Pre GE2025 Mikutano ya CHADEMA yadoda Vunjo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

MTANZANIA620

Member
Joined
Jun 20, 2023
Posts
65
Reaction score
81
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika operesheni ya siku 21 ya kukijenga chama hicho kanda ya Kaskazini inayoongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho Ndugu Freeman Mbowe imekutana na mahudhurio hafifu sana Jimbo la Vunjo, Moshi DC mkoani Kilimanjaro.

Hali hiyo imepelekea Mwenyekiti wa kanda hiyo wa chama hicho anayemaliza muda wake Ndg Godbless Lema kuwafokea wananchi kuwa wanawavunja moyo kwani kazi hii wanayofanya ni ngumu na wanajitolea hivyo kutojitokeza kwenye mikutano kunawavunja moyo viongozi.

Katika mikutano yao katika kata za Kahe na mji mdogo wa Himo mikutano ya chama hicho kilipata mahudhurio hafifu licha ya helikopta waliyokuwa nayo kuzunguka raundi tatu angani kabla ya kutua ili kufanya hamasa.

Wengine walioonekana kwenye ziara hiyo ni pamoja na aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Vunjo Grace Kiwelu ambaye aliachwa na mume wake wa ndoa Ndg Sindato Ndesamburo Kiwelu baada ya kukosa uaminifu kwenye ndoa.


Your browser is not able to display this video.
 
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika operesheni ya siku 21 ya kukijenga chama hicho kanda ya Kaskazini inayoongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho Ndugu...
Erythrocyte njoo useme jambo hapa, huu utakuwa uzushi
 
Hiyo jee
 

Attachments

  • 20240709_233509.jpg
    118.6 KB · Views: 4
Huko si kwa marehemu mrema!
 
Lipumba toka siku ile alipofanya mkutano wa hadhara ukahudhuriwa na waandishi wa habari tu hajafanya tena mkutano.
Mama wa kizimkazi anawaendesha puta wapinzani.
 
Kanda hiyo lema imeshamuelemea aondoshwe kama mkuu wa kanda, pia Watanznaia wameamka kwa sasa, wanataka MATENDO, hawataki MANENO!, ccm imetimiliza matakwa ya Watanznaia.
 
Kila mkutano watu 10 wakikubali na kubatizwa wanatosha kabisa
 
Wananchi hawana imani na wapinzani bado wanajua wanaweza kupata haki chini ya ccm kama ilivyotokea katika awamu ya tano chini ya magufuli. Huko upinzani wanaona ulaghai mtupu wa mbowe na genge lake kwa hivyo bora wakomae na ccm yao kupata uongozi bora wa nchi.
 
Mleta mada ni mpotoshaji
Sio kweli kwamba Chadema haiku pata watu I waS there.
Huyu ana jaribu kuzuia mafuriko kwa mkono kwa nia ya ku ya kumpendeza bwana wake
 
Hayo mambo ya watu wengi au wachache ni ujinga tu. Kinachotakiwa ni dhamira ya kila mmoja, kuelewa ccm si chama kitakachotuletea maendeleo na kutoa umasikini. Kimeshashindwa kwa miaka zaidi ya 60.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…