Mikopo inatisha, yanaenda wapi hayo matrilioni!

Mikopo inatisha, yanaenda wapi hayo matrilioni!

blogger

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2012
Posts
12,112
Reaction score
15,060
Mpaka sasa Mama amekopa Matrilioni mangapi ndugu zangu..!?

Lakini Matrilioni hayo ni kwa ajili ya nani!?? Yanaenda wapi hayo matrilioni!?? Mbona umasikini unazidi kutamalaki wazee.

Lakini mpaka masikini wa kutupa analipa haya madeni. Mbona maisha yanazidi kuwa ya kifukara?

Kuna watu hapa nafikiria kuwaomba msamaha. Ipo siku nitawaomba msamaha hawa watu..

1. Hayati John Joseph Pombe Magufuli
2. Humphrey Polepole
3. Job Ndugai
4. Elvis Musiba..

Ehh! 😞😞😞😞
 
Eti zaidi ya tirion moja imekopwa kwa ajili ya mazingira, inaingia akilini kweli...sawa na Kusema mtu umekopa Hela unaenda kunywea bia badala ya kuwekeza, Sasa hela ya marejesho utaitoa wapi.
 
Mbona unauliza maswali ambayo hata mtoto mdogo hawezi kuuliza,kwamba wewe huoni miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa na serikali yetu? Huoni uwekezaji mkubwa na wakihistoria uliofanywa na serikali hii katika secta karibu zote? Huoni namna vituo vya Afya vinavyojengwa kila Kona ya nchi yetu? Huoni hospitali za mikoa Kanda Hadi Taifa zinavyoboreshwa na kuongezewa uwezo wa kiviifaa na wataalamu ili kuweza kutoa huduma za kibingwa ambazo awali ilikuwa Ni mpaka mgonjwa apelekwe nje ya nchi?

Huoni uboreshaji wa secta ya Elimu? Huoni uwekezaji wa mabillioni ya pesa katika secta hiyo ambayo yamechochea hata ongezeko ya fursa za ajira kwa vijana? Huoni kwa Sasa Hakuna mwanafunzi anayekaa nyumbani kwa kukosa Ada au uhaba wa madarasa?

Huoni kwa Sasa wanafunzi wote wanaripoti shuleni kwa wakati? Huoni kwa Sasa Elimu Ni bure Mpaka kidato Cha sita huku bajeti ya mikopo ya Elimu ya juu ikipaa Hadi kufikia billioni Mia sita na pointi? Huoni ukarabati na ujenzi wa shule mbalimbali kwote nchini unaofanywa na serikali ya Rais wetu mchapa kazi mama Samia?

Huoni mapinduzi katika secta ya kilimo? Kwamba hukusikia kuwa serikali imetoa mabillioni ya Ruzuku takribani billioni Mia moja hamsini katika mbolea na hivyo kupelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni mfano mbolea ya DAP msimu uliopita ilikuwa inauzwa shillingi laki moja na 40 lakini msimu huu inapatikana kwa Elfu 70 tu?

Huoni namna mh Rais Rais alivyogusa maisha ya wakulima kwa uamuzi huo wa kizalendo na kijasiri? Huoni kwa Sasa namna kilimo kinavyowainua wakulima na kuwafuta wengi kujiongoza katika secta hii?

Huoni miradi ya bwawa la umeme na reli ya kisasa vikiendelea kwa Kasi nzuri? Huoni kukamilika kwa miradi hiyo inakwenda kulimulika na kuliangazia Taifa letu kila mahali? Huoni itachochea maendeleo ya viwanda kutokana na uwepo wa umeme wa uhakika?

Huoni itapunguza Bei ya umeme na hivyo Bei ya bidhàa kuwa ya chini? Huoni kukamilika kwa rwli ya kisasa kutachochea usafirishaji wa bidhàa zetu na za majirani? Huoni bandari yetu ya Dar itapokea mizigo mingi na hivyo kuongeza mapato tutakayo wekeza katika secta nyingine Kama vile Elimu na Afya?

Kwamba hayo na mengi huyaoni? Kwamba wewe ni kipofu? Au umetumwa? Au siyo mtanzania? Au unachuki binafsi na mh Rais wetu mpendwa kipenzi Cha watanzania mama Samia suluhu Hassani?
 
Wanapewa wakurugenzi na wengine kwa miradi hewa na vyoo vya watoto kwa 30m
Nyumba za hospitali 700m yaani we unapokea unasepa nazo no problem
 
Nyie sukuma gang hammalizi tu msiba? Enzi zenu za kuchafua nchi zimepita.
Nyie watu ni wajinga sana....yaani mnalipwa kushinda humu kuandika ujinga tu....Umejiuliza hichi ulichokiandika mama au baba yako akikiona atajilaumu kwann alikupeleka shule walau ukafute huo ujinga wako?.Vijana aina yako ni wa kuzibua tu.
 
Mbona unauliza maswali ambayo hata mtoto mdogo hawezi kuuliza,kwamba wewe huoni miradi mikubwa ya kimkakati inayotekelezwa na serikali yetu? Huoni uwekezaji mkubwa na wakihistoria uliofanywa na serikali hii katika secta karibu zote? Huoni namna vituo vya Afya vinavyojengwa kila Kona ya nchi yetu? Huoni hospitali za mikoa Kanda Hadi Taifa zinavyoboreshwa na kuongezewa uwezo wa kiviifaa na wataalamu ili kuweza kutoa huduma za kibingwa ambazo awali ilikuwa Ni mpaka mgonjwa apelekwe nje ya nchi?

Huoni uboreshaji wa secta ya Elimu? Huoni uwekezaji wa mabillioni ya pesa katika secta hiyo ambayo yamechochea hata ongezeko ya fursa za ajira kwa vijana? Huoni kwa Sasa Hakuna mwanafunzi anayekaa nyumbani kwa kukosa Ada au uhaba wa madarasa? Huoni kwa Sasa wanafunzi wote wanaripoti shuleni kwa wakati? Huoni kwa Sasa Elimu Ni bure Mpaka kidato Cha sita huku bajeti ya mikopo ya Elimu ya juu ikipaa Hadi kufikia billioni Mia sita na pointi? Huoni ukarabati na ujenzi wa shule mbalimbali kwote nchini unaofanywa na serikali ya Rais wetu mchapa kazi mama Samia?

Huoni mapinduzi katika secta ya kilimo? Kwamba hukusikia kuwa serikali imetoa mabillioni ya Ruzuku takribani billioni Mia moja hamsini katika mbolea na hivyo kupelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni mfano mbolea ya DAP msimu uliopita ilikuwa inauzwa shillingi laki moja na 40 lakini msimu huu inapatikana kwa Elfu 70 tu?

Huoni namna mh Rais Rais alivyogusa maisha ya wakulima kwa uamuzi huo wa kizalendo na kijasiri? Huoni kwa Sasa namna kilimo kinavyowainua wakulima na kuwafuta wengi kujiongoza katika secta hii?

Huoni miradi ya bwawa la umeme na reli ya kisasa vikiendelea kwa Kasi nzuri? Huoni kukamilika kwa miradi hiyo inakwenda kulimulika na kuliangazia Taifa letu kila mahali? Huoni itachochea maendeleo ya viwanda kutokana na uwepo wa umeme wa uhakika? Huoni itapunguza Bei ya umeme na hivyo Bei ya bidhàa kuwa ya chini? Huoni kukamilika kwa rwli ya kisasa kutachochea usafirishaji wa bidhàa zetu na za majirani? Huoni bandari yetu ya Dar itapokea mizigo mingi na hivyo kuongeza mapato tutakayo wekeza katika secta nyingine Kama vile Elimu na Afya?

Kwamba hayo na mengi huyaoni? Kwamba wewe Ni kipofu? Au umetumwa? Au siyo mtanzania? Au unachuki binafsi na mh Rais wetu mpendwa kipenzi Cha watanzania mama Samia suluhu Hassani?
Mkuu umeandika mambo Mengi ila ni ushabiki tu....hizo secta zinaendeshwa na akina nani wakati Mama kila siku ateua baraza jipya....hicho kilimo kafumua wizara,Njaa ni kali vyakula vimepanda bei mkuu au ww unaandikia ukiwa nje ya nchi hujui kinachoendelea mtaani huku?,Shule zipi na elimu hipi mama kainua tembea walau ata hili tunaita jiji la Dar uone wanafunzi wanakaa chini madawati hakuna madarasa yanavuja vumbi bado msimu wa mvua....Miradi yote imekufa.
Mama anakopa hela vijana wake wanagawana tu...Yaani mpaka kivuko cha 8.7bln kinaenda kulekebishwa tu hapo kenya kwa 7.5bln....mimi nakataa Mama hajafanya lolote ata nikikutana nae namwambia mama unazingua.CHAMA KITAMFIA MIKONONI HASIPOVUA MIWANI.
 
Badala ya kujibu alichouliza wewe umekuja na unayoyajua wewe

Mikopo inaenda wapi na inatumika kufanyia nini?
Jana nilinunua kg 25 za sembe ya mahindi kwa tsh. 44,000/=. Nchi hii kwa Sasa maisha ya mwananchi wa kawaida ni mateso makubwa Sana lakini kila uchao tunaambiwa kuhusu mikopo sijui ya kufanya Nini!.

'Njaa hudhalilisha heshima na Uhuru wa nchi. Njaa utweza UTU wa binadamu". Dr. Bashiru Kakurwa Ali.
 
Inajengea familia ya Magufuli nyumba hapa Dar.
Bajeti ya nyumba za Marais wastaafu Huwa inapangwa katika bajeti Wala haihusiani na mikopo umiza ya Mama Maridhiano.Jibu hoja!
 
Mpaka sasa Mama amekopa Matrilioni mangapi ndugu zangu..!?

Lakini Matrilioni hayo ni kwa ajili ya nani!?? Yanaenda wapi hayo matrilioni!?? Mbona umasikini unazidi kutamalaki wazee...!

Lakini mpaka masikini wa kutupa analipa haya madeni. Mbona maisha yanazidi kuwa ya kifukara..!?

Kuna watu hapa nafikiria kuwaomba msamaha. Ipo siku nitawaomba msamaha hawa watu..

1. Hayati John Joseph Pombe Magufuli
2. Humphrey Polepole
3. Job Ndugai
4. Elvis Musiba..

Ehh! [emoji20][emoji20][emoji20][emoji20]
Hivi tutalipa kwa Uchumi gani tulionao,usije kukuta huyu Mama Maridhiano anakopa Ili kulipa madeni yaliyoziba sehemu zingine.Kile kichwa siyo cha mipango bali matumizi.
Godfathers wa hii nchi wamwambie ajiuzuru au Bendera ipepee nusu mlingoti vinginevyo tutafilisika kama Ghana!
 
Mkuu umeandika mambo Mengi ila ni ushabiki tu....hizo secta zinaendeshwa na akina nani wakati Mama kila siku ateua baraza jipya....hicho kilimo kafumua wizara...
Shule ina wanafunzi elf 3 walimu 40 halafu anajitokeza mpumbavu mmoja anasema mama anaupiga mwingi!. Mwingi wa mafisadi January makamba na mwigulu madelu Nchemba na watoto wa vigogo kule hazina.

Wananchi tunateseka halafu anajitokeza mtu kutulalamikia kuwa mawaziri na makatibu wakuu hawaelewani!. Kama hawaelewani ni kwa nn usiwawekee kandoo uteue lundo la watanzania wataalamu ambao wamejaa mtaaani bila ajira?.

Wananchi tunanjaa anajitokeza mtu kutuambia kuwa anafikiria kuongeza wizara ofisini kwake ili kutengeneza watu ulaji!.
 
Back
Top Bottom