Kuna jukumu Serikali wanalikwepa hapa?kupitia mkataba upya haya kama ni wa kinyojaji ni mkataba tayari ushasainiwa na ni maridhiano ya baina za pande mbili, labda kama wataona huo mkataba haukufatwa ama kutekelezwa wanaweza kusaidia.
Lakini kikubwa hapa ni mazingira na mfumo, Je tumewatengenezea mazingira wezeshi na mfumo utakaowafaidisha?
Hii ni biashara tukumbuke, so unaweza kukuta wasanii wetu wanaambulia umaarufu tu, na Copy zinazogongwa ama kuuzwa zikawa hazizidi 500k.
Nadhani tunahitaji mfumo mzuri na mazingira wezeshi, ili filamu ziwe na hadhi, ili kufanya watu wengi kuzipenda, kuwekeza na kununua kazi za wasanii.
Lakini uwekezaji ni mdogo mno, quality ya filamu zetu na za chini mno, na hakuna mazingira bora ya kufanya wasanii wafaidike na kazi zao.
Wenyewe tu hawajitambui.
Nina uhakika kama Kanumba angekuwa hai leo hii Filamu na wasanii wa Filamu wangefaidika na uwekezaji alioanza kuwekeza, pesa yake nyingi ilikuwa kwenye uwekezaji na kuboresha mazingira, kabla ya Matunda yake ndio akatutoka.
Tumuone Dimond kwa wasanii wa Muziki, alimamua kuwekeza kwa gharama kubwa leo hii uwekezaji ule unamlipa na kupelekea kuwafungulia milango wasanii wengine.
Panahitaji mjadala mpana utakaoshirikisha wadau wote wa Sanaa kuweza kuikomboa Sanaa hapa nchini.
Kushughulikia mikataba ya Mzee Majuto na Kanumba sio kutibu tatizo.
Wizara ianze moja ikiwezekana iwapeleke wataalam wake Nigeria kwenda kujifunza, hawa akina Dimond ni wa kuulizwa imekuwaje wamefika hapo walipo.
Hili si kwa Sanaa ya maingizo na mziki peke yake, kwenye ridhaa, mpira wa miguu n.k.
Lazima tutengeneze mazingira na mfumo utakaofanyika wadau wawekeze na wawekezaji wenye uwezo kuja nchini kuwekeza ili kuvuna matunda mazuri na kupata wanariadha, wasanii, wanamuziki na hata wachezaji wazuri.
Wizara wabebe jukumu Lao na si kuwatumia wasanii wetu kwenye kampeni na kuishia kupiga nao picha za Selfie.
Wenzetu imefika kipindi wametenga hadi maeneo kwa ajili ya shughuli za wasanii.