Mikopo ya miaka ishirini? Kweli Rais Samia anatupeleka pabaya

Mikopo ya miaka ishirini? Kweli Rais Samia anatupeleka pabaya

DaudiAiko

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2012
Posts
372
Reaction score
310
Wanabodi,

Serikali inataka kufanya mengi na katika kufanya hayo, inataka kutumia muda mfupi kutekeleza miradi ya kimkakati kama njia ya kupeleka maendeleo kwa wananchi. Labda kuna uwezekano kwa serikali kukamilisha mipango yake bila kukopa lakini maelezo tuliyoyapata kutoka kwa viongozi wa nchi akiwemo Rais Samia mwenyewe ni kwamba itachukua muda mrefu sana kufikia malengo yaliyopangwa.

Mengi yamejadiliwa haswa katika kueleza umma kuhusu jinsi ambavyo nchi zingine hata zilizoendelea zinavyokopa fedha kwa miradi yao mbalimbali lakini jambo muhimu la kutafakari ni kama fedha hizo zitatunufaisha endapo zitatumika katika miradi isiyoingizia serikali kipato chochote. Mfano mkubwa ni katika miradi ya ujenzi ambayo kiuhalisia inasaidia wananchi lakini haiingizii serikali kipato chochote.

Tafakari,
Jumatano jema.
 
Mradi wowote ni lazima usaidie katika kuzalisha, kusafirisha na kuzambaza bidhaa zinazozalishwa katika nchi. Mradi unaweza kuchukua muda mfupi au mrefu faida zake kuonekana.

Kitu chamsingi ni kuwa makini na masharati ya mikopo itakayochukuliwa kutekeleza hiyo miradi, hasa kuangalia riba na tenure[ muda wa kuanza kulipa mkopo] mkopo huska.

Ikiwa mkopo utaiva kabla haujamalizika na kuanza kuzalisha huo utakuwa sio mkopo mzuri kwa nchi; kwani itabidi ulipiwe kutoka miradi mingine inayozalisha!
 
Wanabodi,

Serikali inataka kufanya mengi na katika kufanya hayo, inataka kutumia muda mfupi kutekeleza miradi ya kimkakati kama njia ya kupeleka maendeleo kwa wananchi...
Wewe ni jinga jinga😂. Hivi watoto mnataka wasome kwenye miembe mpaka lini? Tozo wamesema zinatosha madarasa 500 tu na mahitaji ni madarasa 15,000 sasa wanafunzi hawawezi kisubiri mwaka kesho!

Kuna uwekezaji hauwezi kusibiri hasa elimu. Mikopo ya miaka 20 yenye riba nafuu au zero ndiyo mizuri maana huyu mtoto itamvhukuwa miaka 17 zaidi mpaka aanze shule kwa miaka 7 mpaka aanze kazi miaka 24 na yeye anatakiwa kuwa mzalishaji ili huu mkopo uwe umesaidia .

Ukichukuwa mkopo wa miaka 6 kwa wanafunzi na riba ya juu ni mikopo mibaya
 
Mimi nningekuwa ndio mshauri wa samia kuhusu kukopa ningemshauri kama anapata mikopo ya zero interest na ya muda mrefu kulipa achukue tu bila kupapasa macho!!

Akishachukua hiyo mikopo aitumie kulipa mikopo ya kikwete na mkullo wake waliyokopa toka private banks kwa riba kubwa; kwa nija hiyo atasaidia nchi kupunguza mzigo wa kulipa hizo riba kubwa na mikopo kuiva ndani ya muda mfupi kabla hata hiyo miradi kumalizika!

It is called leveraging nyie mataga!!!
 
Wewe ni jinga jinga[emoji23]. Hivi watoto mnataka wasome kwenye miembe mpaka lini? Tozo wamesema zinatosha madarasa 500 tu na mahitaji ni madarasa 15,000 sasa wanafunzi hawawezi kisubiri mwaka kesho!

Kuna uwekezaji hauwezi kusibiri hasa elimu. Mikopo ya miaka 20 yenye riba nafuu au zero ndiyo mizuri maana huyu mtoto itamvhukuwa miaka 17 zaidi mpaka aanze shule kwa miaka 7 mpaka aanze kazi miaka 24 na yeye anatakiwa kuwa mzalishaji ili huu mkopo uwe umesaidia .

Ukichukuwa mkopo wa miaka 6 kwa wanafunzi na riba ya juu ni mikopo mibaya
Ama kweli ushamba ni mzigo wa kuni. Lazima taasisi za kutoa mikopo zifahamu jinsi ambavyo serikali imepanga kutumia fedha zilizo kopeshwa na mpango wa serikali kurudisha fedha hizo.

Kwasababu hiyo, ni sahihi kukopa hela kwa ajili ya kitu kinacho kuongezea kipato na sio kwa ajili ya matumizi ya kila siku.

Madarasa yata wanufaisha watanzania wengi lakini baada ya kuyajenga, hayawezi kuwa chanzo cha kupata fedha zozote kwa ajili ya kulipa mikopo.

Mwisho kabisa tujaribu kufanya tathmini ya fedha zinazo hitajika kwa ajili ya kukamilisha miradi yote ya maendeleo nchini. Utagundua kwamba Tanzania sio nchi inayo hitaji shilingi trilioni 3 tu.

Hela inayo hitajika kutu kwamua kutoka pahala tulipo na kutufikisha hatua nzuri zaidi ni nyingi sana. Kwa kukopa kila mara, je tutafika?
 
Ama kweli ushamba ni mzigo wa kuni. Lazima taasisi za kutoa mikopo zifahamu jinsi ambavyo serikali imepanga kutumia fedha zilizo kopeshwa na mpango wa serikali kurudisha fedha hizo. Kwasababu hiyo, ni sahihi kukopa hela kwa ajili ya kitu kinacho kuongezea kipato na sio kwa ajili ya matumizi ya kila siku. Madarasa yata wanufaisha watanzania wengi lakini baada ya kuyajenga, hayawezi kuwa chanzo cha kupata fedha zozote kwa ajili ya kulipa mikopo. Mwisho kabisa tujaribu kufanya tathmini ya fedha zinazo hitajika kwa ajili ya kukamilisha miradi yote ya maendeleo nchini. Utagundua kwamba Tanzania sio nchi inayo hitaji shilingi trilioni 3 tu. Hela inayo hitajika kutu kwamua kutoka pahala tulipo na kutufikisha hatua nzuri zaidi ni nyingi sana. Kwa kukopa kila mara, je tutafika?

Tanzania kuna watoto wengi sana na madara kidogo sana hili ni tatizo la kitaifa. Watoto hawawezi kusubiri nyumbani miaka miwili tupate makusanyo ya kodi na kujenga. Umri wa mtoto ni muhimu sana kwenye elimu na jamii. Kukopa kunaonyesha hali mbaya ya mipango huko nyuma na hatuwezi kumlaumu Raisi kwa kutafuta pesa za kusaidia watoto. Hii ni muhimu kiasi kwamba hata world bank walitoa $500M wakati wa Magufuli kusaidia hili kama unakumbuka skendo ya watoto wa mimba hii pesa ilikuwa mkopo nafuu wa elimu. Watoto wanaingia shule wakiwa na miaka 7 serikali inabidi iwe na takwimu za kutosha ili madarasa wajenge kutokana na data mtoo inajulikana akifika miaka 7 anaingia shule hivyo mipango inatakiwa kuanzia akizaliwa tu.
 
Ndugu zangu mikopo sio kitu kibaya, na kwa kampuni kubwa au nchi mikopo ya maendeleo hulipwa kwa muda mrefu. Kwa individual kukopa then ulipe kwa miaka 20 sio rahisi maana nguvu zinakuwa zimeanza kupungua.

Ila kwa nchi, kukopa leo, kuna kizazi ambacho kinafaidika na mkopo sasa na msingi wake uwe wa kuifanya Tanzania ya leo na kesho iwe na neema na matumaini kuliko tusingekopa.

Rais yangu kwa wakubwa ambao wana dhamana ya kukopa kwa niaba yetu ili baadae sisi na wanetu tulipe, kopeni ili riba ya mabenki ya uwekezaji kama TIB na TADB ishuke na masharti ya mikopo kwa start-up investment projects yawe na fursa ya kuwafanya Watanzania wakope sio kama individuals ila watengeneza kampuni za kuzalisha bidhaa na huduma.

Miezi kadhaa imepita nilikuwa naongea na mtu mmoja alifanya kazi serikali ya mchonga, Mzee Ruksa na BWM, nyakati zile Tanzania ilikuwa ina-export wastani wa marobota laki 6 kwa mwaka. Victoria federation enzi hizo ikiwa na ofisi ya mauzo ya Pamba London.
Leo mauzo ya pamba, bila shaka haifiki hata robobota laki 1, maana yake uzalishaji umeshuka..

Kwanini TADB na TIB wasije na investment projects loans ili kampuni za Watanzania ziwekeze kwenye kilimo cha kibiashara kwa ku-mechanize mashamba yawe na mfumo wa umwagiliaji, pamba ivunwe, kampuni zingine ziundwe zikopeshwe textile machinery ili Tanzania iuze nyuzi, vitambaa hata nguo, ili hao wanetu ambao leo 1.3Tril inajenga madarasa yao, in 15 years wawe na sehemu ya kufanya kazi kwenye viwanda vya mnyororo wa thamani wa Pamba.
Hii ikihusisha kuwa na kampuni zingine zinazalisha mbolea na all the agro-chemicals ili hela ya imports ya agro-inputs ibaki ndani izunguke kwa ku-service deni.

Kwanini Tanzania isiwe exporter wa nyama middle east kwa kutumia advatange ya ng'ombe tulionao? Kwanini Tanzania isiwe exporter wa leather products baada ya kuwa tumechakata ngozi za ng'ombe?

Akina Ng'wigulu wataalamu hapo wizarani ya fedha, fikiriene kuifanya agro-commercial projects, dunia ina watu bil 7, tuuze walau SADC all the basic consumables.
Itakuwa aibu kama tutakopa pasi kujenga financial instrument itakayo-stimulate uzalishaji ambao utavutia forex.

Tanzania based on the vast of resources, tusipojiandaa kwenye uwekezaji wa miradi ya kibiashara, ipo siku zile projects za Nyanzaga Gold, Mahenge Graphite na gas ya kusini ziki-peak na kuna fursa ya kuuza kuku laki 1 na mayai say laki 3 kwa siku, tutabaki tunashangaa wakati nchi ndogo kama netherlands yenye idadi ya ng'ombe wachache kuliko Tz, ila kwa kuwa na ubora wa uwekezaji kwenye agribuz, wanauza nyama, mayai, maziwa na kuvuta forex ya kutosha kuliko sisi.


In 2019, the Netherlands exported €94.5 billion worth of agricultural goods. That is a 4.6% increase on the €90.4 billion export figure for 2018.


Dunia ya sasa mauzo ya agri-process ni biashara kubwa sana. Kwanini hatuna mauzo ya sausage from fresh water.

Hela toka kwenye mzunguko huo itasisimua makuzi ya service sector kama lega, insurance, banking, logistics, consultancy just to mention a few;

€90.4 billion ni sawa na TZS 247Tril.

Assume Watanzania tuwe na kampuni zenye mauzo ya wastani wa 20% ya nini Uholanzi walipata na TRA ika-tax hizo biashara, nchi ingepata kiasi gani?

We need the gov. to setup a room availability of financial instrument for Tanzania owned corporations to invest in know-how, technology and hire experienced expertise to make a game change in agri-investment.
Agribuz bado hatujagusa hata 5% ya potential ya nchi hii; ila kama ni kilimo cha kufa na kupona na kutegemea kudra za Mwenyezi ambacho ndicho kilichopo, basi; itapita miaka 20, Tanzania itaendelea ku-import toothpick, chupi, leso, toilet paper, gundi, penseli, chaki vitu ambavyo could be made in Tanzania.

Tunaomba kupata platform ya ku-dialog na madam SSH ili tufanye mambo haya yatokee.
 
Tanzania kuna watoto wengi sana na madara kidogo sana hili ni tatizo la kitaifa. Watoto hawawezi kusubiri nyumbani miaka miwili tupate makusanyo ya kodi na kujenga. Umri wa mtoto ni muhimu sana kwenye elimu na jamii. Kukopa kunaonyesha hali mbaya ya mipango huko nyuma na hatuwezi kumlaumu Raisi kwa kutafuta pesa za kusaidia watoto. Hii ni muhimu kiasi kwamba hata world bank walitoa $500M wakati wa Magufuli kusaidia hili kama unakumbuka skendo ya watoto wa mimba hii pesa ilikuwa mkopo nafuu wa elimu. Watoto wanaingia shule wakiwa na miaka 7 serikali inabidi iwe na takwimu za kutosha ili madara wajenge kutokana na data mtoo inajulikana akifika miaka 7 anaingia shule hivyo mipango inatakiwa kuanzia akizaliwa tu.
Asante mkuu.Hili jambo haliepukiki kwa vyovyote vile.
 
Ndugu zangu mikopo sio kitu kibaya, na kwa kampuni kubwa au nchi mikopo ya maendeleo hulipwa kwa muda mrefu. Kwa individual kukopa then ulipe kwa miaka 20 sio rahisi maana nguvu zinakuwa zimeanza kupungua.

Ila kwa nchi, kukopa leo, kuna kizazi ambacho kinafaidika na mkopo sasa na msingi wake uwe wa kuifanya Tanzania ya leo na kesho iwe na neema na matumaini kuliko tusingekopa.

Rais yangu kwa wakubwa ambao wana dhamana ya kukopa kwa niaba yetu ili baadae sisi na wanetu tulipe, kopeni ili riba ya mabenki ya uwekezaji kama TIB na TADB ishuke na masharti ya mikopo kwa start-up investment projects yawe na fursa ya kuwafanya Watanzania wakope sio kama individuals ila watengeneza kampuni za kuzalisha bidhaa na huduma.

Miezi kadhaa imepita nilikuwa naongea na mtu mmoja alifanya kazi serikali ya mchonga, Mzee Ruksa na BWM, nyakati zile Tanzania ilikuwa ina-export wastani wa marobota laki 6 kwa mwaka. Victoria federation enzi hizo ikiwa na ofisi ya mauzo ya Pamba London.
Leo mauzo ya pamba, bila shaka haifiki hata robobota laki 1, maana yake uzalishaji umeshuka..

Kwanini TADB na TIB wasije na investment projects loans ili kampuni za Watanzania ziwekeze kwenye kilimo cha kibiashara kwa ku-mechanize mashamba yawe na mfumo wa umwagiliaji, pamba ivunwe, kampuni zingine ziundwe zikopeshwe textile machinery ili Tanzania iuze nyuzi, vitambaa hata nguo, ili hao wanetu ambao leo 1.3Tril inajenga madarasa yao, in 15 years wawe na sehemu ya kufanya kazi kwenye viwanda vya mnyororo wa thamani wa Pamba.
Hii ikihusisha kuwa na kampuni zingine zinazalisha mbolea na all the agro-chemicals ili hela ya imports ya agro-inputs ibaki ndani izunguke kwa ku-service deni.

Kwanini Tanzania isiwe exporter wa nyama middle east kwa kutumia advatange ya ng'ombe tulionao? Kwanini Tanzania isiwe exporter wa leather products baada ya kuwa tumechakata ngozi za ng'ombe?

Akina Ng'wigulu wataalamu hapo wizarani ya fedha, fikiriene kuifanya agro-commercial projects, dunia ina watu bil 7, tuuze walau SADC all the basic consumables.
Itakuwa aibu kama tutakopa pasi kujenga financial instrument itakayo-stimulate uzalishaji ambao utavutia forex.

Tanzania based on the vast of resources, tusipojiandaa kwenye uwekezaji wa miradi ya kibiashara, ipo siku zile projects za Nyanzaga Gold, Mahenge Graphite na gas ya kusini ziki-peak na kuna fursa ya kuuza kuku laki 1 na mayai say laki 3 kwa siku, tutabaki tunashangaa wakati nchi ndogo kama netherlands yenye idadi ya ng'ombe wachache kuliko Tz, ila kwa kuwa na ubora wa uwekezaji kwenye agribuz, wanauza nyama, mayai, maziwa na kuvuta forex ya kutosha kuliko sisi.


In 2019, the Netherlands exported €94.5 billion worth of agricultural goods. That is a 4.6% increase on the €90.4 billion export figure for 2018.


Dunia ya sasa mauzo ya agri-process ni biashara kubwa sana. Kwanini hatuna mauzo ya sausage from fresh water.

Hela toka kwenye mzunguko huo itasisimua makuzi ya service sector kama lega, insurance, banking, logistics, consultancy just to mention a few;

€90.4 billion ni sawa na TZS 247Tril.

Assume Watanzania tuwe na kampuni zenye mauzo ya wastani wa 20% ya nini Uholanzi walipata na TRA ika-tax hizo biashara, nchi ingepata kiasi gani?

We need the gov. to setup a room availability of financial instrument for Tanzania owned corporations to invest in know-how, technology and hire experienced expertise to make a game change in agri-investment.
Agribuz bado hatujagusa hata 5% ya potential ya nchi hii; ila kama ni kilimo cha kufa na kupona na kutegemea kudra za Mwenyezi ambacho ndicho kilichopo, basi; itapita miaka 20, Tanzania itaendelea ku-import toothpick, chupi, leso, toilet paper, gundi, penseli, chaki vitu ambavyo could be made in Tanzania.

Tunaomba kupata platform ya ku-dialog na madam SSH ili tufanye mambo haya yatokee.
Hongera sana mkuu kwa maono ya faida.
 
Jana Rais alisema kwamba Waziri wa fedha alimshauri kwamba mkopo utakaofuatia sehemu yake tutumie kulipa baadhi ya madeni ambayo yamemature.

Sasa Ndugu yangu Mwigulu??

Kweli unataka tutumie mkopo kulipa mkopo mwingine??

Hakuna chanzo kingine cha fedha serikali inaweza kukitengeneza??

Makusanyo yote haya tunayoambiwa yamefanyika yametumika kwenye jambo gani??
 
Mfano mkubwa ni katika miradi ya ujenzi ambayo kiuhalisia inasaidia wananchi lakini haiingizii serikali kipato chochote.
Tulitakiwa kukamilisha bwawa la umeme Rufiji kwanza kisha SGR kabla ya kuangaika na vyumba vya madarasa. Nawaza.
 
Halafu watoto wasisome. Nani ata endesha hizo treni?
Vyumba vya madara ufundusha ama walimu ndiyo ufundisha? Yanaweza kutengezwa madarasa ya dharura wakati tunakamirisha miradi itayotuingizia pesa ili tuepuke kukopa kwa riba ya aina yoyote. Jiongeze Mkuu nchi ijitegemee!
 
Vyumba vya madara ufundusha ama walimu ndiyo ufundisha? Yanaweza kutengezwa madarasa ya dharura wakati tunakamirisha miradi itayotuingizia pesa ili tuepuke kukopa kwa riba ya aina yoyote. Jiongeze Mkuu nchi ijitegemee!
Elimu ni hitaji la msingi la binadamu, hiyo treni kukulipa ni gambling huna uhakika ni sawa usinunue chakula nyumbani ili ununue tv ufungue banda umiza
 
Wanabodi,

Serikali inataka kufanya mengi na katika kufanya hayo, inataka kutumia muda mfupi kutekeleza miradi ya kimkakati kama njia ya kupeleka maendeleo kwa wananchi. Labda kuna uwezekano kwa serikali kukamilisha mipango yake bila kukopa lakini maelezo tuliyoyapata kutoka kwa viongozi wa nchi akiwemo Rais Samia mwenyewe ni kwamba itachukua muda mrefu sana kufikia malengo yaliyopangwa.

Mengi yamejadiliwa haswa katika kueleza umma kuhusu jinsi ambavyo nchi zingine hata zilizoendelea zinavyokopa fedha kwa miradi yao mbalimbali lakini jambo muhimu la kutafakari ni kama fedha hizo zitatunufaisha endapo zitatumika katika miradi isiyoingizia serikali kipato chochote. Mfano mkubwa ni katika miradi ya ujenzi ambayo kiuhalisia inasaidia wananchi lakini haiingizii serikali kipato chochote.

Tafakari,
Jumatano jema.
Umeandika nini sasa? Kama kitu hujui tulia,sio kazi ya serikali kufanya biashara bali ni Kazi ya serikali kuweka mazingira wezeshe kwa kutumia pesa ziwe za mkopo au hapana na miradi itakuwa kote kwenye sekta za miundombinu hadi sekta za huduma za jamii.

Na kwa taarifa yako ,tutaendelea Kukopa na mwaka ujao wa Fedha tutakopa Til.5

Screenshot_20220116-122331.png
 
Back
Top Bottom