Wachina wana mitaji toka kwenye serikali yao. Pia wanapata mikopo toka China construction bank (kaigoogle hiyo bank). Pia wanavibali na vigezo vya kushindania tenda za kimataifa. Wanao utaalam na uzoefu wa hali ya juu wa ishu za ujenzi 90% ya wafanya kazi ni wafungwa na wamesomea gerezani. Uwezo wao ni mkubwa kuliko maprof mnaowasikia.
Wanavyo vifaa sio mchezo na ni vya bei ghali sana, tipper ni 170m, kijiko 360m, gari la zege 190m, Gari la kuweka lami 400m, mtambo wa kutengeneza zege 2B, greda 300m-400m, gari la kushindilia barabara 350m, Gari la kuchemsha lami 250m, mitambo ya kusaga kokoto 800m-2b, malori ya kuspray maji 160m-180m, lori lenye crane 180m aisee yaani vifaa ni gharama sana yaani unakuta vifaa vingine mkandarasi anavyo vinne mpaka 30 na wanapewa spare zote na mitambo inadumu kwa miaka kati ya minne mpaka 10.
Pia hizi sinotruck,faw,sany,shackman,xcmg, shantui,liulong,liugong na komatsu zinatumia mafuta kidogo sana ukilinganisha na mascania,volvo na caterpillar. Yaani gharama ya mitambo tu ni kama 15B kwa hiyo kwakuwa anavifaa vyake anakuwa na uwezo wa kufanya kazi sehemu yoyote nchini na akapata faida mpaka 40% na zaidi. Pia hao wachina ni waaminifu sana na wakiiba au wakipata hasara wanakula shaba kwao.
Huu ukandarasi kwa mdomo ni rahisi ila kwa uhalisia sio rahisi kwanza Tambua mswahili ni mwizi sana kama grader ni 360m si anaweza akaingia na kichaa cha kupiga pesa ya grader? Au unakuta matumizi ya mafuta kwa siku ni mpaka 20m, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?
Vibarua kwa siku ni 12500 na unakuta wapo vibarua 300, je mswahili ataacha hizo pesa salama? Material kama kokoto, cement, lami, nondo, murram unakuta zinanunuliwa mpaka za 5B, je mswahili ataziacha hizo pesa salama?
Punguzeni kuleta siasa kwenye masuala ya ukandarasi.
Samahani kwa comment ndefu.