zile za "tafiti."

Ahsante.
 
Unam-underrate sana! He fully knows what he's doing! Analikoroga kwa makusudi.
 
Unam-underrate sana! He fully knows what he's doing! Analikoroga kwa makusudi.
Hana hizo akili, wala tamaa ya vileee ya utajiri; ni fisadi mwenye kuridhika.

Vinginevyo kama ni tamaa ya hela kuna watu walikuwa na stock za maboksi ya viroba kwenye warehouse zao awajui wapeleke wapi.

Kama ni swala la kuwaongezea muda tu wauzaji angetaka na kuvuta mabilioni in the process angeweza.

Kila mtu ana njaa ila Makamba ni mtu mwenye political ambitions zaidi which leaves a legacy; only that he is very stupid to accomplish that mission ukimsikiliza.
 
Ndio maana ukaambiwa nchi imekabidhiwa kwa wenyewe.
Hivi hujaelewa maana ya hii kauli??
Ngoja nikanywe chai kwanza
 
Wewe mtoa mada ni mjinga kweli,kwa hiyo waziyanaingia kwa niaba ya nani? Unaweza ingia mkataba kwa kujiskia bila kufuata sheria na ushauri wa mwanasheria mkuu wa serikali?

Nyie ni aina ya wale watu wapumbavu ambao mliaminishwa na Jiwe eti Katibu Mkuu na Waziri wa Mambo ya ndani kwamba waliingia mkataba bila Serikali kujua.
 
Issue kibwa hapa ni Makamba anayeiingia je ana uadilifu kiasi gani, Bunge limeidhinisha mikataba ya namna hii. Hakuna harufu ya 13% kwa waziri na wadau wake.

Kila linalofanyika linatuelekeza twende kwenye Katiba mpya ili walau nusu ya wananchi waelewe kisheria kwa hii mikataba kuwekwa wazi, Je ni kweli mikataba hii itatatua changamoto zilizopo. Mfano Mkataba wa TICTs u etatua changamoto ya Port congestion? Gharama za Port clearance jibu ni kwa kiasi kidogo sana.

Mkataba wa Mahindra haujatatua shida yoyote sababu tunaona mpaka waziri anawatumbua maafisa uhusiano wa Tanesco sababu kuu ikiwa Umeme haupatikani kwa wakati na unakatika sana na wananchi wanahitaji kujua nini tatizo na litaisha lini. Kiufupi mikataba hapa nchini kwetu ni vichaka vya wahusika kupata millioni 500 kama kick backs tuu.

Na serikali ni ileile iliyoingia mikataba kama Richmond, Dowans, IPTL isipokuwa watu wamebadilishana wizara tuu na utamaduni wao ni uleule. Waziri anataka kumiliki hoteli kubwa, kampuni za kubet, Real estate za maana lazima awaze mikataba ili apate cha mfukoni. Wa kina Rex attorney ni walewale hakuna kilichobadilika. Ni michongo kwenda forward.
 
Sitakuwa na mengi ya kusema kwa sababu nipo occupied na kwahiyo nimeshindwa kutafuta details za hicho kilichofanywa na Makamba. Hata hivyo, kwa jinsi nilivyo mbishi, lazima nirudi tena baadae!

Pamoja na yote hayo, hebu tuwe wakweli! Hao watalaamu waliopo hapo kwa AG ni wataalamu wa nini hasa?! Kwamba eti ni watalaamu wa mafuta na gesi... walikuwa wanafanyia wapi?! Kumbuka, kwa mambo kama haya huwezi kutegemea mtu wawili watatu wenye huo utalaamu kushikilia mustakabali wa taifa bali unahitaji kuwa na TIMU YA WATALAAMU kwenye eneo husika!

Hivi kabisa unaamini hao watu wapo pale kwa AG?!

Kwa upande mwingine, nili-Google kuifahamu kampuni aliyoitaja mleta mada, huku interest yangu ikiwa upande wa energy sector, na hiki ndicho nimekuta kwenye website yao (more research is needed ku-justify uwepo wao).

Upande wa Energy Sector wanajipakulia minyama kwamba:-
Kisha wanaendelea:-

Also:-
We handle disputes involving all aspects of the exploration, production, distribution, and marketing of energy products, including:
  • Upstream Oil and Gas Operations
  • Royalty Disputes-Private Litigation
  • Royalty Disputes-Government Actions
  • Supply Contract Litigation
  • Service Contract Litigation
  • Energy Project Construction Disputes
  • Downstream Operations and Contracts
  • Market Manipulation and Consumer Price-Fixing Litigation
  • Regulatory Reviews and Rate-Making Proceedings
  • Government Investigations and Litigation
  • Trans-national Litigation
Kwenye Energy Sector peke yake, wana team ya watu zaidi ya 60! Kwahiyo hivi unaamini kabisa kwamba uko kwa AG na kwingineko tuna wataalamu wa kutosha wa ku-handle hayo mambo?!

Na pia tusichanganye mambo! Kazi ya hiyo kampuni haiwezi kuwa kuingia mikataba bali kutoa ushauri kwa Serikali including GNT.
 
Wewe ndo umemaliza kila kitu mkuu
 
We na huyo Makamba akili zenu sawa in your little pathetic heads mnadhani watanzania wote ni wapuuzi kama nyie.

Ebu mwambie waziri achunguze hapo wizarani since Dr Mpango amekuwa waziri ni watanzania wangapi wamepekekwa Aberdeen University kusomea maswala ya Oil and Gas.

If you don’t know about Aberdeen University ipo very close to North Sea na ndio chuo kikubwa shell Uk ina sponsor in oil and gase degrees.

Makamba is just stupid
 
Unaangaika na huyo ndezi hana anachujua ubongo wake unamakamasi
Transaction advisor ndio kero kubwa ya ule mradi??

Wewe unatuletea shobo za usomi wa kibongo bongo humu wakati hamuwezi hata kutoboa soko la ajira kwa majirani zetu??

Tunawapimia tu.....

Mnateteana watoto wa wajomba na mashabgazi......
 
L
It is difficult to explain what kind of an idiot you are
 
https://www.afdb.org/fileadmin/uplo...sor_for_Government_Negotiation_Team__GNT_.pdf ,tupe jibu hilo tangazo ni la lini ?
 
Wameishapewa ruhusa wale kulingana na urefu wa kamba yao so lazima wafanye hivyo# tunataka katiba mpya#
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…