Mbogo nyeusi
JF-Expert Member
- Dec 27, 2019
- 233
- 541
Najiuliza Kama katibu mkuu CCM ametangaza kufanyika mikutano ya hadhara nchi nzima itakayo fanywa na wabunge, madiwani, wenyeviti wa CCM wilaya,kata,vijiji na mitaa,zuio la Rais lilikuwa linawahusu watu gani?
Pia Rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM naye anazunguka kiaina kukutana na wananchi na anajibu hoja za washindani wenzake Kama mwenyekiti wa chama CCM, je hafanyi mikutano ya hadhara aliyoizuia yeye mwenyewe?
Sababu ya kuzuia mikutano ya hadhara kwa vyama vingine vya upinzani ni zipi na chama tawala kujifanyia mikutano chenyewe kina hofu gani? Kama chama wanazunguka kujiimarisha kwa nini wazuie wengine kwa kutumia dola wao wasijiimarishe?
Alipo Rais kama wenyekiti wa chama CCM huwa pia wapo wenyeviti wa mkoa,wilaya na hata viongozi wengine kitaifa na wanachama waliovalia sare za chama, je hiyo siyo nafasi ya mwenyekiti wa CCM anaitumia kuimarisha chama?
Je, hiyo mikutano iliyo agizwa na katibu mkuu wa chama CCM kufanyika na wabunge wa CCM madiwani na viongozi wengine watakuwa hawavai sare za chama?
Kwa huu uonevu ipo siku utatugarimu Kama taifa kila chama kina haki sawa kwa mujibu wa katiba,je CCM wanaogopa wapinzani kwa kuwa viongozi wake hawana uwezo wa kujibu hoja jukwaani?
Ni aibu mwenyekiti wa CCM kuzuia wenyeviti wa vyama vingine kufanya mikutano ya hadhara kwa uoga wa kushambuliwa majukwaani,
Hoja ya kwamba mikutano inarudisha uchumi nyuma,je hao watu watakao hudhuria kwenye hiyo mikutano iliyo agizwa kufanyika nchi nzima si wataacha kazi zao na kuhudhuria hiyo mikutano? Je, hapo hawajarudisha uchumi nyuma kwa huo muda wanaoenda kusikiliza viongozi wao?
Ni vyema tuambiwe ni jinsi gani mikutano ya hadhara inaharibu uchumi na kurudisha maendeleo nyuma lakini ilifanywa na wanaccm inapaisha uchumi juuuuuu!!
Pia Rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM naye anazunguka kiaina kukutana na wananchi na anajibu hoja za washindani wenzake Kama mwenyekiti wa chama CCM, je hafanyi mikutano ya hadhara aliyoizuia yeye mwenyewe?
Sababu ya kuzuia mikutano ya hadhara kwa vyama vingine vya upinzani ni zipi na chama tawala kujifanyia mikutano chenyewe kina hofu gani? Kama chama wanazunguka kujiimarisha kwa nini wazuie wengine kwa kutumia dola wao wasijiimarishe?
Alipo Rais kama wenyekiti wa chama CCM huwa pia wapo wenyeviti wa mkoa,wilaya na hata viongozi wengine kitaifa na wanachama waliovalia sare za chama, je hiyo siyo nafasi ya mwenyekiti wa CCM anaitumia kuimarisha chama?
Je, hiyo mikutano iliyo agizwa na katibu mkuu wa chama CCM kufanyika na wabunge wa CCM madiwani na viongozi wengine watakuwa hawavai sare za chama?
Kwa huu uonevu ipo siku utatugarimu Kama taifa kila chama kina haki sawa kwa mujibu wa katiba,je CCM wanaogopa wapinzani kwa kuwa viongozi wake hawana uwezo wa kujibu hoja jukwaani?
Ni aibu mwenyekiti wa CCM kuzuia wenyeviti wa vyama vingine kufanya mikutano ya hadhara kwa uoga wa kushambuliwa majukwaani,
Hoja ya kwamba mikutano inarudisha uchumi nyuma,je hao watu watakao hudhuria kwenye hiyo mikutano iliyo agizwa kufanyika nchi nzima si wataacha kazi zao na kuhudhuria hiyo mikutano? Je, hapo hawajarudisha uchumi nyuma kwa huo muda wanaoenda kusikiliza viongozi wao?
Ni vyema tuambiwe ni jinsi gani mikutano ya hadhara inaharibu uchumi na kurudisha maendeleo nyuma lakini ilifanywa na wanaccm inapaisha uchumi juuuuuu!!