Mikopo kwa njia ya simu kilio kipya kwa Watanzania

Mikopo kwa njia ya simu kilio kipya kwa Watanzania

Benki hawaangalii Hayo...wao wanachoangalia ni uhakika wa pesa yao kurudi...Sasa una dhamana mfano nyumba na mzunguko wa biashara mzuri watakuachaje ? Na tena wao ndio watakutafuta.
Sio kweli kuna kigezo kingine lazima waulize credit reference bureau kama wewe ni mdaiwa sugu sehemu yeyote ya mikopo iwe ya taasisi au online na uwezo wa kujua hilo wanao sababu hao wakopesha mikopo online nyuma yake kuna taasisi zilizosajiliwa kukopesha ndizo huendesha hiyo mikopo

Kipengele cha kwanza sasa hivi ukiomba mkopo kabla kuangalia vigezo vingine huanza kwanza kupata taarifa zako za ulipaji mikopo kutoka credit reference bureau na kujihakikishia kwanza kama wewe sio mdaiwa sugu popote ndipo waendelee na hivyo vigezo umetaja hawaanzii huko sasa hivi hiyo ni sehemu ya pili siyo ya kwanza kama zamani kabla ya ujio wa credit reference bureau

Dawa ya deni kulipa liwe la mkopo kupitia simu au online au popote kuepuka matatizo mbele ya safari

Wajinga wengine hutupa line akidhani akitupa line ya simu mkopo unafutika.na line aliyotupa haufutiki ng'oo laini ukisajili unasajili kwa kitambulisho cha taifa na dole gumba kitambulisho cha taifa na dole gumba popote vinabeba taarifa zako zote
Ukitupa line deni linazidi kukua tu na riba yake siku wakikuzukia watauza mali zako zote kufidia deni lao waweza kukufilisi kabisa
 
Hii ni hatari kwa wakopaji, yaani madeni madogo tu yamkoseshe mtu mkopo, dah!!

Itabidi tuhamie kwenye vikundi vya mtaani kama ndio hivyo, vipo vingi...kuanzia 1m hadi 5m unapata bila usumbufu.
 
Mkuu mimi nilinyimwa mkopo niliouomba kupitia crdb kisa deni la songesha!
Songesha mkopo uko chini ya Tanzania Commercial Bank wajinga hudhani ni mkopo wa line ya simu ya Vodacom ni mkopo wa benki ule wa Tanzania Commercial Bank zamani ikiitwa benki ya posta

Walichofanya kupunguza tu foleni kukopa watu wakope kupitia tu simu ambayo wameingia makubaliano lakini mkopo wenyewe huidhinishwa na benki yenyewe ukiomba
 
Songesha mkopo uko chini ya Tanzania Commercial Bank wajinga hudhani ni mkopo wa line ya simu ya Vodacom ni mkopo wa benki ule wa Tanzania Commercial Bank zamani ikiitwa benki ya posta

Walichofanya kupunguza tu foleni kukopa watu wakope kupitia tu simu ambayo wameingia makubaliano lakiji mkopo wenyewe huidhinishwa na benki yenyewe ukiomba
Na Mgodi ipo chini ya DTB, ukikopa hizi platforms ni kama umekopa Bank tu. Umakini ni muhimu sana.
 
Songesha mkopo uko chini ya Tanzania Commercial Bank wajinga hudhani ni mkopo wa line ya simu ya Vodacom ni mkopo wa benki ule wa Tanzania Commercial Bank zamani ikiitwa benki ya posta

Walichofanya kupunguza tu foleni kukopa watu wakope kupitia tu simu ambayo wameingia makubaliano lakini mkopo wenyewe huidhinishwa na benki yenyewe ukiomba
Kupunguza foreni ya wateja wanao kuja benki kukopa 2000, 10,000, 50,000 100,000[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Hivi songesha inaweza kukukopesha 1m na zaidi?
 
Umeonewa tafuta ofisa mkopo alio nyooka, mkopo utapata faster tu.
Hata hivyo waliniambia nikajaze fomu, mimi tu nijafanya hivyo. Ina maana kwa watumishi huu mfumo wa ESS umeunganishwa na hizo system za kungamua wadaiwa sugar!
 
Na Mgodi ipo chini ya DTB, ukikopa hizi platforms ni kama umekopa Bank tu. Umakini ni muhimu sana.
Tatizo baadhi ya watanzania ujuaji mwingi anadhani akikopa online au pesa kwa simu basi huyo mkopeshaji bwege hajielewi anajitia ooh ananiķopesha mimi wakati hanijuì

Kumbe online wanaokopesha wanamjua vizuri kupitia line aliyosajili kupitia kitambulisho cha taifa na dole gumba lake

Mtu akitaka kujua kuwa wanamjua vizuri apoteze line aombe kurudishiwa line anaambiwa taja tu namba ya NIDA wataomba namba tu ya NIDA na dole gumba kila kitu cha taarifa zake hiki hapa
 
Tatizo baadhi ya watanzania ujuaji mwingi anadhani akikopa online au pesa kwa simu basi huyo mkopeshaji bwege hajielewi anajitia ooh ananiķopesha mimi wakati hanijuì

Kumbe online wanaokopesha wanamjua vizuri kupitia line aliyosajili kupitia kitambulisho cha taifa na dole gumba lake

Mtu akitaka kujua kuwa wanamjua vizuri apoteze line aombe kurudishiwa line anaambiwa taja tu wataomba namba tu ya NIDA na dole gumba kila kitu cha taarifa zake hiki hapa
Mkuu sio ujuaji ni ushamba na umasikini, ukiwa na kitambulisho cha taifa huwezi kupotea popote, kama we ni mhalifu bora usijisajiri ta kitambulisho cha taifa, kabisa
 
Kupunguza foreni ya wateja wanao kuja benki kukopa 2000, 10,000, 50,000 100,000[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Hivi songesha inaweza kukukopesha 1m na zaidi?
Ni wewe tu una ongezewa viwango kadiri unavyokopa na kulipa wanakupima uaminifu wako tu

Wako watu wengi tu mbona akihitaji milioni sekunde tu mzigo unaingia na wako kibao mitandao yote tu milioni kitu kidogo mno cha msingi kuwa mwaminifu kukopa na kulipa .Huhitaji kupanga foleni kukopa benki au kujaza mikaratasi kibao na midhamana kibao kukopa milioni moja

Pesa kama hiyo ni kukopa simu kiganjani tu au online si ya kuzurura hata kwa ndugu kuomba

Simu zimekuja kurahisisha maisha kuna watu hawataki
 
Wanajamvi habari zenu,

Kama kawaida nikikutana na kitu kipya lazima nikileta hapa kwa faida ya wengine. Ni kwamba wiki iliyopita nilikuwa nimeomba mkopo wa milioni 30 hivi kwenye mojawapo ya benki hapa nchini. Hii benki nimekuwa mteja wao tangu 2006 kama sikosei nimeshakopa kwao kwa zaidi ya mara tatu hii ikiwa ya nne. Ajabu ni kwamba, baada ya kufanya process zote za mkopo nilipigiwa simu nikaambiwa sitopewa mkopo kwa sababu mimi ni mdaiwa wa Sugu wa Mpewa nina deni la tangu mwaka 2020. Nilistuka kidogo lakini nikasema ngoja nifuatilie, hatua ya kwanza nilipiga simu Vodacom huduma kwa wateja kujua katika line zangu mbili za voda ni ipi ina deni?

Majibu kutoka Vodacom walinambia line zote hazina madeni isipokuwa kuna line moja likopa shilingi elfu 5 na ikawa muda wa kurejesha umepita. Hivo wakati deni linalipwa tayari taarifa zangu zilishaenda huko CRB kama mdaiwa Sugu. HII NI LINE AMBAYO ALIKUWA ANAITUMIA KIJANA WANGU CHUO kwa sababu wakati anaingia chuo alikuwa na miaka 16 kwa sababu alichagua kusoma kwa njia ya Cert, Diploma & Degree.

NI NINI CHA KUFANYA hili lilikuwa swali la pili. Jibu likawa kwamba nenda ofisi za vodacom zilizokaribu nawe ili upate ufafanuzi zaidi. Baada ya kufika Vodashop. Majibu ya Vodacom nenda NCBA Benki upate ufafanuzi zaidi. NCBA kwa official letter kabisa wakajibu hakuna deni na wakaonyesha tarehe ya mkopo na tarehe ambayo mkopo ulilipwa.

SWALI TENA NINI CHA KUFANYA KUCLEAR TAARIFA ZANGU HUKO CREDITINFO, jibu wapigie Simu, baada ya kupiga simu nikajieleza kisha nikaelekezwa kwenye Website yao ambapo nilijaza form ili kupewa taarifa zangu.
Majibu yalikuja ya ina mbili kwamba lile deni la Mpawa lilipwa lakini kwa kuchelewa hivo hizo taarifa zitabaki hivo kwa kipindi cha miaka sita tangu deni kulipwa.

MAAJABU SASA: Hata hii benki niliyokuwa ninaomba mkopo kwao nayo imeniorodhesha kama mdaiwa sugu kwa mikopo yote miwili ambayo yote nilishalipa nikamaliza. mkopo 2019 - 2022 na mkopo 2023 - 2024 ambayo yote imelipwa. Kwani baada ya kumaliza mkopo wa pili niliomba mkopo mwingine ambao ni watatu na sijafanya TOPUP.

Hili la benki nimefungua Dispute kupitia CRB ambaye ataawandikia ili wanijibu ndani ya siku 15 wakishindwa kufanya hivo nitakuwa huru kuwashitaki kwa Defamention. KUHUSU MKOPO WA BENKI NISUBIRI MPAKA MIAKA 6 IPITE.

Wasi wasi wangu ni kuwa kuna watu wengi sana ambao ama kwa kujua au kutojua huenda majina yao yako CRB na wako Blacklisted, kwa sababu kuna watu wamesajiri line za simu ambazo zinatumiwa na ama watoto, house girl, shamba boy nk. Katika hili nadhani CRB wangeangalia namna nyingine ya kurekodi taarifa wanazopokea kutoka kwa CREDITORS.

Mwisho nimenyimwa loan ya milioni 30 kwa sababu tu ya kucheleweshwa Deni la shilini elfu 5 ambayo iko chini ya NCBA.


Usikope! Naenda taratibu, wakati mwingine ukinyimwa Mkopo shukuru tu, hivi 30m riba yake ni kiasi gani? Utumwa huu Ndugu zangu, unaweza kukuza biashara taratibu tu bila presha pia!
 
Back
Top Bottom