Lanlady
JF-Expert Member
- Feb 27, 2019
- 1,836
- 6,303
Nimeuliza swali hili kutokana na kauli ya rais Samia leo kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi.
Kwamba hapa nchini waajiri wengi wa wasaidizi wa kazi za ndani, hawazingatii maslahi ya hao wafanyakazi pamoja na mikataba ya kimailtaifa.
Natamani kujua, hivi kila mkataba ni lazima taifa likubaliane nao hata kama hauendani na mazingira ya nchi husika?
Kwa mfano aliposema kwamba, kama mfanyakazi ana mwenza wake, basi anatakiwa kupewa chumba chake yeye na mwenza wake. Je, uchumi wa watanzania unaendana na mkataba huo?
Ikiwa baadhi ya watumishi wa serikali hawana hata makazi bora, wanapanga chumba na sebule, na anatakiwa kukaa kazini kwa saa 8-9.
Na kwa kuwa ana familia, inabidi atafute msaidizi.
Je, ni lazima kukubali kila mkataba?
Kwamba hapa nchini waajiri wengi wa wasaidizi wa kazi za ndani, hawazingatii maslahi ya hao wafanyakazi pamoja na mikataba ya kimailtaifa.
Natamani kujua, hivi kila mkataba ni lazima taifa likubaliane nao hata kama hauendani na mazingira ya nchi husika?
Kwa mfano aliposema kwamba, kama mfanyakazi ana mwenza wake, basi anatakiwa kupewa chumba chake yeye na mwenza wake. Je, uchumi wa watanzania unaendana na mkataba huo?
Ikiwa baadhi ya watumishi wa serikali hawana hata makazi bora, wanapanga chumba na sebule, na anatakiwa kukaa kazini kwa saa 8-9.
Na kwa kuwa ana familia, inabidi atafute msaidizi.
Je, ni lazima kukubali kila mkataba?